Museveni alarmed by human capital flight

Mishahara ya kufuru? Hiyo mnayogombea na waheshimiwa wabunge!Wewe ndugu yangu uliye nje nilieze mshahara gani na marupurupu ambao unaona utakuridhisha kurudi nyumbani? Ambao hiyo nchi yenye GDP/capita haifiki $300 kwa mwaka itaweza kukupa? Nani amesema anataka aimbiwe ngonjera? Kwangu mimi kuthaminiwa ni kupewa nafasi ya kufanya kazi kadri ya uwezo wangu bila kuingiliwa na mtu,ushauri wangu kuthaminiwa kama mtaalam, kupatiwa mazingira mazuri ya kufanyia kazi,kujua nikifanya kazi vyema nipanda hadi hapo nitakapostaili, n.k. Kwa kukazania mshahara peke yake hatutafika mbali.
Mheshmiwa Koba, huyo ndugu yako aliye planning officer huko mkoani angepewa mshahara mzuri, mazingira mzuri ya kufanya na kufanya kazi aliyoisomea sidhani kama angelalamika! Tunachofanya ni kumfrustrate mpaka nae ataona heri aende watakomthamini. Ninachosema serikali badala ya kutubembeleza sisi tulio nje iwaangalie hao walioko nyumbani kwanza.
Wako waliorudi kutokana na wito wa Rais Ali Hassan Mwinyi. Wengine walikuwa matapeli, wakagundulika na sasa hawapo tena kwenye ajira. Wengine nadhani mazingira yaliwashinda. Wengine waliorudi baadae ndio hao tunawasemea vibaya leo.
Kuna ndugu mmoja alizungumzia wananchi wanaotembea kwa mguu kutoka Kimara kwa vile hawana nauli! sasa kwa taarifa yako hawa ndio wenye bahati. Nenda huko vijijini ukaone maisha wanaoishi watanzania wenzako halafu uniambie kama hawa hawataona hiyo mishahara mnayogombeana si kufuru. Watu wanapata kichaa kwa shilingi 80,000 wakati sisi tunazungumzia ka laki 3! Ah, nimesahau, walikimbia umande!
 
Hivi sasa Tanzania inawalipa engineers kwenye consultancies kutoka nje ya nchi mishahara ya kati ya $10 000 hadi $20 000 ambapo kodi imesamehewa pamoja na magari ya kifahari na nyumba bure. Sasa kwa nini wasiweze kumlipa mzawa kiwango kama hicho na analipa kodi?

Hii danganya toto ya kila siku kwamba hatuna uwezo umepitwa na wakati, tungekuwa hatuna uwezo wa kulipa mishahara hiyo kusingekuwa na exparts wanaokuja Tanzania. Madaktari, wataalamu ambao wamebobea katika fani nyingi wapo nje kwa sababu hawawezi kulipwa vizuri nyumbani. Wataalamu wa madini wapo tele bongo lakini wanalipwa kiduchu na haya makampuni uchwara etc.
 
Hivi sasa Tanzania inawalipa engineers kwenye consultancies kutoka nje ya nchi mishahara ya kati ya $10 000 hadi $20 000 ambapo kodi imesamehewa pamoja na magari ya kifahari na nyumba bure. Sasa kwa nini wasiweze kumlipa mzawa kiwango kama hicho na analipa kodi?

Hii danganya toto ya kila siku kwamba hatuna uwezo umepitwa na wakati, tungekuwa hatuna uwezo wa kulipa mishahara hiyo kusingekuwa na exparts wanaokuja Tanzania. Madaktari, wataalamu ambao wamebobea katika fani nyingi wapo nje kwa sababu hawawezi kulipwa vizuri nyumbani. Wataalamu wa madini wapo tele bongo lakini wanalipwa kiduchu na haya makampuni uchwara etc.

Hiyo mishahara inatokana na mikataba tunayoingia na hao tunaowaita wahisani. Hizo $10,000 hadi $ 20,000 (?) inakuwa katika hiyo misaada(?) tunayopewa. Kama ni consultant firm (Cowi, Howard Humphreys n.k) hiyo mishahara ni kutokana na mapato yao. George Ali akiamua kuwalipa wahandisi wake $10,000 nae tutamlaumu?
Hao madaktari walio nje si mishahara tu iliyowakimbiza. Hivi mnaamini kweli nchi ya Tanzania inaweza kuwalipa wataalam wake wote hizo Benjamin mnazoshupalia? Nchi ya watu milioni 35 na yenye kupata mapato yasiyozidi $billioni moja kwa mwaka kutokana na exports zake. Linganisha na kipato cha mauritius yenye watu milioni moja. Tusigombee ulaji tu. Tuangalie namna gani ya kuhakikisha kuwa tunatoka katika hili dimbwi la umasikini! Na hii ndio maana inabidi tuwe wakali pale tunapoona hata hiki kidogo kinachukuliwa na wajanja. Na sio kudai ati na sisi tugaiwe sehemu ya hicho kiduchu bila kuwaangalia walio nyuma yetu. Hatutafika mbali kwa mwendo huo.
Ya hao wataalamu wa madini siyajui, isipokuwa katika fani yeyote uzoefu unathaminiwa kama vile ambavyo elimu inathaminiwa. Kuwa na digrii peke yake haitoshi. Inabidi uthibitishe kuwa unaweza kweli kutumia elimu yako. Sasa hayo machimbo yameanza hivi karibuni, hao wataalamu wetu wamepata wapi uo utalaamu wa kwenye migodi?
 
Hiyo mishahara inatokana na mikataba tunayoingia na hao tunaowaita wahisani. Hizo $10,000 hadi $ 20,000 (?) inakuwa katika hiyo misaada(?) tunayopewa. Kama ni consultant firm (Cowi, Howard Humphreys n.k) hiyo mishahara ni kutokana na mapato yao. George Ali akiamua kuwalipa wahandisi wake $10,000 nae tutamlaumu?
Hao madaktari walio nje si mishahara tu iliyowakimbiza. Hivi mnaamini kweli nchi ya Tanzania inaweza kuwalipa wataalam wake wote hizo Benjamin mnazoshupalia? Nchi ya watu milioni 35 na yenye kupata mapato yasiyozidi $billioni moja kwa mwaka kutokana na exports zake. Linganisha na kipato cha mauritius yenye watu milioni moja. Tusigombee ulaji tu. Tuangalie namna gani ya kuhakikisha kuwa tunatoka katika hili dimbwi la umasikini! Na hii ndio maana inabidi tuwe wakali pale tunapoona hata hiki kidogo kinachukuliwa na wajanja. Na sio kudai ati na sisi tugaiwe sehemu ya hicho kiduchu bila kuwaangalia walio nyuma yetu. Hatutafika mbali kwa mwendo huo.
Ya hao wataalamu wa madini siyajui, isipokuwa katika fani yeyote uzoefu unathaminiwa kama vile ambavyo elimu inathaminiwa. Kuwa na digrii peke yake haitoshi. Inabidi uthibitishe kuwa unaweza kweli kutumia elimu yako. Sasa hayo machimbo yameanza hivi karibuni, hao wataalamu wetu wamepata wapi uo utalaamu wa kwenye migodi?

Politics na longolongo kibao..

ingekuwa maendeleo ya nchi yanatokana na namna ya kujieleza basi wabongo tungekuwa dunia ya Kwanza!
 
Hiyo mishahara inatokana na mikataba tunayoingia na hao tunaowaita wahisani. Hizo $10,000 hadi $ 20,000 (?) inakuwa katika hiyo misaada(?) tunayopewa. Kama ni consultant firm (Cowi, Howard Humphreys n.k) hiyo mishahara ni kutokana na mapato yao. George Ali akiamua kuwalipa wahandisi wake $10,000 nae tutamlaumu?
Hao madaktari walio nje si mishahara tu iliyowakimbiza. Hivi mnaamini kweli nchi ya Tanzania inaweza kuwalipa wataalam wake wote hizo Benjamin mnazoshupalia? Nchi ya watu milioni 35 na yenye kupata mapato yasiyozidi $billioni moja kwa mwaka kutokana na exports zake. Linganisha na kipato cha mauritius yenye watu milioni moja. Tusigombee ulaji tu. Tuangalie namna gani ya kuhakikisha kuwa tunatoka katika hili dimbwi la umasikini! Na hii ndio maana inabidi tuwe wakali pale tunapoona hata hiki kidogo kinachukuliwa na wajanja. Na sio kudai ati na sisi tugaiwe sehemu ya hicho kiduchu bila kuwaangalia walio nyuma yetu. Hatutafika mbali kwa mwendo huo.
Ya hao wataalamu wa madini siyajui, isipokuwa katika fani yeyote uzoefu unathaminiwa kama vile ambavyo elimu inathaminiwa. Kuwa na digrii peke yake haitoshi. Inabidi uthibitishe kuwa unaweza kweli kutumia elimu yako. Sasa hayo machimbo yameanza hivi karibuni, hao wataalamu wetu wamepata wapi uo utalaamu wa kwenye migodi?

Na hao wabunge wanaolipwa mishahara na marupurupu mazuri kwa kukutana kwa siku zisizozidi 90 kwa mwaka waliingia mktaba na nani? Je serikali haiwezi kuingia mkataba na wafanyakazi nao wakalipwa vizuri? Inakuwaje nchi kama Namibia, Botswana ziweze kuwalipa vizuri wataalamu wetu wakati Tanzania inashindwa kufanya hivyo!? Botswana na Namibia wametuzidi nini!?
 
Musevi anasema nini?

Watu kama yeye ndio wamechangia wasomi wakimbie!Ni uongozi mbaya .Angalia amin,obote waliua watu wangapi.Museven huyo naye hataki kuacha madaraka!
 
Fundi mchundo said:
Hiyo mishahara inatokana na mikataba tunayoingia na hao tunaowaita wahisani. Hizo $10,000 hadi $ 20,000 (?) inakuwa katika hiyo misaada(?) tunayopewa. Kama ni consultant firm (Cowi, Howard Humphreys n.k) hiyo mishahara ni kutokana na mapato yao. George Ali akiamua kuwalipa wahandisi wake $10,000 nae tutamlaumu?

Hivi unaamini kwa nafsi yako kabisa hayo ni mapato yao? Kwa nini wasiende kufanya kazi huko kwao walipane bila kutupatia sisi longo longo. Tanzania tumekuwa conduit ya kunyonywa na hawa vibaka. Leo hii Japan akitoa msaada wa kujenga barabara anafahamu jinsi tusivyo na akili kwani tutanunua magari mikweche ambayo hana sababu ya kuwa nayo na ataweza kuingiza pesa nyingi kwa njia hiyo bila sisi wenyewe kujua nini kinaendelea. Hatuhitaji hii misaada ambayo inatafunwa na wenye meno makali, rejea import support pesa zilivyotafunwa BOT.

Fundi mchundo said:
Hao madaktari walio nje si mishahara tu iliyowakimbiza. Hivi mnaamini kweli nchi ya Tanzania inaweza kuwalipa wataalam wake wote hizo Benjamin mnazoshupalia? Nchi ya watu milioni 35 na yenye kupata mapato yasiyozidi $billioni moja kwa mwaka kutokana na exports zake. Linganisha na kipato cha mauritius yenye watu milioni moja. Tusigombee ulaji tu. Tuangalie namna gani ya kuhakikisha kuwa tunatoka katika hili dimbwi la umasikini! Na hii ndio maana inabidi tuwe wakali pale tunapoona hata hiki kidogo kinachukuliwa na wajanja. Na sio kudai ati na sisi tugaiwe sehemu ya hicho kiduchu bila kuwaangalia walio nyuma yetu. Hatutafika mbali kwa mwendo huo.

Sasa wewe unapenda jinsi WTZ wanavyokufa kama inzi pale Muhimbili wakati viongozi pekee ndio hawaishi kwenda kujipima kila mwaka kwa pesa ya walipa kodi? Gharama hiyo ni lazima ilipwe hakuna cha bure ndio sababu tunapiga kelele hapa kwamba tunaibiwa hadi rasilimali zetu kwa bei ya peremende. Hivi hujiulizi kwa nini mashangingi yamejaa TZ kuliko hata miji kama LA na sehemu nyinginezo? Ujinga umewatawala viongozi wetu kwa majibu mepesi ambayo yanahitaji majibu magumu. Huwezi kukwepa gharama ni lazima uongeze export au ufe uchaguzi ni wako. Tuachane na misaada na tuweze kuchangia bajeti yetu sisi wenyewe.

Fundi mchundo said:
Ya hao wataalamu wa madini siyajui, isipokuwa katika fani yeyote uzoefu unathaminiwa kama vile ambavyo elimu inathaminiwa. Kuwa na digrii peke yake haitoshi. Inabidi uthibitishe kuwa unaweza kweli kutumia elimu yako. Sasa hayo machimbo yameanza hivi karibuni, hao wataalamu wetu wamepata wapi uo utalaamu wa kwenye migodi?

Kwa taarifa yako WTZ wengi sana walisomea pale chuo cha madini Dodoma wakati wa enzi zile, hicho chuo kama sikosei kilijengwa na wajerumani (natumaini unaifahamu historia vizuri waliondoka lini) wengi wao wanafanya kazi nje ya Tanzania unaweza kuwapata Botswana, Norway, South Africa na nchi nyinginezo hata hivi sasa ukienda Bulyanhulu wapo wabongo wenye sifa kuliko hao wakubwa wao ambao waliletwa kuwa ndio wajuzi. WTZ hawakuacha kusoma geology ni mchepuo ambao uko kwenye Civil engineering (baadaye una-specialize) sasa hili la kusema tumeanza leo sijui linatoka wapi pengine wewe unafikiria kwa sababu madini yameuzwa kinyemela juzi juzi ndio tumeanza kusomesha. Mwalimu alisema ni bora tuyaache huko huko chini hadi wabongo wawe na akili lakini vibaka wameingia ni jukumu letu kuwasafisha.
 
Hivi unaamini kwa nafsi yako kabisa hayo ni mapato yao? Kwa nini wasiende kufanya kazi huko kwao walipane bila kutupatia sisi longo longo. Tanzania tumekuwa conduit ya kunyonywa na hawa vibaka. Leo hii Japan akitoa msaada wa kujenga barabara anafahamu jinsi tusivyo na akili kwani tutanunua magari mikweche ambayo hana sababu ya kuwa nayo na ataweza kuingiza pesa nyingi kwa njia hiyo bila sisi wenyewe kujua nini kinaendelea. Hatuhitaji hii misaada ambayo inatafunwa na wenye meno makali, rejea import support pesa zilivyotafunwa BOT.

Sasa nadhani Mheshimiwa Duwa unakosea. Kampuni ya CowiCosult, Howard Humphrey ni kama kampuni yeyote inayofanya biashara.
apato yanatokana na kazi za ushauri wanazofanya. Kama Tan Consult na nyingizeyo. Hawa wote, wanalipana kutokana na kazi wanazozifanya. Sasa leo unataka tukawaingilie hata wanavyolipana? Na kwa taarifa yako humo humo wako watanzania ambao ni maboss. Makampuni mengine ya kigeni kama CarlBro, yalishindwa biashara wakafunga ofisi wakaondoka. Hao maengineer unaowazungumzia wanakuja kama technical support, ambao wanaunganishwa katika hiyo misaada tunayoomba. Dawa ni kutoomba misaada! tunaweza hilo? na ni busara?
Hizo pesa za import support si tulishirikiana kuzitafuna?


Sasa wewe unapenda jinsi WTZ wanavyokufa kama inzi pale Muhimbili wakati viongozi pekee ndio hawaishi kwenda kujipima kila mwaka kwa pesa ya walipa kodi? Gharama hiyo ni lazima ilipwe hakuna cha bure ndio sababu tunapiga kelele hapa kwamba tunaibiwa hadi rasilimali zetu kwa bei ya peremende. Hivi hujiulizi kwa nini mashangingi yamejaa TZ kuliko hata miji kama LA na sehemu nyinginezo? Ujinga umewatawala viongozi wetu kwa majibu mepesi ambayo yanahitaji majibu magumu. Huwezi kukwepa gharama ni lazima uongeze export au ufe uchaguzi ni wako. Tuachane na misaada na tuweze kuchangia bajeti yetu sisi wenyewe.
Nani aliesema mimi nafurahia kufa kwa wagonjwa wetu pale Muhimbili? Ninachokata ni majibu ya kirahisi kutoka kwenu ati tukiuza mashangangi dawa zitamiminika mahospitalini!Nakubaliana na wewe kuwa hizo rasilimali tunazoibiwa ni lazima tukemee kwa juhudi zetu zote. Haya niambie, wewe mtaalam, tutaongeza vipi hizo export? Kwa kuuza korosho?
Kwa taarifa yako WTZ wengi sana walisomea pale chuo cha madini Dodoma wakati wa enzi zile, hicho chuo kama sikosei kilijengwa na wajerumani (natumaini unaifahamu historia vizuri waliondoka lini) wengi wao wanafanya kazi nje ya Tanzania unaweza kuwapata Botswana, Norway, South Africa na nchi nyinginezo hata hivi sasa ukienda Bulyanhulu wapo wabongo wenye sifa kuliko hao wakubwa wao ambao waliletwa kuwa ndio wajuzi. WTZ hawakuacha kusoma geology ni mchepuo ambao uko kwenye Civil engineering (baadaye una-specialize) sasa hili la kusema tumeanza leo sijui linatoka wapi pengine wewe unafikiria kwa sababu madini yameuzwa kinyemela juzi juzi ndio tumeanza kusomesha. Mwalimu alisema ni bora tuyaache huko huko chini hadi wabongo wawe na akili lakini vibaka wameingia ni jukumu letu kuwasafisha.
Chuo cha madini Dodoma hakifundishi utaalamu wa kuchimba madini. Wanafundisha utaalam wa kutafuta madini. Geology haimo kwenye Civil engineering, ni fani pekee.Wataalamu wa vitabu tuko wengi lakini nasisitiza kuwa utaalam wa nadharia nao ni muhimu. Hii kuheshimu mno makaratasi kwa upande ndio kumetufikisha hapa tulipo. Angalia wenye Ph.D na maprofesa wanavyohema katika kuongoza. Academics ni kitu kingine na uongozi kitu kingine.
 
Na hao wabunge wanaolipwa mishahara na marupurupu mazuri kwa kukutana kwa siku zisizozidi 90 kwa mwaka waliingia mktaba na nani? Je serikali haiwezi kuingia mkataba na wafanyakazi nao wakalipwa vizuri? Inakuwaje nchi kama Namibia, Botswana ziweze kuwalipa vizuri wataalamu wetu wakati Tanzania inashindwa kufanya hivyo!? Botswana na Namibia wametuzidi nini!?

Kwa haraka haraka:
Human Development Index 2006:
Namibia 125
Botswana 131
Tanzania 162

Population
Namibia 2,009,000
Botswana 1,800,000
Tanzania 37,627,800

GDP
Namibia US$ 5.7 billion
BotswanaUS$ 9.0 billion
Tanzania US$ 10.9 billion

GDP/Capita (PPP US$) 2004
Namibia 7,418
Botswana 9,946
Tanzania 674

GDP/Capita (US $)
Namibia 2,843
Botswana 5,073
Tanzania 288

Under 5 Infant Mortality Rate per 1000 live births
Namibia 63
Botswana 84
Tanzania 126

Sasa bado unataka kujua wametuzidi nini? Tukubali umasikini wetu, tupambane nao ili tufike huko waliko wenzetu. Na hizi sio nchi zilizoendelea! Nenda kwenye site ya Human Development Report ya UNDP halafu linganisha nchi yako na vinchi kama Mauritius!

Hao wabunge ni sehemu ngapi ya watanzania 37 millioni? Nakubali kabisa kuwa mishahara wanayolipana ni aibu tupu na inastahili kukemewa! Lakini si kwa kusema na sisi tunataka hiyo hiyo! Tutawaua wenzetu.
 
Asante Mzalendo!
Hivi nimeenda kasi mno? samahani kama nimewaudhi walionitangulia! Sikukusudia hivyo.Nilitaka tu kukumbushia hali halisi ilivyo. Nitajirekebisha, Mkuu.
 
Fundi Mchundo

Chuo cha madini Dodoma hakifundishi utaalamu wa kuchimba madini. Wanafundisha utaalam wa kutafuta madini. Geology haimo kwenye Civil engineering, ni fani pekee.Wataalamu wa vitabu tuko wengi lakini nasisitiza kuwa utaalam wa nadharia nao ni muhimu. Hii kuheshimu mno makaratasi kwa upande ndio kumetufikisha hapa tulipo. Angalia wenye Ph.D na maprofesa wanavyohema katika kuongoza. Academics ni kitu kingine na uongozi kitu kingine.
Ni wapi nimesema hicho chuo kinafundisha utaalamu wa kuchimba madini?

Labda hufahamu geology inafundishwa kwenye Civil engineering kama somo pamoja na geotechnics na baada ya kumaliza ndio unafanya specialization. (muulize Civil engineer yoyote atakwambia) Siku hizi wameiweka kwenye kozi inayoitwa Earth Science and Engineering lakini ina uhusiano mkubwa na Civil Engineering kama huelewi hilo siwezi kueleza zaidi ya hapo.
 
Politics na longolongo kibao..

ingekuwa maendeleo ya nchi yanatokana na namna ya kujieleza basi wabongo tungekuwa dunia ya Kwanza!

Mwafrika wa kike uishie Marekani! Longolongo iko wapi? Kwamba nchi yetu ni masikini? Politics ziko wapi? Nimempigia debe nani? Tumezoea majibu ya haraka haraka ya kufurahisha jamii. Kweli watanzania tunapenda sana siasa ( angalia wanaosoma thread hizi). Basi nyinyi ambao mnavipata hivi vitu kwa vile mko kwenye neema, tufahamisheni tutafikaje kwenye hiyo dunia ya kwanza!
 
Fundi Mchundo


Ni wapi nimesema hicho chuo kinafundisha utaalamu wa kuchimba madini?

Labda hufahamu geology inafundishwa kwenye Civil engineering kama somo pamoja na geotechnics na baada ya kumaliza ndio unafanya specialization. (muulize Civil engineer yoyote atakwambia) Siku hizi wameiweka kwenye kozi inayoitwa Earth Science and Engineering lakini ina uhusiano mkubwa na Civil Engineering kama huelewi hilo siwezi kueleza zaidi ya hapo.

Kama hawafundishi utaalam wa kuchimba madini mbona unawalaumu wenye migodi kwa kutowaajiri. Au pengine kuna kazi nyingine wanayoweza kufanya kwenye hio migodi?

Mheshimiwa, unajuaje kuwa mimi sio Civil engineer? Kusoma geology kama basic studies hakuwafanyi kuwa geologists. Ukimaliza digrii ya kwanza unaweza kuspecialise kwenye structures, civil, traffic(?) engineering n.k.Geo tech. engineering ni fani inayochunguza uwezo wa udongo kuhimili uzito juu yake, kama majengo, barabara na civil works nyingine. Kama nimekosea basi nifahamishwe.
 
Fundi Mchundo

Nafikiri una haja ya kuangalia ninachoandika bila kukurupuka. Nimekuuliza 'ni wapi niliposema chuo cha Dodoma kinafundisha utaalamu wa kuchimba madini? Hukuja na jibu na sasa unakuja na ngonjera nyingine kwamba nawalaumu wenye migodi kwa kutowaajiri, wapi hapo unaweza kunionyesha?

Sasa kama wewe ni Civil Engineer ilikuwaje ukasema 'Geology haimo kwenye Civil engineering?' Hivi kama hufahamu swali ni bora kuuliza kuliko kukurupuka. Huwezi kuwa Geologist bila kuelewa Geophysics na core geology foundation.
Mwenyewe unakiri hapo juu kwamba wanasoma as a basic sasa kama halina umuhimu kwa nini walisome? Unakula matapishi yako sasa.
 
....jidanganye tuu,this guy went to LSE then home tena serikalini kapangiwa planning officer mkoani,kilichotokea baada ya hapo God knows!

Sasa na nyie watu, kama wote tunasema hatutaki kwenda kuwa planning officer kisa tumesoma LSE, nani ataendeleza hiyo nchi? Halafu sisi hatutaki hizo kazi, wakishika nafasi vilaza wanavurunda tunaanza kulalamika tena wakati sisi hatutaki kufanya hizo kazi! Hivi, haya maisha tunayoyafaida ya wazungu inabidi tujue kwamba kuna watu waliyahangaikia kipindi fulani, hayakushushwa mbinguni! Tunawajibika kuboresha maisha home ili vizazi vijavyo vije vifaidi kama sisi tunavyofaidi huku kwa wazungu. Tatizo letu wabongo/wafrika, tunataka tupande na kuvuna sasa hivi, katika hali ya kawaida haiwezekani!
 
Kwa haraka haraka:
Human Development Index 2006:
Namibia 125
Botswana 131
Tanzania 162

Population
Namibia 2,009,000
Botswana 1,800,000
Tanzania 37,627,800

GDP
Namibia US$ 5.7 billion
BotswanaUS$ 9.0 billion
Tanzania US$ 10.9 billion

GDP/Capita (PPP US$) 2004
Namibia 7,418
Botswana 9,946
Tanzania 674

GDP/Capita (US $)
Namibia 2,843
Botswana 5,073
Tanzania 288

Under 5 Infant Mortality Rate per 1000 live births
Namibia 63
Botswana 84
Tanzania 126

Sasa bado unataka kujua wametuzidi nini? Tukubali umasikini wetu, tupambane nao ili tufike huko waliko wenzetu. Na hizi sio nchi zilizoendelea! Nenda kwenye site ya Human Development Report ya UNDP halafu linganisha nchi yako na vinchi kama Mauritius!

Hao wabunge ni sehemu ngapi ya watanzania 37 millioni? Nakubali kabisa kuwa mishahara wanayolipana ni aibu tupu na inastahili kukemewa! Lakini si kwa kusema na sisi tunataka hiyo hiyo! Tutawaua wenzetu.

Usituletee longolongo lako hapa. Tanzania ina uwezo kabisa wa kulipa mishahara mizuri kwa wafanyakazi wake ili waweze kumudu gharama za maisha. Kuna savings chungu nzima ambazo zinaweza kufanywa ili kupunguza gharama za uendeshaji wa siri kali. Kwa mfano wanaostahili kuwa na magari ya siri kali ni watu wachache sana kama vile Rais, Waziri Mkuu labda na spika wabunge wengine wote wawe na magari yao binafsi na gharama za uendeshaji ziwe juu yao wenyewe. Hapa tutapunguza gharama chungu nzima. Mikataba kama ikiandikwa kwa kuwekwa mbele maslahi ya Taifa basi mapato ya Taifa yataongezeka kwa kiasi kikubwa sana haya pia yanaweza kuhakikisha ulipwaji wa mishahara mizuri kwa Watanzania.

Wimbo wako wa 'Tanzania nchi maskini umeshapitwa' na wakati ulikuwa unaimbwa mwaka 47 lakini sasa hivi haukubaliki tena. Nchi gani maskini ambayo viongozi wake wote wanatibiwa UK, US, SA, France, Germany, India!? Wakati huo huo wakiacha hospitali zetu zikiwa katika hali ya kutisha. Tuna rasilimali chungu nzima ambazo kama zikitumiwa vizuri pamoja na kuwa na population ya 39 million, tunaweza kabisa kuhakikisha maisha mazuri kwa kila Mtanzania. Lakini viongozi wamekuwa mafisadi, wizi, wanaopenda kujitajirisha kupitia nyadhifa zao. Leo hii kuna tofauti kubwa sana kati ya wenye nacho na wasiokuwa nacho. Inakuwaje watu wengine wana maisha kama ya wacheza sinema wa Hollywood wakati huo huo mamilioni ya Watanzania hawajui hata mlo wao mwingine wataupata wapi!?

Wewe kama unataka kuishi kwa shida basi ni wewe pekee yako, Watanzania wote na wao wanataka waone matunda ya elimu yao na kuajiriwa kwao kwa kulipwa mishahara inayoendana na gharama halisi za maisha siyo kuwalalia. Hakuna Mtanzania yeyote atakayekufa kwa kuwa na mishahara na marupurupu mazuri, labda utakufa wewe usiyetaka mshahara wa kufuru. Usipende kujishushia hadhi kaka (mie mshahara huu mkubwa sana, sistahili kuupata) :confused: , ukijidharau mwenyewe hapa duniani basi kila mtu atakudharau.
 
Sasa na nyie watu, kama wote tunasema hatutaki kwenda kuwa planning officer kisa tumesoma LSE, nani ataendeleza hiyo nchi? Halafu sisi hatutaki hizo kazi, wakishika nafasi vilaza wanavurunda tunaanza kulalamika tena wakati sisi hatutaki kufanya hizo kazi! Hivi, haya maisha tunayoyafaida ya wazungu inabidi tujue kwamba kuna watu waliyahangaikia kipindi fulani, hayakushushwa mbinguni! Tunawajibika kuboresha maisha home ili vizazi vijavyo vije vifaidi kama sisi tunavyofaidi huku kwa wazungu. Tatizo letu wabongo/wafrika, tunataka tupande na kuvuna sasa hivi, katika hali ya kawaida haiwezekani!


....haahaha hah it does make sense ulichoandika Kitila lakini reality ni kama usiku na mchana hapo.
 
Fundi Mchundo

Nafikiri una haja ya kuangalia ninachoandika bila kukurupuka. Nimekuuliza 'ni wapi niliposema chuo cha Dodoma kinafundisha utaalamu wa kuchimba madini? Hukuja na jibu na sasa unakuja na ngonjera nyingine kwamba nawalaumu wenye migodi kwa kutowaajiri, wapi hapo unaweza kunionyesha?

Sasa kama wewe ni Civil Engineer ilikuwaje ukasema 'Geology haimo kwenye Civil engineering?' Hivi kama hufahamu swali ni bora kuuliza kuliko kukurupuka. Huwezi kuwa Geologist bila kuelewa Geophysics na core geology foundation.
Mwenyewe unakiri hapo juu kwamba wanasoma as a basic sasa kama halina umuhimu kwa nini walisome? Unakula matapishi yako sasa.

Hivi unaamini kwa nafsi yako kabisa hayo ni mapato yao? Kwa nini wasiende kufanya kazi huko kwao walipane bila kutupatia sisi longo longo. Tanzania tumekuwa conduit ya kunyonywa na hawa vibaka. Leo hii Japan akitoa msaada wa kujenga barabara anafahamu jinsi tusivyo na akili kwani tutanunua magari mikweche ambayo hana sababu ya kuwa nayo na ataweza kuingiza pesa nyingi kwa njia hiyo bila sisi wenyewe kujua nini kinaendelea. Hatuhitaji hii misaada ambayo inatafunwa na wenye meno makali, rejea import support pesa zilivyotafunwa BOT.



Sasa wewe unapenda jinsi WTZ wanavyokufa kama inzi pale Muhimbili wakati viongozi pekee ndio hawaishi kwenda kujipima kila mwaka kwa pesa ya walipa kodi? Gharama hiyo ni lazima ilipwe hakuna cha bure ndio sababu tunapiga kelele hapa kwamba tunaibiwa hadi rasilimali zetu kwa bei ya peremende. Hivi hujiulizi kwa nini mashangingi yamejaa TZ kuliko hata miji kama LA na sehemu nyinginezo? Ujinga umewatawala viongozi wetu kwa majibu mepesi ambayo yanahitaji majibu magumu. Huwezi kukwepa gharama ni lazima uongeze export au ufe uchaguzi ni wako. Tuachane na misaada na tuweze kuchangia bajeti yetu sisi wenyewe.



Kwa taarifa yako WTZ wengi sana walisomea pale chuo cha madini Dodoma wakati wa enzi zile, hicho chuo kama sikosei kilijengwa na wajerumani (natumaini unaifahamu historia vizuri waliondoka lini) wengi wao wanafanya kazi nje ya Tanzania unaweza kuwapata Botswana, Norway, South Africa na nchi nyinginezo hata hivi sasa ukienda Bulyanhulu wapo wabongo wenye sifa kuliko hao wakubwa wao ambao waliletwa kuwa ndio wajuzi. WTZ hawakuacha kusoma geology ni mchepuo ambao uko kwenye Civil engineering (baadaye una-specialize) sasa hili la kusema tumeanza leo sijui linatoka wapi pengine wewe unafikiria kwa sababu madini yameuzwa kinyemela juzi juzi ndio tumeanza kusomesha. Mwalimu alisema ni bora tuyaache huko huko chini hadi wabongo wawe na akili lakini vibaka wameingia ni jukumu letu kuwasafisha.

Mimi nakiri si mzoefu wa debate. Ulipounganisha suala la chuo cha madini na Bulyankulu nikajua unazungumzia migodi!

Civil engineers wanasoma structural analysis and design, soil mechanics,hydraulics, geotech, transportation etc kama core subjects halafu wanachukua moja kama elective( si kuspecialise). Wanaspecialise katika post graduate stage ambapo kwa UDSM wanaweza kuchukua structural, construction technology and management, transportation and geotechnicalengineering, water resources management. Huwezi kuwa geologist kutokea kwenye civil engineering. Geotechnical engineering sio geology!

Hiyo migodi tunayozungumzia ya Bulyankulu n.k imeanza lini? Nisahihishe kama nimekosea lakini kwa uelewa wangu baada ya machimbo ya Mwadui hiyo ndiyo ilikuwa ya mwanzo. sasa hao wataalam wetu walipata wapi uzoefu kwenye migodi? Au ndio hao walitaka kurudi kutoka Botswana, Afrika Kusini, Norway lakini mishahara duni ikawashinda?

Hivi unaelewa vilevile mikataba ya consultancies inaendaje? Hivi unaelewa miradi inayoitwa donor supported inakuwa na vipengele gani?

Unasema dawa ni kuongeza export na kuacha kukubali misaada. Tufahamishe basi ni bidhaa gani tutakazoweza kuongeza kuexport ili zitosheleze bajeti yetu na kuweza kutuletea maendeleo yalio sustainable? Madini? Au hayo mafuta ambayo wajerumani waliyagundua wakatuficha?

Naona, mheshimiwa, unachotaka ni kushinda na si kufahamishana.
 
Usituletee longolongo lako hapa. Tanzania ina uwezo kabisa wa kulipa mishahara mizuri kwa wafanyakazi wake ili waweze kumudu gharama za maisha. Kuna savings chungu nzima ambazo zinaweza kufanywa ili kupunguza gharama za uendeshaji wa siri kali. Kwa mfano wanaostahili kuwa na magari ya siri kali ni watu wachache sana kama vile Rais, Waziri Mkuu labda na spika wabunge wengine wote wawe na magari yao binafsi na gharama za uendeshaji ziwe juu yao wenyewe. Hapa tutapunguza gharama chungu nzima. Mikataba kama ikiandikwa kwa kuwekwa mbele maslahi ya Taifa basi mapato ya Taifa yataongezeka kwa kiasi kikubwa sana haya pia yanaweza kuhakikisha ulipwaji wa mishahara mizuri kwa Watanzania.

Wimbo wako wa 'Tanzania nchi maskini umeshapitwa' na wakati ulikuwa unaimbwa mwaka 47 lakini sasa hivi haukubaliki tena. Tuna rasilimali chungu nzima ambazo kama zikitumiwa vizuri pamoja na kuwa na population ya 39 million, tunaweza kabisa kuhakikisha maisha mazuri kwa kila Mtanzania. Lakini viongozi wamekuwa mafisadi, wizi, wanaopenda kujitajirisha kupitia nyadhifa zao. Leo hii kuna tofauti kubwa sana kati ya wenye nacho na wasiokuwa nacho. Inakuwaje watu wengine wana maisha kama ya wacheza sinema wa Hollywood wakati huo huo mamilioni ya Watanzania hawajui hata mlo wao mwingine wataupata wapi!?

Wewe kama unataka kuishi kwa shida basi ni wewe pekee yako, Watanzania wote na wao wanataka waone matunda ya elimu yao na kuajiriwa kwao kwa kulipwa mishahara inayoendana na gharama halisi za maisha siyo kuwalalia. Hakuna Mtanzania yeyote atakayekufa kwa kuwa na mishahara na marupurupu mazuri, labda utakufa wewe usiyetaka mshahara wa kufuru. Usipende kujishushia hadhi kaka (mie mshahara huu mkubwa sana, sistahili kuupata) :confused: , ukijidharau mwenyewe hapa duniani basi kila mtu atakudharau.

Sina la kuongezea. Umewekewa statistics na uzioni! Nchi yenye kipato cha US$ 288 bado tunadai ni tajiri? Haya mimi na wenzangu kama mimi tukichukua stahili yangu ya US$ 24,000 kwa mwaka, ambao si wa kukufuru, kutabaki nini? Nani alikuambia nataka kuishi maisha ya shida au ninaishi maisha ya shida? Ninachokataa ni hii tabia ya kusimplify mambo. Tukiuza magari, wote tutapata neema? Tunamdanganya nani? Tatizo ni kubwa zaidi. Pamoja na kubanana mbavu inatubidi wote taufanye kazi ya ziada kujikomboa. Na haitatokea kesho. Na nyinyi mnaokaa nje sio panacea. Msome Kitila Mkumbo na umuelewe.
 
Back
Top Bottom