kaangwa
JF-Expert Member
- Jan 30, 2011
- 644
- 192
mi naona wote wana makosa japo la yule mtoto halitakuwa kubwa sababu tu ya umri wake..kile kitabu ni cha jumuia!
Watoto hawana malezi toka kwa wazazi wao..
mkuuu hapa nyosha maelezo vizuri, mimi naamini kuna malezi mengine yamepinda.Huyo mtoto wa kwanza aliyemwambia mwenzake kuwa akikojolea qoran atakuwa mnyama naye amefundishwa hivyo na wazazi wake,badala ya kumfundisha kuheshimu kitabu hicho,matokeo yake akawasimulia wenzake alichofundishwa na wazazi/waalimu wake hili limetufikisha hapa tulipo.Wakristo wanamheshimu Yesu kuliko hata biblia,mbona Yesu anatukanwa kwenye misikiti na kwenye mihadhara na watu wazima wala siyo watoto mbona hatujaona maandamano.AMANI YA NCHI YETU IKO MIKONONI MWETU SISI WENYE DINI ,TUIDUMISHE KWA KUVUMILIANA.Ningekuwa mimi hao watoto wote wawili ningewachapa viboko na kuwafundisha kuheshimu kitabu cha mungu.