lupasulwisye
Senior Member
- Sep 5, 2012
- 104
- 21
Si muda mrefu Waziri Mkuu, Mizengo Pinda amemaliza kikao chake na Masheikh pamoja na Maaskofu hapa Mwanza katika ukumbi wa BoT kuhusu nani achinje kitoweo.
Katika mazungumzo yake na waandishi wa habari waliotaka kujua msimamo wa Serikali kuhusu nani hasa mwenye uhalali wa kuchinja wanyama kati ya Wakiristo na Waislam, Waziri Mkuu, Pinda amesema mazoea ya tangu zama za kale yanayowaruhusu Waislamu kuchinja yaendelee hadi hapo maamuzi mengine yatapofikiwa na Serikali.
Ameagiza pia kuundwa kamati maalumu itakayohusisha pande zote mbili za Waislamu na Wakiristo, ambayo itashughulikia mgogoro huo, na kamati hiyo iundwe na kufanyakazi zake na kukamilisha haraka sana!.
Zaidi soma -> Pinda ‘aelemewa' mgogoro wa nani achinje nyama | Fikra Pevu
​Mtoto wa mkulima waziri mkuu MIZENGO PINDA ameishiwa cha kuwambia Watanzania.Anataka tuishi kwa mazoea hata kama mazoea hayo hayana tija kwa wakati huu.Tumekupata vizuri mheshimiwa.