Luteni
JF-Expert Member
- Jan 9, 2010
- 2,274
- 302
MWENYEKITI wa Chama Cha Democratic (DP), Mchungaji Christopher Mtikila, amesema kitendo cha serikali kutaka kuilipa Kampuni ya Dowans ni sawa na ujambazi na kwamba Mungu ameitumia kampuni hiyo kumuondoa Rais Jakaya Kikwete madarakani.
Akizungumza jijini Dar es Salaam, Mtikila aliungana na Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta, kupinga serikali kuilipa kampuni hiyo Sh94 bilioni zilizotokana na hukumu ya Mahakama ya Usuluhishi ya Biashara ya Kimataifa (ICC).
Unajua mwisho wa utawala wa Rais Kikwete unaweza ukawa umejifinya nyuma ya hili suala la Dowans, kwa kuwa kila mtu sasa anajua Dowans ni nini, na kila mtu anajua ni uporaji, alisema Mtikila.
Alihoji sakata hilo kuwa gumzo nchini bila kutolewa ufafanuzi wowote na rais na kuongeza kuwa, ukimya wa Rais Kikwete unaibua maswali mengi ndani ya vichwa vya Watanzania.
Kwa nini Rais Kikwete hataki kuzungumzia Dowans, silence implies concerned (kimya kinamaanisha husika), siafiki kabisa serikali kuilipa Dowans, huu ni wizi na kama wananchi wakiamua kuingia mtaani kupinga jambo hili sidhani kama polisi wataweza kuwazuia, kwa kuwa wako wachache na risasi zao hazitatosha, alisema Mtikila.
Source: Gazeti la Mwananchi.