Elli
Platinum Member
- Mar 17, 2008
- 55,499
- 86,037
Wapendwa, mwaka 2011 umekuwa na changamoto zake nyingi tu; Je umejenga utamadauni wa kujitathmini? Je yale uliyoyataka yametimia kwa kiasi gani? Je mipango yako na ndoto zako ulijitahidi kuifikia kwa kiasi gani?
Kwangu mimi na wewe ni kipindi muhimu sana cha kumshukuru MUNGU au yeyote yule unayeona alikuwa muhimu kwa mafanikio yako ( Mimi na Nyumba yangu tutamshukuru MUNGU).
Wapo wengi walitamani waione leo hii, wauone mwaka huu, wakapanga na mipango, wakaota na ndoto, leo hatunao, wengine wako vitandani, wengine wamefanikiwa, ni wakati wa kumuomba na kumshukuru MUNGU.
Samehe, sahau, jitathmini pale ambapo ulishindwa usipaite TATIZO but pachukulie kama changamoto ya kukuwezesha kuvuka na kuendelea mbele zaidi, pengine lile ulilolitaka halikua, pengine ndoto yako haikutimia, badala ya kukaa na kuanza kuangalia ya nyuma (ambayo hayasaidii kwa future) angalia what you have now, angalia ni namna gani utafanikiwa zaidi kwa mwaka 2012, panga mipango sasa, ota ndoto zako zote sasa kisha jenga na weka misingi ya kuzigeuza ndoto hizo kuwa kweli.
Tuwasemehe hata wale wanaoitakia mabaya nchi yetu, wanaotunyanyasa na kutuibia kwa wizi wa mchana kweupe, tuombe kwa ajili ya wanafunzi wote walionyimwa mikopo huku billions zikiteketea kwa one day event, tuombe kwa ajili ya watoto wetu na ndugu zetu wanaosoma chini ya miembe na mikorosho huku wakikaa chini na wengine waliojengewa mabanda yasiyo na walimu wala elimu ambapo wengi wao wameishia kuvuta babgi na binti zetu kugeuzwa bidhaa za majangili, ndio shule za kata tutanzojivunia. Tumombe hata kwa ajili ya akina Mama wajawazito wanaofariki njiani kwa kukosa huduma za afya na Ambulance huku magari ya kifahari yakinunuliwa kila siku, tuombe hata kwa ajili ya wazee wetu ambao wamedhulumiwa haki zao za kuishi na kulipwa ujira usiostahili, tuombe hata kwa ajili ya wale wanaowanywesha ndugu zetu sumu kwenye migodi huku wakilindwa kwa mitutu ya bunduki, MUNGU tuangazie wana wako ili mwaka 2012 haya yapungue.
Nawependa sana na nawatakia Mapumziko mema ya mwisho wa mwaka, tujihadhari kwa mambo ya dunia (anasa)ili tuyafikie malengo yetu.
Kwangu mimi na wewe ni kipindi muhimu sana cha kumshukuru MUNGU au yeyote yule unayeona alikuwa muhimu kwa mafanikio yako ( Mimi na Nyumba yangu tutamshukuru MUNGU).
Wapo wengi walitamani waione leo hii, wauone mwaka huu, wakapanga na mipango, wakaota na ndoto, leo hatunao, wengine wako vitandani, wengine wamefanikiwa, ni wakati wa kumuomba na kumshukuru MUNGU.
Samehe, sahau, jitathmini pale ambapo ulishindwa usipaite TATIZO but pachukulie kama changamoto ya kukuwezesha kuvuka na kuendelea mbele zaidi, pengine lile ulilolitaka halikua, pengine ndoto yako haikutimia, badala ya kukaa na kuanza kuangalia ya nyuma (ambayo hayasaidii kwa future) angalia what you have now, angalia ni namna gani utafanikiwa zaidi kwa mwaka 2012, panga mipango sasa, ota ndoto zako zote sasa kisha jenga na weka misingi ya kuzigeuza ndoto hizo kuwa kweli.
Tuwasemehe hata wale wanaoitakia mabaya nchi yetu, wanaotunyanyasa na kutuibia kwa wizi wa mchana kweupe, tuombe kwa ajili ya wanafunzi wote walionyimwa mikopo huku billions zikiteketea kwa one day event, tuombe kwa ajili ya watoto wetu na ndugu zetu wanaosoma chini ya miembe na mikorosho huku wakikaa chini na wengine waliojengewa mabanda yasiyo na walimu wala elimu ambapo wengi wao wameishia kuvuta babgi na binti zetu kugeuzwa bidhaa za majangili, ndio shule za kata tutanzojivunia. Tumombe hata kwa ajili ya akina Mama wajawazito wanaofariki njiani kwa kukosa huduma za afya na Ambulance huku magari ya kifahari yakinunuliwa kila siku, tuombe hata kwa ajili ya wazee wetu ambao wamedhulumiwa haki zao za kuishi na kulipwa ujira usiostahili, tuombe hata kwa ajili ya wale wanaowanywesha ndugu zetu sumu kwenye migodi huku wakilindwa kwa mitutu ya bunduki, MUNGU tuangazie wana wako ili mwaka 2012 haya yapungue.
Nawependa sana na nawatakia Mapumziko mema ya mwisho wa mwaka, tujihadhari kwa mambo ya dunia (anasa)ili tuyafikie malengo yetu.