Muswada wa kukusanya maoni juu ya Marekebisho ya Katiba watinga Bungeni leo

Ndugu Waberoya,

Wenye akili kama wewe humu ndani, katika dakika chache ulizo-panic nazo hapo juu - wengine tumeng'amua kile ambacho hakika usingependa kijulikane kwa wapambanaji nchini. Nasema tumekuelewa zaidi ya hata kama ungalitumia maneno 1,000 na zaidi kujieleza. Lakini usijali katiba ya wananchi iko njiani itapatikana na wajuku zako pia wataifurahia sana.

Kwa sasa niko bize kidogo, niko kwenye suala zito la Katiba Mpya ambayo kwako kumbe si kitu kabisa, hivyo nitakujibu ipasavyo kwa wakati mwingine kwa hilo la kuuliza kama utakua umetegwa kitu. A green snake in the grass!!!

You are right! wananchi ndio wa kulaumiwa mno.. we are slumbering



Habari gani kamili ya mimi kukupa wewe? kuwa muswada umebeba maoni ya watu ni lini yamechukuliwa? unanitega?

Nikisoma tu post yako naona ni walewale...jambo zito kuliko yote?.. hilo zito kwako kaka!! watanzania wengi hawana hata mpango na hiyo katiba..Guys tunaposema kazi ipo na tuamshane na sio kupena moyo I know I have see that we have big problem!!

eti? unasema na unaamini kabisa Makinda ataenda kinyume na CCM na serikali yake?? you must be dreaming! kama unasubiri Anna abadilike na CCM ibadilike pole sana..pole we!! at a glance, nothing good comes out of CCM nothing!
 
Vyama vya upinzani na wananchi haviwezi kazi na wala havitaleta tija, nakuambieni ni maoni yangu. Ukombozi utapatikana tu pale wazanzibar watakapofanya kweli, ndio sense jamaa itawarudia. Vinginevyo sahauni.
 
Zitto anasisitiza muswada wenyewe ndio kwanza wabunge wameupata na hawajaupeleka kwa wananchi kuujadili, anaona hakuna udharura kwani wabunge lazima kwanza washauriane na wananchi juu ya mabadiliko haya - Invisible

Spika anadai mmoja wa watu walotaka uwe na uharaka ni Zitto hivyo anamshangaa kuwa inakuwaje atoe hoja hiyo - Invisible

Tukisema spika ni kiazi mnachukia... tukisema viongozi wa CCM wengi kazi yao ni kushangaa-shangaa, pia mnasema tunawananga

Zitto kutaka mswada kuwahi haina maana usifuate taratibu!! ANNE you need to act like a real speaker of a serious Bunge
 
Waberoya,

Nipo nawe aslimia 110, tatizo lako kwangu ni haya;
  • unahisi wewe unajua na u wish mawazo yako ndo sahihi, well, have you practise what you say? kama unahisi unayoamini why usichukue hatua? nilikuuliza ujuzi wako katika haya mambo hukujibu,
  • Huwa husemi as if unashauri ila unakuwa na jazba, sisi tunazo but we used to appreciate hatua zilizofanyika na wengine wewe unalaumu mpaka unawaombea SANDA.
Fanya unaloweza kwa nafasi yako badala ya kulaumu tu as if ulishatumia resources zako na wengine wakamis-use. Wananchi hawa wataelewa watu kama nyie na sisi tutakapo kubali na kuongezea pale palipofikia sio kulauumu as if Slaa, Mbowe, Kitila, Baregu, Zitto, Julias na wengine hawataki. Wamefanya pao na bado wanazidi na sio kweli kuwa hawajui wapo wapi, wanafanya nini na wanaishia wapi.

Sisi sote twende kwa wananchi, tutumie rasmimali zetu (time, money nk) kuwaelimisha, kupiga kelele, na vitisho.

asante sana

2 that i can say, THIS IS REAL THE HOME OF GREAT THINKERS.
 
==============
MASAHIHISHO:

Muswada uliowasilishwa ni wa namna ya kukusanya maoni ya wananchi juu ya mabadiliko ya Katiba; public hearing itafanyika Dar na Dodoma - Invisible

Hata Zanzibar nao wameomba kupewa fursa ya Public hearing lakini Spika anadai kuwa Zanzibar wameshauriwa watumie kituo cha Dar es Salaam; Wabunge toka Zanzibar wanapinga hoja hii ya Spika - Invisible

Wabunge wanapendekeza muswada huu ubadilishwe uende katika lugha ya Kiswahili ili wananchi waelewe nini kimo; serikali inadai inafahamu umuhimu wa kutumia kiswahili lakini hawakufanya tafsiri ya kiswahili na wanatambua kuwa huo ni upungufu, wanaamini wananchi watapata watu wa kupata tafsiri na wao hawadhani kama ni kikwazo sana - Invisible

Zitto anasisitiza muswada wenyewe ndio kwanza wabunge wameupata na hawajaupeleka kwa wananchi kuujadili, anaona hakuna udharura kwani wabunge lazima kwanza washauriane na wananchi juu ya mabadiliko haya - Invisible

Spika anadai mmoja wa watu walotaka uwe na uharaka ni Zitto hivyo anamshangaa kuwa inakuwaje atoe hoja hiyo - Invisible

Asante Invi. kwa sahihisho.
 
Pia nimeipata ratiba ya kikao hiki, ni hii

TAREHE SIKU/SAA TUKIO
2/04/2011na3/04/2011 Jumamosi na Jumapili Wabunge kueleke Dodoma.
4/04/2011 Jumatatu Saa 10.00 Jioni Kikao cha Briefing cha Wabunge wote.
Saa 11.30 Jioni Vikao vya Kamati za Vyama vya Siasa.
5/04/2011 Jumanne Kipindi cha Maswali ya Bunge-Azimio la kuridhia Mkataba wa UNESCO kuhusu kuhifadhi
ya urithi wa Utamaduni usioshikika wa mwaka, 2003
[The Convention for Safeguard of the Intangible Cultural Heritage]
Azimio la kuridhia Mkataba wa UNESCO kuhusu kulindwa na kukuzwa kwa
anuai ya kujieleza kiutamaduni wa, 2005 [The Convention on the Protection
and Promotion of the Diversity of Cultural Expressions].
6/04/2011 Jumatano-Kipindi cha Maswali ya Bunge, Taarifa za Kamati za Bunge zinazosimamia fedha za Umma (PAC, POC na LAAC).
7/04/2011 Alhamisi- Siku Kuu ya Kumbukumbu ya Karume (Karume Day).
8/04/2011 Ijumaa-Kipindi cha Maswali ya Bunge, Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali wa Mwaka 2011, [The Written Laws (Miscellaneous Amendments) Bill, 2011].
9/04/2011 Jumamosi -MAPUMZIKO
10/04/2011 Jumapili-MAPUMZIKO
11/04/2011 Jumatatu-Kipindi cha Maswali ya Bunge. Muswada wa Sheria ya Famasi wa Mwaka 2010 [The Pharmacy Bill, 2010].
12/04/2011 Jumanne-Kipindi cha Maswali ya Bunge, Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria za Maeneo ya Maendeleo ya Kiuchumi wa Mwaka 2011 [The Economic Zones Laws (Miscellaneous Amendments) Bill, 2011].
13/04/2011 Jumatano, Kipindi cha Maswali ya Bunge, Uchaguzi wa Wenyeviti wa Bunge, Uchaguzi wa Wajumbe wawili wa SADC-PF, Uchaguzi wa Wajumbe wa "Pan African Parliament" (PAP), Uchaguzi wa Mjumbe wa APRM, Azimio la Kuridhia Itifaki ya Sayansi, Teknolojia na Ubunifu ya Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika [The SADC Protocol on Science, Technology and Innovation].
14/04/2011 Alhamisi- Kipindi cha Maswali kwa Waziri Mkuu, Kipindi cha Maswali ya Bunge ya kawaida, Muswada wa Sheria ya Manunuzi ya Umma wa Mwaka 2010 [The Public Procurement Bill, 2010].
15/04/2011 Ijumaa-Kipindi cha Maswali ya Bunge, Muswada wa Sheria ya Manunuzi ya Umma wa Mwaka 2010 [The Public Procurement Bill, 2010].
16/04/2011 Jumamosi-Muswada wa Sheria ya Utawala wa Mahakama wa Mwaka 2011[The Judicial Administration Bill, 2011].
17/04/2011 Jumapili-Mapumziko.
18/04/2011 Jumatatu-Kipindi cha Maswali ya Bunge, Muswada wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ya Nchi [The Constitutional Review Bill, 2011].
19/04/2011 Jumanne-Kipindi cha Maswali ya Bunge, Muswada wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ya Nchi [The Constitutional Review Bill, 2011].
· HOJA YA KUAHIRISHA BUNGE.
 
Waberoya,

Nipo nawe aslimia 110, tatizo lako kwangu ni haya;
  • unahisi wewe unajua na u wish mawazo yako ndo sahihi, well, have you practise what you say? kama unahisi unayoamini why usichukue hatua? nilikuuliza ujuzi wako katika haya mambo hukujibu,
  • Huwa husemi as if unashauri ila unakuwa na jazba, sisi tunazo but we used to appreciate hatua zilizofanyika na wengine wewe unalaumu mpaka unawaombea SANDA.
Fanya unaloweza kwa nafasi yako badala ya kulaumu tu as if ulishatumia resources zako na wengine wakamis-use. Wananchi hawa wataelewa watu kama nyie na sisi tutakapo kubali na kuongezea pale palipofikia sio kulauumu as if Slaa, Mbowe, Kitila, Baregu, Zitto, Julias na wengine hawataki. Wamefanya pao na bado wanazidi na sio kweli kuwa hawajui wapo wapi, wanafanya nini na wanaishia wapi.

Sisi sote twende kwa wananchi, tutumie rasmimali zetu (time, money nk) kuwaelimisha, kupiga kelele, na vitisho.

asante sana

Kaka mara nyingi nimekuwa sieleweki kwa sababu ya kuwa nikitaka kueleweka huwa sieleweki vile ninavyotaka nieleweke. Nimebaki kulaumu na kugumia kimyakimya!!!

Pole na asante sana kwa angalizo

Uko tayari sasa nikupe solution and are strategic moves, au kabla...... wewe tumaini lako la katiba lilikuwa kwenye tume ya Rais na serikali.. I MEAN LEO HII ULIKUWA UNATEGEMEA AJENDA YA KATIBA WAIJADILI BUNGENI , bunge letu hili?

Are we here discussing katiba na mapendekezo yatakayotolewa na chama cha mapinduzi? ambao wako wengi bungeni??

The first question is are we serious?? CCM ninayoifahamu mimi kwa miaka zaidi ya 30 sikumbuki ni lini bungeni waliweza kuamua kitu ambacho kikawa tangible na kila mmoja akasema KWELI bunge la MWAKA HUU limetusaidia.. sikumbuki kuanzia Nyerere mpaka Kikwete...

Sasa tunapoamshana tuondokane na ukoko huu wengine tunaonekana tuna matusi...! I am happy someone should consider me that way


ANGALIZO

1. Hakuna haja ya mswaada wa katiba kwenda bungeni!
2. Jinsi ya kuchukua maoni watakao dictate ni CCM!.period


Baada ya kuona tulishindwa na tuiporwa hoja ya katiba --AMBAYO HAIKUWA YA CCM, vita ingeamia kwenye tume ya uchaguzi ambayo kwangu naona kama ni rahisi sana kuliko katiba ambayo itakamilika miaka 70 ijayo!! note tha down, wakati mimi na wewe tumekufa au tumevunja rekodi ya kuishi duniani! KATIBA IS A LONGTERM process...tusitegemee kuisha kabla ya 2015

Umenielewa?

I mean hatuna clear strategic move, katiba hata ikibadilishwa kesho haina maana ikulu kunaingilika kirahisi

Ila tume ya uchaguzi ikibadilika leo, tukapiga maandamano na kuitisha operations nyingi basi kuna uwezekano 2015 CCM wakaondoka!

Narudia hata kama mabadiliko ya NEC inaweza ikawa lazima ibadilike katiba kwanza, basi cha kwanza tu-deal na marekebisho ya katiba UPANDE WA NEC tu..ambapo within one year au miwili iwe imeisha na 2014 tuwe na NEC mpya na sura mpya!!!

wanachofanya CCM ni kuwa mchakato wa kutaka maoni ya wananchi utahitaji hela ambazo watasema hawana na watasubiri mchakato uanze 2015 November!!!


I repeat

strategy hatuna na kuna WAKATI HUWA SIAMINI kuwa vichwa vyooote uko kwenye upinzani hawalijui hili!! SIAMINI,..labda unieleze kivingine


How far have we gone to replace the existing election committee?? umesikia watu wanaipigia kelele hili? unajua aliyekuwa makamu wa NEC , akateuliwa na shein kuwajaji mkuu zanzibar? kuna connection kubwa kati ya serikali, NEC na CCM! we need FREE NEC!!

Au unasemaje mkubwa?
 
Naomba watanzania tufanye subira kilichopelekwa bungeni ni kuomba ridhaa ya bunge ili tuanze kujadili katiba mpya.
 
Salaam,

Wabunge wanapendekeza muswada huu ubadilishwe uende katika lugha ya Kiswahili ili wananchi waelewe nini kimo; serikali inadai inafahamu umuhimu wa kutumia kiswahili lakini hawakufanya tafsiri ya kiswahili na wanatambua kuwa huo ni upungufu, wanaamini wananchi watapata watu wa kupata tafsiri na wao hawadhani kama ni kikwazo sana - Invisible

Ukisoma maneno hayo juu unashindwa kuelewa kuwa hapa ni serikali inawajibika kwa wananchi? au wananchi ndo inabidi wawajibike kwa serikali? hii ni fedheha kabisa
-wanakili ni upungufu lakini WANAAMINI wananchi watapata watu wa kutafsiri!!, does this make sense? yani serikali inaacha kutekeleza badala yake inasema inaamini? kwahiyo ata kwenye matatizo mengine kama ukosefu wa walimu yawezekana wanaamini watoto watakwenda tuition?
mfano;
kwakuwa mimi elimu nilipata kwa kujilipia, je nikiamua kuwatafsiria wananchi kwa malipo talipwa na nani? na hao wananchi kwakuwa waliowapa kodi zao wamegoma kuwatafsiria?
NINACHOKIONA.
serikali yetu inapambana na wananchi badala ya kuwajibika kwa wananchi na ndomana si ajabu kuona wanatumia mbinu nyingi kama
1.KUPOTOSHA.mfano wanasema Tanzania ina AMANI, na kuwatisha wananchi harakati kama maandamano zinachochea upotevu wa amani,
lakini, ni kweli tunaamani? maanndamano yanachochea vurugu(wao usema kupoteza amani)?
2.KUFICHA.Na ndomana hawataki kutafsiri, sio kwasababu awafahamu, HAPANA,ndomana wamekili wanafahamu,sio ilikua baati mbaya
HAPANA ndomana hawatatafsiri pamoja na wananchi(kupitia wawakilishi) kuwataka wafanye hivyo.
 
Eti Watanzania wala hawana mpango wowote na katiba mpya na kwamba kwanza hata hawajui nini hicho????????????? This is too sick and mos irritating for someone to utter in his mouth!!!!!!!!!!

Sasa mtajua kwa vitendo kwamba kumbe suala la katiba mpya haswaaa ndio mapigo yetu ya moyo kila mmoja wetu nchini na kwamba haki yetu tutaitetea kwa gharama yoyote ile!!!!!!!!


Umekopi wrong post, dont be coward, copy post, ijibu right under mjadala uendelee!! ukiogopa watu usiowaona je ukiowaona inakuwaje? hoja yako nzuri sana lakini hatujui nani kasema na kwa nini..that is real intelectual discussion!
 
inatia huruma kuona huu muswada umeandikwa kingereza, asilimia kubwa ya wabunge wetu hata kinegreza hawajui, sijui watajadili nini tu. Waishia kujadili wakina Lowassa, Chenge na Rostam, wengine ni kupiga mikono kwenye meza zao kupitisha kila kitu....
 
Kaka mara nyingi nimekuwa sieleweki kwa sababu ya kuwa nikitaka kueleweka huwa sieleweki vile ninavyotaka nieleweke. Nimebaki kulaumu na kugumia kimyakimya!!!
Waberoya, usijali kutoeleweka, as long as you have the clear concious ulitaka uelewekaje. Galileo Galilei aliuwawa aliposema dunia ni duara. Hukumu hiyo ilifuatia hoja kuwa anambeza Mungu ambaye ndio muumba.

Ili ueleweke, kunahitaji kiwango fulani cha uelewa kinachohitajika mli mtu akuelewe level yako, bahati mbaya humu jukwaani na Watanzania kwa ujumla, kiwango chetu ni kile cha kuelewa zaidi nyimbo za sifa shangwe na mapambio ndio maana tumetendwa sana, na tunaendelea kuwakumbatia waliotutenda ili waendelee kututenda tena na tena. Hata kina Confucious, Socrates, Plato na wengine wengi, hawakueleweka kwa urahisi.

Ila pia kitendo cha kubaki ukilaumu na kugumia kimya kimya is not heathy, utaishia kupata pressure, ulcers na hata depression.
 
Back
Top Bottom