Mwiba
JF-Expert Member
- Oct 23, 2007
- 7,607
- 1,744
Nilikwisha kusema CUF hawatorudi katika mazungumzo hayo hata kwa bakora ,wameshatega na mtego umenasa na jinsi nchi ilivyochafuka ndio kabsaa hawakai mezani wala kwenye jamvi ,Ubabe wa CCM unaelkea ukingoni hizi alama zote zinazotutokelea zina maana na si dalili nzuri kwa chama tawala na kiongozi wao ,kama hawajui ndivyo au mwanzo wa kitu kinachoporomoka na kuanguka ,tusitegemee CCM itaanguka kama nazi lakini itaporomoka kaa mlima kwa luga ya kigeni wanaita landslide au mudslide ndio hivyo hivyo.
Nikirudi kwa Makamba yeye alitakiwa kujiuzulu palepale Butiama bila ya kuchelewa ili alinde heshima yake lakini sasa amekuwa kama mbao ya mkonge au bua ,tatizo ni kwa hawa wanaojiita CCM ni kuwa wengi wao hawajiamini na ubaya uliokuwemo ndani ya Chama chao ni tishio na wanahisi huenda wakadhurika au kupata shinikozo la damu ugonjwa maarufu kwa viongozi wa CCM.
Nikirudi kwa Makamba yeye alitakiwa kujiuzulu palepale Butiama bila ya kuchelewa ili alinde heshima yake lakini sasa amekuwa kama mbao ya mkonge au bua ,tatizo ni kwa hawa wanaojiita CCM ni kuwa wengi wao hawajiamini na ubaya uliokuwemo ndani ya Chama chao ni tishio na wanahisi huenda wakadhurika au kupata shinikozo la damu ugonjwa maarufu kwa viongozi wa CCM.