Mtonyaji: CHADEMA mshukuruni Lissu na waandishi wa Habari sakata la Mwangosi vinginevyo...

Wakuu,
Nilipata fursa ya kuwasiliana na mtonyaji wetu ambaye ameseniambia kwamba Chadema tuwashukuru sana waandishi wa habari za Iringa na Tundu Lissu kwa sababu wameifanya serikali ishindwe cha kufanya katika sakata la Mwangosi.
Awali ya yote alisema Ifahamike kuwa;
Serikali haikutaka kabisa kumshtaki askari wake kwa kuwa hilo litawafanya Askari kupungukiwa na ujasiri wa kuwathibiti Chadema kwa hofu ya kushtakiwa mbele ya safari, na ndo maana walichelewa kuchukua hatua wakipisha upepo wa Mwangosi upite – upepo ukagoma kupita hasa baada ya waandishi kuandamana. Hili jambo nalo lilizua mjadala wa ndani lakini mwisho ikalazimika walau kumshtaki.
Pili, Serikali kwa sasa haiko tayari kuunda tume ya uchunguzi ya kimahakama kama inatavyotakiwa kisheria na kama ilivyoombwa na Chadema, wanahabari, wananchi nk.

Nini kimeitatiza serikali?
Mosi, uundaji wa Tume ya kiuchunguzi wa kimahakama umekwama kwa sababu Majaji wote ambao wangeweza kuisaidia serikali endapo uchunguzi utaleta sura mbaya zaidi dhidi ya Serikali, wako ktk Listi ya Tundu Lissu. Hili ndilo tatizo kubwa sana. Tatizo kubwa ktk ripoti ile ya Lissu ni ripoti ya mapendekezo ya kamati ya Rais ya kuchunguza majaji ambayo iko mikononi mwa Tundu Lissu. Ripoti hiyo ilionesha kwamba majaji waliomaliza muda wao wakaongezewa muda na Rais ni kinyume na katiba ya nchi kama ilivyoelezwa na Lissu Bungeni kwa kujiamini ktk sakata lake. (Kumbuka utetezi wa tundu Lissu Bungeni). Hawa ndio walikuwa wawe tegemeo la Serikali ktk sakata hili na ndio hawateuliki kwa sababu itaanzisha mjadala wa Lissu na kuupanua zaidi.
Lengo lilikuwa ni tume ambayo uchunguzi wake usiiumize serikali badala yake uelekeze tuhuma kwa ama chadema au vurugu wananchi. Na pili, upendekeze kuundwa kwa sheria ya kudhibiti mienendo ya vyama vya siasa na hasa maandamano. Kwa hiyo, azimio lililopo ni kwamba Tume hiyo haitaundwa kwa kuwa serikali ina hofu kuchafuka zaidi.


Pili, sakata la Iringa kwa jinsi lilivyorekodiwa ktk kamera na picha zilizokwisha kurushwa ktk vyombo vya habari ni tatizo. Tatizo jingine kubwa ni hofu ya serikali kutojua vitu vilivyopo ktk kamera za waandishi wahusika kama vipo vilivyofichwa hadi sasa. Kwa hiyo, mambo haya (kama yapo yaliyofichwa) yakiletwa kwenye tume ya kimahakama yanaweza kuleta sura ambayo ingeshindikana kwa tume ya kimahakama kuisafisha serikali badala yake serikali ikaingia ktk tope kubwa zaidi bila kujali kama Tume inaongozwa na jaji wa aina gani (neutral au one sided).

Kwa hiyo, mambo mawili hapo juu yameiharibia kabisa serikali ktk mpango wake wa kuithibiti sakata hili na sasa tuko njia panda.
Na ni mambo hayo hayo ndo yalimfanya Rais ashindwe kuongea na wananchi kwa sababu hana cha kusema, jambo lililowafanya walazimike kumtuma Steven Wasira aje aongee kwa Niaba ya Rais kupunguza hasira za wananchi. Hata hivyo, wengi wanamlaumu Wasira huku serikali kwa madai kuwa heri asingeongea kwa kuwa hakufanikiwa kabisa kufanya kile alichotumwa. (Awali hotuba ya Wasiri ilikuwa aitoe Rais mwenyewe)
Nakumbuka kuliko na uzi wa Rais kuongea na waandishi humu JF kabla ya wasira kama sikosei.


Ushauri wake.
Chadema waendelee kudai Tume ya uchunguzi ya Kimahakama kwa kuwa tume ya Nchimbi ni danganya toto. Ina lengo la kuisafisha serikali. Upepo huo ukizidi serikali pengine inaweza kulazimika kuiunda tume hiyo bila kumhusisha jaji yo yote aliyetajwa na Lissu.
Pili, washukuruni sana waandishi majasiri wa Iringa walioweza kupiga picha matukio yale kwa uwazi kabisa na kuilazimisha serikali ilazimike kusema kweli na hoja ya Tundu Lissu kuhusu uwapo wa majaji wasiotambuliwa na katiba, vinginevyo mngechafuliwa sana na sheria husika kutungwa.
My take;
Hivi propaganda ya Mwangosi kupigwa na kitu kizito imeota mbawa?.
Hivi kama siyo Mungu, kwanini polisi walishindwa kuwazuia waandishi kurekodi tukio lile badala yake walichukua tukio lote wakaondoka na kamera zao Na sasa limekuwa kitanzi kwa serikali?


kwanza iliyoundwa na nchimbi si tume ni kamati (kichwa maji, kila siku unasahau) waziri hana mamlaka ya kuunda tume kikatiba, na kubwa kabisa kesi ipo mahakamani, lets waits and see.
 
Michael kwa mara nyingine tena asante sana.

Naunga mkono, sana tu, hoja ya kwanza 110%.

Hoja ya pili, ni kweli kabisa waandishi wale ukianzia na Mwangosi mwenyewe walikuwa na ujasiri wa ajabu. Ndiposa naunganisha na hoja yako KAMA SIO MUNGU...! Kwa wengi wetu ni mkono na mpango wa Mungu kuwa CCM na vibaraka walikuwa waumbuke hadharani big time. Nazidi kuwapo hongera nyingi sana wale waandishi; kwa heshima niwataje mashujaa wetu wa Iringa:-

1) Daudi Mwangosi (R.I.P.) - aliyebeba ujasiri na umahiri wa kipekee ktk matukio yote ya siku ya kifo chake.
2) Khamis Abdallah - Tanzania Daima
3) J. Mushi - Nipashe
4) Sanga - ?
5) F. Godwin - kujitegemea
6) Assenga - ?

Heshima kwenu wazalendo wetu.

Ahsante sana,
Kuna na wale 2 waliotoa ushuhuda wao kupitia ITV mmoja mrefu wa Tanzania Daima namjua mwingine simjui. Sijajua majina yao vizuri. Hawa ndio mashujaa wetu waliobadilisha mwelekeo wa sakata lote mpaka serikali ikakwama. Sasa wamekwama inabidi wajipange upya kama alivyoandika Ansbert Ngurumo Jumapili hii (maswali magumu)

 
Tumeshindwa kila kitu..., ukiachia wizi wa mali za umma tunachoweza ni kuunda tume. Maji machafu wanatiririka barabarani,naunda tume! Mbuzi amekula ktk shamba la mkulima, NAUNDA TUME! Ni tume juu ya tume ktkat ya tume pembeni ya tume


Halafu zimeundwa tume ngapi na matokeo ya tume hizo ni nini? Na gharama ya kuwezesha hizi tume huwa ni kubwa sana, forget not.
Tume huwa zinaundwa ili kuwasahaulisha watu, hata hivyo, this time tunadai na matokeo hayo tutayadai hata kwa maandamano.
 
Kweli serikali ya CCM imechoka haswa, waachie madaraka kwa amani tu coz kila kitu sasa kinafika ukingoni.

Wako busy wanapanga mitandao ya ushindi ya 2015. Sasa nasikia mitandao inafikia karibu 4.
God forbid.

 
ni ukweli mtupu uliosemwa hapa...na hivi ndivyo serikali zisiyowajibika kwa wananchi zifanyavyo! Tuiondoe CCM madarakani hata tukiweka punda will be a better leader kuliko CCM
 
Dawa ya watawala wetu ni kumwaga mboga na ugali vikiwa bado jikoni vinachemka kama hivi.

Safiii safi sanaaaaaa!!
 
Juzi kwenye maandamano ya Waandishi wa habari nilisikia tamko la kutaka Jeshi la Polisi warudishe Video Camera na Laptop za Marehemu Mwangosi.Je. zimesharudishwa? Kama hazijarudishwa ziko wapi na kwanini Polisi hawataki kuziachia?????


Hawajarudisha wala kutolea maelezo mpaka muda tunapoongea.
 
kwanza iliyoundwa na nchimbi si tume ni kamati (kichwa maji, kila siku unasahau) waziri hana mamlaka ya kuunda tume kikatiba, na kubwa kabisa kesi ipo mahakamani, lets waits and see.

Asante mkuu, maana vitabu vitakatifu vinasema shukuruni kwa kila jambo ikiwemo matusi kama yako japo sijawahi kuandika uzi wo wote kuhusu kamati ya Nchimbi. Nimesha edit.
 
Ahsante kwa kutuelemisha uzoefu wako, lakini ingekuwa vema kama ungetumwagia mchele tulinganishe na pumba.
Ukishaingia ktk mabishano na Zomba & co maana yake wao wameshashinda na watastahili kulipwa posho halali na wewe umeshashindwa. Lengo lao ni kututoa ktk mada hii wasiyopenda ijadliwe - system at work.
 
Ukishaingia ktk mabishano na Zomba & co maana yake wao wameshashinda na watastahili kulipwa posho halali na wewe umeshashindwa. Lengo lao ni kututoa ktk mada hii wasiyopenda ijadliwe - system at work.

Hilo linaeleweka lakini lazima ajibiwe. Mgojwa (km kichaa) anatabiwa siyo kwa kuamua mwenyewe bali ni kwa wajibu wa wale walio wazima. Zomba & Co hawajui wanaumwa, sisi wazima tusichoke kuwapa vidonge hata kwa kulazimishwa.
 
Michael kwa mara nyingine tena asante sana.

Naunga mkono, sana tu, hoja ya kwanza 110%.

Hoja ya pili, ni kweli kabisa waandishi wale ukianzia na Mwangosi mwenyewe walikuwa na ujasiri wa ajabu. Ndiposa naunganisha na hoja yako KAMA SIO MUNGU...! Kwa wengi wetu ni mkono na mpango wa Mungu kuwa CCM na vibaraka walikuwa waumbuke hadharani big time. Nazidi kuwapa hongera nyingi sana wale waandishi; kwa heshima niwataje mashujaa wetu wa Iringa:-

1) Daudi Mwangosi (R.I.P.) - Channel 10, huyu ndiye aliyebeba (epitomise) ujasiri na umahiri wa kipekee ktk matukio yote ya siku ya kifo chake.
2) Abdallah Khamis - Tanzania Daima
3) Godfrey Mushi - Nipashe
4) Clement Sanga - Mwananchi
5) F. Godwin - kujitegemea (?)
6) Joseph Assenga - Tanzania Daima
7) Renatus Mtabuzi - ITV

Heshima kwenu wazalendo wetu, majina yenu nimeyaandika kwa wino wa dhahabu.

Kama siyo hawa makamanda wa ukweli pengine leo story ingekuwa tofauti kabisa. Chadema ikiingia madarakani na kubadilisha maisha ya watz hawa nao wajue kuwa mchango wao wa kiprofession ulikuwa mkubwa sana. ktk siasa tukio moja linaweza kubadilisha kila kitu.
 
Habari za uhakika pia zilimshuhudia mwkt wa bunge sylivester mabumba akisema mwangosi amekomeshwa na kihelehele chake!
 
Tatizo sio matukio, Tatizo ni jinsi nyaraka za serikali zinavyo vuja, mara tu baada ya kutolewa. Nahofu, mkuu wa kaya anazungukwa na watu wa karibu yake kuliko hata anavyo weza kufikiri.
Raisi Fidel Castro alipokuja Dar, miaka ile ya 1979, aliulizwa kwa nini anatembea na bastora kila mahali anapoenda, alijibu kuwa ni kwa sababu hana imani hata na kivuli chake. Mkuu wa kaya ajihadhari, asiwe na imani hata kwa ubavu wake.
 
Hilo linaeleweka lakini lazima ajibiwe. Mgojwa (km kichaa) anatabiwa siyo kwa kuamua mwenyewe bali ni kwa wajibu wa wale walio wazima. Zomba & Co hawajui wanaumwa, sisi wazima tusichoke kuwapa vidonge hata kwa kulazimishwa.

Umenifanya nicheke mwenyewe. Changamoto ni kwamba mpaka sasa almost 1/3 ya wachangiaji wanamjibu yeye - ni idadi kubwa na hapo waka kama 2 tu, wangekuwa 10 ingekuwaje? Na mafanikio yao ni kubadili mjadala. Hata hivyo, nakubaliana na wewe kuwa lazima wajibiwe ila uwongo wao usije ukaaminiwa na baadhi yetu.
 
Mkuu kumwamini au kutomwamini kunategemea logic na ukweli wa yale anayoyasema. Wewe nishawishi kwa hoja kutomwamini.

wachumia tumbo wengi sana dunia ya sasa! huwa unampa shilingi ngapi .. akishamaliza kupika hizo story ambazo huwa anakutonya! .. nimekupa pole sababu habari hazina ukweli wowote na inaelekea akishakupa kisogo anakucheka kimoyomoyo
 
yapingwe maneno ya kinafiki kama hao ya mbowe,,wenye mungu sio yeye ni hawa wananchi wa kawaida wanaomwagwa damu,yy na familia yake wako salama salimiin

Mkuu mbona una hasira sana na mbowe? Taratibu.
Viongozi wetu wa kitaifa nao wanazunguka huko vijijini akiwemo Mbowe mwenyewe hivyo, hata Mbowe naye hayuko salama kama wanachi wengine Morogoro alikuwepo. Siku ya kuuawa kwa Mwangosi Dr Slaa naye hakuwa Dsm. Alikuwepo huko huko Iringa na si Iringa mjini bali vijijini.

 


wachumia tumbo wengi sana dunia ya sasa! huwa unampa shilingi ngapi .. akishamaliza kupika hizo story ambazo huwa anakutonya! .. nimekupa pole sababu habari hazina ukweli wowote na inaelekea akishakupa kisogo anakucheka kimoyomoyo
mkuu Unakumbuka story JK ya Mbayu wayu na Kigong'ota? Huwa akili za kuambiwa nachanganya na Zangu. Kwa maoni yangu, huyu ni mtanzania mpenda amani amani wa nchi yetu.
Halafu nitamlipa shilingi ngapi mkuu, mtu mwenyewe anaendesha Shangingi hata kumchangia mafuta siwezi angalau kwa sasa.
 
Mkuu hizi habari ndo napata kwako.
Lakini hopefully viongozi wetu wa ngazi ya wilaya na mkoa na hata Taifa hawawezi kukaa kimya. Nitawataarifu wahusika. Hatulali mkuu.

a


Micahel.

Hili kama ni kweli kuna watu wamekamatwa tunaomba wapate msaada wa kisheria hata ikibidi wachangiw ili wapate mdhamana na taratibu nyingine za kisheria ziendelee. Sambamba na hili naomba wewe kama mjube wa vijana utujuze ni lini mchango kwa familia ya marehemu utafanywa
 
Back
Top Bottom