Mwanasheria wa CCM achukua fomu

sir.JAPHET

JF-Expert Member
May 18, 2012
699
133
Na Amon Mtega,

Songea


MWANASHERIA wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kutoka makao makuu Dodoma, Glorious Luoga, amejitosa kuchukua fomu ya kuwania ujumbe wa Halmashauri Kuu ya chama hicho (NEC).

Luoga anawania nafasi hiyo kupitia Wilaya ya Songea vijijini mkoani Ruvuma, huku akiwataka wananchi mkoani hapa kuona umuhimu wa kujitokeza kuchangia shughuli za maendeleo.

Hayo aliyasema juzi wakati akichukuwa fomu ya kugombea nafasi hiyo katika Ofisi ya Katibu wa CCM Wilaya ya Songea Vijijini.

Luoga alisema, kila mwananchi ana wajibu wa kimsingi kuhakikisha kuwa, anachangia shughuli za maendeleo katika eneo analoishi na kuachana na tabia ya kupenda kuchangia harusi.

Alisema wilaya hiyo imekuwa na changamoto nyingi ikiwemo shule za sekondari za kata ambazo nyingi zimekuwa hazina maabara, walimu, vitabu pamoja na madawati.

"Lengo langu la kuchukuwa fomu nikuja kuunga mkono jitihada zilizofanywa na wezee wangu pamoja na Serikali ukizingatia wilaya yetu inachangamoto nyingi.

"Hizi changamoto utatuzi wake sio lazima zikasemewe bungeni kwani mkongojo wa wazee hupokelewa na vijana," alisema Luoga.

Luoga alisema CCM bado inanguvu kubwa na mfumo wake ni mzuri wa kupambana na vyama vingine vya siasa ambavyo vimekuwa vikijitahidi kujaribu kutaka kukichafua lakini watu wengi wenye uelewa wamekuwa wakikiamini.

Luoga alisema mfumo wa kujivua gamba katika chama hicho ulikuwa na lengo la kukisafisha chama na si vinginevyo, kama baadhi ya vyama vya upinzani vinavyodai kuwa kumejaa mafisadi.

Toa Maoni yako kwa habari hii


 
Amefundishwa na PalaMAGAMBA Kabudi!

Jamani, si kila aliyesoma sheria ni mwanasheria. Wengine wana LLB na hawajawahi kukanyaga kwenye mlango wa mahakama. Kuna rafiki yangu ana LLB lakini ni mfugaji mzuri wa kuku huko Kitunda, na hakumbuki kifungu hata kimoja cha sheria.
 
Kashaijabutege ni kweli hilo ulisemalo, huyo Luoga alikuwa anafanya kazi BRELA baada ya kutumiwa na mafisadi kuregister vikampuni uchwara ndio wamempa kazi hapo CCM, huyo hata mlango wa Mahakama hajui unafafanaje na hata hiko cheti cha sheria ni yale masomo yetu ya jioni ndio aliyopitia yeye.

2010 Aliujaribu moto wa Makangoro Mahanga kwenye kura za maoni za CCM ubunge wa Segerea akamsambaratishia mbali ndio maana hata hii NEC kakimbilia Songea ndio labda Mama yake mzazi anaweza kumsaidia maana mama yake ni Gamba zoefu linalojulikana kule Songea.
 
Last edited by a moderator:
Na Amon Mtega,

Songea

MWANASHERIA wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kutoka makao makuu Dodoma, Glorious Luoga, amejitosa kuchukua fomu ya kuwania ujumbe wa Halmashauri Kuu ya chama hicho (NEC).

Luoga anawania nafasi hiyo kupitia Wilaya ya Songea vijijini mkoani Ruvuma, huku akiwataka wananchi mkoani hapa kuona umuhimu wa kujitokeza kuchangia shughuli za maendeleo.


Hayo aliyasema juzi wakati akichukuwa fomu ya kugombea nafasi hiyo katika Ofisi ya Katibu wa CCM Wilaya ya Songea Vijijini.

Luoga alisema, kila mwananchi ana wajibu wa kimsingi kuhakikisha kuwa, anachangia shughuli za maendeleo katika eneo analoishi na kuachana na tabia ya kupenda kuchangia harusi.

Alisema wilaya hiyo imekuwa na changamoto nyingi ikiwemo shule za sekondari za kata ambazo nyingi zimekuwa hazina maabara, walimu, vitabu pamoja na madawati.

"Lengo langu la kuchukuwa fomu nikuja kuunga mkono jitihada zilizofanywa na wezee wangu pamoja na Serikali ukizingatia wilaya yetu inachangamoto nyingi.

"Hizi changamoto utatuzi wake sio lazima zikasemewe bungeni kwani mkongojo wa wazee hupokelewa na vijana," alisema Luoga.

Luoga alisema CCM bado inanguvu kubwa na mfumo wake ni mzuri wa kupambana na vyama vingine vya siasa ambavyo vimekuwa vikijitahidi kujaribu kutaka kukichafua lakini watu wengi wenye uelewa wamekuwa wakikiamini.

Luoga alisema mfumo wa kujivua gamba katika chama hicho ulikuwa na lengo la kukisafisha chama na si vinginevyo, kama baadhi ya vyama vya upinzani vinavyodai kuwa kumejaa mafisadi.

Toa Maoni yako kwa habari hii
Ni Mkuu wa wilaya ya Tarime na ikibidi Mheshimiwa Rais Magufuli amteua kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mara kwa utendaji wa kazi nzuri aliyoifanya Tarime
 
Na Amon Mtega,

Songea

MWANASHERIA wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kutoka makao makuu Dodoma, Glorious Luoga, amejitosa kuchukua fomu ya kuwania ujumbe wa Halmashauri Kuu ya chama hicho (NEC).

Luoga anawania nafasi hiyo kupitia Wilaya ya Songea vijijini mkoani Ruvuma, huku akiwataka wananchi mkoani hapa kuona umuhimu wa kujitokeza kuchangia shughuli za maendeleo.


Hayo aliyasema juzi wakati akichukuwa fomu ya kugombea nafasi hiyo katika Ofisi ya Katibu wa CCM Wilaya ya Songea Vijijini.

Luoga alisema, kila mwananchi ana wajibu wa kimsingi kuhakikisha kuwa, anachangia shughuli za maendeleo katika eneo analoishi na kuachana na tabia ya kupenda kuchangia harusi.

Alisema wilaya hiyo imekuwa na changamoto nyingi ikiwemo shule za sekondari za kata ambazo nyingi zimekuwa hazina maabara, walimu, vitabu pamoja na madawati.

"Lengo langu la kuchukuwa fomu nikuja kuunga mkono jitihada zilizofanywa na wezee wangu pamoja na Serikali ukizingatia wilaya yetu inachangamoto nyingi.

"Hizi changamoto utatuzi wake sio lazima zikasemewe bungeni kwani mkongojo wa wazee hupokelewa na vijana," alisema Luoga.

Luoga alisema CCM bado inanguvu kubwa na mfumo wake ni mzuri wa kupambana na vyama vingine vya siasa ambavyo vimekuwa vikijitahidi kujaribu kutaka kukichafua lakini watu wengi wenye uelewa wamekuwa wakikiamini.

Luoga alisema mfumo wa kujivua gamba katika chama hicho ulikuwa na lengo la kukisafisha chama na si vinginevyo, kama baadhi ya vyama vya upinzani vinavyodai kuwa kumejaa mafisadi.

Toa Maoni yako kwa habari hii
Waache wafu wazike wafu wao!
 
Back
Top Bottom