Mwanangu amepoteza uwezo wakusimama na kutembea

Mzee wajaribu kucheki uti wa mgongo, usiende kwa mganga utaharibu kila jambo, muombe sana mungu akufanyie wepesi, kama ni mambo ya wanadamj yeye anaweza kuondoa na kama ni ugonjwa kqa amri yake, pia yeye anaweza kuondoa.. We komaa hospital na dua kqenye moyo wako.
Uti wa mgongo kipimo kimeonyesha upo sawa
 
Wahi kwa Mwamposa Kawe,kama uko mbali fatilia maombi ya operation komboa familia kila siku saa tatu usiku..Mungu awavushe,poleni sana
 
Ooh poleni sana mkuu, Mungu amsaidie binti taifa la kesho apone haraka, ana umri sawa na mdogo angu nimefikiria 😪. Poleni atakua sawa🙏
 
Hao madaktari ni wazembe sana, especially uliowafata baada ya mwanao kushindwa kutembea, wajinga kama hao ndo hufanya mauaji hospital bila kujijua, nimesoma nao wengi, wengine wanafaulu ila mtu unajua kabisa huyu hafai na hana maamuzi sahihi
Anyways, ningependa kujua au ungemuuliza mwanao aliangukaje na akielezee kiufasaha kabisa bila kupindisha neno(every small detail matter), kuna possibilities nyingi za ugonjwa wake ila the most ovious sitaki kuikimbilia uku sijamuona mgonjwa kabisa,
Ukimshika mguu wake bila hizo dawa za maumivu inakuaje, na ukimbinya kidogo kwenye nyama za mapajani au kwenye kigimbi inakuaje??
Na je anaweza kuhamisha mguu wake ata kidogo kwa sasa??
Nijibu please, maana uku Jf ni kusaidiana

Ila kikubwa umeelezwa vizuri na baadhi ya watu humu, nenda muhimbili tafta daktari mzoefu na alieona mengi, uzuri matatizo ya binadam hujirudia, ukipata mzoefu yawezekana ashaona mengi ya ugonjwa huo na pia ashafanya makosa mpaka akajirekebisa
Kuna vipimo inabidi wavifanye kama MRI na kupima fluid iliyoko kwenye vertabral colum, ni maumivu ila hey, bora maumivu ya maramoja na diagnosis ikapatikana
Kibaya cha magonjwa mengi ni kuchelewa kufika hospitalini, hao madaktari wa mwanzo ilibidi wajiulize kwann mtoto anaumia na anachechemea wakati hakuna palipoumia, ilibid wajue situation iliyomkuta, ila myb myb nao wanapata wagonjwa wengi ambao matatizo yao sio serious ndo maana wakaja na hizo judgement

So please nenda muhimbili pia tafta madaktari wazoefu ata kama wamestaaf wafate kwenye hospital zao
Walikua wanauliza ameangukaje nikwamba anasema amengukia makalio..
-ukimshika mguu hapat maumivu yoyote
-ukimbinya nyama zinabonyea na ukimuachia zinarud kama kawaida
-hawezi kuhamisha mguu kabisa anafanya kuinyanyua kwamikono kuisogeza
 
Pole sana Mkuu,
i wish hao madaktrai hata wange brainstorm nakukupa mwanaga angalau ushauri basi dah..!

Kama wadau walivyoelezea jitahidi sana uje huku Dar, uende muhimbili,

Pia jaribu kuchanganya na mawazo ya wadau ujaribu kumdadisi daktari.
 
Pole sana Majan...Mungu akufanyie wepesi kwenye hili...

Ukiweza sana mpeleke na kwenye maombi..
Kwa sasa Anaendeleaje?
 
Pole Sana. Mpate Neuro physician haraka Sana. Wapo hospital kubwa. Pia mkande na Mafuta ya Karafuu. Pia ukipata Seaweed kiswahili Mwani inapatikana maduka machache Kariakoo mpatie. Pia maombi.
 
pole sana kwa changamoto iliyokupata

kuna mtoto wa jiran yangu nae alishawahi kupata ttzo linakokaribia kufanana na la kwako

ila huyu tatizo liligindulika Pale NSK hsp kwa dk wa mifupa anayekuja kutokea KCMc

mtoto aligindulika kuwa na jipu kwenye nyonga na alifanyiwa operation KCMC hsp na akapona

ila ndo mpk leo mguu wake mmoja ni mfupi.

usihangaike na waganga bado ni mapema mno
 
Pole Sana. Mpate Neuro physician haraka Sana. Wapo hospital kubwa. Pia mkande na Mafuta ya Karafuu. Pia ukipata Seaweed kiswahili Mwani inapatikana maduka machache Kariakoo mpatie. Pia maombi.
Hiyo mwani inatumikaje
 
kwasasa tunaendelea na tiba yakumchua kwa dawa zakisuni, yale maumivu makali usiku yameanza kupungua nakwasasa angalau vidole anaweza kuvichezesha
Cc Makiwendo
Safi Sana. Nijibu tu yote hapa. Umesema uko Mbeya na Mwani ni zao la Baharini. Inapatikana Sana DSM Yale maduka ya Kisuna na wanautoa Zanzibar. Binafsi ninautumia kama kirutibisho na tiba kwa mambo mengi hasa mifupa na misuli. Mwani au Seaweed iko ya Unga imesagwa na nzima. Ya Unga unakoroga kijiko kidogo cha chai kwa kikombe cha maji ya Moto unakunywa. Mtoto mpe nusu kijiko cha chai. Ulio mzima unachukua vipande viwili au vitatu unaloweka saa nzima(ni ngumu Sana) halafu unatafuna au unablend hata na matunda upate juice unakunywa). Itasaidia Sana. Kama Una ndugu mtume aende Kariakoo akutafutie akutumie. Ni maduka machache yanayouza Mwani hapo Kariakoo. Siku hizi mi ninaagiza Zanzibar maana bei pia iko chini kidogo Kwa 15,000 packet badala ya 20,000 Kariakoo. Naagiza za kunitosha hata 6 months. Ni food supplement nzuri Sana Kwa Sisi watu wazima umri umesogea mifupa na nerves zinachoka hivyo tuna boost.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom