Mikael Aweda
JF-Expert Member
- Dec 17, 2010
- 2,973
- 3,901
Wakuu,
Nilipata fursa ya kuwasiliana na mtonyaji wetu ambaye ameniambia kwamba Chadema tuwashukuru sana waandishi wa habari za Iringa na Tundu Lissu kwa sababu wameifanya serikali ishindwe kitu cha kufanya katika sakata la Mwangosi.
Awali ya yote alisema Ifahamike kuwa;
Serikali haikutaka kabisa kumshtaki askari wake kwa kuwa hilo litawafanya Askari kupungukiwa na ujasiri wa kuwathibiti Chadema kwa hofu ya kushtakiwa mbele ya safari, na ndo maana walichelewa kuchukua hatua wakipisha upepo wa Mwangosi upite – upepo ukagoma kupita hasa baada ya waandishi kuandamana. Hili jambo nalo lilizua mjadala wa ndani lakini mwisho ikalazimika walau kumshtaki.
Pili, Serikali kwa sasa haiko tayari kuunda tume ya uchunguzi ya kimahakama kama inatavyotakiwa kisheria na kama ilivyoombwa na Chadema, wanahabari, wananchi nk.
Nini kimeitatiza serikali?
Mosi, uundaji wa Tume ya kiuchunguzi wa kimahakama umekwama kwa sababu Majaji wote ambao wangeweza kuisaidia serikali endapo uchunguzi utaleta sura mbaya zaidi dhidi ya Serikali, wako ktk Listi ya Tundu Lissu. Hili ndilo tatizo kubwa sana. Tatizo kubwa ktk maelezo/utetezi wa Lissu ni Lissu kuwa na ripoti ya mapendekezo ya kamati ya Rais ya kuchunguza majaji walio kinyume na katiba. Ripoti hiyo ilionesha kwamba majaji waliomaliza muda wao wakaongezewa muda na Rais ni kinyume na katiba ya nchi kama ilivyoelezwa na Lissu Bungeni kwa kujiamini. (kisha Kumbuka maelezo ya utetezi wa tundu Lissu hapa JF). Hawa ndio walikuwa wawe tegemeo la Serikali ktk sakata hili na ndio hawateuliki kwa sababu itaanzisha mjadala wa Lissu na kuupanua zaidi.
Lengo lilikuwa ni tume ambayo uchunguzi wake usiiumize serikali badala yake uelekeze tuhuma kwa ama chadema au vurugu wananchi. Na pili, upendekeze kuundwa kwa sheria ya kudhibiti mienendo ya vyama vya siasa na hasa maandamano. Kwa hiyo, azimio lililopo ni kwamba Tume hiyo haitaundwa kwa kuwa serikali ina hofu ya kuchafuka zaidi.
Pili, sakata la Iringa kwa jinsi lilivyorekodiwa ktk kamera na picha zilizokwisha kurushwa ktk vyombo vya habari ni tatizo. Tatizo jingine kubwa ni hofu ya serikali kutojua vitu vilivyopo ktk kamera za waandishi wahusika kama zipo taarifa zilizofichwa hadi sasa. Kwa hiyo, mambo haya (kama yapo yaliyofichwa) yakiletwa kwenye tume ya kimahakama yanaweza kuleta sura ambayo ingeshindikana kwa tume ya kimahakama kuisafisha serikali badala yake serikali ikaingia ktk tope kubwa zaidi bila kujali kama Tume inaongozwa na jaji wa aina gani (neutral au one sided).
Kwa hiyo, mambo mawili hapo juu yameiharibia kabisa serikali ktk mpango wake wa kuithibiti sakata hili na sasa tuko njia panda.
Na ni mambo hayo hayo ndo yalimfanya Rais ashindwe kuongea na wananchi kwa sababu hana cha kusema, jambo lililowafanya walazimike kumtuma Steven Wasira aje aongee kwa Niaba ya Rais kupunguza hasira za wananchi. Hata hivyo, wengi wanamlaumu Wasira huku serikali kwa madai kuwa heri asingeongea kwa kuwa hakufanikiwa kabisa kufanya kile alichotumwa. (Awali hotuba ya Wasiri ilikuwa aitoe Rais mwenyewe)
Nakumbuka kulikuwa na uzi wa Rais kuongea na waandishi humu JF kabla ya wasira kama sikosei.
Ushauri wake:
Chadema waendelee kudai Tume ya uchunguzi ya Kimahakama kwa kuwa tume ya Nchimbi aka kamati ya Nchimbi ni danganya toto. Ina lengo la kuisafisha serikali. Upepo huo ukizidi serikali pengine inaweza kulazimika kuiunda tume hiyo bila kumhusisha jaji yo yote aliyetajwa na Lissu.
Pili, washukuruni sana waandishi majasiri wa Iringa walioweza kupiga picha matukio yale kwa uwazi kabisa na kuilazimisha serikali isema kweli bila kusahau hoja ya Tundu Lissu kuhusu uwapo wa majaji wasiotambuliwa na katiba, vinginevyo mngechafuliwa sana na sheria husika kutungwa.
My take:
Hivi propaganda ya Mwangosi kupigwa na kitu kizito imeota mbawa?
Hivi kama siyo Mungu, kwanini polisi walishindwa kuwazuia waandishi kurekodi tukio lile badala yake walichukua tukio lote wakaondoka na kamera zao Na sasa limekuwa kitanzi kwa serikali?
FREEMAN MBOWE; WAO WANA RISASI NA MABOMU SISI TUNA MUNGU.
Nilipata fursa ya kuwasiliana na mtonyaji wetu ambaye ameniambia kwamba Chadema tuwashukuru sana waandishi wa habari za Iringa na Tundu Lissu kwa sababu wameifanya serikali ishindwe kitu cha kufanya katika sakata la Mwangosi.
Awali ya yote alisema Ifahamike kuwa;
Serikali haikutaka kabisa kumshtaki askari wake kwa kuwa hilo litawafanya Askari kupungukiwa na ujasiri wa kuwathibiti Chadema kwa hofu ya kushtakiwa mbele ya safari, na ndo maana walichelewa kuchukua hatua wakipisha upepo wa Mwangosi upite – upepo ukagoma kupita hasa baada ya waandishi kuandamana. Hili jambo nalo lilizua mjadala wa ndani lakini mwisho ikalazimika walau kumshtaki.
Pili, Serikali kwa sasa haiko tayari kuunda tume ya uchunguzi ya kimahakama kama inatavyotakiwa kisheria na kama ilivyoombwa na Chadema, wanahabari, wananchi nk.
Nini kimeitatiza serikali?
Mosi, uundaji wa Tume ya kiuchunguzi wa kimahakama umekwama kwa sababu Majaji wote ambao wangeweza kuisaidia serikali endapo uchunguzi utaleta sura mbaya zaidi dhidi ya Serikali, wako ktk Listi ya Tundu Lissu. Hili ndilo tatizo kubwa sana. Tatizo kubwa ktk maelezo/utetezi wa Lissu ni Lissu kuwa na ripoti ya mapendekezo ya kamati ya Rais ya kuchunguza majaji walio kinyume na katiba. Ripoti hiyo ilionesha kwamba majaji waliomaliza muda wao wakaongezewa muda na Rais ni kinyume na katiba ya nchi kama ilivyoelezwa na Lissu Bungeni kwa kujiamini. (kisha Kumbuka maelezo ya utetezi wa tundu Lissu hapa JF). Hawa ndio walikuwa wawe tegemeo la Serikali ktk sakata hili na ndio hawateuliki kwa sababu itaanzisha mjadala wa Lissu na kuupanua zaidi.
Lengo lilikuwa ni tume ambayo uchunguzi wake usiiumize serikali badala yake uelekeze tuhuma kwa ama chadema au vurugu wananchi. Na pili, upendekeze kuundwa kwa sheria ya kudhibiti mienendo ya vyama vya siasa na hasa maandamano. Kwa hiyo, azimio lililopo ni kwamba Tume hiyo haitaundwa kwa kuwa serikali ina hofu ya kuchafuka zaidi.
Pili, sakata la Iringa kwa jinsi lilivyorekodiwa ktk kamera na picha zilizokwisha kurushwa ktk vyombo vya habari ni tatizo. Tatizo jingine kubwa ni hofu ya serikali kutojua vitu vilivyopo ktk kamera za waandishi wahusika kama zipo taarifa zilizofichwa hadi sasa. Kwa hiyo, mambo haya (kama yapo yaliyofichwa) yakiletwa kwenye tume ya kimahakama yanaweza kuleta sura ambayo ingeshindikana kwa tume ya kimahakama kuisafisha serikali badala yake serikali ikaingia ktk tope kubwa zaidi bila kujali kama Tume inaongozwa na jaji wa aina gani (neutral au one sided).
Kwa hiyo, mambo mawili hapo juu yameiharibia kabisa serikali ktk mpango wake wa kuithibiti sakata hili na sasa tuko njia panda.
Na ni mambo hayo hayo ndo yalimfanya Rais ashindwe kuongea na wananchi kwa sababu hana cha kusema, jambo lililowafanya walazimike kumtuma Steven Wasira aje aongee kwa Niaba ya Rais kupunguza hasira za wananchi. Hata hivyo, wengi wanamlaumu Wasira huku serikali kwa madai kuwa heri asingeongea kwa kuwa hakufanikiwa kabisa kufanya kile alichotumwa. (Awali hotuba ya Wasiri ilikuwa aitoe Rais mwenyewe)
Nakumbuka kulikuwa na uzi wa Rais kuongea na waandishi humu JF kabla ya wasira kama sikosei.
Ushauri wake:
Chadema waendelee kudai Tume ya uchunguzi ya Kimahakama kwa kuwa tume ya Nchimbi aka kamati ya Nchimbi ni danganya toto. Ina lengo la kuisafisha serikali. Upepo huo ukizidi serikali pengine inaweza kulazimika kuiunda tume hiyo bila kumhusisha jaji yo yote aliyetajwa na Lissu.
Pili, washukuruni sana waandishi majasiri wa Iringa walioweza kupiga picha matukio yale kwa uwazi kabisa na kuilazimisha serikali isema kweli bila kusahau hoja ya Tundu Lissu kuhusu uwapo wa majaji wasiotambuliwa na katiba, vinginevyo mngechafuliwa sana na sheria husika kutungwa.
My take:
Hivi propaganda ya Mwangosi kupigwa na kitu kizito imeota mbawa?
Hivi kama siyo Mungu, kwanini polisi walishindwa kuwazuia waandishi kurekodi tukio lile badala yake walichukua tukio lote wakaondoka na kamera zao Na sasa limekuwa kitanzi kwa serikali?
FREEMAN MBOWE; WAO WANA RISASI NA MABOMU SISI TUNA MUNGU.