Mwali: Mmiliki wa DOWANS ni huyu!

Status
Not open for further replies.

Halisi

JF-Expert Member
Jan 16, 2007
2,802
613
Jamani, hiki ni kitendawili, DOWANS ni nani hasa?!!!!!! Kazi kwenu.

dowans1.jpg


dowans_adawy.jpg

Kuanzia leo tutaanza kufunua na kuunganisha vipande vipande vya Dowans. Jumamosi iliyopita (tarehe 7 Machi, 2009) tulipata nafasi ya kuzungumza kwa kirefu na Brig. Gen. Al-Adawi mtu ambaye jina lake, na anuani vinaonekana kwenye nyaraka za BRELA kuwa ndiye mmiliki wa kampuni iliyoko kwenye songombingo ya tuhuma za ufisadi ya Dowans. Jumamosi hii iliyopita pia tulipata nafasi ya kuzungumza tena na Brigedia huyo baada ya kugundua kuwa ametuongopea. Kati ya mahojiano ya Jumamosi ile na Jumamosi hii kulifanyika kikao huko Dubai Jumapili ya tarehe 8 Machi, baada ya mahojiano yetu na maamuzi mbalimbali yakachukuliwa.

Leo katika kuifunua Dowans tunaanza na wamiliki tu halafu habari zaidi ya nini kimejiri inakuja wiki hii katika kile tunachokiita "kumfunua Mwali". Kwa vile Waziri Ngeleja amesema anataka mjadala huu wa Dowans ufungwe, tumedhamiria kuhakikisha kuwa tunaufunga kwa namna yetu wenyewe.

Sehemu zote mbili za mahojiano na Gen. Al-Adawi zitarushwa katikati ya wiki hii kupitia mwanakijiji.com na bongoradio.com... USIKOSE KUONGEZEWA MASWALI KWENYE MAJIBU UNAYOFIKIRI UTAYAPATA

NB:*
  • Tutaonesha pia jinsi gani Rostam Aziz aliwadanganya watanzania kuwa hakuhusika na suala la ujio wa Dowans na kudai kuwa yeye ni "mkandarasi tu" aliyeomba kazi na "kuambiwa kuacha anuani" yake...

Na mambo mengine ambayo yatakufungua macho kuthibitisha kile unachoweza kuwa umefikiria.. Dowans
 
Last edited by a moderator:
Hiyo kampuni ya Ringo & Associates ni kampuni ya Dr. Ringo Tenga?
 
The scanned document doesn't say much....could we get more pages if there are any?
 
Yes, Nyani Ngabu, more pages pse, anaweza akawemo Zitto as shareholder, who knows?
 
The scanned document doesn't say much....could we get more pages if there are any?

Nyani, utamu wa pilau unaanza kwa harufu!!

from The Citizen Feb 8, 2008 "December 17, 2006: Richmond Development Company approaches South African based company, Dowans Holdings, to cut a deal in a desperate effort by Richmond to hang on to the lucrative $172.5million emergency power supply contract."

Pay attention to the dates...
 
Kwa hiyo hiyo Ringo and advocates ina represent serikali ya tanzania au...me i am condused na huyo dowsan sijui Kgoda,.

Hapana si Kagoda bali ni ndugu yake Kagoda aitwaye Afritainer, inayomilikiwa na familia ya Rostam Aziz, kama ilivyoandikwa hapa na Raia Mwema.... Ndio mujue, Kagoda, Dowans zote ni moto


Siri mpya ya EPA yaiumbua Kagoda

Nyaraka zilizotumiwa na Afritainer kuchota mabilioni ya fedha za EPA mwaka 2000 zinaonyesha kwamba kampuni hiyo imetumia namba za simu 2861371 na 2861372 ambazo pia ndizo zimetumiwa na Kagoda katika kuchota fedha za EPA mwaka 2005. Namba hizo zinaonekana katika nyaraka za kampuni nyingine yenye uhusiano na wamiliki wa Afritainer.

Nyaraka kutoka Wakala wa Usajili wa Makampuni na Leseni (BRELA) zinaonyesha kwamba Tabu Omari Masula na Barati A. Goda, walidaiwa kuingizwa kuwa wakurugenzi wa kampuni hiyo Mei 15, 2000 kinyume cha sheria.

Barua ya BRELA ya Februarin 18, 2002, miaka miwili baada ya Tabu na Barati kuchota fedha za EPA, ilieleza kwamba wakurugenzi hao hawakuwa halali kutokana na kutokuwa na hisa katika kampuni ya Afritainer.

Kwa mujibu wa barua hiyo kwenda kwa kampuni ya mawakili ya M.A.Imail, Tabu na Barati walikiuka kifungu cha 50 cha hati ya usajili ya kampuni hiyo kinachomlazimu mkurugenzi kuwa na hisa katika kampuni kwanza ili aweze kuwa na maamuzi.

Waraka wa Afritainer uliowasilishwa BRELA Mei 15, 2000, ulieleza kwamba wakurugenzi pekee na waazilishi wa Afritainer ni Bahram Abdurasul Chakaar na Gulam Abdurasul Chakaar, wamejiuzulu ukurugenzi na kuwaachia Tabu na Barat.

Hata hivyo, BRELA katika barua ya Februari 18, 2002 iliyoandikwa na Msajili Msaidizi wa wakala huo, L. Kimaro, ilieleza wazi kwamba hadi wakati huo ubadilishaji wa wakurugenzi haukuwa umeidhinishwa kutokana na kutokufuata masharti ya usajili.

Tabu anatajwa kufanya kazi katika kampuni moja ya jijini Dar es Salaam yenye ofisi zake eneo la viwanda barabara ya Nyerere na Upanga.

Kwa mujibu wa habari ambazo Raia Mwema imezipata fedha hizo kiasi cha Sh. Bilioni 13 zilichukuliwa Agosti 2000 kabla ya uchaguzi wa pili wa vyama vingi ambao Benjamin Mkapa aligombea tena urais.

Waidhinishaji wakuu wa mikataba ya uchukuaji wa fedha hizo walikuwa ni mawakili maarufu wa kampuni ya uwakili ya Law Associates chini ya mkuu wake Dk. Ringo Tenga. Dk. Tenga sasa ni mwanasheria wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT).
 
Last edited:
Nilikuwa nadhani Dowans ni Richmond iliyopitia mlango wa uani. Unajua jina Richmonduli,lilikuwa wazi sana. Hakuna jipya hapa ili kuwa ni Zuma style of bouncing back.
 
Huyu Advocate Ringo Tenga, mbona anaachwa tu wala hapewi msukosuko kuulizwa who is behind Dowans?

Lakin hii ndiyo imekuwa style ya tassisi zetu za kipelelezi ambazo nazo zinaendeshwa na mafisadi -- kwa maana ya wanazoziongoza. Kwa mfano Hosea alishindwa kabisa kum-confront Kimei na kumuuliza yale mabilioni ya Kagoda yaliyolipwa cash over the counter kutoka matawi ya benki yake yalilipwa kwa nani?
 
Halisi
Jamani, hiki ni kitendawili, DOWANS ni nani hasa?!!!!!! Kazi kwenu. Nipeni mji

nakupa mji Mkuu, Morogoro (mji kasoro bahari). Leta pilau kaka...
 
Watu hawa wanafahamika ila tunaowategemea wawaseme wanashirikiana nao.Serikali isingekuwa pamoja nao wangeshawataja,kwa hiyo huu ni mchezo ambao Serikali yetu inashiriki kuucheza,uvumbuzi pekee ni 2010 kuwaondoa wasanii katika uongozi wa nchi yetu.
 
Ningekuwa mimi Rostam... ningetangaza kujiuzulu Ubunge na kuamia Dubai ndani ya siku saba maana... wiki ijayo inshallah... mwali atatolewa ndani!!
 
Ningekuwa mimi Rostam... ningetangaza kujiuzulu Ubunge na kuamia Dubai ndani ya siku saba maana... wiki ijayo inshallah... mwali atatolewa ndani!!


Ngoja niongeze stock ya popcorns picha ndo linafikia patamu

thanks mkuu MMM
 
Ningekuwa mimi Rostam... ningetangaza kujiuzulu Ubunge na kuamia Dubai ndani ya siku saba maana... wiki ijayo inshallah... mwali atatolewa ndani!!

M.M.M, hapo ndipo pale mahali watu wanakubaliana nawe..... lete maneno twangojea kama mpira wa kona!!!
 
Ningekuwa mimi Rostam... ningetangaza kujiuzulu Ubunge na kuamia Dubai ndani ya siku saba maana... wiki ijayo inshallah... mwali atatolewa ndani!!

Mwanakijiji,
Wewe hushangai kwa mara ya kwanza TZ gabacholi anakuwa na kasheshe kibao lakini hakimbii nchi?

Rostam ana kinga ya Kikwete na as long as Kikwete ni mfalme, basi hakuna atakayeweza kumgusa Rostam, hata akiliuza jengo la bunge.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom