BornTown
JF-Expert Member
- May 7, 2008
- 1,716
- 481
Naombeni jamani tusaidiane hili. Mume wangu alikuwa masomoni nje ya nchi kwa muda wa miaka miwili, amerudi hivi karibuni. Aliporudi kanunua line ya Airtel ambayo ndio ninayoifahamu. Mie sikujua kumbe mwenzangu kanunua line ya tigo, ambayo hakunambia. Sasa siku moja usiku nashangaa msg inaingia:-
YEYE: Darling mambo vipi? Naona tangu jamaa yako arudi umenitosa
MIE: Mbona mie sikufahamu?
YEYE: Hee! kumbe tuko wengi tunaoiba? Njoo basi tukutane hapa Rose garden
Na mengine meeengiiiii.
Mie nkaushtukia mchezo hapo, ila nkasema wacha nione hii movie mwisho wake utakuwaje. Tukapanga hadi kukutana, bahati nzuri sikuwa na papara. ALHADULILAH! mara nafika eneo la tukio ni yeye huyooo!
Nilighafilika kwa kweli, ingawa hisia zangu zishantuma kuwa kama sio yeye basi ameweka watu wanitrace. Hivi ingekukuta wewe mwana JF mwenzangu, ungeliamuaje hili?
Pole sana umejiharibia menyewe umepoteza uwaminifu kwa mumeo, hapo alipo hakuamin hata chembe anakuona wewe ni kiruka njia anais kipindi yuko nje ya nchi ulimsaliti, ulichotaiwkukifanya ni kumweleza day one ile msg ilipoingia tu ungemshirikisha sasa hadi umfika pahali mmepangana mihadi unakuja kuomba ushauri hapa kwani wakati unatoka ulimuagaje ulimwambia unakwenda wapi.