Binafsi naona limefilisika kimawazo na kiuchambuzi.
Mimi ni msomaji sana wa Mwanahalisi ila toleo la jana kuna makala ya Kubenea ihusuyo UDINI KUINGIA BUNGENI, likijenga hoja kuwa mawaziri waislamu wanaonewa ama kukamiwa kwa sababu ni waislamu likitolea mfano wa mgongano wa Ghasia na Jenista, Dialo na Kawambwa na likahoji Mbona hao wabunge hawakuwa wakali baada ya serikali kupitia Chikawe kutoa tamko la mahakama ya kadhi? Kubenea akamailizia kwa uchambuzi wa kama mtoto wa chekechea eti ni kwa sababu chikawe ni Mkristo.
Kila mwenye akili timamu aliyesoma hiyo makala hawezi akasadiki kama imeandikwa na Kubenea na kuchapishwa na Mwanahalisi. UKWELI NADHANI MWANAHALISI IMEANZA KUFILISIKA KIUCHAMBUZI.
Nilijiuliza hivi kweli hata Ndimara Tegambwage hakuweza kumshauri, maana namwamini yule mzee ni kichwa.
Hivi kweli Kubenea alitaka wabunge wawe wakali kuhusu kadhi wakati akijua ni suala linalosigana na KATIBA YA JAMHURI? Hivi kweli Kubenea alitaka hao wabunge wawe wakali ili hali Tanzania ni nchi isiyo na dini? Iweje Mabudha nao wakitaka mahakama yao, na Wakristo watake mahakama yao katika mfumo wa KISERIKALI?
Kuanzia jana nimeingiwa na mashaka sana na uwezo wa kufikiri, na kuchambua wa Kubenea.
Mimi ni msomaji sana wa Mwanahalisi ila toleo la jana kuna makala ya Kubenea ihusuyo UDINI KUINGIA BUNGENI, likijenga hoja kuwa mawaziri waislamu wanaonewa ama kukamiwa kwa sababu ni waislamu likitolea mfano wa mgongano wa Ghasia na Jenista, Dialo na Kawambwa na likahoji Mbona hao wabunge hawakuwa wakali baada ya serikali kupitia Chikawe kutoa tamko la mahakama ya kadhi? Kubenea akamailizia kwa uchambuzi wa kama mtoto wa chekechea eti ni kwa sababu chikawe ni Mkristo.
Kila mwenye akili timamu aliyesoma hiyo makala hawezi akasadiki kama imeandikwa na Kubenea na kuchapishwa na Mwanahalisi. UKWELI NADHANI MWANAHALISI IMEANZA KUFILISIKA KIUCHAMBUZI.
Nilijiuliza hivi kweli hata Ndimara Tegambwage hakuweza kumshauri, maana namwamini yule mzee ni kichwa.
Hivi kweli Kubenea alitaka wabunge wawe wakali kuhusu kadhi wakati akijua ni suala linalosigana na KATIBA YA JAMHURI? Hivi kweli Kubenea alitaka hao wabunge wawe wakali ili hali Tanzania ni nchi isiyo na dini? Iweje Mabudha nao wakitaka mahakama yao, na Wakristo watake mahakama yao katika mfumo wa KISERIKALI?
Kuanzia jana nimeingiwa na mashaka sana na uwezo wa kufikiri, na kuchambua wa Kubenea.