Muungano wa Tanganyika na Zanzibar bila ya Tanganyika – halali?

GHIBUU

JF-Expert Member
Jan 13, 2011
4,432
3,006
Zanzibar imeungana na nani ? Na chini ya mfumo gani?

Na Laila Abdulla,

Katika makala iliopita, nilizusha swali : Zanzibar imeungana na nani ?.Jibu wazi ni kuwa , Zanzibar haikuungana na Tanzania,April,26,1964,kwavile, tuliona hadi tarehe ile, nchi kwa jina hilo haikuwapo katika ramani ya dunia. Tanganyika ilioungana na Zanzibar tarehe hiyo,ilifutwa na kutoweka kwa kanuni yaani -decree-alioitunga Mwalimu Nyerere mara tu baada ya kuapishwa kuwa Rais wa Jamhuri hiyo mpya. Hiyo,ilikuwa ndio kanuni yake ya kwanza kuipitisha kama Rais wa Muungano.

Mwalimu Nyerere, alifahamika kuwa tayari kuchelewesha uhuru wa Tanganyika ili nchi zote 4 za Afrika Mashariki:Kenya,Uganda,Tanganyika na Zanzibar, zijiunge na Shirikisho la Afrika Mashariki.

SWALI:
Laiti ndoto hiyo ingetimilia na haingetiwa munda na mzee Kenyatta wa Kenya, je, Mwalimu angeliifuta Tanganyika katika ramani ya dunia kama alivyoifuta siku ilipozaliwa Jamhuri ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar?

Inafahamika kuwa ,Marekani na washirika wake wa Kambi ya Magharibi hasa Uingereza na Ujerumani Magharibi-FRG- hazikupendezwa na upepo uliokuwa ukivuma kisiwani Zanzibar kama vile kuanzisha uhusiano wa kibalozi na China ya kikominist,Urusi,Ujerumani Mashariki na Cuba. Waziri wa nje wa Marekani, Dean Rusk,aliwati shindo Marsi Kenyatta,Obote na Nyerere, kuchukua hatua dhidi ya kile alichokiita "communist menance in Zanzibar" – ushawishi wa kikoministi visiwani Zanzibar alioiita "Cuba of East Africa"-Cuba ya Afrika Mashariki.

Mwalimu akiitikia mwito huo, alivaa njuga kuyazima mapinduzi ya Zanzibar .Katika ziara pekee Zanzibar, April,1964, Rais Kenyatta alifika Uwanja wa Ndege kwa mazungumzo na Sheikh Karume lakini, aliishia hapo tu na baadae kurdi Kenya.

Obote, Rais wa Uganda, alikuwa tayari kwa shirikisho.Mwalimu ndie alieshika bendera. Alikuwa hata tayari kwa muujibu wa taarifa, kumuachia mzee Kenyatta urais.Sielewi kwanini hata hivyo,mzee Kenyatta alikataa mpango wa shirikisho la Afrika Mashariki na kuhiyari Kenya ifuate mkondo wake pekee.Je, hakumuamini Mwalimu?

Shabaha ilikua dola kuu 3 za Afrika ya Mashariki-Kenya,Uganda na Tanganyika kuidhbiti Zanzibar na kuyazima mapinduzi yake pamoja na kuzuwia Zanzibar kuendelea kuwa Mecca ya Afrika Mashariki ya kueneza UISLAMU.. Marekani,Uingwereza na hata Ujerumani Magharibi iliokasirishwa kwa Zanibar kuitambua (GDR) au Ujerumani Mashariki,hazikutaka kuona Cuba ya Afrika Mashariki ambayo mwaka 1 baadae ilikua kumpokea Che Guevera katika maadhimisho ya mwaka wa kwanza wa mapinduzi hapo Januari, 1965 kabla hajaelekea Kongo (D.R.C) kupitia Tanzania-bara.

Mwalimu akawaambia Marekani ana Karata nyengine :Vipi kudhibiti mambo Zanzibar. Karata yenyewe, ni MUUNGANO kati ya Tanganyika na Zanzibar na Marekani ikatoa baraka zake. Tanganyika kubwa yenye wakaazi milioni 20 wakati ule kuidhibiti Zanzibar iliokua na wakaazi laki 5. Nkurumah, alimkosoa Mwalimu kwa kusaidia kuyazima mapinduzi ya Zanzibar.

Tarehe 18,April,1964 akamwita mzee Karume aende Dar-es-salaam kwa mazungumzo.Sielewi, Mwalimu alimtikisa mzee Karume kiasi gani siku hiyo,kwani, hakurudi Zanzibar kama ilivyopangwa siku ile na akalala Dar hadi siku ya pili yake April, 19,1964.

Tarehe 22 April, washirika 2 wakubwa wa mzee Karume wakiwa nje ya Zanzibar- Abdulrahman Babu ( waziri wa nje na biashara) akiwa Indonesia kwa ziara rasmi na Sheikh Aboud Jumbe ,waziri wa ndani akiwa kisiwani Pemba kwa maswali ya usalama,Mwalimu Nyerere alitua Zanzibar na hati ya "MUUNGANO". Jumbe anaeleza katika kitabu chake "The Partner-ship" ndege yake ikitua Zanzibar ile ya Mwalimu ikiruka kurudi Dar. Mzee Karume alinyimwa washauri wake wakubwa na wasomi-Babu na Jumbe.

Sisi Wazanzibari, kila JANUARI 12, tangu 1964, tunasherehekea "mapinduzi" na tunaiita serikali yetu hata hii ya leo ya "UMOJA WA TAIFA" inayotuunganisha sote, "serikali ya Mapinduzi" bila ya kufahamu kuwa,MUUNGANO ulipikwa kama jungu la kuyaua mapinduzi.Sababu ni kuwa, mkondo wa mapinduzi ya Zanzibar haukuipendeza Marekani na washirika wake wa Magharibi.Kumbuka wiki tu baada ya mapinduzi ya Zanzibar, hapo Januari 20, Jeshi la Tanganyika nalo liliasi na Mwalimu akaenda kujificha.Jeshi la Kenya na hata la Uganda yakafuata.Kidole kilinyoshewa Zanzibar.Mwalimu alirudishwa madarakani na majeshi ya Uingereza yaliozima uasi. Ni majeshi ya serikali ile ile iliomkatalia msaada Sultani huko Zanzibar.

Mzee Karume, hakuridhia MUUNGANO kwa hiyari kinyume na hekaya nyingi tunazosikia.Ni dhahiri kuwa, April 18,1964, alitikiswa mno kule Dar-essalaam. Mwalimu yasemekana ,alitishia kuondoa askari wake kiasi 300 aliowaleta Zanzibar kuimarisha mapinduzi bila ya hata kuwapo Makubaliano ya Kimataifa kufanya hivyo. Na Mwalimu angefunga mapatano hayo na serikali gani ,ile ya Sultani ? Mzee Karume, alitaka kulinda usalama wa serikli yake kutokana na vitisho vya manuwari za Marekani, zilizokuwa zikizunguka Bahari ya Hindi wakati ule.

Mzee Karume, hakuwa na haki ya kuiunganisha Zanzibar bila ya ridhaa ya Wazanzibari ambao hadi leo miaka 47 baadae,hawakuulizwa wanataka Muungano au hawataki na serikali ya Tanzania haithubutu kuwauliza. Zanzibar si shamba lake binafsi mzee Karume bali ni mali ya wazanzibari na wala si mali ya ASP au CCM Zanzibar. Lakini, kutokana na hali ya mambo , Karume alihisi bora nusu-shari kuliko shari kamili. Mmoja aliekuwa karibu nae sana mzee Karume,aliwahi kuninon'goneza usia aliowapa "wandani wake" wa Afro-shirazi party: Aliwausia wasiregeze kamba katika mawasili 3 kwa Tanzania- bara:

  1. Msiunganishe Jeshi
  2. Msiunganishe fedha (sio sarafu bali akiba ya Zanzibar na muulizeni Jamali aliemuita "chori wee alipomuendea kwa swali hilo".
  3. Msiunganishe chama-yaani ASP kuungana na TANU.
Hadi kuuwawa kwa Mzee Karume,April 7, 1972, Mwalimu hakuyapata mambo hayo kutoka kwa mzee Karume. Ni baada ya kifo chake, ndipo alipofanikiwa na kuudhibiti mpini. Kuna wale wanaosema kuwa, mzee Karume hakusoma au kuelimika.Hatahivyo, alikuwa mwerevu na alijua ni mihimili gani inayosimamia dola na hakuiachia :Jeshi -fedha na chama -ASP-kinachotunga siasa za dola.

Rais aliemfuatia- Sheikh Aboud Jumbe,aliregeza kamba na laiti hangeunganisha chama ASP na TANU,Mwalimu Nyerere , asingeweza kumuuzulu kule Dodoma, 1984.Jumbe, angelimzindua Mwalimu ambae wakati ule ndie kinara wa CCM -supreme. Jumbe, amesoma na kuelimika,lakini Karume alionesha busara.

Kuna taarifa kuwa mwaka kabla kuwawa kwa Karume,hakujakuwa na mawasiliano ya moja kwa moja baina yake na Mwalimu bali kupitia wajumbe kama Bohke Munanke. Sijui nini ingelikuwa hatima ya MUUNGANO huu bila ya Tanganyika ,laiti mzee Karume angelikuwa hadi leo yuhai?

MFUMO WA MUUNGANO NI UPI ?
Wakati mzee Karume alitumia busara kubakisha mihimili ile 3 ya dola mikononi mwa Zanzibar,Rais Aboud Jumbe, msomi,hakukawia kutambua makosa yake na haraka akataka kurekebisha makosa. Kupitia mawakili wake- Wolfgang Dourado na Swanzi, (Mghana) Jumbe, alimkumbusha Mwalimu kuwa ,MFUMO wa MUUNGANO wetu ni wa aina ya "Shirikisho".

Na tafsiri ya "Shirikisho" ni unakuwa na shina ( centre) na Tawi ( constituency) na madaraka ya kila upande, hufafananuliwa wazi ili kila mmoja, asimuingilie mwenziwe katika mambo yake.(Ya MUUNGANO NA YSIO MUUNGANO). Sasa ukiunda CHOMBO cha 3-yaani chama na kukifanya kina kauli ya mwisho "supreme", basi unakuwa umevunja Mapatano ya MUUNGANO au (Articles of the Union ). Mwalimu akatanabahi hawezi kushinda mbele ya wanasheria.

Dourado aliwahi kudai eti Mwalimu ni mwepesi wa kuwachezea akili wanasiasa ,lakini hudunda kwa wanasheria.Hoja yake ikawa nguvu za dola: kuwatia korokoroni wanasheria wa Jumbe : Dourado na Swanzi. Hatima ya Jumbe, ilijulikana Dodoma,1984 alipouzuliwa na kutoruhusiwa kurudi Zanzibar. Swali langu linabaki lile lile:

KIONGOZI GANI ATAIBUKA ZANZIBAR KUMVIKA PAKA KENGELE na kuwazindua wenzetu wa Tanzania-bara kwamba, Zanzibar haikubadilisha "SULTANI wa kiarabu" kwa "SULTANI wa Dodoma"?

Bila ya Tanganyika, hakuna Muungano,kwani haingii akilini mwa wazanzibari na hata watanganyika wenye kuwaza na kufikiri kuwa , siku ya kuzaliwa mtoto -Tanzania- April,26,1964 ,kwa kiini macho cha kuchanganya udongo, mzee mmoja kati ya 2-Tanganyika, anafariki dunia?

Zanzibar bila ya Tanganyika hapo imeungana na nani wenzetu?

SULUHISHO LIWAPI?
Suluhisho ni kuifufua Tanganyika na kuunda Muungano mpya wa serikali 3 na unaokubalika au kama ilivyopangwa awali na waasisi. Mfumo ni shirikisho, ndoto ya awali ya Mwalimu Nyerere alioachana nayo akishika njia ya "UNITARY STATE"-nchi moja. Lakini, Mwalimu aliwakemea wabunge 55 waliodai serikali ya Tanganyika na aliwaambia kwamba, kwa "CCM haiingii akilini kutoka serikali 2 kwenda 3." Wazanzibari wanamwambia na wao "haiingii akilini kutoka serikali 2 kwenda 1,kwani, kuridhia hivyo, ni kujitia kitanzi dola ya Zanzibar.

Kwa CCM-Zanzibar (zamani ASP) wakati wa kuchagua umewadia: ina jukumu kubwa kwa Zanzibar :ama kuachana na sera ya CCM-bara (ambayo waziri mzalendo Mansour Himidi, ameshasema ni butu) ya serikali 2 kwendea 1 au kushikamana na sera hiyo na Kuihini Zanzibar na vizazi vyake vijavyo . Historia hapo itawahukumu ni "MAHAINI" wa Zanzibar.Sidhani viongozi wa CCM- Zanzibar, wangependa kuingia katika historia na doa hilo. Kwani, NANI ANGEPENDA KUMKHINI MAMA YAKE MZAZI?

View attachment 34549
 
Ghibuu,
Hivi hizi topics unazitoaga wapi?
kuna wasomi maalum ambao wamesoma hisotry ya zanzibar,na africa mashariki kwa ujumla,na pia ni wana sheria,wanafahamu everything unachokijua wewe,ndio maana wanachambua mambo kama unavyoona hapo juu.
 
kuna wasomi maalum ambao wamesoma hisotry ya zanzibar,na africa mashariki kwa ujumla,na pia ni wana sheria,wanafahamu everything unachokijua wewe,ndio maana wanachambua mambo kama unavyoona hapo juu.
Sasa kuziweka hapa itatusaidia vipi? Visiwa vya Hawaii vilivamiwa na Wamarekani, wakaua mfalme wao na kuifanya Hawaii sehemu ya Marekani.
Leo sijawasikia Wahawaii wakilalamika kama Wazanzibari wanavyolalamika na kunukuu historia.
 
Sasa kuziweka hapa itatusaidia vipi? Visiwa vya Hawaii vilivamiwa na Wamarekani, wakaua mfalme wao na kuifanya Hawaii sehemu ya Marekani.
Leo sijawasikia Wahawaii wakilalamika kama Wazanzibari wanavyolalamika na kunukuu historia.
Umejuaje kama hawalalamiki ? Umeenda huko Hawaii ? Wewe uko dunia gani wewe ? Hebu fuwatilia kwa makini.

Hiyo habari hebu soma kwanza ndio uwongee na jazba yako,kwanini nyinyi watanganyika mukiambiwa ukweli munakasirika na kupayuka payuka ? Ukweli unawauma sana,mtu alisoma hasa na anaye jua sheria basi ukimuuliza huu muungano tulionao upo vipi kisheria ? Na jee huu mungano upo haupo ni mazingaombwe tu ? Kwanza soma ikisha lete hoja zako.

Hapo ndipo nitakuona wewe mtu makini sana na una uwelewa na ni binadamu kamili,kwani hawa viongozi wanatuendesha kama wanyama vile,mkubwa kunyanyasa mdogo,wakati huo umeshapitwa na wakati,angalia TUNISIA,EGYPT,Yemen,libya,kote huko wameaka na wanapigania haki zao,kwa hio sisi kupigania nchi yetu ambayo yenye history miaka 400 ilopita na ilitawala africa ya mashariki kuanzia somalia hadi malawi,yote ilikuwa ni zanzibar.

Soma history ya zanzibar kama hujui.
 
Umejuaje kama hawalalamiki ? Umeenda huko Hawaii ? Wewe uko dunia gani wewe ? Hebu fuwatilia kwa makini.

Hiyo habari hebu soma kwanza ndio uwongee na jazba yako,kwanini nyinyi watanganyika mukiambiwa ukweli munakasirika na kupayuka payuka ? Ukweli unawauma sana,mtu alisoma hasa na anaye jua sheria basi ukimuuliza huu muungano tulionao upo vipi kisheria ? Na jee huu mungano upo haupo ni mazingaombwe tu ? Kwanza soma ikisha lete hoja zako.

Hapo ndipo nitakuona wewe mtu makini sana na una uwelewa na ni binadamu kamili,kwani hawa viongozi wanatuendesha kama wanyama vile,mkubwa kunyanyasa mdogo,wakati huo umeshapitwa na wakati,angalia TUNISIA,EGYPT,Yemen,libya,kote huko wameaka na wanapigania haki zao,kwa hio sisi kupigania nchi yetu ambayo yenye history miaka 400 ilopita na ilitawala africa ya mashariki kuanzia somalia hadi malawi,yote ilikuwa ni zanzibar.

Soma history ya zanzibar kama hujui.
Ndiyo, nimeenda Hawaii mara kadhaa. Sijawasikia wale watu wakilalamika hata siku moja. Tena wale walikuwa na sababu za kulalamika kwa sababu
kabila lao karibu limemezwa na wazungu. Uwekezaji mkubwa katika mahoteli umefanywa na wazungu, lakini wametulia ndani ya USA. Sasa ninyi Wazanzibari sijui mnajiona sana kwamba kuungana na wamatumbi kunawashushia hadhi, sijui. Nina hakika kama Zanzibar ingemezwa na Oman musingelalamika kiasi hichi. Na kwa kukufahamisha tu, Zanzibar haikutawala Afrika mashariki miaka 400 iliyopita. Alikuwa ni mkoloni sultani wa Oman ambaye alianzisha ubwana na utwana katika visiwa vya Zanzibar. Historia hiyo tunaijua. Ilifutwa na mapinduzi ya 1964 ambapo kwa mara ya kwanza Zanzibar ilikuwa huru.
 
Sasa kuziweka hapa itatusaidia vipi? Visiwa vya Hawaii vilivamiwa na Wamarekani, wakaua mfalme wao na kuifanya Hawaii sehemu ya Marekani.Leo sijawasikia Wahawaii wakilalamika kama Wazanzibari wanavyolalamika na kunukuu historia.
Mkuu Jasusi heshima mbele. Usituletee habari na mifano ya Hawaii hapa. Haikhusu. Sawa na Paka na muwa. Fikiri kabla ya kukurupuka kuongea.
 
Ndiyo, nimeenda Hawaii mara kadhaa. Sijawasikia wale watu wakilalamika hata siku moja. Tena wale walikuwa na sababu za kulalamika kwa sababukabila lao karibu limemezwa na wazungu. Uwekezaji mkubwa katika mahoteli umefanywa na wazungu, lakini wametulia ndani ya USA. Sasa ninyi Wazanzibari sijui mnajiona sana kwamba kuungana na wamatumbi kunawashushia hadhi, sijui. Nina hakika kama Zanzibar ingemezwa na Oman musingelalamika kiasi hichi. Na kwa kukufahamisha tu, Zanzibar haikutawala Afrika mashariki miaka 400 iliyopita. Alikuwa ni mkoloni sultani wa Oman ambaye alianzisha ubwana na utwana katika visiwa vya Zanzibar. Historia hiyo tunaijua. Ilifutwa na mapinduzi ya 1964 ambapo kwa mara ya kwanza Zanzibar ilikuwa huru.
Kasome historia vizuri, bado hujaijua. Wewe wa wapi? Usituletee upuuzi wako. Historia haifutiki abadan.
 
Dawa ni serikali moja. Mkoa wa Zanzibar wenye wilaya 2 za Unguja na Pemba. Nakiri Zanzibar ni nchi kwa sababu ina eneo ila halina mipaka, ina rais 'Kilemba cha Ukoka' ambaye hana nguvu za dola, ina waziri wa fedha asiye na sarafu. Haina jeshi bali JKU na KMKM etc. etc
 
Mkuu Jasusi heshima mbele. Usituletee habari na mifano ya Hawaii hapa. Haikhusu. Sawa na Paka na muwa. Fikiri kabla ya kukurupuka kuongea.
Inahusu sana ndugu yangu kwa sababu huchelei kuniambia nisome historia. Hawaii walivamiwa na kuingizwa kwenye union kwa nguvu. Hata Scotland Ireland na Wales ziliunganishwa kwenye himaya ya Uingereza bila kufanya referrendum. Sasa leo mnataka Zanzibar iwe ya kwanza kufanya referrendum? Kwa hakika mimi ningekuwa katika nafasi aliyokuwa nayo Nyerere ningeviunganisha visiwa hivyo baada ya kumtimua mkoloni wa Kiarabu na mambo kwishney. Hizi kelele mngekuwa mnazipiga kwenye uvungu wa vitanda vyenu.
 
Inahusu sana ndugu yangu kwa sababu huchelei kuniambia nisome historia. Hawaii walivamiwa na kuingizwa kwenye union kwa nguvu. Hata Scotland Ireland na Wales ziliunganishwa kwenye himaya ya Uingereza bila kufanya referrendum. Sasa leo mnataka Zanzibar iwe ya kwanza kufanya referrendum? Kwa hakika mimi ningekuwa katika nafasi aliyokuwa nayo Nyerere ningeviunganisha visiwa hivyo baada ya kumtimua mkoloni wa Kiarabu na mambo kwishney. Hizi kelele mngekuwa mnazipiga kwenye uvungu wa vitanda vyenu.
Msisitizo: kasome history ya Zenj Empire, bado hujaielewa. Mambo ya Scotland mara England sijui Hawaii haihusiani kabisa na hii mada.
 
Msisitizo: kasome history ya Zenj Empire, bado hujaielewa. Mambo ya Scotland mara England sijui Hawaii haihusiani kabisa na hii mada.
Nawe kasome historia ya ukoloni Afrika. Zenj empire ilikuwa enzi ya ukoloni wa Waarabu. Ulifikia tamati 1964 kama vile ukoloni wa Mwingereza ulivyofikia tamati yake Tanganyika 1961. The difference is the same.
 
Nawe kasome historia ya ukoloni Afrika. Zenj empire ilikuwa enzi ya ukoloni wa Waarabu. Ulifikia tamati 1964 kama vile ukoloni wa Mwingereza ulivyofikia tamati yake Tanganyika 1961. The difference is the same.

jamanii wana historia.. hivi ni kweli kwamba sultani alipofika zanzibar alikuta kisiwa cheupee! hakina watu...??! ni story nilipewa na mzenji flani

sasa najiuliza kwanini akakiita kile kisiwa Negro cost! ? inamaana alikuta watu weusi pale
The word ZANZIBAR is of Persian or Arabic origin. The Persians derive the name from Zangh Bar, meaning "the Negro Coast."

Zanzibar People and Culture

hebu nisaidieni kwa hili mliosoma history! sanasana ninyi wazenji
 
Mpaka sasa hakuna mtu ambaye alileta hoja hasa ya ukweli .

Haya yatakuwa maoni yangu binafsi baada ya kusoma makala hii, nitoe shukurani zangu za dhati kwa Bi.Laila

Nitarudia kifunguio cha makala ambacho kinajadili suluhusho ya ngwe hii ya muungano.Nimeshangaa kidogo kuona makala pamoja na Mansour kusema serekali 3 ndio suluhusho, wakati makala nzima imeonesha lengo na madhumuni ya muungano kuwa si mema kwa Zanzibar na watu wake.
Sasa ikiwa ushahidi wote huo wa kuwa Marekani na nchi za magharibi zilikuwa na manuari na huku Mwalimu akitishia nyau kwa Mzee Karume.Huu wote ni ushahidi kuwa wazanzibari tokea awali hawakutaka muungano, na wala hawajaulizwa ridhaa yao juu ya suala hili.Kwanini turukie kwamba suluhusho ni serekali 3.

Ni ushahidi gani unatuonesha kama serekali 3 ndio suluhusho la kudumu ? Zifuatazo ni sababu za msingi za kuamini kuwa hili la serekali 3 si suluhusho ya gonjwa lilodumu kwa miaka 47.

1.Hoja ya mwanzo, inaonesha miaka ambayo Zanzibar haikuwa ndani ya muungano ilifanya vizuri zaidi kiuchumi kuliko miaka hio 47 ya muungano.Hii inaingia akilini, kwa vile muungano wenyewe haukuwa na malengo ya kiuchumi bali kisiasa zaidi.
2.Serekali 3, sidhani kama kwa Tanganyika wanaweza faidika ukizingatia ukubwa wa taifa lao sidhani kama watafaidika na kuwa na serekali ya muungano ambayo wao kama mdau watahijika kugharimia fedha za kuendesha serekali hio.

3.Muungano wa Tanganyika na Zanzibar hauna tena maana, ukizingatia kuna muungano wa EAC au nchi za afrika mashariki.Kuendelea kujadili muungano wa serekali 3 ni kupoteza resources za wananchi, ni kheri serekali zote ile ya Tanganyika na Zanzibar zikawekeza kwenye muungano wa EAC.
Suluhusho sahihi:
Nadhani hata kusema kuvunja yaweza kuwa ni kukupuruka, pengine suluhusho ni kuuliza kwa njia ya demokrasia na kupata jibu sahihi.
 
Zanzibar ni kama koloni la Tanzania, kiasili watu wake ni wavivu wa miili na akili ndio maana mpaka leo wapo chini ya Tanzania
 
Suluhisho kamili ya historical injustice na agression ilofanyiwa Zanzibar hadi kuburuzwa reluctantly ndani ya muungano ni/ ndani ya shirikisho la EA Zanzibar iwe na hadhi ya partner among equals kama ilivo Uganda ,Burundi,Rwanda,Kenya na "Tanganyika". Zanzibar kujiunga na shirisho nyuma ya mgongo wa jamhuri ni kukaribisha kero nyengine mpya kwa sababu structure nzima ya utawala in respect to zanzibar will lack clarity kwa hivo haki na hadhi ya zanzibar ndani ya shirikisho la EA kutotambuliwa.
 
Suluhisho kamili ya historical injustice na agression ilofanyiwa Zanzibar hadi kuburuzwa reluctantly ndani ya muungano ni/ ndani ya shirikisho la EA Zanzibar iwe na hadhi ya partner among equals kama ilivo Uganda ,Burundi,Rwanda,Kenya na "Tanganyika". Zanzibar kujiunga na shirisho nyuma ya mgongo wa jamhuri ni kukaribisha kero nyengine mpya kwa sababu structure nzima ya utawala in respect to zanzibar will lack clarity kwa hivo haki na hadhi ya zanzibar ndani ya shirikisho la EA kutotambuliwa/diminished
 
Dawa ni serikali moja. Mkoa wa Zanzibar wenye wilaya 2 za Unguja na Pemba. Nakiri Zanzibar ni nchi kwa sababu ina eneo ila halina mipaka, ina rais 'Kilemba cha Ukoka' ambaye hana nguvu za dola, ina waziri wa fedha asiye na sarafu. Haina jeshi bali JKU nyoronyoro etc. etc

Pascoooooooooo
 
Back
Top Bottom