Nshuti divine muheto
Member
- Jun 1, 2023
- 40
- 174
Miaka kadhaa iliyopita mume wangu alimtambulisha mtoto wa nje katika familia yake ni wa kiume alikuwa ni mtu wa furaha sana na kujisifu kuwa kapata mtoto wa kiume na ndugu zake walimpongeza hasa mtoto alifanana nae. Japo mimi nilibaki na maumivu, kwani nimezaa nae watoto wawili wa kike tuu.
Katika maisha yangu nilipenda kuwa na mwanaume ambaye tutakuwa na watoto wetu tuu. Ila haijakuwa hivyo. Nimelipokea japo nina maumivu.
Mume wangu ni mtu wa mfumo dume niseme. Akiongea ndani ya nyumba ndo ishakuwa hivyo. Aliniambia tuu mtoto huyu ni wangu na ataishi hapa kama hutaki basi waweza ondoka.
Nikasema tuu sawa, basi mtoto tunaishi nae hapa.
Tulijenga nyumba moja tulikuwa tunashirikiana kwa kila kitu kwa sababu mimi nina kazi na mume wangu pia na baadhi ya biashara. Na tulishaanza nyumba nyingine kujenga. Ila nilisimama baada ya tukio hilo lililonipa maumivu.
Nilishangaa sana mume wangu ana tabia ya kusema tuu yeye hana uwoga. Anasema kuwa huyu ni mtoto wangu wa kiume ndio atarithi mali zangu kwa kuwa anaendeleza jina langu. Mimi namuangalia tuu. Mtoto anapita nae mtaani kwa kujisifu hata mbele ya marafiki zake kwa kuwa mtoto kafananae. Na yeye mali zetu zipo kwa jina lake na mimi hata ushahidi kuwa nimeweka mkono sina ninabaki namuangalia tuu.
Miaka 3 iliyopita kuna kiwanja kimoja aliniachia marehemu Baba kipo Kigamboni kule ni kikubwa kiasi. Na mume wangu hajui hiko kiwanja. Ni mimi tu na ndugu zangu. Sasa nilipigania kuwa niwajengee watoto wangu nyumba pale japo mimi mama yao sina sio tajiri. Nikasema nitapambana tuu. Nilikuwa naweka vipesa vyangu baadhi na kujinyima. Hata pesa ya mume wangu ya matumizi nilikuwa naibana sana.
Biashara zetu na mume wangu nilikuwa nachota kiasi bila mume wangu kujua kabisa.
Nilianza msingi wa nyumba mbili kwenye eneo moja. Nyumba sio kubwa ni vyumba viwili tuu vya kulala, living na dining room, choo na store na jiko. Sio kubwa kivile.
Ilikuwa ngumu sana kwangu kuanza kujenga. Sasa siku moja nilikutana na Baba mmoja mtu mzima na ana mke na watoto wakubwa tuu. Nilikutana nae Karikoo kwenye duka moja hivi. Tulizoeana mapaka kupanga nichepuke nae.
Mkewe kuna kipindi nikamjua mpaka nyumbani kwake. Ni Baba mwenye uwezo tuu tena sana.
Mimi ni mwanamke nina mvuto kwa hio niliamini hawezi nikataa yule Baba. Mara nyingi tulikuwa tunakutana kwenye hotel. Nilimueleza shida zangu akasema atanisaidia.
Alinisaidia kumaliza msingi mpaka boma kuisha za vijumba vyangu. Nilijitahidi sana mume wangu asijue kwani yeye namjua reaction yake endapo akijua.
Yule Baba alikuwa ananifurahia sana, ila alikuwa ananionya kuwa kuwa makini mumeo asijue kabisa. Mimi namwambia tuu usijali ni kweli nilijitahidi mume wangu asijue kabisa. Nilikaa nae miaka 2 yote hio niliendelea nae bila my hubby kujua.
Yeye yuko busy na mtoto wake maana namuangalia tuu jinsi anavyomuhangaikia. Mwaka jana alinisaidia sana kuezeka vijumba vyangu.
Ila mwishoni mwa mwaka jana alihamishwa na kwenda Dodoma kikazi na mahusiano na mimi yaliisha.
Nikiri tuu alinisaidia sana yule Baba. Kwa kiasi kikubwa.
Sasa mwaka huu nilikutana na kijana mmoja mgahawa mmoja nilimpenda, nilijitahidi nikapata tukabadilishana namba najua hawezi kunikataa coz mimi ni mzuri najiamini. Niliingia nae kwenye mahusiano. Na sijamwambia kuwa ni mke wa mtu. Japo vijana ni wagumu kutoa pesa ila anajitahidi kiasi chake. Naamini atanisaidia hata kwenye biashara zangu binafsi, coz yeye anaagiza vitu China.
Najua wanaume mnakasirishwa na usaliti kama huu, najua wapo watanitukana na maneno juu. Lakini hata nyinyi ni wasaliti kwa wake zenu, thread zenu za michepuko mnashauriana sana humu JF.
Mume wangu kanipa donda kubwa sana, tena hata aibu anasema huyu ndo mrithi wangu. Yeye ni wale wanaume akisema basi wote mtii.
Namuangalia tuu na mwanae.
Sijaleta kama sifa ni matokeo ya maumivu niliyopata sikuwa na hiyo tabia kabisa.
Mwenye kuleta povu na alete tuu.
Katika maisha yangu nilipenda kuwa na mwanaume ambaye tutakuwa na watoto wetu tuu. Ila haijakuwa hivyo. Nimelipokea japo nina maumivu.
Mume wangu ni mtu wa mfumo dume niseme. Akiongea ndani ya nyumba ndo ishakuwa hivyo. Aliniambia tuu mtoto huyu ni wangu na ataishi hapa kama hutaki basi waweza ondoka.
Nikasema tuu sawa, basi mtoto tunaishi nae hapa.
Tulijenga nyumba moja tulikuwa tunashirikiana kwa kila kitu kwa sababu mimi nina kazi na mume wangu pia na baadhi ya biashara. Na tulishaanza nyumba nyingine kujenga. Ila nilisimama baada ya tukio hilo lililonipa maumivu.
Nilishangaa sana mume wangu ana tabia ya kusema tuu yeye hana uwoga. Anasema kuwa huyu ni mtoto wangu wa kiume ndio atarithi mali zangu kwa kuwa anaendeleza jina langu. Mimi namuangalia tuu. Mtoto anapita nae mtaani kwa kujisifu hata mbele ya marafiki zake kwa kuwa mtoto kafananae. Na yeye mali zetu zipo kwa jina lake na mimi hata ushahidi kuwa nimeweka mkono sina ninabaki namuangalia tuu.
Miaka 3 iliyopita kuna kiwanja kimoja aliniachia marehemu Baba kipo Kigamboni kule ni kikubwa kiasi. Na mume wangu hajui hiko kiwanja. Ni mimi tu na ndugu zangu. Sasa nilipigania kuwa niwajengee watoto wangu nyumba pale japo mimi mama yao sina sio tajiri. Nikasema nitapambana tuu. Nilikuwa naweka vipesa vyangu baadhi na kujinyima. Hata pesa ya mume wangu ya matumizi nilikuwa naibana sana.
Biashara zetu na mume wangu nilikuwa nachota kiasi bila mume wangu kujua kabisa.
Nilianza msingi wa nyumba mbili kwenye eneo moja. Nyumba sio kubwa ni vyumba viwili tuu vya kulala, living na dining room, choo na store na jiko. Sio kubwa kivile.
Ilikuwa ngumu sana kwangu kuanza kujenga. Sasa siku moja nilikutana na Baba mmoja mtu mzima na ana mke na watoto wakubwa tuu. Nilikutana nae Karikoo kwenye duka moja hivi. Tulizoeana mapaka kupanga nichepuke nae.
Mkewe kuna kipindi nikamjua mpaka nyumbani kwake. Ni Baba mwenye uwezo tuu tena sana.
Mimi ni mwanamke nina mvuto kwa hio niliamini hawezi nikataa yule Baba. Mara nyingi tulikuwa tunakutana kwenye hotel. Nilimueleza shida zangu akasema atanisaidia.
Alinisaidia kumaliza msingi mpaka boma kuisha za vijumba vyangu. Nilijitahidi sana mume wangu asijue kwani yeye namjua reaction yake endapo akijua.
Yule Baba alikuwa ananifurahia sana, ila alikuwa ananionya kuwa kuwa makini mumeo asijue kabisa. Mimi namwambia tuu usijali ni kweli nilijitahidi mume wangu asijue kabisa. Nilikaa nae miaka 2 yote hio niliendelea nae bila my hubby kujua.
Yeye yuko busy na mtoto wake maana namuangalia tuu jinsi anavyomuhangaikia. Mwaka jana alinisaidia sana kuezeka vijumba vyangu.
Ila mwishoni mwa mwaka jana alihamishwa na kwenda Dodoma kikazi na mahusiano na mimi yaliisha.
Nikiri tuu alinisaidia sana yule Baba. Kwa kiasi kikubwa.
Sasa mwaka huu nilikutana na kijana mmoja mgahawa mmoja nilimpenda, nilijitahidi nikapata tukabadilishana namba najua hawezi kunikataa coz mimi ni mzuri najiamini. Niliingia nae kwenye mahusiano. Na sijamwambia kuwa ni mke wa mtu. Japo vijana ni wagumu kutoa pesa ila anajitahidi kiasi chake. Naamini atanisaidia hata kwenye biashara zangu binafsi, coz yeye anaagiza vitu China.
Najua wanaume mnakasirishwa na usaliti kama huu, najua wapo watanitukana na maneno juu. Lakini hata nyinyi ni wasaliti kwa wake zenu, thread zenu za michepuko mnashauriana sana humu JF.
Mume wangu kanipa donda kubwa sana, tena hata aibu anasema huyu ndo mrithi wangu. Yeye ni wale wanaume akisema basi wote mtii.
Namuangalia tuu na mwanae.
Sijaleta kama sifa ni matokeo ya maumivu niliyopata sikuwa na hiyo tabia kabisa.
Mwenye kuleta povu na alete tuu.