Mtu yeyote anaetaka kuwa kiongozi awe amezaliwa baada ya 1961. Makamba Januari

wanaotaka madaraka utawajua tu watafanya kila kitu kuwapoteza akili zenu
 
Alijifanya mwanaharakati kumbe njaa tu hana lolote badala ya kujadili mambo ya msingi anaeleza masuala ya urais nakubaliana na mdau kwamba watu wa nyinyiem wanafikiri kwa kutumia tumbo na siyo akili shame on you jnr
 
kiongozi wa nini....wa mbio za mwenge au? Ufafanuzi mkuu

mweenge ooh mwengeee... Mbioo mbiooo ...mwenge tunaukimbiza...mbioombioo...mpaka makao makuu..! Nadhan ndo ujinga anaouzungumzia huyo mtoto kigogo!
 
Genocide inaanza hivyo hivyo, mtu kujenga chuki dhidi ya kundi fulani. Tatizo la Tanzania ni mfumo wala sio wazee au vijana. Tukiweza kubadili mfumo na kuwa na utamaduni wa kuwajibika tutasonga mbele kwa kasi zaidi.
 
Urais sio bongofleva hahitajiki mtoto aambaye bado tukamasi tunachungulia puani. Anahitajika mtu mwenye umri wa kutosha, busara ya kutosha, akili safi, coz ikulu ukiingia na VI-KATA 'K' watakuletea mikataba sophisticated utaiingiza nchi mkenge.
 
Genocide inaanza hivyo hivyo, mtu kujenga chuki dhidi ya kundi fulani. Tatizo la Tanzania ni mfumo wala sio wazee au vijana. Tukiweza kubadili mfumo na kuwa na utamaduni wa kuwajibika tutasonga mbele kwa kasi zaidi.


...Umenena vyema Mkuu nakuunga Mkono. Kesho na keshokutwa huyu huyu anaweza kusema raisi lazima awe Mweupe na Mwenye Sura ya Kuvutia, Raisi awe wa Urefu Fulani, Raisi atokee Upande fulani wa nchi nk. Genocide huwa haianzi ghafla. Huwa inaanza taratiibu kwa kufumbia macho matamshi ya wapuuzi wachache wanaotaka kuhodhi madaraka...! Tuchukue Tahadhari.
 
Kijana januari, anutaka urais kama baba yake yosefu alivyomuombea uwaziri kwa swaiba jk naye akazuga na baadaye akaachia.
 
Kijana januari, anutaka urais kama baba yake yosefu alivyomuombea uwaziri kwa swaiba jk naye akazuga na baadaye akaachia. Akumbuke kuwa kwa kufanya hivyo anamwaga sumu kwa rika jingine na kueneza ubaguzi wa kiumri. kinachotakiwa ni hekima na dhamira ya dhat i ya kulikomboa taifa hili katika lindi la umaskini uliotawaliwa na bahari ya ufisadi.
 
hapa Makamba umenena ulikuwa wapi toka mwanzo

Nilipozaliwa miaka hiyo taarifa ya habari iliongozwa na ngoma za Mzee Moris Nyunyusa akiwa anapiga ngoma 7. Kisha zinafuata; "nyot!, nyot!, nyot!, nyot!, nyot!, nyot!," Kisha wasomamaji; mmoja anataja muda (Eda Sanga: Hivi sasa ni saa 1 kamili) David Wakati anaitikia; "Na hii ni taarifa ya habari kutoka Radio Tanzania Dar es Salaam, Msomaji David Wakati, kwanza muhtasari wa habari.


1. "Waziri asiye na wizari maalum Bw Kingunge Ngombale Mwiru............"

2. "Waziri wa nchi ofisi ya Makamo (siyo Makamu) Bw Steven Meng'anyi Wassira leo ametembelea nyumbani kwa Mtukufu Rais Julius Kambarage Nyerere, huko Butiama..........."

Habari kamili, Dar es Salaam....


Basi majina hayo yametajwa hadi sasa tumekuwa wakubwa na sasa tunaelekea kuchungilia nusu karne lakini wapo tu. Wapo tu mpaka MENO YAO YA ASILI YAMETANGULIA MBELE YA HAKI WENYEWE WAPO TU. SASA HIVI HATA CHAI YA MOTO HAWAWEZI KUNYWA KWA SABABU HAWANA MENO ZIMEBAKI FIZI WANAKUNYWA CHAI BARIDI KAMA MTINDO (FASHION) KWA KUOGOPA KUUNGUA FIZI ZAO WAPO TU...

JAMANI PUMZIKENI SASA....... HAMNA JIPYA MTAKALOTUACHIA TUACHIENI NCHI TUANZE KUIKARABATI UPYA KAMA ALIVYOFANYA MWL NYERERE 1950S.

ASANTENI JAMANI.......!!!!!!???????:A S thumbs_up::horn:

 
Makamba jnr sikujua kama amerithi akili za baba yake! Kwa mawazo kama haya mtu kama January si anaweza kuuza hata nchi maana naona uwezo wake wa kufikiri ni mdogo sana. Hawa ndio viongozi waliokubali kushikiwa akili zao na watu wengine. Kwahiyo waliozaliwa baada ya 1961 ndio wanafaa kugombea urais ! sasa kwa akili unayoionyesha wewe uliyezaliwa baada ya 1961 ndio hivyo mbona tumeshawaona bogus. Fanyeni kazi. Age is nothing but number
 
Back
Top Bottom