Uzalendo wa Kitanzania
JF-Expert Member
- Mar 8, 2020
- 2,250
- 4,802
Wadau hamjamboni nyote
Taarifa kamili hapo chini:
Hatimaye Samaha Mufti wa Tanzania Dr. Abubakar Zubeir Ali Mbwana jana Jumanne amekabidhi tiketi kwa wanafunzi wanaokwenda kusoma elimu ya Dini ya Kiislamu nchini Morocco kupitia Skolashipu alizoziomba kwa mfalme wa Morocco.
Ukumbi wa Mfalme Mohammed VI BAKWATA Makao Makuu uligubikwa na furaha ya aina yake kwenye hafla maalum ya kuwaaga wanafunzi hao iliyohudhuriwa na viongozi wa taasisi mbalimbali za kiislamu nchini
Wanafunzi hao ambao ni kundi la kwanza kati ya wanafunzi mia mbili wanaotarajiwa kwenda nchini Morocco wataondoka mapema leo Jumatano tayari kwa ajili ya kuanza masomo ya miaka mitatu
Baadhi ya wanafunzi walishindwa kuongea kwa furaha na mwanafunzi mmoja kutoka Kigoma alipoulizwa anavyochukulia skolashipu hiyo akasema kwa ufupi ....
"Sasa Mufti ameanza Kazi.. Naam ! Kwa sababu kutayarisha masheikh ndiyo kushika hatamu" Amesema
Skolashipu hizo zinajumuisha Tiketi ya kwenda Morocco, Tiketi ya Kuja Tanzania na kurudi Morocco kila Mwaka wakati wa Likizo, Posho ya Dola mia Mbili kila Mwezi, Chakula, malazi, matibabu, Vitabu na vifaa vingine vya masomo, masomo na huduma zingine za jamii.
....
Dr. Harith Nkussa
Msemaji Maalum wa Mufti
Jumatano 8.5.2024
Dar es salaam
Taarifa kamili hapo chini:
Hatimaye Samaha Mufti wa Tanzania Dr. Abubakar Zubeir Ali Mbwana jana Jumanne amekabidhi tiketi kwa wanafunzi wanaokwenda kusoma elimu ya Dini ya Kiislamu nchini Morocco kupitia Skolashipu alizoziomba kwa mfalme wa Morocco.
Ukumbi wa Mfalme Mohammed VI BAKWATA Makao Makuu uligubikwa na furaha ya aina yake kwenye hafla maalum ya kuwaaga wanafunzi hao iliyohudhuriwa na viongozi wa taasisi mbalimbali za kiislamu nchini
Wanafunzi hao ambao ni kundi la kwanza kati ya wanafunzi mia mbili wanaotarajiwa kwenda nchini Morocco wataondoka mapema leo Jumatano tayari kwa ajili ya kuanza masomo ya miaka mitatu
Baadhi ya wanafunzi walishindwa kuongea kwa furaha na mwanafunzi mmoja kutoka Kigoma alipoulizwa anavyochukulia skolashipu hiyo akasema kwa ufupi ....
"Sasa Mufti ameanza Kazi.. Naam ! Kwa sababu kutayarisha masheikh ndiyo kushika hatamu" Amesema
Skolashipu hizo zinajumuisha Tiketi ya kwenda Morocco, Tiketi ya Kuja Tanzania na kurudi Morocco kila Mwaka wakati wa Likizo, Posho ya Dola mia Mbili kila Mwezi, Chakula, malazi, matibabu, Vitabu na vifaa vingine vya masomo, masomo na huduma zingine za jamii.
....
Dr. Harith Nkussa
Msemaji Maalum wa Mufti
Jumatano 8.5.2024
Dar es salaam