Antar bin Shaddad
JF-Expert Member
- Oct 11, 2010
- 202
- 101
Leo mjini Arusha majira ya saa 10 za jioni mwandishi wa habari wa kujitegemea Joseph Ngilisho amekamatwa na maafisa wa takukuru kwa tuhuma za kupokea rusha ya shilingi milioni 2 kutoka kwa afisa wa Jumuiya ya Afrika Mashariki katika hoteli ya African Tulip.
Awali kabla ya kutiwa mbaroni mwandishi huyo aliandika habari katika gazeti la Dira wiki iliyopita kuwa jengo jipya la Jumuiya ya Afrika Mashariki linavuja na limejengwa chini ya kiwango madai ambayo kimsingi yalikuwa ya uongo na baada ya kuandika habari hiyo akawa anampigia simu mhandisi wa jumuiya Dr. Kleruu akimtisha ampe fedha la sivyo ataendelea kuwaandika na ndipo maafisa wa jumuiya wakaripoti Takukuru na mtego wa kumnsa ukaandaliwa hadi jioni ya leo alikuwa bado mahabusu.
Awali kabla ya kutiwa mbaroni mwandishi huyo aliandika habari katika gazeti la Dira wiki iliyopita kuwa jengo jipya la Jumuiya ya Afrika Mashariki linavuja na limejengwa chini ya kiwango madai ambayo kimsingi yalikuwa ya uongo na baada ya kuandika habari hiyo akawa anampigia simu mhandisi wa jumuiya Dr. Kleruu akimtisha ampe fedha la sivyo ataendelea kuwaandika na ndipo maafisa wa jumuiya wakaripoti Takukuru na mtego wa kumnsa ukaandaliwa hadi jioni ya leo alikuwa bado mahabusu.