Musiba ni mwanachama wa CCM si kweli hana chama ushahidi huu hapa 2010 alijitosa kugombea,CCM wana haki kumjadili kwenye vikao vya chama

YEHODAYA

JF-Expert Member
Aug 9, 2015
36,906
51,924
Musiba ajitosa ubunge Mwibara



MCHAKAMCHAKA wa uchaguzi Mkuu ujao, umeanza kuchukua sura mpya katika Jimbo la Mwibara Wilaya ya Bunda Mkoani Mara, baada ya Mwandishi wa habari na Mtangazaji mwandamizi wa Televisheni ya Channel Ten, Cyprian Musibaambaye ametangaza kugombea Ubunge wa jimbo hilo kupitia CCM, kuonekana kukubalika zaidi jimboni humo.

Musiba ambaye ni kijana, wiki iliyopita alizuru katika jimbo hilo la Mwibara kwa lengo la kujitambulisha na kutangaza nia yake ya kugombea ubunge wa jimbo hilo, alipokelewa kifalme na watu wa wengi wa rika zote kila alipokuwa akienda kujitambulisha kwake.

Akizungumza kwa nyakati tofauti na wanachama wa CCM katika vijiji vya vya Karukekere, Chingurubila, Mugara, Mwiruruma, Sikiro, Igundu, Muranda na Buramba, Musiba alisema ameamua kugombea ubunge katika jimbo hilo, ili kuwakomboa wananchi kimaendeleo, kwani jimbo hilo lipo nyuma zaidi kimaendeleo huenda kuliko majimbo yote nchini.

Alisema, tangu nchi ipate Uhuru hadi sasa, wananchi wa Mwibara bado wanapata shida kubwa sana katika suala zima la maendeleo, kwani barabara zilizopo hazipitiki kirahisi, huduma za afya mbovu jambo ambalo inaonekana wananchi kutelekezwa.

Jimbo la Mwibara hivi sasa linawakilishwa na mbunge anayemaliza muda wake, John Kajege (CCM), ambaye amekuwa akilalamikiwa na wananchi wengi wa jimbo hilo kwa madai ya kushindwa kutekeleza ahadi alizowaahidi, hivyo anakabiliwa na hali ngumu zaidi.

Kutokana na hilo, Musiba ambaye anaonekana kukubalika kwa wananchi wa jimbo hilo kwa asilimia kubwa, alisema iwapo atateuliwa na chama chake kugombea nafasi hiyo na hatimaye kushinda atahakikisha anaboresha barabara, afya, elimu, huduma ya maji pamoja na kujenga ofisi za CCM kila tawi na Kata.

Lengo jingine ni pamoja kujenga ushawishi mkubwa kwa wafadhili na wawekezaji kujenga viwanda vya samaki Mwibara, huduma za kibenki kusogezwa pamoja na kuimarisha ushirikiano kati yake na wananchi wa rika zote jimboni humo.

“Tangu uhuru Mwibara haina hospitali ya jimbo, barabara mbovu, huduma za afya nazo mbovu, wananchi wanakunywa maji machafu wakati Ziwa tunalo ubavuni hapa! Nikiwa mbunge wenu matatizo yote haya nitayatatua kwa haraka sana”, alisema Musiba.

Katika ziara yake hiyo ya kujitambulisha, Musiba ambaye ni mzaliwa wa Iramba Mwibara alikumbana na adha mbali mbali ikiwa ni pamoja na kukwama mara kadhaa kwa gari lake alilokuwa akilitumia kutokana na barabara kuwa mbovu zisizopitika.

Mbali na Mtangazaji huyo wa Channel Ten, Musiba kutangaza kugombea ubunge wa Mwibara, watu wengine waliotangaza kugombea ubunge wa jimbo hilo kupitia CCM ni pamoja na mbunge wa sasa anayemaliza muda wake, Kajege na Rubola Kange ambaye amewahi kugombea chaguzi tatu zilizopita mfululizo anashindwa.

Kulingana na hali hiyo, Tanzania Daima imeshuhudia siasa chafu jimboni Mwibara, kwani baadhi ya wagombea wa jimbo hilo (majina tunayo), wameanza kutembeza rushwa ya fedha kwa wananchi, kwa lengo la kuwashawishi wawachague.

Akizungumzia suala la afya jimboni humo, Musiba alisema wanawake wengi wakiwemo wajawazito na watoto wamekuwa wakitembea umbali mrefu kufuata huduma ya afya katika hospitali ya binafsi ya Mission, hivyo baadhi yao hupoteza maisha yao ovyo.

Aidha, aliwasihi wanaCCM wenzake kuwapima kwa sera wagombea wote wa ubunge jimboni humo, yupi mwenye sera nzuri na anayewafaa na yupi asiyewafaa kisha kuchagua kiongozi bora na siyo bora kiongozi.

SOURCE:https://musiba4mwibara.wordpress.com/2010/04/15/musiba-ajitosa-ubunge-mwibara/

MYTAKE: CCM wana haki zote kumjadili vikao vya CCM
 
Ushahidi mwingine huu hapa alichukua fomu kugombea NEC 2012

MPIGANAJI CYPRIAN MUSIBA 'AKA'MZEE WA MWIBARA AJITOSA KUWANIA UJUMBE NEC YA CCM
August 28, 2012



ALIYEKUWA mwandishi Mwandamizi wa Televisheni ya Channel Ten, Cyprian Musiba (34), amechukuwa fomu ya kugombea nafasi ya Ujumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM taifa (NEC), na Mkutano Mkuu wa chama hicho ngazi ya taifa wilayani Bunda mkoani Mara.
Musiba ambaye amechukua fomu hizo juzi mchana na kuzirudisha jana asubuhi Makao Makuu ya Ofisi ya CCM Bunda, amesema dhamira yake ya kuomba nafasi hizo mbili ni kwenda kukijenga chama katika nyanja zote
za kijamii, kiuchumi na kisiasa.
Alisema atapambana kwa nguvu zake zote kudhibiti rushwa, siasa za chuki, fitna na makundi ndani ya chama chake hicho tawala.
Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kuchukuwa fomu hizo, Musiba alisema moja ya mambo yanayokichafua chama chake mbele ya umma wa Watanzania, ni vitendo vya rushwa, siasa chafu yakiwemo makundi na fitna.
Musiba alimuomba Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa(TAKUKURU), Dk. Edward Hoseah kuwapanga vema makamanda wake kwa ajili ya kuwakamata wagombea na watu watakaobainika kutoa rushwa ili wachaguliwe kwenye ngwe hiyo ya kuwania uongozi.
"Nimechukua fomu hii kwa lengo la kwenda kupigania maendeleo ya
chama changu tawala. Nitapambana kuhakikisha rushwa, siasa chafu ndani ya CCM vinaondoka, maana ndiyo vitu vinavyokiharibu kabisa chama.
"Kwa maana hiyo, kuanzia sasa naiomba TAKUKURU ianze kuwafuatilia na kuwakamata wagombea wote watakaoonekana kutoa rushwa
wakati huu wa uchaguzi," alisema Musiba.
Musiba ni miongoni mwa wanachama 13 waliochukuwa fomu ya kuomba kuteuliwa kugombea nafasi ya U-NEC kupitia wilaya hiyo

SOURCE:http://dinaismail.blogspot.com/2012/08/mpiganaji-cyprian-musiba-akamzee-wa.html
 
Hata nyarando miaka hiyo alikuwa CCM, lowassa alikuwa CCM akaondoka sasa amerudi, n.k. pointi hapa ni kwamba hata angekuwa CCM bado ni mtu mdogo sana wa kujadiliwa ngazi ya CCM taifa
 
Hata nyarando miaka hiyo alikuwa CCM, lowassa alikuwa CCM akaondoka sasa amerudi, n.k. pointi hapa ni kwamba hata angekuwa CCM bado ni mtu mdogo sana wa kujadiliwa ngazi ya CCM taifa
Wewe hangaika na mambo ya chadema chama chako ya CCM Tuachie wenyewe.Mwende mkajadiliane uchaguzi mkuu wa chadema mtafanya lini kwani muda wa kikatiba ulishapita kitambo msije futiwa chama mkapiga yowe.
 
Wewe hangaika na mambo ya chadema chama chako ya CCM Tuachie wenyewe.Mwende mkajadiliane uchaguzi mkuu wa chadema mtafanya lini kwani muda wa kikatiba ulishapita kitambo msije futiwa chama mkapiga yowe.
Wewe tunakujua upo upande wa mzee makamba, subirini ubatizo wa moto, musiba atapata ubatizo wa mafuta
 
Musiba kabla ya Matusi na Kashfa zake kwa Watu huwa anajitambulisha..

Mwanaharakati huru asiye na Chama.

Hatumwi na CCM.

Anamtetea Rais kwa Mapenzi yake binafsi.
Je? Ni kweli hakumbuki kuwa aliwahi Kugombea kura za maoni ndani ya CCM!
Chizi Musiba 😂
 
Musiba ajitosa ubunge Mwibara



MCHAKAMCHAKA wa uchaguzi Mkuu ujao, umeanza kuchukua sura mpya katika Jimbo la Mwibara Wilaya ya Bunda Mkoani Mara, baada ya Mwandishi wa habari na Mtangazaji mwandamizi wa Televisheni ya Channel Ten, Cyprian Musibaambaye ametangaza kugombea Ubunge wa jimbo hilo kupitia CCM, kuonekana kukubalika zaidi jimboni humo.

Musiba ambaye ni kijana, wiki iliyopita alizuru katika jimbo hilo la Mwibara kwa lengo la kujitambulisha na kutangaza nia yake ya kugombea ubunge wa jimbo hilo, alipokelewa kifalme na watu wa wengi wa rika zote kila alipokuwa akienda kujitambulisha kwake.

Akizungumza kwa nyakati tofauti na wanachama wa CCM katika vijiji vya vya Karukekere, Chingurubila, Mugara, Mwiruruma, Sikiro, Igundu, Muranda na Buramba, Musiba alisema ameamua kugombea ubunge katika jimbo hilo, ili kuwakomboa wananchi kimaendeleo, kwani jimbo hilo lipo nyuma zaidi kimaendeleo huenda kuliko majimbo yote nchini.

Alisema, tangu nchi ipate Uhuru hadi sasa, wananchi wa Mwibara bado wanapata shida kubwa sana katika suala zima la maendeleo, kwani barabara zilizopo hazipitiki kirahisi, huduma za afya mbovu jambo ambalo inaonekana wananchi kutelekezwa.

Jimbo la Mwibara hivi sasa linawakilishwa na mbunge anayemaliza muda wake, John Kajege (CCM), ambaye amekuwa akilalamikiwa na wananchi wengi wa jimbo hilo kwa madai ya kushindwa kutekeleza ahadi alizowaahidi, hivyo anakabiliwa na hali ngumu zaidi.

Kutokana na hilo, Musiba ambaye anaonekana kukubalika kwa wananchi wa jimbo hilo kwa asilimia kubwa, alisema iwapo atateuliwa na chama chake kugombea nafasi hiyo na hatimaye kushinda atahakikisha anaboresha barabara, afya, elimu, huduma ya maji pamoja na kujenga ofisi za CCM kila tawi na Kata.

Lengo jingine ni pamoja kujenga ushawishi mkubwa kwa wafadhili na wawekezaji kujenga viwanda vya samaki Mwibara, huduma za kibenki kusogezwa pamoja na kuimarisha ushirikiano kati yake na wananchi wa rika zote jimboni humo.

“Tangu uhuru Mwibara haina hospitali ya jimbo, barabara mbovu, huduma za afya nazo mbovu, wananchi wanakunywa maji machafu wakati Ziwa tunalo ubavuni hapa! Nikiwa mbunge wenu matatizo yote haya nitayatatua kwa haraka sana”, alisema Musiba.

Katika ziara yake hiyo ya kujitambulisha, Musiba ambaye ni mzaliwa wa Iramba Mwibara alikumbana na adha mbali mbali ikiwa ni pamoja na kukwama mara kadhaa kwa gari lake alilokuwa akilitumia kutokana na barabara kuwa mbovu zisizopitika.

Mbali na Mtangazaji huyo wa Channel Ten, Musiba kutangaza kugombea ubunge wa Mwibara, watu wengine waliotangaza kugombea ubunge wa jimbo hilo kupitia CCM ni pamoja na mbunge wa sasa anayemaliza muda wake, Kajege na Rubola Kange ambaye amewahi kugombea chaguzi tatu zilizopita mfululizo anashindwa.

Kulingana na hali hiyo, Tanzania Daima imeshuhudia siasa chafu jimboni Mwibara, kwani baadhi ya wagombea wa jimbo hilo (majina tunayo), wameanza kutembeza rushwa ya fedha kwa wananchi, kwa lengo la kuwashawishi wawachague.

Akizungumzia suala la afya jimboni humo, Musiba alisema wanawake wengi wakiwemo wajawazito na watoto wamekuwa wakitembea umbali mrefu kufuata huduma ya afya katika hospitali ya binafsi ya Mission, hivyo baadhi yao hupoteza maisha yao ovyo.

Aidha, aliwasihi wanaCCM wenzake kuwapima kwa sera wagombea wote wa ubunge jimboni humo, yupi mwenye sera nzuri na anayewafaa na yupi asiyewafaa kisha kuchagua kiongozi bora na siyo bora kiongozi.

SOURCE:https://musiba4mwibara.wordpress.com/2010/04/15/musiba-ajitosa-ubunge-mwibara/

MYTAKE: CCM wana haki zote kumjadili vikao vya CCM
Kwani mtu hawezi kutoka mkuu. Unatoa povu kubwa kwa kitu kidogo tu. Mbona mimi nilikuwa ccm lakini kwa sasa sipo
 
Musiba ajitosa ubunge Mwibara



MCHAKAMCHAKA wa uchaguzi Mkuu ujao, umeanza kuchukua sura mpya katika Jimbo la Mwibara Wilaya ya Bunda Mkoani Mara, baada ya Mwandishi wa habari na Mtangazaji mwandamizi wa Televisheni ya Channel Ten, Cyprian Musibaambaye ametangaza kugombea Ubunge wa jimbo hilo kupitia CCM, kuonekana kukubalika zaidi jimboni humo.

Musiba ambaye ni kijana, wiki iliyopita alizuru katika jimbo hilo la Mwibara kwa lengo la kujitambulisha na kutangaza nia yake ya kugombea ubunge wa jimbo hilo, alipokelewa kifalme na watu wa wengi wa rika zote kila alipokuwa akienda kujitambulisha kwake.

Akizungumza kwa nyakati tofauti na wanachama wa CCM katika vijiji vya vya Karukekere, Chingurubila, Mugara, Mwiruruma, Sikiro, Igundu, Muranda na Buramba, Musiba alisema ameamua kugombea ubunge katika jimbo hilo, ili kuwakomboa wananchi kimaendeleo, kwani jimbo hilo lipo nyuma zaidi kimaendeleo huenda kuliko majimbo yote nchini.

Alisema, tangu nchi ipate Uhuru hadi sasa, wananchi wa Mwibara bado wanapata shida kubwa sana katika suala zima la maendeleo, kwani barabara zilizopo hazipitiki kirahisi, huduma za afya mbovu jambo ambalo inaonekana wananchi kutelekezwa.

Jimbo la Mwibara hivi sasa linawakilishwa na mbunge anayemaliza muda wake, John Kajege (CCM), ambaye amekuwa akilalamikiwa na wananchi wengi wa jimbo hilo kwa madai ya kushindwa kutekeleza ahadi alizowaahidi, hivyo anakabiliwa na hali ngumu zaidi.

Kutokana na hilo, Musiba ambaye anaonekana kukubalika kwa wananchi wa jimbo hilo kwa asilimia kubwa, alisema iwapo atateuliwa na chama chake kugombea nafasi hiyo na hatimaye kushinda atahakikisha anaboresha barabara, afya, elimu, huduma ya maji pamoja na kujenga ofisi za CCM kila tawi na Kata.

Lengo jingine ni pamoja kujenga ushawishi mkubwa kwa wafadhili na wawekezaji kujenga viwanda vya samaki Mwibara, huduma za kibenki kusogezwa pamoja na kuimarisha ushirikiano kati yake na wananchi wa rika zote jimboni humo.

“Tangu uhuru Mwibara haina hospitali ya jimbo, barabara mbovu, huduma za afya nazo mbovu, wananchi wanakunywa maji machafu wakati Ziwa tunalo ubavuni hapa! Nikiwa mbunge wenu matatizo yote haya nitayatatua kwa haraka sana”, alisema Musiba.

Katika ziara yake hiyo ya kujitambulisha, Musiba ambaye ni mzaliwa wa Iramba Mwibara alikumbana na adha mbali mbali ikiwa ni pamoja na kukwama mara kadhaa kwa gari lake alilokuwa akilitumia kutokana na barabara kuwa mbovu zisizopitika.

Mbali na Mtangazaji huyo wa Channel Ten, Musiba kutangaza kugombea ubunge wa Mwibara, watu wengine waliotangaza kugombea ubunge wa jimbo hilo kupitia CCM ni pamoja na mbunge wa sasa anayemaliza muda wake, Kajege na Rubola Kange ambaye amewahi kugombea chaguzi tatu zilizopita mfululizo anashindwa.

Kulingana na hali hiyo, Tanzania Daima imeshuhudia siasa chafu jimboni Mwibara, kwani baadhi ya wagombea wa jimbo hilo (majina tunayo), wameanza kutembeza rushwa ya fedha kwa wananchi, kwa lengo la kuwashawishi wawachague.

Akizungumzia suala la afya jimboni humo, Musiba alisema wanawake wengi wakiwemo wajawazito na watoto wamekuwa wakitembea umbali mrefu kufuata huduma ya afya katika hospitali ya binafsi ya Mission, hivyo baadhi yao hupoteza maisha yao ovyo.

Aidha, aliwasihi wanaCCM wenzake kuwapima kwa sera wagombea wote wa ubunge jimboni humo, yupi mwenye sera nzuri na anayewafaa na yupi asiyewafaa kisha kuchagua kiongozi bora na siyo bora kiongozi.

SOURCE:https://musiba4mwibara.wordpress.com/2010/04/15/musiba-ajitosa-ubunge-mwibara/

MYTAKE: CCM wana haki zote kumjadili vikao vya CCM
Anaweza kuwa alikuwa mwanachama wakati huo, je sasa ni mwanachama?
 
Hata nyarando miaka hiyo alikuwa CCM, lowassa alikuwa CCM akaondoka sasa amerudi, n.k. pointi hapa ni kwamba hata angekuwa CCM bado ni mtu mdogo sana wa kujadiliwa ngazi ya CCM taifa
hakuna anayetaka kumjadili huyo fisi maji bali kamati ya maadili ya CCM itamuhitaji atoe ushahidi juu ya tuhuma za uasi alizotoa kwa wazee wa CCM.
 
Wewe hangaika na mambo ya chadema chama chako ya CCM Tuachie wenyewe.Mwende mkajadiliane uchaguzi mkuu wa chadema mtafanya lini kwani muda wa kikatiba ulishapita kitambo msije futiwa chama mkapiga yowe.
Hahaha chadema hata siwaelewi, why waitetee ccm?!
 
Kumbe huyu ana kila sifa ya kuitwa MCHOCHEZI maana anasema hana chama..anawaanika viongozi na in chanzo cha mgogoro wote huu
Itashnagaza asipo wekwa korokoroni
 
Musiba ajitosa ubunge Mwibara



MCHAKAMCHAKA wa uchaguzi Mkuu ujao, umeanza kuchukua sura mpya katika Jimbo la Mwibara Wilaya ya Bunda Mkoani Mara, baada ya Mwandishi wa habari na Mtangazaji mwandamizi wa Televisheni ya Channel Ten, Cyprian Musibaambaye ametangaza kugombea Ubunge wa jimbo hilo kupitia CCM, kuonekana kukubalika zaidi jimboni humo.

Musiba ambaye ni kijana, wiki iliyopita alizuru katika jimbo hilo la Mwibara kwa lengo la kujitambulisha na kutangaza nia yake ya kugombea ubunge wa jimbo hilo, alipokelewa kifalme na watu wa wengi wa rika zote kila alipokuwa akienda kujitambulisha kwake.

Akizungumza kwa nyakati tofauti na wanachama wa CCM katika vijiji vya vya Karukekere, Chingurubila, Mugara, Mwiruruma, Sikiro, Igundu, Muranda na Buramba, Musiba alisema ameamua kugombea ubunge katika jimbo hilo, ili kuwakomboa wananchi kimaendeleo, kwani jimbo hilo lipo nyuma zaidi kimaendeleo huenda kuliko majimbo yote nchini.

Alisema, tangu nchi ipate Uhuru hadi sasa, wananchi wa Mwibara bado wanapata shida kubwa sana katika suala zima la maendeleo, kwani barabara zilizopo hazipitiki kirahisi, huduma za afya mbovu jambo ambalo inaonekana wananchi kutelekezwa.

Jimbo la Mwibara hivi sasa linawakilishwa na mbunge anayemaliza muda wake, John Kajege (CCM), ambaye amekuwa akilalamikiwa na wananchi wengi wa jimbo hilo kwa madai ya kushindwa kutekeleza ahadi alizowaahidi, hivyo anakabiliwa na hali ngumu zaidi.

Kutokana na hilo, Musiba ambaye anaonekana kukubalika kwa wananchi wa jimbo hilo kwa asilimia kubwa, alisema iwapo atateuliwa na chama chake kugombea nafasi hiyo na hatimaye kushinda atahakikisha anaboresha barabara, afya, elimu, huduma ya maji pamoja na kujenga ofisi za CCM kila tawi na Kata.

Lengo jingine ni pamoja kujenga ushawishi mkubwa kwa wafadhili na wawekezaji kujenga viwanda vya samaki Mwibara, huduma za kibenki kusogezwa pamoja na kuimarisha ushirikiano kati yake na wananchi wa rika zote jimboni humo.

“Tangu uhuru Mwibara haina hospitali ya jimbo, barabara mbovu, huduma za afya nazo mbovu, wananchi wanakunywa maji machafu wakati Ziwa tunalo ubavuni hapa! Nikiwa mbunge wenu matatizo yote haya nitayatatua kwa haraka sana”, alisema Musiba.

Katika ziara yake hiyo ya kujitambulisha, Musiba ambaye ni mzaliwa wa Iramba Mwibara alikumbana na adha mbali mbali ikiwa ni pamoja na kukwama mara kadhaa kwa gari lake alilokuwa akilitumia kutokana na barabara kuwa mbovu zisizopitika.

Mbali na Mtangazaji huyo wa Channel Ten, Musiba kutangaza kugombea ubunge wa Mwibara, watu wengine waliotangaza kugombea ubunge wa jimbo hilo kupitia CCM ni pamoja na mbunge wa sasa anayemaliza muda wake, Kajege na Rubola Kange ambaye amewahi kugombea chaguzi tatu zilizopita mfululizo anashindwa.

Kulingana na hali hiyo, Tanzania Daima imeshuhudia siasa chafu jimboni Mwibara, kwani baadhi ya wagombea wa jimbo hilo (majina tunayo), wameanza kutembeza rushwa ya fedha kwa wananchi, kwa lengo la kuwashawishi wawachague.

Akizungumzia suala la afya jimboni humo, Musiba alisema wanawake wengi wakiwemo wajawazito na watoto wamekuwa wakitembea umbali mrefu kufuata huduma ya afya katika hospitali ya binafsi ya Mission, hivyo baadhi yao hupoteza maisha yao ovyo.

Aidha, aliwasihi wanaCCM wenzake kuwapima kwa sera wagombea wote wa ubunge jimboni humo, yupi mwenye sera nzuri na anayewafaa na yupi asiyewafaa kisha kuchagua kiongozi bora na siyo bora kiongozi.

SOURCE:https://musiba4mwibara.wordpress.com/2010/04/15/musiba-ajitosa-ubunge-mwibara/

MYTAKE: CCM wana haki zote kumjadili vikao vya CCM
Kwani wapi kakanusha kuwa siyo mwanachama? Mbona hata Membe analijua hilo sijui lengo la huu uzi ni lipi
 
Wewe hangaika na mambo ya chadema chama chako ya CCM Tuachie wenyewe.Mwende mkajadiliane uchaguzi mkuu wa chadema mtafanya lini kwani muda wa kikatiba ulishapita kitambo msije futiwa chama mkapiga yowe.
Kiswahili ni lugha ya taifa Musiba anasema yeye siyo msemaji wa serikali wala ccm hajasema siyo mwanachama wa ccm
 
Back
Top Bottom