Mwendo wa Kupigania Amani, Tatizo la kuondosha Silaha

Pile F

Senior Member
Aug 15, 2020
121
170
Wasalaam wanajamvi... Poleni na majukumu na Mwenyezi awawekee wepesi kila wakati mema yazidi kuongezeka kwa kila mmoja wetu

JE MNAAMINI KUWA KUNA UWEZEKANO HALISI WA KUONDOSHA SILAHA ULIMWENGUNI?

Uwezekano kama huo upo bila ya kujali kwamba tangu mwanzoni kabisa mwa historia yao, binadamu walikuwa wakiendesha vita, wakiunda na kukamilisha silaha za aina mbalimbali, huku serikali zao zikitegemea utumiaji wa mabavu kama chombo cha kudhaminia hali ya kuishi kwa usalama na kupuuza kabisa miito yoyoye ile ya mara kwa mara juu ya uondoshaji wa silaha.

Naam, hivyo ndivyo hali ya mambo hayo ilivyokuwa mpaka sasa, lakini haipasi wala haiwezi kuachiwa kuendelea mbele tena, kwani zama hizi ndizo zama za kupatikana kwa silaha kali sana za KINYUKLIA, jambo ambalo limeyafanya matarajio yoyote yale juu ya utumiaji mabavu kama njia ya kutanzua matatizo ya kimataifa kuwa ni maruirui matupu
 

Attachments

  • Screenshot_20220923-175307_1.jpg
    Screenshot_20220923-175307_1.jpg
    36.2 KB · Views: 5
Katika maandishi fulani ya Magharibi nimewahi kusoma kwamba pindi vita vya KINYUKLIA vikifumuka, matokeo yake yatakuwa ni kuangamizwa kwa nchi zile tu zilizo wanachama wa miungano mikuu miwili inayopambana, yaani mwahada wa WARSAW na ule wa NATO

Dai hili nalo halina kabisa msingi wowote. Kwa mujibu wa mabingwa maarufu wa mambo ya kijeshi, vita kama hivyo havitalipita upande bara lolote lile wala pembe yoyote ya dunia.
 
Kuhusika na haya, Tume ya Kimataifa Isiyofungamana na Upande Wowote, ambayo inajishughulisha na tatizo la kuondosha SILAHA na kudhaminia usalama duniani imesisitiza:

" Baadaye Maisha yenyewe ya binadamu wote yatakabiliwa na hatari ya kifo. Wingi mkubwa wa mipasuko ya mabomu ya kinyuklia utakuwa na athari ya muda mrefu na kupelekea kuziharibu tabia za mirathi ya binadamu na kuenea kwa maradhi ya saratani, kuchafua hewa duniani kote, na kwa hivyo kusababisha maangamizi ya ulimwengu wa wanyama na mimea pamoja na kuumbuka kwa maumbile yote kabisa. Matokeo yake yatakuwa ni kutokomezwa kwa jamii ya binadamu "
 
Ni kwa nini unafikiri haiwezekani Count Capone
Swali zuri sana.

Asili ya mwaadamu ni Ubinafsi, Ukatili, Uchoyo na Ushindani. Na suala la Usalama kwa mwanaadamu ni kitu cha kwanza kabisa na ndiyo sababu leo wanaadamu wanaishi kwenye jamii tunazoziita nchi. Kiasili mwanaadamu ndiye kiumbe anayetumia miaka mingi akiwa vulnerable, hajiwezi hajikwezi, mnyama akizaliwa porini hapohapo huanza kusimama, kutembea na sekunde kadhaa anakimbia, inaonesha jinsi gani yuko tayari kujilinda hatari ikitokea.

Lakini tazama maisha ya mwanaadamu tangu azaliwe mpaka afikie hatua ya kuweza kujilinda huchukua zaidi ya miaka mi 5. Hivyo suala la Usalama kwetu ni la msingi sana na silaha hutuhakikishia hilo.

ASILI YA MWANAADAMU
Sifa za asili kama nilivyotaja hapo juu hujionesha katika uwanja wa kimataifa ambapo nchi sasa ndizo hujivika sifa za asili ya mwanadamu simply because wanaadamu ndiyo wanaoendesha nchi.

kimataifa sasa ndiko asili hiyo hudhihirika maana nchi zinafanya kila lililo ndani ya uwezo wao kutimiza maslahi yao binafsi ikiwemo matumizi ya silaha vitani, mfano Ujerumani wakati wa WWI &WWII, vita vya ukombozi Afrika, vita vya Afghan na Uingereza, Afghan na USSR, Afghan na Marekani n.k

Vilevile harakati za mataifa yanayotaka kujitenga kama Barotseland, Biafra, Catalonia, Scotland, SADR, Sudan Kusini n.k

Kwa msingi huo basi hakuna nchi itakayokubali kuweka suala ya silaha kando, hata wanapozungumzia Nuclear Disarmament huoni suala hili katika utekelezaji kwa maana hakitekelezeki, Ukweli ni kuwa kila nchi inaona huo ni mpango unaoweza kutumiwa na nchi hasimu kuishinda

Wanapozungumzia swala la Non Proliferation halitekelezeki maana mataifa yasio na silaha za nyuklia katu hayajihisi salama mbele na mataifa yenye nyuklia mfano Israel, Iran na Korea Kaskazini

Leo hii Binaadamu akikutana na hatari yeyote atalazimika kuidhibiti haraka, inawezekanaje kuidhibiti kama hana silaha? Hapo ndipo umuhimu wa silaha huonekana.
 
Nakubaliana nawe kuwa athari zake ni dunia nzima ila zitakazo athirika zaidi ni zenye nyuklia.
Katika maandishi fulani ya Magharibi nimewahi kusoma kwamba pindi vita vya KINYUKLIA vikifumuka, matokeo yake yatakuwa ni kuangamizwa kwa nchi zile tu zilizo wanachama wa miungano mikuu miwili inayopambana, yaani mwahada wa WARSAW na ule wa NATO

Dai hili nalo halina kabisa msingi wowote. Kwa mujibu wa mabingwa maarufu wa mambo ya kijeshi, vita kama hivyo havitalipita upande bara lolote lile wala pembe yoyote ya dunia.
 
Wasalaam wanajamvi... Poleni na majukumu na Mwenyezi awawekee wepesi kila wakati mema yazidi kuongezeka kwa kila mmoja wetu

JE MNAAMINI KUWA KUNA UWEZEKANO HALISI WA KUONDOSHA SILAHA ULIMWENGUNI?

Uwezekano kama huo upo bila ya kujali kwamba tangu mwanzoni kabisa mwa historia yao, binadamu walikuwa wakiendesha vita, wakiunda na kukamilisha silaha za aina mbalimbali, huku serikali zao zikitegemea utumiaji wa mabavu kama chombo cha kudhaminia hali ya kuishi kwa usalama na kupuuza kabisa miito yoyoye ile ya mara kwa mara juu ya uondoshaji wa silaha.

Naam, hivyo ndivyo hali ya mambo hayo ilivyokuwa mpaka sasa, lakini haipasi wala haiwezi kuachiwa kuendelea mbele tena, kwani zama hizi ndizo zama za kupatikana kwa silaha kali sana za KINYUKLIA, jambo ambalo limeyafanya matarajio yoyote yale juu ya utumiaji mabavu kama njia ya kutanzua matatizo ya kimataifa kuwa ni maruirui matupu
Uzi mrefu sana. Aliyesoma wote anielimishe kwa muhtasar
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom