Mwakyembe: Sikusinzia...

TRL walijua kuwa mkuu anasafiri?
Maana lazima wabehave na kurekebisha mambo kama wanajua the big boss yumo ndani ya mchuma.
Angekata ticket kwa kutumia jina la mtu mwingine, halafu akasema anaangalia tu treni then anazama mchumani bila maafisa kujua.

Hilo ndilo swali nililokuwa najiuliza. Kama alitangaza na akaja na VX yake kwenye treni basi matatizo yote yaliishia pale. Watendaji ndo chanzo na service ya train pia ni tatizo so si ajabu maofisa walibehave vizuri tu.
 
Kama mtanzania mzalendo, kama waziri mwenye dhamana wa hii sekta,mimi namuunga na nitaendelea kumuunga mkono kama hizi safari za kutumia public transport zitafanyika mara kwa mara bila kufanya hivyo na vyombo vya habari ile akakutane na uhalisia then aje kutuambia amekutana na nini.Isije ikawa ameambukizwa na Dr Magufuli kwa kufanya kazi na media wakati wakiwa wizara moja to get cheap attention while matatizo ya watanzania yako pale pale.Hatutaki siasa kwenye mambo muhimu yanayotugusa sisi wote.
 
ni sawa kupita na kuona lakini hili ni jambo moja upande mwingine kufanyia kazi yale yaliyo onekana maana nataka kusema kuwa talking is cheap
 
Hapa ndipo nashindwa kuwaelewa watu. Hivi hata mtu akifanya jambo jema kwa kuwa itikadi yako ni tofauti na ya kwake linabadilika na kuwa baya???? Hapa Mwakyembe kakosea nini? Hivi yeye kufuatilia utendaji wa Shirika hili ambalo limekuwa kama ndoo mbovu ambayo kila jitihada za kujaza maji zimeshindikana kutokana na kuvuja nalo limekuwa kosa!!!!!!!!!! You are not serious. Kutokana na kupitia physically masuala yaliyo chini ya Wizara yake anajiweka katika nafasi nzuri ya kutoa maamuzi au ushauri sahihi tofauti na kukaa kwenye kiyoyozi na kungojea kila siku apokee taarifa za walio chini yake ambazo sometimes zinakuwa sugar quoted. Kwa kusafiri na wananchi ni sehemu mojawapo ya kupata mawazo raw from horses mouth. Maana mawazo aliyoyapata hayajachakachuliwa kwa maslahi ya yeyote maana ameyapata live kutoka kwa wadau wa usafiri huo. Hivyo nina hakika amejifunza jambo jipya.
Hongera bro. Mwakyembe keep it up lakini uyafanyie kazi na uyaweke bayana uliyoyaona na jinsi unavyokusudia kuyafanyia kazi.

Achana na Mwakyembe, wewe binafsi hauelewi matatizo wanayokabiriana nayo wasifiri wanaotumia treni? haya, ufahamu wa matatizo hayo unaweza kukusaidi vipi kulikwamua shirika la reli kutoka kwenye mning'inio lililokuwa nao.

Kwa mfano, kuna tatizo la wafanyakazi kutokulipwa mishahara yao, unatatuaje tatizo hili kwa kusafiri kwa treni? miundombinu ya reli imezeeka na haiwezi kuimili safari za mara kwa mara na shehena nzito, unatatuaje na hili kwa kusafiri? kuna tatizo la wafanyakazi kurusha ticketi, unalitatuaje hili kwa kusafiri na treni?
 
Waziri wa Uchukuzi Dr.Harrison Mwakyembe amesema kuwa hakupata kusinzia njia nzima, wakati akisafiri kutoka Dar es Salaam hadi Dodoma kwa treni, kwakuwa anafanya utafiti wake.

Waziri Mwakyembe amesema kuwa hakuweza kusinzia kwakuwa alihitaji kujiridhisha na hali ya usafiri wa treni na pia kujionea hali halisi ya wananchi wa Tanzania sehemu ambapo treni linapita.

'Nimejifunza mengi sana;ya Wizara yangu na Wizara nyinginezo' alisema Dr.Mwakyembe. 'Nitatumia niliyoyaona kwa maslahi ya Taifa' aliongeza.

Chanzo: Mimi mwenyewe niliyeambatana naye kwenda Dodoma kwa treni...
Kimsingi ni uongozi dhaifu kutaka kuhusika na kila linalo tokea kwenye wizara;kwa mfano eti magufuli asafiri kwa basi ili kujua udhaifu wa barabara!Uongozi mzuri ni pale mkuu anapojenga uwezo kusimamia watendaji walio chini yake ili mambo yaende!!!!
Hatuhitaji waziri wa mambo ya ndani kwa mfano,kukamata wezi na kuwapeleka polisi ili tuseme ni kiongozi bora!
Kwa hili simuungi mkono mwakyembe hata kidogo.
 
Inakuingia Akilini mwako kwamba Mtu ambaye amekuwa kiongozi katika serikali na mashirika yetu ya UMA kwa muda mrefu Kama mwakyembe analazimika kufanya safari ya namna hii ili kujifunza au kujionea mwenyewe ama matatizo ya usafiri wa treni au ya wananchi huko treni inakopita kama anavyoropoka huyu jamaa.

Maisha ya hao wananchi hao yanatofauti gani na yale ya wananchi wa Jimboni kwake Kyela? Majuzi alisema amepanda daladala kutoka mwenge kwenda tegeta na anadai kwamba tatizo pekee aliloliona na gharama kubwa ya nauli, matatizo ya wanaotumia usafiri wa daladala yanatofauti gani na wale wanaotumia treni?

Ni tatizo gani la usafiri wa treni mwakyembe amejifunza kupitia safari hiyo? alienda kuona kama kweli injini inazima zima? haya sasa siku hiyo haikuzima, kwa hiyo ametoka na picha gani hapo? kwamba habari za kuzima zima kwa injini za treni na hujuma za kishenzi zinazofanywa za kung'oa mataruma ya reli ni za uongo?

Give me a break.

mkuu nikumbushe shirika lipi la umma Mwakyembe alifanya.
 
Acha upofu wa fikra wewe. Mtu yeyote ambaye analazimika kufanya ziara ama experiements kama unavyosema wewe ili kubaini matatizo yanayowakabili wananchi wake hafai kupewa nafasi yoyote ile ya kisiasa. na kwa msingi huu Mwakyembe anakalia hiyo ofisi kinyume na matarajio ya kisiasa.

Huyo mtu na experiment yake mimi siwafahamu, labda unipe taarifa zake zaidi, hivyo mpaka sasa mfano wake hauna uhusiano wowote ni utoto aliofanya mwakyembe.

Utoto kutumia gogo kwenda Dom au ni upi mkuu? Mbona ni usafiri ambao wanapaswa kuutumia wote hao?
 
Kimsingi ni uongozi dhaifu kutaka kuhusika na kila linalo tokea kwenye wizara;kwa mfano eti magufuli asafiri kwa basi ili kujua udhaifu wa barabara!Uongozi mzuri ni pale mkuu anapojenga uwezo kusimamia watendaji walio chini yake ili mambo yaende!!!!
Hatuhitaji waziri wa mambo ya ndani kwa mfano,kukamata wezi na kuwapeleka polisi ili tuseme ni kiongozi bora!
Kwa hili simuungi mkono mwakyembe hata kidogo.

wengi wameshasahau usanii aliowafanyia kwenye ile riport ya richmond hata hivi majuzi....
 
Utoto kutumia gogo kwenda Dom au ni upi mkuu? Mbona ni usafiri ambao wanapaswa kuutumia wote hao?

mwakyembe hana tofauti na wale jamaa wanaolalamika kuwa vijana wengi hawana ajira na hili ni bomu litalipuka wakati huo huo watu hao majumbani mwao wamepaki magari zaid ya 6 kwa matumizi yao binafsi...kumbe wangeweza kuwa na viwanda vidogo vidogo wanavyomiliki wao wangeweza kutoa ajira kwa wantanzia wengi vijana huku akimiliki gari moja au mbili.. .....

na pia huyu mwakyembe hana tofauti na yule kiongozi aliyekuwa anasimama majukwaani na kuwapiga wenzake vita kuwa ni mafisadi na wezi wakubwa...wakati huo huo nyumbani kwake ameunganisha maji kwa njia ya wizi na halipi bili kwa zaidi ya miaka 5....viongozi wasanii hawafai....
 
umefanya vizuri waziri, tunasubiri maboresho. tukiona kimya tutajua ile ilikuwa ni trip tu, ulipenda kubadilisha njia ya usafiri. kazi njema baba
 
Waziri wa Uchukuzi Dr.Harrison Mwakyembe amesema kuwa hakupata kusinzia njia nzima, wakati akisafiri kutoka Dar es Salaam hadi Dodoma kwa treni, kwakuwa anafanya utafiti wake.

Waziri Mwakyembe amesema kuwa hakuweza kusinzia kwakuwa alihitaji kujiridhisha na hali ya usafiri wa treni na pia kujionea hali halisi ya wananchi wa Tanzania sehemu ambapo treni linapita.

'Nimejifunza mengi sana;ya Wizara yangu na Wizara nyinginezo' alisema Dr.Mwakyembe. 'Nitatumia niliyoyaona kwa maslahi ya Taifa' aliongeza.

Chanzo: Mimi mwenyewe niliyeambatana naye kwenda Dodoma kwa treni...

haya, ila wenye maroli ukae nao vizuri sijui watakufanya nini ukiboresha reli. Kama vipi waite wawe sehemu ya umiliki wa reli unaweza ishia ongea mh waziri.
 
Ingekuwa kulazimishwa kila waziri lazima a-experience hali halisi ya wananchi wa kawaida kwenye goods/services ambazo wizara zao zinatoa, kuna wizara zisingekuwa na mawaziri
 
Back
Top Bottom