Mume ananichosha kwa kupenda haki ya ndoa

M-bongotz

JF-Expert Member
Jan 7, 2010
1,734
405
HII NIMEQUOTE TOKA SEHEMU NIKIAMINI KUNA WATU WENGINE WENYE TATIZO LINALOFANANA NA HILI..

HEBU TUWASAIDIE MAWAZO..


"Mimi nina mume ambaye tumekuwa tunaheshimiana na pale tunapokorofishana tunawekana wazi. Ila naona mume wangu anatake advantage of the situation.kila tunapogombana tunaombana msamaha na kila nikimkanya mume wangu kwa tabia yake mbaya huwa anaomba msamaha na tunakuwa na amani lakini sasa yeye haamini nimemsamehe mpaka apate "chakula cha ndoa".

Yaani hata ukimwambia umemsamehe mpaka apate hiyo kitu ndiyo anaamini nimesamehe.

Tatizo siyo kutoa hiyo kitu lakini ni kwamba atataka mshinde siku nzima mkifanya hayo mambo. Tumeoana tuna miezi sita na bado hatuna watoto so we are free in the house.

Najitahidi kumridhisha lakini mwenzangu anahamu kubwa ambayo nashindwa kukabiliana nayo.

Wakati mwingine mpaka nafanya kukimbia kitandani au najichelewesha kwenda kitandani ili nikute ameshalala maana akianza hiyo kitu ni usiku mzima anataka haniachi nafasi ya kulala usingizi. Nikimueleza anasema atapunguza lakini wapi , mchezo ni uleule.

Sitaki aone nafanya mapenzi kama wajibu tu. Ila mwili pia huchoka na hamu huwa pia inaisha.Yaani mimi nafanywa kila siku na pata likizo siku nikiwa mwezini na hata hivyo nitaulizwa kama period imeisha ana hamu na mimi.

Naogopa nikisafiri sijui atafanya na nani maana bila hiyo kitu mume wangu atanifanyia vurugu za kila aina mpaka apate halafu atatulia kama vile si yeye.

Mlioolewa/kuoa mnafanya nini kukabiliana na hali hii inapotokea ? naomba ushauri"

Source: harusiyangu.com
 
Mmhhhhh....
Wenzio siku ya kuolewa huwa wanalia....
Kwa mambo kama hayo...

Wewe siku ya kuolewa ulichekelea?????

Ukikubali kuolewa,kubali yote.
 
Pole.. Ndio maisha ya ndoa, yaani kuvumiliana.. Atachoka na atapunguza usichoke kumpa asije akaenda nje, then ikawa majuto kwako.
 
These are matrimonial matters, and you are supposed to keep silent...utazowea tu.
Au ulikuwa bik**ra nini wakati jamaa anachukua..
 
Mmhhhhh....
Wenzio siku ya kuolewa huwa wanalia....
Kwa mambo kama hayo...

Wewe siku ya kuolewa ulichekelea?????

Ukikubali kuolewa,kubali yote.


Hee! Yaani nimecheka kweli. Boss jamani si umshauri sasa afanyeje, maana mpaka ameweka mambo hadharani jua kuna shida hapo...


Annina
 
Mambo ya nyumba hayo. Kaeni mjadili kero mbalimbali zinazo wakabili. Hilo pia sababu limekuzidi ni kero kwako. Liweke wazi kwa mumeo nadhani nae ni muelewa mambo yatakuwa shwari.
 
Hapa ni mwamba ngoma.................!

i wish i could hear from FL1, Prety, Womanofsubstance inc. etc tupate opinion balanced.

my take, ni kuwa binti hajajua kuwa wenzie wanalalamika huduma inapunguzwa kila akina baba wanapokuwa na pressure, kazini, mitaani puls nyumbaa ndogo. She is supposed to be happy for overservice.
 
Tumeoana tuna miezi sita na bado hatuna watoto so we are free in the house. Najitahidi kumridhisha lakini mwenzangu anahamu kubwa ambayo nashindwa kukabiliana nayo.

...ee mama wee, furahia Fungate mama. 'mazoea' yakishaingia utahesabu miezi ukihesabu 'boriti!'...
 
Ushauri wangu shoga, kula tende, cindamon mixed na asali hizi ni natural viagra zinazoleta nyege. Kwa kweli ukitumia hivi vitu utapata hamu na wewe kwa sana tuu wala hutaona hiyo karaha. Hata hivyo give him time atapunguza tuu speed...simnawajua tena hawachoki kukinai haraka hawa wadudu!.
 
Duh, nilitaka kukushauri kuwa usimpe kila siku lakini nikakumbuka kuwa siku atakapo omba msamaha na kukubaliwa,itabidi u prove kama umemsamehe.
Nawe mbona mnagombana mara kwa mara wakati ndoa yenyewe changa?
Bora uende kwa Chrispin na Wapwaaaz,wenyewe hawagombani na kama wakigombana,suluhisho ni kwenda out kupunguza mawazo.
 
Au ulikuwa bik**ra nini wakati jamaa anachukua..
Mimi nahisi labda jamaa ndie alikuwa bikra ndio maana toka ajue game amekuwa anapiga non stop. Nway whatever the case hapa hawezi....................
 
Mimi nilidhani kula tende,asali na karanga ni kwa wanaume tu! Huyo jamaa anahitaji kuchuna ngamia mzima akiwa amechutama ili kupunguza kiraru!
 
Ushauri wangu shoga, kula tende, cindamon mixed na asali hizi ni natural viagra zinazoleta nyege. Kwa kweli ukitumia hivi vitu utapata hamu na wewe kwa sana tuu wala hutaona hiyo karaha. Hata hivyo give him time atapunguza tuu speed...simnawajua tena hawachoki kukinai haraka hawa wadudu!.
Penny dada wadudu unamaanisha nini au akina nani hapa?
 
Badilishana mme na huyu:
Mumewangu ndio chanzo cha mimi kuwa na uhusiano nnje ya ndoa!
https://www.jamiiforums.com/members/pape.html
Suala la nyumba ndogo halipo kwa wanaume tu hata wanawake pia wanalo! Hii inawapunguzia stress wazipatazo kwa waume zao! ikiwa ni pamoja na kunyimwa uroda mara kwa mara kwani mwanaume akishajichapia nje basi hamjali mkewe! Kwahiyo wanawake nao uamua kujitafutia vijana ili wawe wanajipongeza! Mzee akienda zake nje na mama naye anatoka kwenda kujipongeza. Mwisho wa siku ni ngoma droo!

Mimi na mumewangu tumekuwa katika ndoa kwa muda wa miaka 15 sasa. Kuna wakati mumewangu alianza kuwa na uhusiano na msichana fulani (jina kapuni) na nilipogundua yule binti alinijia juu na kusema kwamba mimi simfikishi kokote 'buzi' lake (mumewangu)!!!

Nilivumilia sana lakini mumewangu alikuwa akirudi amelewa na wakati mwingine harudi siku 2-3, hasa wakati wa mwisho wa wiki! Mumewangu alipoteza kabisa hamu ya kufanya tendo la ndoa na mimi! Niliumia sana mpaka siku moja nilipkwenda kufanya manunuzi ya vitu vya ndani sokoni kariakoo! Nilikutana na 'kijana' mmoja mtanashati katika duka wanalouza nguo na viatu! Kijana huyo alinisemesha kwa maneno matamu na mwisho wa yote tuliagana na kupeana namba za simu!

Baada ya siku kama 3, kijana huyo alinipigia simu na kunijulia hali! Ikawa ndiyo kawaida yake kupiga mara kwa mara kwani mzee wangu si 'hayupo'.... Nilianza kuvutiwa na kijana na siku aliponitamkia kwamba anaomba twende nje kwa ajili ya chakula cha jioni (dinner) nikawa sina pingamizi!

Baada ya muda kama wa mwezi mzima nikatokea kumpenda sana huyo kijana na hali yangu ilibadirika kabisa nikawa na furaha hata mumewangu akirudi nyumbani au asiporudi mimi sina wasiwasi kwani kabla sijalala nitaongea na mtu ambaye anayenijari!

Mwisho wa siku aliponitamkia kwamba anaomba nimtembelee kwake sikusita kwani niliona ndio wakati mwafaka wa 'kujuana' vizuri! Na mambo yalienda hivyo kama unavyofikiria! Nina amani na sina hata haja ya mumewangu!

Sasa imeshafika miaka mi 2 mimi na mumewangu hatujawahi kulala kitanda kimoja kwani yeye akirudi amelewa na anarudi usiku sana! Na hata akirudi anakuwa ameshamalizana huko kwa nyumba ndogo yake!

Wito: Enyi waume wapendeni wake zenu na jitahidini kuheshimu ndoa zenu kwani nyie ndio chanzo cha sisi wanawake kutoka nje ya ndoa! Kama wewe hunitimizii mahitaji yangu....unataka nifanyeje? Nibaki nateseka wakati kuna watu weeeeeeeengi kama wewe?
 
Ushauri wangu shoga, kula tende, cindamon mixed na asali hizi ni natural viagra zinazoleta nyege. Kwa kweli ukitumia hivi vitu utapata hamu na wewe kwa sana tuu wala hutaona hiyo karaha. Hata hivyo give him time atapunguza tuu speed...simnawajua tena hawachoki kukinai haraka hawa wadudu!.

Penny,

Mdudu mwenyewe lol.
 
Ushauri wangu shoga, kula tende, cindamon mixed na asali hizi ni natural viagra zinazoleta nyege. Kwa kweli ukitumia hivi vitu utapata hamu na wewe kwa sana tuu wala hutaona hiyo karaha. Hata hivyo give him time atapunguza tuu speed...simnawajua tena hawachoki kukinai haraka hawa wadudu!.
...Si unajua kipya kinyemi?? Miezi sita tu lazima mkulu atakuwa bado ana hamu nayo sana.. Keep it up bana acha kulalamika wenzio wanazikosa hizo....
 
Back
Top Bottom