MwanaHalisi limedoda, limekwisha sasa

Originally posted by mnozya
Kila mwenye akili timamu aliyesoma hiyo makala hawezi akasadiki kama imeandikwa na Kubenea na kuchapishwa na Mwanahalisi. UKWELI NADHANI MWANAHALISI IMEANZA KUFILISIKA KIUCHAMBUZI. Nilijiuliza hivi kweli hata Ndimara Tegambwage hakuweza kumshauri, maana namwamini yule mzee ni kichwa.

Mtu anaweza kuwa na chuki/ugomvi/wivu/hasira binafsi na Kubenea as a person, lakini lazima wote tukubali kuwa gazeti la Mwanahalisi limekuwa ndiyo chombo pekee cha habari hapa Tanzania chenye kuthubutu kuwataja mafisadi wakubwa nchi hii wa Richmond, EPA na wengine bila kuogopa.

Wahariri wa magazeti mengi Tanzania wameshakuwa compromised na mafisadi (wanakunywa nao chai) au wamefungwa minyororo na wamiliki wa vyombo vya habari ambao wamekuwa wanaingilia sana uhuru wa vyombo hivyo. Pamoja na mapungufu yake makubwa as a person, Kubenea bado amekuwa anatoa mchango mkubwa kwenye mapambano dhidi ya ufisadi kupitia kwenye gazeti lake.

Tumpe mtu sifa yake hata kama hatumpendi kwa sababu binafsi au kwa mapungufu yake. MWANAHALISI so far limekuwa kiboko cha mafisadi na ndiyo limeweza kumgonga JK bila uoga.

Long live MWANAHALISI, pamoja na mapungufu yake
 
Mimi ni msomaji mzuri wa gazeti la mwanahalisi. naweza kusema ktk nakala walizotoa hazizidi nakala 10 kuzikosa. lkn siku hizi kila siku zikienda naona limeanza kupteza mwelekeo. kama nitatembelea kwenye meza ya magazeti hapa dar huliona likipgwa na jua siku 3 baada ya kutoka, limechakaa, watu huliangalia tu halitoki na inaonekana wasomaji wengi limewachosha na hata mauzo yake inawezekana yameshuka ajabu. kwani habari zinazotoka kwa sasa hazina mvuto . naona hata lile gazeti la rai linaoenekana kupanda chati na mwanahalisi kushuka kama vile kimbao mbao anvyoruka na kutaka kuligonga jiwe
naangalia kutafuta gazeti jengine mbadala ili kusoma


Habari ni biashara na gazeti ndio product yenyewe. Product zote kama ilivyo maisha ya binadamu, huzaliwa, hukua, huzeeka na kisha hufa (PRODUCT LIFE CYCLE). Inatofautiana kipindi tu kulingana na management ya hiyo kampuni, aina ya bidhaa na mahali unapofanyia hiyo bizinesi yako. Kwa hiyo kuchuja kwa gazeti ni kitu cha kawaida.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom