LAGOSA
Member
- Jan 8, 2014
- 69
- 54
Ndugu wanajamvi habari zenu,
Mwana JamiiForums mwenzetu amevamiwa na watu wasioulikana nyumbani kwake usiku wa kuamkia leo. Watu hao walifanikiwa kuvunja mlango wa nyumba yake na kumkuta akiwa na simu mikononi. Kwa maelezo yake, alikuwa katika Jukwaa la Siasa akijaribu kusoma baadhi ya taarifa ndani ya JF.
Ghafla alishitushwa na sauti ya kubomolewa kwa mlango kisha tochi ikimulika macho yake na kuambiwa atulie papohapo. Akapigwa Mapanga kichwani, mdomoni, mikononi, na tumboni; walisikika wakisema aoneshe mahali pesa zipo. Waliweza kuchukua Pikipiki, TV 2, Deki 1, Baiskeli 1 na Pesa taslimu 270,000/=.
Humu anatumia ID ya MOTOCHINI.
Tumuombee mwenzetu akiwa kalazwa mpaka sasa!
===================
Mwana JamiiForums mwenzetu amevamiwa na watu wasioulikana nyumbani kwake usiku wa kuamkia leo. Watu hao walifanikiwa kuvunja mlango wa nyumba yake na kumkuta akiwa na simu mikononi. Kwa maelezo yake, alikuwa katika Jukwaa la Siasa akijaribu kusoma baadhi ya taarifa ndani ya JF.
Ghafla alishitushwa na sauti ya kubomolewa kwa mlango kisha tochi ikimulika macho yake na kuambiwa atulie papohapo. Akapigwa Mapanga kichwani, mdomoni, mikononi, na tumboni; walisikika wakisema aoneshe mahali pesa zipo. Waliweza kuchukua Pikipiki, TV 2, Deki 1, Baiskeli 1 na Pesa taslimu 270,000/=.
Humu anatumia ID ya MOTOCHINI.
Tumuombee mwenzetu akiwa kalazwa mpaka sasa!
===================
Taarifa hii ni sahihi, ilikuwa mida ya saa 7:45 usiku ikiwa ni siku 2 toka nitoke jijini Mwanza kumpumzisha Bibiangu alietangulia mbele za haki, nami nimepatwa na mkasa huu. Japo si vyema kufurahia kifo cha mwanadam mwenzie, ila nilifanikiwa kumpiga mmoja kichwani na kipande cha chuma na nikaweza kutoroka na kukimbia huku nikivuja damu nyingi sehem za kichwa.
Taarifa nilizoletewa asubuhi niikuwa yule niliempiga kichwani amekutwa amekufa nyuma ya nyumba yangu, nasikitika kusikia kufa mwanadamu lakini ni katika kujihami.
Picha na maelezo zaidi nitajitahid hapo kesho niziweke hapa pindi nimalizapo mahojiano na police, kwani naogopa kupost picha za mharifu akiwa ni marehemu wakati police wakiendelea na taratibu zao. NIMEPUNGUKIWA DAMU, NAONGEZEWA DAMU.
NAOMBENI KUDRA ZENU. jMali LAGOSA kadoda11 MK254 uaminifukazi