Ms Judith
JF-Expert Member
- Dec 24, 2010
- 2,563
- 918
wapendwa,
nnatumaini mnakumbuka vizuri thread yangu hii hapo chini:
https://www.jamiiforums.com/mahusia...0-nzito-za-maisha-yangu-ooh-glory-to-god.html
kwa sasa niko safarini kurudi dar. safari hii ni ya pekee kwangu kwa sababu huko dar pamoja na mambo mengine, nitayahitimisha rasmi maisha yangu ya sasa na kuanza maisha mapya kabisa ya ndoa.
sasa huu ndio wakati ambao mchakato wotw ule unafikia hitimisho kwa ndoa itakayofungwa katikati ya mwezi huu. awali nilitegemea ingefungwa mapema zaidi ila kuna mambo yaliingilia hapo kati na tukalazimika kuisogeza mbele.
nawashukuru wote mnaendelea kuniombea na kwa kweli bado nahitaji maombi yenu ili tukio hili likamilike salama na pia tuendelee kuombeana kwa maisha salama na matulivu ndani ya ndoa.
nawashukuru sana kwa yote na kuwatakia kila la heri katika mwaka huu 2012, tuzidi kuombeana bila kuchoka.
Mungu awabariki sana wapendwa
Glory to God!
nnatumaini mnakumbuka vizuri thread yangu hii hapo chini:
https://www.jamiiforums.com/mahusia...0-nzito-za-maisha-yangu-ooh-glory-to-god.html
kwa sasa niko safarini kurudi dar. safari hii ni ya pekee kwangu kwa sababu huko dar pamoja na mambo mengine, nitayahitimisha rasmi maisha yangu ya sasa na kuanza maisha mapya kabisa ya ndoa.
sasa huu ndio wakati ambao mchakato wotw ule unafikia hitimisho kwa ndoa itakayofungwa katikati ya mwezi huu. awali nilitegemea ingefungwa mapema zaidi ila kuna mambo yaliingilia hapo kati na tukalazimika kuisogeza mbele.
nawashukuru wote mnaendelea kuniombea na kwa kweli bado nahitaji maombi yenu ili tukio hili likamilike salama na pia tuendelee kuombeana kwa maisha salama na matulivu ndani ya ndoa.
nawashukuru sana kwa yote na kuwatakia kila la heri katika mwaka huu 2012, tuzidi kuombeana bila kuchoka.
Mungu awabariki sana wapendwa
Glory to God!