Prof. Janabi: Kujifungua Mtoto 'Bonge' si nzuri Kiafya

BARD AI

JF-Expert Member
Jul 24, 2018
3,376
8,120
Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo na Mkurugenzi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili, Prof. Mohamed Janabi amesema Wajawazito wanaojifungua Watoto Wanene wasidhani Watoto wao wana Afya njema.

Amesema "Pale Wodini unakuta mtu amejifungua Mtoto ana Kilo 4, ndugu wanasema Mashallah, hapo hakuna Mashallah, Mtoto ni 'Over Weight' huyo, si jambo la kufurahia ni tatizo hilo.

Ameongeza kuwa unene uliopitiliza kwa Mtoto unamuweka hatarini kuja kupata Magonjwa Yasiyoambukiza yakiwemo ya Figo, Moyo, Shinikizo la Juu la Damu pamoja na Kisukari anachoweza kupata kutoka kwa Mama.

Aidha, ameshauri Wajawazito kuzingatia ulaji mzuri wa Vyakula kwasababu una athari za moja kwa moja kwa Mtoto atakayezaliwa.

=============

Pia, mama anapokuwa mnene zaidi wakati wa ujauzito kutokana na ulaji wa mara kwa mara, hususan ulaji wa wanga kwa wingi, mafuta na mayai pamoja na chips, hatari yake ni uwezekano wa kujifungua mtoto mnene kupita kiasi.

Profesa Janabi, Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), aligusia suala hilo juzi usiku wakati wa hafla uzinduzi wa Taasisi ya Profesa Jay jijini Dar es Salaam, yenye lengo la kuchangia fedha za matibabu ya wagonjwa wa figo.

Taasisi hiyo imeanzishwa na Mbunge wa zamani wa Mikumi (Chadema) na msanii wa Hip Hop, Joseph Haule maarufu Profesa Jaybaada ya kuugua ugonjwa wa figo uliomfanya kulazwa hospitalini siku 462, matibabu aliyosema yalikuwa ya gharama kubwa.

Katika maelezo yake, Profesa Janabi alisema ugonjwa figo ambao Profesa Jay anapambana nao chanzo chake kikubwa ni ugonjwa wa kisukari ambao unaendana na mfumo mbovu wa maisha.

Akifafanua, alisema huo mfumo wa maisha unaoleta madhara hadi kuambukiza mtoto aliyeko tumboni.

Alitolea mfano, kuwa mama mwenye kisukari ni rahisi kuzaa mtoto mwenye uzito kupita kiasi kwa kutokana na ile sukari inayozalishwa kwenye damu kumfikia.

“Mtoto aliyezaliwa na uzito mkubwa yuko hatarini kupata magonjwa yasiyo ya kuambukiza na jamii haipaswi kufurahi mama anapojifungua mtoto mwenye uzito mkubwa kwa kuwa ni hatari kiafya.

"Pale wodi ya wazazi unaona mtu amejifungua mtoto mwenye kilogramu nne, ndugu wanasema mashallah, hapo hamna mashallah mtoto ni over weight (amezidi uzito), si jambo kufurahia ni tatizo,” alisema.

Profesa janabi alisema “si sahihi kwa mtoto kuzaliwa akiwa na uzito mkubwa kupita kiasi, tujitahidi kupunguza uzito.”

Alisema ukiwa mzazi mnene hali hiyo unaiambukiza kwa mtoto.

“Sasa hivi tunashuhudia watoto wadogo wanakuja Muhimbili figo zimeharibika tunalazimika kuwapandikiza,” alisema Profesa Janabi.

Mariana Luvanga, mama mwenye watoto watatu alisema mara zote anapokuwa mjamzito hujitahidi kuzingatia maelekezo anayopewa kliniki na hajawahi kukutana na changamoto ya kupata mtoto mwenye uzito mkubwa au mdogo kupita kiasi.

“Ninachofahamu msisitizo mkubwa kwa mama mjamzito ni kula lishe bora ili kutoa virutubisho muhimu kwa mtoto anayekua tumboni. Hii ni pamoja na kula matunda, mboga, nafaka nzima, nyama, samaki, maziwa na bidhaa za maziwa.

“Kingine ni mazoezi mepesi ambayo ni msaada kwa mama hata kuufanya mwili wake usichoke na kumuondolea uwezekano wa kujifungua kwa upasuaji. Binafsi sijawahi kukutana na changamoto kubwa zaidi ya zile za kawaida za miezi mitatu ya mwanzo,” alisema Mariana

Wakati Mariana akieleza hayo, mmoja wa wazazi ambaye amewahi kupata mtoto mwenye uzito mkubwa aliliambia gazeti hili kwa miaka 11 mtoto wake ameendelea kuongezeka uzito, hali inayomfanya kuwa mvivu.

“Mtoto wangu alizaliwa na kilo 5.8 na alizaliwa kwa upasuaji, hadi sasa hatujagundua ugonjwa wowote ila naweza kusema mwili wake unamfanya kuwa mvivu. Sio mtu wa kujichanganya na licha ya kufanya mazoezi kidogo lakini uzito wake unaendelea kuongezeka,” alisema mzazi huyo ambaye hakutaka jina lake liwekwe wazi.

Gazeti hili lilizungumza na mkunga mstaafu, Salome Milinga aliyesema yapo mambo yanayochangia mjamzito kujifungua mtoto mwenye uzito kupita kiasi, ikiwemo mama kuwa na asili ya uzito mkubwa kabla ya ujauzito, kuongezeka uzito kupita kiasi wakati wa ujauzito na mama kuzaliwa na uzito mkubwa.

“Uzito wa mama unachangia kwenye uzito wa mtoto atakayezaliwa, ndiyo maana wakati wote kliniki huwa tunawasisitiza wazingatie mlo kamili, wasiache kula kwa sababu ni kipindi ambacho mwili unahitaji chakula lakini lazima iwe ni kiasi, si kutwa vyakula vya wanga na mafuta.

Sababu nyingine, anasema hutokea kwa akina mama wenye kisukari kwa sababu kwenye damu ya mama, hapa upo uwezekano wa mtoto kuzaliwa na uzito mkubwa kwa sababu anapata glucose nyingi mno kutoka kwenye damu,” alisema mkunga huyo.

MWANANCHI
 
Prof Janabi unatakiwa uelezee aina za vyakula na uzito wa kina Mama na mtoto kwa kuanzia mwezi wa kwanza mpaka kipindi cha kujifungua kuelezea hivi hivi tu bila kutatua tatizo ni sawa na wanasiasa haya tufanyeje ili kutatua hilo tatizo kwa Watoto watakaozaliwa hapo baadae njoo na Suluhuhisho sio vitisho tu kila kukicha...
 
Prof Janabi unatakiwa uelezee aina za vyakula na uzito wa kina Mama na mtoto kwa kuanzia mwezi wa kwanza mpaka kipindi cha kujifungua kuelezea hivi hivi tu bila kutatua tatizo ni sawa na wanasiasa haya tufanyeje ili kutatua hilo tatizo kwa Watoto watakaozaliwa hapo baadae njoo na Suluhuhisho sio vitisho tu kila kukicha...
Nikuhakikishie hili hawezi....yeye ni mzee wa sound tu...
 
Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo na Mkurugenzi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili, Prof. Mohamed Janabi amesema Wajawazito wanaojifungua Watoto Wanene wasidhani Watoto wao wana Afya njema.

Amesema "Pale Wodini unakuta mtu amejifungua Mtoto ana Kilo 4, ndugu wanasema Mashallah, hapo hakuna Mashallah, Mtoto ni 'Over Weight' huyo, si jambo la kufurahia ni tatizo hilo.

Ameongeza kuwa unene uliopitiliza kwa Mtoto unamuweka hatarini kuja kupata Magonjwa Yasiyoambukiza yakiwemo ya Figo, Moyo, Shinikizo la Juu la Damu pamoja na Kisukari anachoweza kupata kutoka kwa Mama.

Aidha, ameshauri Wajawazito kuzingatia ulaji mzuri wa Vyakula kwasababu una athari za moja kwa moja kwa Mtoto atakayezaliwa.

=============

Pia, mama anapokuwa mnene zaidi wakati wa ujauzito kutokana na ulaji wa mara kwa mara, hususan ulaji wa wanga kwa wingi, mafuta na mayai pamoja na chips, hatari yake ni uwezekano wa kujifungua mtoto mnene kupita kiasi.

Profesa Janabi, Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), aligusia suala hilo juzi usiku wakati wa hafla uzinduzi wa Taasisi ya Profesa Jay jijini Dar es Salaam, yenye lengo la kuchangia fedha za matibabu ya wagonjwa wa figo.

Taasisi hiyo imeanzishwa na Mbunge wa zamani wa Mikumi (Chadema) na msanii wa Hip Hop, Joseph Haule maarufu Profesa Jaybaada ya kuugua ugonjwa wa figo uliomfanya kulazwa hospitalini siku 462, matibabu aliyosema yalikuwa ya gharama kubwa.

Katika maelezo yake, Profesa Janabi alisema ugonjwa figo ambao Profesa Jay anapambana nao chanzo chake kikubwa ni ugonjwa wa kisukari ambao unaendana na mfumo mbovu wa maisha.

Akifafanua, alisema huo mfumo wa maisha unaoleta madhara hadi kuambukiza mtoto aliyeko tumboni.

Alitolea mfano, kuwa mama mwenye kisukari ni rahisi kuzaa mtoto mwenye uzito kupita kiasi kwa kutokana na ile sukari inayozalishwa kwenye damu kumfikia.

“Mtoto aliyezaliwa na uzito mkubwa yuko hatarini kupata magonjwa yasiyo ya kuambukiza na jamii haipaswi kufurahi mama anapojifungua mtoto mwenye uzito mkubwa kwa kuwa ni hatari kiafya.

"Pale wodi ya wazazi unaona mtu amejifungua mtoto mwenye kilogramu nne, ndugu wanasema mashallah, hapo hamna mashallah mtoto ni over weight (amezidi uzito), si jambo kufurahia ni tatizo,” alisema.

Profesa janabi alisema “si sahihi kwa mtoto kuzaliwa akiwa na uzito mkubwa kupita kiasi, tujitahidi kupunguza uzito.”

Alisema ukiwa mzazi mnene hali hiyo unaiambukiza kwa mtoto.

“Sasa hivi tunashuhudia watoto wadogo wanakuja Muhimbili figo zimeharibika tunalazimika kuwapandikiza,” alisema Profesa Janabi.

Mariana Luvanga, mama mwenye watoto watatu alisema mara zote anapokuwa mjamzito hujitahidi kuzingatia maelekezo anayopewa kliniki na hajawahi kukutana na changamoto ya kupata mtoto mwenye uzito mkubwa au mdogo kupita kiasi.

“Ninachofahamu msisitizo mkubwa kwa mama mjamzito ni kula lishe bora ili kutoa virutubisho muhimu kwa mtoto anayekua tumboni. Hii ni pamoja na kula matunda, mboga, nafaka nzima, nyama, samaki, maziwa na bidhaa za maziwa.

“Kingine ni mazoezi mepesi ambayo ni msaada kwa mama hata kuufanya mwili wake usichoke na kumuondolea uwezekano wa kujifungua kwa upasuaji. Binafsi sijawahi kukutana na changamoto kubwa zaidi ya zile za kawaida za miezi mitatu ya mwanzo,” alisema Mariana

Wakati Mariana akieleza hayo, mmoja wa wazazi ambaye amewahi kupata mtoto mwenye uzito mkubwa aliliambia gazeti hili kwa miaka 11 mtoto wake ameendelea kuongezeka uzito, hali inayomfanya kuwa mvivu.

“Mtoto wangu alizaliwa na kilo 5.8 na alizaliwa kwa upasuaji, hadi sasa hatujagundua ugonjwa wowote ila naweza kusema mwili wake unamfanya kuwa mvivu. Sio mtu wa kujichanganya na licha ya kufanya mazoezi kidogo lakini uzito wake unaendelea kuongezeka,” alisema mzazi huyo ambaye hakutaka jina lake liwekwe wazi.

Gazeti hili lilizungumza na mkunga mstaafu, Salome Milinga aliyesema yapo mambo yanayochangia mjamzito kujifungua mtoto mwenye uzito kupita kiasi, ikiwemo mama kuwa na asili ya uzito mkubwa kabla ya ujauzito, kuongezeka uzito kupita kiasi wakati wa ujauzito na mama kuzaliwa na uzito mkubwa.

“Uzito wa mama unachangia kwenye uzito wa mtoto atakayezaliwa, ndiyo maana wakati wote kliniki huwa tunawasisitiza wazingatie mlo kamili, wasiache kula kwa sababu ni kipindi ambacho mwili unahitaji chakula lakini lazima iwe ni kiasi, si kutwa vyakula vya wanga na mafuta.

Sababu nyingine, anasema hutokea kwa akina mama wenye kisukari kwa sababu kwenye damu ya mama, hapa upo uwezekano wa mtoto kuzaliwa na uzito mkubwa kwa sababu anapata glucose nyingi mno kutoka kwenye damu,” alisema mkunga huyo.

MWANANCHI
professor janabi anatrend sana siku izi,,tangu mzee wa chato adanji basi dar!!!!!!!!!!!!!!
 
Back
Top Bottom