Ngalikivembu
JF-Expert Member
- Oct 6, 2010
- 1,959
- 872
Nimesoma makala ya mwandishi wa muda mrefu Mayage S Mayage katika gazeti la Raia Mwema wiki hii.Nitangulie kusema nilimjua ndugu huyu kupitia maandishi yake katika magazeti ya Habari Corporation wakti huo.Ndo kwanza nilianza kumsoma nikiwa kidato cha tano pale mwanza magazeti yaliyokuwa yananunuliwa na shule.Nilimpenda kwa wakati huo,kwa namna alivyokuwa anajenga hoja zake.Na nilikuwa kipenzi cha magazet hayo kabla ya kusitisha rasmi kuyasoma mara baada ya kuingia mwekezaji mpya aliyekuwa na sera mpya za kupamba chama.
Baadae kidogo nilikuja kumjua kumbe alikuwa kada wa ccm ambaye alitaka kujaribu bahati ya ubunge kule Muhambwe Kigoma.Akatupwa nje.Nilikuwepo huko wakati huo.Sikubahatika kumsoma tena kutokana na kisa cha hapo juu.Leo nimemsoma tena katika gazeti la Raia mwema.Nimelazimika kuandika baada ya kile alichoeleza katika makala yake,"CCM imejivua gamba,lakini...."
Kwa waliosoma makala hiyo watabaini kuwa kumbe pale Newhabari wanaandika kuchumia tumbo tu na kusubiri makombo ya wanasiasa wanaomiliki magazeti hayo.Kushuku kwetu kuwa magazet hayo yanaandika kuwahadaa watanzania kumbe ni kweli.Msome Mayage uone anaeleza nini.Eti kumbe kazi ya uhariri ina siri nzito sana.Nilivyobaini ni kuwa wahariri hao ni symbol tu lakini wahariri rasmi ni wanasiasa wenyewe wenye kumiliki magazet hayo.Ushauri alioutoa kwa CCM ni kuwatosa wanajidai wanaipamba ccm na kuipenda kumbe wapo kwa ajili ya maslahi yao.Anashauri kwa sasa inabidi isitumie tena vyombo vya mafisadi kama inataka kurudisha heshima yake.
Hakika kama ameamua kuhama huko na kubain wanalishwa "sumu" hilo ni wazo la busara sana.Kina Muhingo na Balile bado hawajabaini kama wanawatendea watanzania isivyo ipo siku watakuja jutia kazi yao hiyo.
Baadae kidogo nilikuja kumjua kumbe alikuwa kada wa ccm ambaye alitaka kujaribu bahati ya ubunge kule Muhambwe Kigoma.Akatupwa nje.Nilikuwepo huko wakati huo.Sikubahatika kumsoma tena kutokana na kisa cha hapo juu.Leo nimemsoma tena katika gazeti la Raia mwema.Nimelazimika kuandika baada ya kile alichoeleza katika makala yake,"CCM imejivua gamba,lakini...."
Kwa waliosoma makala hiyo watabaini kuwa kumbe pale Newhabari wanaandika kuchumia tumbo tu na kusubiri makombo ya wanasiasa wanaomiliki magazeti hayo.Kushuku kwetu kuwa magazet hayo yanaandika kuwahadaa watanzania kumbe ni kweli.Msome Mayage uone anaeleza nini.Eti kumbe kazi ya uhariri ina siri nzito sana.Nilivyobaini ni kuwa wahariri hao ni symbol tu lakini wahariri rasmi ni wanasiasa wenyewe wenye kumiliki magazet hayo.Ushauri alioutoa kwa CCM ni kuwatosa wanajidai wanaipamba ccm na kuipenda kumbe wapo kwa ajili ya maslahi yao.Anashauri kwa sasa inabidi isitumie tena vyombo vya mafisadi kama inataka kurudisha heshima yake.
Hakika kama ameamua kuhama huko na kubain wanalishwa "sumu" hilo ni wazo la busara sana.Kina Muhingo na Balile bado hawajabaini kama wanawatendea watanzania isivyo ipo siku watakuja jutia kazi yao hiyo.