Mustakabali wa ufisadi, Richmond na usalama wa aliyekuwa Waziri Mkuu Edward Lowassa

Wewe gimmy's una matatizo kichwani. Wakati ripoti ya Richmond ikisomwa bungeni Mwakyembe alituaminisha kwamba hakuisoma ripoti yote ili kunusuru amani ya nchi, huwezi hata kutafakari na kuhoji kwa nini hakuisoma yote? Sababu kubwa ni kuhusika moja kwa mija kwa JK.
Lowassa aliwaambia waliompa nafasi ya kujiangalia kwamba kuna waatu wanataka uwaziri mkuu wake kwa hiyo akaondoka wauchukue. EL ni mtu ambaye namwona kama shujaa na sugu wa kuhimili matusi na kejeli kutoka CCM. Amesisitiza mara nyingi kwamba yeyote mwenye ushahidi kwamba yeye ni fisadi aupeleke mahakamani. Na mara alipoachana na CCM aliweka bayana kilichotokea wakati wa mchakato mzima wa Richmond.
Nyie msiopenda kufikiri na kupambanua mambo hamkumbuki kwamba baada ya Richmond ilikuja Dowans ambayo kuna kitu serikali ilifanya na kujikuta inalipa faini kubwa mno. Mhusika mkubwa (yule aliyejivua gamba kwa kusema anachana na siasa uchwara) akauza mitambo hiyo kwa wamarekani kwa faida kuubwa tu. Hayo yote mnayajua???
Kinaachfanyika CCM sasa hivi ni kama kilichotokea serikalini, kutumbua vipele. Mijizi mikubwa hakuna anayeweza kuigusa akiwa ndani ya chama kibovu cha mafisadi.
Watamkaba na kumwambia kwamba hakupata urais kwa ridhaa ya wananchi (na hii si siri hata yeye anajua) na watamtahadharisha kukosa imani naye na pia watamkumbusha skandali zake nyingi za nyuma: nyumba za serikali zilivyouzwa, meli mbovu na wale samaki wa kichina. Na sasa hivi ameisha ingizwa mkenge na washauri wake kuzuia wawekezaji wenye mikataba halali wasipeleke mchanga nje. Hii ni hatari.
CCM ina wenyewe, ambao yeye si mmojawapo.
Pesa inapopitiliza ni hatari sana,ni wengi sana wameweza kununuliwa ili tu wamtetee huyu mzee.Hizi kwenye histori ya nchi hiii ilishawahi kutokea kwa kiongozi kugawa pesa mamilioni kwa mamilioni kiholela akijifanya kusaidia kisa tu uraisi?Huwenda tunawezakosa kuthibitisha kwa ushahidi,lakini hata ushahidi wa mazingira tu wewe huuoni?Hivi umegawiwa sh ngapi na hata unalisaliti taifa lako?Au wewe unaitwa Fuledi mkuu?
 
ndiyo mpelekeni mahakamani fisadi mkuu acheni kulia-lia.
Kama ni hivyo kwamba mnayemwita fisadi akija kwenu anakuwa msafi basi yawezekana hizi kelele za kuwepo Escrow, lugumi, Richmond ni kelele zisizo na ukweli maana nyie hamsimamii madai yenu zaidi ya kuangalia faida zenu kisiasa kuliko taifa,
Inashangaza sana kama viongozi wenu kwa ufahamu wao na makusudi wakaanza kuzunguka nchi nzima wakimchafua mzee lowassa kuwa ni fisadi namba moja Tanzania, sasa kama hakufanya huo ufisadi kwa nini viongozi wenu walishiriki hiyo dhambi na baadae wakaja kumpokea na kudhihirisha unafiki wao?

Je, chama chenu kina falsafa gani na mbinu zipi mathubuti za kupambana dhidi ya ufisadi? Kama lowassa si fisadi, viongozi wa chadema wana mawazo gani mpaka kufikia hatua ya kusingizia mtu mwaminifu?

#Naamini mzee lowassa siku moja atapandishwa kizimbani ili ajibu hizi tuhuma zenye mkanganyiko wa kisiasa, lakini kama ni kweli alifanya ufisadi kama chadema walivyokuwa wakimtuhumu basi lazima sheria ifuate mkondo wake bila kusita.
 
Kama ni hivyo kwamba mnayemwita fisadi akija kwenu anakuwa msafi basi yawezekana hizi kelele za kuwepo Escrow, lugumi, Richmond ni kelele zisizo na ukweli maana nyie hamsimamii madai yenu zaidi ya kuangalia faida zenu kisiasa kuliko taifa,
Inashangaza sana kama viongozi wenu kwa ufahamu wao na makusudi wakaanza kuzunguka nchi nzima wakimchafua mzee lowassa kuwa ni fisadi namba moja Tanzania, sasa kama hakufanya huo ufisadi kwa nini viongozi wenu walishiriki hiyo dhambi na baadae wakaja kumpokea na kudhihirisha unafiki wao?

Je, chama chenu kina falsafa gani na mbinu zipi mathubuti za kupambana dhidi ya ufisadi? Kama lowassa si fisadi, viongozi wa chadema wana mawazo gani mpaka kufikia hatua ya kusingizia mtu mwaminifu?

#Naamini mzee lowassa siku moja atapandishwa kizimbani ili ajibu hizi tuhuma zenye mkanganyiko wa kisiasa, lakini kama ni kweli alifanya ufisadi kama chadema walivyokuwa wakimtuhumu basi lazima sheria ifuate mkondo wake bila kusita.
mkuu usipoteze muda wako kuandika gazeti zima kwakua hata sisomi zaidi ya sentensi mbili.
Narudia tena, mpelekeni Lowasa mahakamani.
 
Kuna lile jengo moja lilianguka maeneo ya chang'ombe, miezi ambapo awamu ya nne ndio kwanza ilikuwa imeingia madarakani. Nadhani mleta uzi utakuwa unaikumbuka hii issue.
 
serikali iko chini ya CCM.
kama Lowasa ni fisadi mpelekeni mahakamami upesi.
By the way, kwa maelezo yao, Lowassa alianza 'kuwa fisadi' tangu wakati wa chama kimoja...na serikali sikivu ya chama cha mapinduzi iliendelea kumtumia katika ngazi mbalimbali ili azidi 'kufanya ufisadi' kote huko maana alionekana ni 'fisadi hodari' na CCM ilitaka fisadi aliyebobea kwa kuwa wao lengo lao kuu ni kufanikisha ufisadi.

Otherwise, sioni ni kwa vipi fisadi wa calibre hiyo aliendelea kujipatia nafasi za uongozi hadi kufikia kuwa waziri mkuu katika serikali zisizokuwa za kifisadi.
 
siku magufuli akipata ujasiri wa kumshitaki lowassa kwa ishu ya richmond nitaacha kula siku mbili!!magu kamwe hawezi kuichokonoa richmond
 
Sina Lengo lakumchafua ndugu Lowasa ila lengo ni kutizama kashfa mbalimbali zilizomkabili huku nikitizama usalama wake hasa kutokana na mazingira ya utawala wa sasa chini ya ndugu John Pombe Joseph Magufuli.

Kwanza naomba niyanukuu maneno ya mh Mwakyembe ambayo alishawahi kuyatoa siku moja alipokua akihojiwa mwaka jana wakati Tanzania ikiwa kwenye hekaheka za uchaguzi mkuu ambao hatimaye ulimuweka madarakani ndugu John Pombe Magufuli.Mh mwakyembe alisema hivi na hapa namnukuu,

"nina imani siku moja Lowasa atatinga mahakamani kujibu tuhuma zinazomkabili".

Leo tunashuhudia ndani ya CCM kwenyewe hakuko salama,wote waliotenda vitendo vya kufisadi mali za chama sasa wamekumbwa na taharuki kwani rungu la Magufuli limekua likiwashukia kokote walipo.

Tunafahamu Lowasa anahistoria ndefu sana zakiutendaji ndani ya CCM na nje ya CCM na kote huko amekua akitajwatajwa vibaya kutokana na mienendo yake yenye kutilia shaka.Ukiachilia mbali tuhuma za ufisadi wa richmond ambazo zilipelekea yeye kujiuzuru lakini bado kuna mashaka makubwa kwamba inawezekana kabisa yakapatikana madoa yake ndani ya CCM pia.

Wengine wanazungumza habari ya AICC,Wengine watazungumza habari za lile jengo refu na lenye kuvutia pale umoja wa vijana,wengine watazungumzia ranchi za taifa,wengine watazungumzia richmond.Kwa msingi huo utaona mlolongo ni mrefu sana na kama mtu atataka ashinde akichambua basi ingemuhitaji muda mrefu sana kufanya hivyo.

Lakini pia Mh Makamba akiwa Morogoro mwaka jana alipokua anamnadi magufuli alijaribu kugusia habari za ukosefu wa uadilifu waLowasa na ngoja kwa ruhusa yenu nimnukuu,

"Nashangaa wanaostahili kwenda jela ccm ndio wanachukua form,na ccm ikawagundua wanaostahaili kwenda jela ni pamoja na mh lowasa".Hapa mh makamba aliyanukuu maneno yaliowahi kusemwa na mh Lipumba yaliomuhusu Lowasa.

Mh Makamba aliendelea kusema kwamba yapo mambo ambayao hamyajui kutoka kwa mh lowasa ngoja niyaseme,na nikisha yasema nitamuomba mh lowasa asimame hadharani ayakane.

"Lowasa alitaka kuondoka ccm mwaka 1995 na aliniandikia barua mimi".Makamba alisema chanzo ni Lowasa kukatwa jina lake kwenye mchakato wa kusaka raisi wa Tanzania na chanzo kilikua ni utajiri usio elezeka huku akiwa na umri mdogo.

Makamba aliendelea kusema.

"Kuna ranchi ya mkata lowasa kampa rafiki yake na yeye yumo.Pale handeni ipo ranchi ya mzeri wapo wamasai wakibrashi hawana maeneo yakufugia lowasa alipo kua waziri wa mifugo kajipa ranchi mwenyewe''.Makamba alieleza mengi kuhusu mashaka ya uadilifu wa aliyekua waziri mkuu ndugu Lowasa.

Niseme wazi hizi zote si hatia kwani hakuna mmoja aliyempeleka Lowasa mahakamani na mahakama ikamshika na hatia kwani mahakama ndio chombo pekee chenye kuthibitisha shutuma kama ni za kweli ama la.

Utawala uliopita uliacha wengi wenye shutuma wakiachwa pasipo kuthibitisha ki mahakama juu ya ukweli wa shutuma hizo tofauti na utawala wa sasa ambao tunaona jambo hili limekua si la mzaha tena.

Je Lowasa atabaki salama chini ya Magufuli pasipo kufikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazomkabili?

Lakini pia lazima kujiuliza kwamba japo ni shutuma tu lakini je ilikua ni halali kwa Lowasa kua kiongozi mkuu ndani ya serikali?Hapa naomba kuyanukuu maneno ya mh Hamfrey Polepole ambayo siku moja akiwa channel ten alisema na hapa namnukuu,

''Tunapaswa kuangalia hivi je na jambo hili katika mantiki ya uadilifu linapaswa lithibitishwe mahakamani?,mtu huyu si muadilifu hafai kua kiongozi wa taifa letu,kwasababu hawezi kutoa hamasa yakua mtu bora katika nchi yetu."

Pole pole aliendelea kusema,

"kunatofauti kati ya legitimacy na ligality,haihitaji wewe tukusafishe kisheria kusema wewe ni muadilifu.Wewe si muadilifu,huna legitimacy,huna uhalali,ni tajiri,tukikuuliza pesa zote hizi unapata wapi?unasema pesa zote hizi ni zamarafiki zangu,hivi hao marafiki zako wanatoa pesa zote hizi ili wewe uende ikulu kwa maslah gani,wameoa dada yako?".

Kwa uchambuzi huu ni dhahiri mh Lowasa anatuhuma lukuki akituhumiwa juu ya matumizi mabovu ya madaraka lakini pia na ufisadi,swali ni je Lowasa atabaki salama chini ya utawala huu wa Magufuli pasipo kufikishwa mahakamani kujibu tuhuma alizokua akituhumiwa maramara kwa mara?

Tatizo la wengi hawajui Lowasa alikuwa na akina nani na wajibu gani ndani ya serikali ya CCM. Ukielewa waziri mkuu anakuwa karibu na akina nani katika maamuzi au matendo yake utaamini kuwa ni raisi ngamia kupenya kwenye tundu la sindano kuliko kukabiliana na huyu Masai!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Bado ngonjera zinaendelea tuu! Mwenyewe alishasema kama kuna ushahidi wa ufisadi hata mmoja nendeni nao mahakamani mna mahakama ya mafisadi badala ya vitendo vya kupeleka shauri mahakamani nyie mko busy nyuma ya keyboard mnatupigisha chenga ya ahadi zenu ehh.
Ukitaka kumkamata kobe lazima umlie timing!
 
Back
Top Bottom