Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,318
- 33,125
MWANAMKE aliyebadilishiwa mtoto wake wodini alimpata baada ya kuanza msako mkali uliofanyika wodini humo Wakunga na wauguzi waliokuwa zamu walianza kuwahoji wakinamama waliokuwa wodini humo na kubaini kuwa kuna mama mwingine alimchukua mtoto huyo ambaye hakuwa wake.
Kwa mujibu wa chanzo cha habari hii kilisema kuwa, mama yule alirudi wodini na kuwaeleza kuwa aliondoka na mtoto ambaye hakuwa wake na manesi kuanza kulishughulikia suala hilo kwa kuwa lilikuwa ni jambo hatari la kumfukuzisha mtu kazi.
Kwa juhudi za manesi wakishirikiana na wakunga walipita kwa kila mwanamke ambaye alijifungua kwa wakati ule na huku wakiwa na faili lililoonyesha kuwa mwanamke amejifungua mtoto gani na kubaini kuwa kuna mama mmoja alimbadilisha mtoto wake na kumchukua mtoto ambaye hakuwa wake.
Mama huyo alibainika baada ya kuonekana amembeba mtoto wa kike wakati yeye alijifungua mtoto wa kiume na wakati akihojiwa alikuwa hana jibu.
Hivyo manesi walimchukua mtoto yule na mama aliyeibiwa mtoto wake alimgungua mtoto yule kuwa ni wa kwake kwa kuwa alimuweka alama katika moja ya sehemu katika mwili wa mtoto yule na alikiona kitenge alichomviringisha mtoto yule.
Hatua iliyofuata mama yule alikabidhiwa mtoto wake na yule mwingine kupewa mtoto wake ambaye alimbadilisha.
Kwa vitisho vilivyotoka kwa manesi mama yule alipohojiwa alikiri kuwa alimbadilishia mwenzake wakati alipokwenda ****** na kukiri na yeye alikuwa anatamani mtoto wa kike kwa muda mrefu.
Kwa huruma za manesi wengine ambao walimuonea huruma mama huyo na kuamua kutomchukulia hatua kwakuwa alitoka kujifungua lakini manesi wengine wenye hasira walionekana kumpachika maneno makali mama huyo na wengine walionekana kuwa na jazba ya kutaka kumpiga kwa kuwa alikuwa anataka kuwafukuzisha kazi.
http://www.nifahamishe.com/NewsDetails.aspx?NewsId=2626902&&Cat=1
Kwa mujibu wa chanzo cha habari hii kilisema kuwa, mama yule alirudi wodini na kuwaeleza kuwa aliondoka na mtoto ambaye hakuwa wake na manesi kuanza kulishughulikia suala hilo kwa kuwa lilikuwa ni jambo hatari la kumfukuzisha mtu kazi.
Kwa juhudi za manesi wakishirikiana na wakunga walipita kwa kila mwanamke ambaye alijifungua kwa wakati ule na huku wakiwa na faili lililoonyesha kuwa mwanamke amejifungua mtoto gani na kubaini kuwa kuna mama mmoja alimbadilisha mtoto wake na kumchukua mtoto ambaye hakuwa wake.
Mama huyo alibainika baada ya kuonekana amembeba mtoto wa kike wakati yeye alijifungua mtoto wa kiume na wakati akihojiwa alikuwa hana jibu.
Hivyo manesi walimchukua mtoto yule na mama aliyeibiwa mtoto wake alimgungua mtoto yule kuwa ni wa kwake kwa kuwa alimuweka alama katika moja ya sehemu katika mwili wa mtoto yule na alikiona kitenge alichomviringisha mtoto yule.
Hatua iliyofuata mama yule alikabidhiwa mtoto wake na yule mwingine kupewa mtoto wake ambaye alimbadilisha.
Kwa vitisho vilivyotoka kwa manesi mama yule alipohojiwa alikiri kuwa alimbadilishia mwenzake wakati alipokwenda ****** na kukiri na yeye alikuwa anatamani mtoto wa kike kwa muda mrefu.
Kwa huruma za manesi wengine ambao walimuonea huruma mama huyo na kuamua kutomchukulia hatua kwakuwa alitoka kujifungua lakini manesi wengine wenye hasira walionekana kumpachika maneno makali mama huyo na wengine walionekana kuwa na jazba ya kutaka kumpiga kwa kuwa alikuwa anataka kuwafukuzisha kazi.
http://www.nifahamishe.com/NewsDetails.aspx?NewsId=2626902&&Cat=1