mume wangu kanizidi mshahara lakini kila mara yuko kwenye money crisis

Pole sana mleta mada!!! Kuanzia leo acha kumlea mume huyo!!!!!!!!!!!!!!!!!! Ulianza kumlea pale uliporuhusu kugawana majukumu 50%!!!! Sijajua wewe ni imani gani ila kwa wakristu imeandikwa kuwa mke ni msaidizi wako na kuwa unatakiwa kumtunza. Bi mkubwa wa Lara 1 alikuwa sahihi kabisa na wanawake wote mnatakiwa mjifunze hili. Wale wanaume ambao wanataka kulelewa huwa wanataka wake au wapenzi wao wawe ni financier, Ninaamini kuwa nikiwa kama mwanaume heshima yangu inapanda pale ninapokuwa na uwezo na jukumu la kuilisha familia yangu na mke anachangia tu. Tena niwaambie kuwa kama mke wako anaona unajituma kuangalia familia vizuri huwa inampa motivation sana ya yeye kuchangia ili kuonesha upendo wake. Cha msingi kama mke anafanya kazi kuna majukumu madogomadogo kama mishahara ya watumishi, vitu vidogovidogo vya watoto n.k. Ninakumbuka wakati tunasomesha, kulikuwa hakuna hizi shule zenu za hela nyingi, shule za serikali tulikuwa tunalipa 750,au 1,500 hivi mara ya mwisho ila uniform na pocket money na mambo mengine ilikuwa juu ya mzazi. Mwenzangu kuna wakati kabisa ananiambia kuwa analipa ada na si kwa kuwa nilimlazimisha ila kwa kuwa alikuwa ana appreciate matunzo yangu kwa familia. I tell you ninapotumika kwa familia yangu, najiona chief au king Fulani hivi na heshima inakuwepo full kuanzia kwa watoto hadi mama. Sasa wewe mwanaume goigoi unamwachia mke wako aheme mwishowe anachoka na sura haivutii kabisa mwisho wa siku unaanza kutafuta wa sura za kung'aa wakati ya mkeo uliharibu kwa kumpa kazi za mitulinga. Wanawake ni maua, na maua haya need handling with care!!! Extra care!!!! I wish you all the best, those who are still searching for their better half to get the rib of their ribs!!!! Usipoweza kufanya hivyo ndiyo yatajeuka ya huyu mzee Kalbandika wa huyu mleta mada. Pole sana dada yangu ila kuanzia sasa weka mikakati ya kumuwajibisha huyu mumeo. Akishasimama imara ndipo uanze kumsaidia kile kinachowezekana.

asante kwa ushauri mzuri, yaani nahisi nishazeeka hata kabla ya siku zangu...unajua hata hiyo 50% yenyewe tulikubaliana baada ya kuona ananiachia kila kitu, yaani hajishughulishi, nikaona bora tugawane ili ijulikane nani yuko responsible na nini ndio ikaja hiyo 50%, kwangu mimi ilikuwa ni ahueni...lkn na yenyewe hatimizi, sasa nikimuachia less say 90% ataweza?
niliposoma maoni yako umenifurahisha sana, yaani ww ni baba na uko proud na familia yako kwa unavyoihudumia..sisi wengine tulipata bahati mbaya tukakutana na vimeo, ndio tunahangaika huku jf saa izi...mi mwenyewe nakumbuka vile baba yangu alivyokuwa anatuhudumia kwa kila kitu mpaka mimi nimeolewa nakumbuka baba yangu alikuwa ananinipa hela ile miaka ya mwanzoni mwa ndoa(mpk nilikuwa naona aibu) na hajaacha mpk nilipopata kazi ndio akaacha kunipa hela..huyu baba yangu kwa sasa ni marehemu Mungu amlaze mahala pema kwa kweli niko proud sana na baba yangu.
 
mshahara ukitoka daka ATM kadi yake, akitaka kutoa hela nendeni wote benki, mnatoa na anakupa budget yake kwa siku, wiki na hatimaye mwezi

hapo sasa si atakuwa mtumwa, kwanza atakubali? hiyo itakuwa naanzisha ugomvi usio na maana...sipendi kumuingilia sana uhuru wake ninachotaka ni yeye mwenyewe ajipange na awe responsible man...sasa atajipangaje au atabadilikaje hapo ndio pagumu
 
nimesoma comments za wadau zote hadi hapa, nalazimika kuamini kuwa tatizo la mumeo ni pombe na marafiki. Ukifanikiwa kusolve hilo la marafiki, hata pombe atapunguza na hivyo hela zitaonekana nyumbani. Sasa namna ya kutenganisha na marafiki ndo kizungumkuku kilipo!

hapo tu ndio kwenye shida, nifanyaje sasa ili arudi kwenye mstari? kuna wakati natamani hata tuahamie mikoa mingine labda atabadilika akikutana na watu wapya..
 
Pole dada...ni mtihani tu wa dunian...embu wacha kumpa hela na kutimiza wajibu wake..lazima atarekebika..akikuomba hela na wewe mwambie huna...na account za watoto weka in watotoz name...

asante ndugu yng, kuacha kumpa yeye hela naweza lkn kuacha majukumu ya nyumbani si ntawaumiza watoto? kuna wakati nilisafiri nje ya nchi kama mwezi mzima sijaacha chochote zaidi ya shoping ya vyakula nilivyofanya kabla sijaondoka, niliporudi watoto walilalamika kuwa vyakula vilikuwa substandard, baba hanunui nyama,samaki matunda n.k..yyani ni ugali na mchicha au wali maharage throughout..you can imagine
 
Sasa haya ndio maelezo niliyokuwa nikiyahitaji, maana pale juu hukufunguka uzuri kuhusu yenu historia na ukaanza moja kwa moja kutupatia michapo...



kwa kuwa nawe una hela na umekiri kuwa zatosheleza basi usizue ya kuzua...

Ushauri:

Kama kuna miradi mlioanzisha na kaifilisi basi hakuna haja ya kuifufua hiyo miradi....

Akikuomba hela nawe anza kumwambia kuwa huna hela kabisa labda mwezi ujao...

Yaani kimsingi igilizia A - Z tabia yake yote ya kubania hela zake, nawe fanya vivyo hivyo...

asante labda nijaribu hii staili nione kama itasaidia
 
ngoja niendelee kusoma kwanza....

kwa maana hili ni janga.. usipokuwa makini mydia litawamaliza.
 
mshahara ukitoka daka ATM kadi yake, akitaka kutoa hela nendeni wote benki, mnatoa na anakupa budget yake kwa siku, wiki na hatimaye mwezi
ATM mkuu siyo suluhisho, siku hizi kuna SIM BANKING ngoma inahamishwa na kupelekwa aidha M-PESA au Tigo PESA or else, Utashikilia ATM kadi wakati mapene watu wameshamaliza.

Cha kufanya hapo dada aendelee na uchunguzi chini kwa chini nina pengine jamaa ana mji mwingine anauhudumia au kama walivyosema wadau hapo kabla huyo jamaa ndiyo wale akina Kassim walioimbwa na Maalim Muhidin Gurumo:

Sasa pesa zimemuishia Kassim hana la kufanya aeeeeeeeeeee.
 
Hapana soma mpaka mwisho ushauri wangu coz watachukua pesa wakiwa wamesaini hundi kwa saini zao wote wawili.
 
hapo tu ndio kwenye shida, nifanyaje sasa ili arudi kwenye mstari? kuna wakati natamani hata tuahamie mikoa mingine labda atabadilika akikutana na watu wapya..

No kuhamia mikoa mingine haitasaidia cho chote unless unihakikishie kuwa utapata mkoa ambao hauna bar wala watu. Hata kama ni watu wapya as long as anaenda bar atawapata huko huko wa taipu yake. Hata wanaokwambia usimpe pesa, ni kwamba utaokoa pesa zako tu, za kwake bado ataendelea kuzitumbua bar na marafiki.

Solution ni kumfanya aache pombe kwanza. Nasikiaga kuna dawa za kumfanya mtu aache pombe, jaribu kuulizia zaidi kuhusu hizo dawa. Pia jaribu ku-convince awe mcha Mungu. Ili ufanikiwe hili inabidi kwanza wewe uwe deep kwenye dini, maombi yasipungue home, unam-convince na yeye awepo kwenye hayo maombi kama kichwa cha nyumba, tena sometimes unamuombea (hasa khs kuacha pombe) na yeye anasikia - ila angalia isiwe too much na iwe wakati mko wawili ili asione unam-attack au kumwaibisha kitendo kitakachomfanya aanze kukwepa kipindi cha maombi.

Ukifanikiwa hilo obvious bar hataenda tena, hata marafiki zake watakuwa wa taipu nyingine kabisa. Bila kumshirikisha Mungu hawezi kuacha pombe hivi hivi aisee
 
sikia kamusi pamoja na mengine uliyosahuriwa..

nafikiri haya
1. mumeo ni mtu wa totoz
2. si muwazi (lack of transparency) .. anafanya miradi yake kwa siri, au anasaidia ndgu kwa siri n.k

napendekeza
1. anza kumind mambo yako( save, anzisha miradi n.k)
2. au muwe na akaunti ambazo hawezi kutoa pesa bila sign yako.
3. mwisho kabisa usikome/usiache kumwomba Mungu,,, wakati mwingine huenda muhusika hajapenda na wala hajitambui.. kwa njia ya maombi tu ndio unaweza kumnusuru. Yapo mambo mengine yanatokea kwa sababu ya urithi.. babu wa baba yake, babu yake baba yake na wengineo walifanya hivyo.. na huo ni mwendelezo.
 
Last edited by a moderator:
Kwanza nakupongeza jinsi ulivyo,jinsi unavyojieleza uko unique na wanawake nawezasema 80%,unamkubali mumeo na unania ya kumsaidia Kiupendo matatizo aliyo nayo,hayo ndio maisha na sio ugomvi au kumsimanga vibaya kwa watu,tatizo la mumeo nafkiri hao marafiki zake ndio chanzo na naamini mnayopanga lazima anawaadisia hao marafiki zake na kwa sababu ni watu wa pombe basi lazima wamjaze ujinga,cha msingi mtengeneze mazingira ambayo atapunguza kuonana na hao marafiki zake,mrudishe kwenye imani zaidi atajitambua,tatua matatizo sio kwa kukomoa bali kwa kusaidia..

i agree with u!
wakati mwingine inabidi ifike mahala mume/mke awe ana uwezo wa kumwambia mwenzie sitaki urafiki wako na fulani.. au hata kuwachagulia wenzi wetu wawe na marafiki wa aina gani. Friends wana impact kubwa sana katika maisha yetu..birds of the same colour flew together.

Tujichunguze .. kama marafiki ulionao wewe mwenyewe huwasomi..they are not adding anything to you rather than kukuharibu TUPA KULEEEEE (friendship is by choice not force).
 
Ni kukaa nae chini tu na kumweleza juu ya tabia yake asipokusikiliza nadhani ana mtu ambaye unajua kabisa mumeo huwa anamsikiliza, yaweza kuwa ndugu yake, rafiki yake hata mtumishi wa Mungu hebu mshirikishe ili aweze kuongea nae pia maybe itasaidia, na kingine kama wadau wengi walivyoshauri anza kujitoa taratibu kwenye majukumu ya familia hasa kwa yale yanayomuhusu ili na yeye atimize wajibu wake kama baba


hapo tu ndio kwenye shida, nifanyaje sasa ili arudi kwenye mstari? kuna wakati natamani hata tuahamie mikoa mingine labda atabadilika akikutana na watu wapya..
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom