J.K.Rayhope
JF-Expert Member
- Oct 26, 2011
- 316
- 31
Kama mlivyosikia na kuona kwenye vyombo vya habari kwamba Waheshimiwa Samson Kiwia(Ilemela) na Machemuli(Ukerewe) wamejeruhiwa vibaya sana.Nikujuze tu mwanaJF kwamba ilikuwa ni hesabu kali ilipigwa na watu wa CCM Mwanza na ingekwenda sawa tungekuwa tunaongea mengine kwamba Kiwia na wenzake wangekuwa ndani kwa kosa la kuua au kujeruhi kwa bastola.Alipigiwa simu usiku wa manane na watu kwamba CCM wanagawa rushwa na alipofika huko akakuta sio.Ktk kurudi ndio akakuta ameshawekwa kati ya gari mbili zenye watu hao waliomjeruhi.Lakini nao pia walipiga simu polisi na kudai CHADEMA walikuwa wakigawa rushwa.Kwa mujibu wa ManaCCM aliyerejea Chadema leo,ilikuwa vyombo vya habari viripoti"MBUNGE AUA KWA RISASI MWANZA"au"MBUNGE AJERUHI KWA RISASI MWANZA" Ili kwamba watu wa Kirumba wasiichague Chadema.Kwa busara zake Mh.Kiwia aling'amua mtego huo na alijeruhiwa.Kwa ufupi tu hilo ndilo pozi lililoandaliwa na CCM.