Mtei amefilisika kimawazo - Zitto

mwasisi wa chadema edwin mtei anahitaji kupewa ushauri wa kinasaha na si kumlaumu na kumtolea kauli za kumdhalilisha, kwani ugonjwa huu wa udini unaomsumbua Mtei, dawa dawa yake ni ushauri na nasaha si kumlaumu au kumtusi.
 
si kwamba amefilisika kimawazo bali hayo ndiyo mawazo yake..ye sasa ndo anataka kuonyesha chama chake ni cha ukatoliki!! kwa hilo amechemka
 
Labda nikusaidie hivi, Memorundum of understanding sio Mkataba. Ukisha elewa tunachozungumzia rtudi tena..

1. Memorandum of understanding (MoU)
is a document describing a bilateral or multilateral agreement between parties. It expresses a convergence of will between the parties, indicating an intended common line of action. It is often used in cases where parties either do not imply a legal commitment or in situations where the parties cannot create a legally enforceable agreement. It is a more formal alternative to a gentlemen's agreement..

2. Contract
A contract is an agreement entered into voluntarily by two parties or more with the intention of creating a legal obligation..


Kitu gani kipya ulichozungumza hapa? Hebu wewe kwanza tuonyeshe ni kifungu gani cha Katiba kinachokataza serikali kuingia kwenye MoU na mashirika ya kidini? MoU inaingiwa mara nyingi kama hatua ya awali ya kuingia kwenye Mkataba au kama ambavyo wikipaedia inavyosema pale ambapo wahusika wasingependa kuingia katika mkataba. Hii si lazima iwe ni kutokana na kuzuiwa na Katiba bali hata kuogopa kutoeleweka mbele ya wananchi. Hii MoU iliingiwa baada ya serikali kutambua kuwa haina uwezo wa kutoa huduma bora katika nyanja za elimu na afya kwa wananchi wake. Serikali ilikuwa imeshindwa kukarabati au kuendeleza shule na hospitali walizotaifisha kutoka kwa mashirika ya kidini. Mfano hai ni kaangalie hali ya shule ya Tambaza na ulinganishe na pale ilipokuwa Aga Khan Secondary School. Kutokana na ukweli huo ndipo mawasliano yalipofanyika kati ya serikali na wale waliokuwa wakimiliki shule na hospitali hizo kabla ya kutaifishwa. Mashirika ya kikristu yalikubali kurudishiwa shule na hospitali ili mradi serikali iwahakikishie kuwa haitakuja kuzitaifisha tena pale itakapoona hali imebadilika. Bila shaka ni sababu za kisiasa zaidi kuliko za kisheria ndizo zilizowafanya waone kuwa ni heri waingie kwenye MoU badala ya Mkataba. Tukumbuke kuwa ingawa MoU sio mkataba lakini haizuii pande moja kuutumia katika kudai haki zake kama upande mwingine hautamtendea haki. Leo hii tuanweza kuwapeleka watoto wetu St. marian au Feza bila wasiwasi wowote. Leo hii tunaweza kuwapeleka wagonjwa wetu Bugando au KCMC bila wasi wasi wowote. halafu nyie bado mnaibeza MoU!

Pili. Ingekuwa Mahakama ya Kadhi inatakiwa iwe nje ya mfumo wa serikali basi pasingekuwa na haja ya kudai ipate kibali cha bunge. Ni kama vile wakatoliki waende Bungeni kudai kuwa Bunge lipitishe sheria ya kuzuia matumizi ya Kondom kwa vile matumizi hayo kwao ni dhambi.



Ninatofautiana nawe kuhusu Mtei. Mzee Mtei ni Mbunge wa Zamani, Gavana wa Benki kuu ya Tanzania na Waziri wa fedha. Kwa katiba iliyokuwepo wakati wake, yeye alikuwa ni mmoja wa 'watarajiwa wa urais' yangetokea yasiyotarajiwa.


Nina maana sifa zake za elimu, uzoefu wake, pamoja na kuwa waziri mwandamizi (senior minister)
Mzee Mtei ni mwanasiasa na mwanzilishi wa Chadema. Sifa za mzee wetu zinamweka mahali tofauti sana na rai kama wewe na mimi. Edwin Mtei yenyewe ni habari kabla ya habari.


Kauli zake zinapewa uzito sana ndiyo maana unaona badala ya kujadili katiba watu wanabadilishana kashfa utadhani tupo katika makanisa na misikiti, utadhani tunaandika biblia na misahafu.
Hali isingekuwa hivyo kama kauli hiyo ningeitoa kapuku mimi, lakini ni upele na sasa umewapata wenye kucha


Ni kutokana na influency yake kitaifa kauli alizozitoa zinapaswa zilinganiwe na yeye mwenyewe. Ima azitolee ufafanunuzi au kama hana aombe radhi. No more no less

Mtei ni raia na ni mwanachama wa Chadema asiye msemaji wa Chama chake. Pamoja na misifa yote mnayommwagia ana haki ya kuzungumzia chochote akitakacho bila kujali chama chake kina mtazamo gani. Mbowe hana haki hiyo, Slaa hana haki hiyo, Zitto hana haki hiyo, Mnyika nae hana haki hiyo. Kama kweli ana influence kubwa kiasi hicho kwa nini basi hakuwashawishi viongozi wake watoe tamko linalofanana na alilolisema? Hauoni kuwa pengine alijua kuwa viongozi wa chama chake wasingeweza ndio maana akajisemea mwenyewe? Kama alivyofanya Nyerere kabla yake. Sasa tuseme kwa vile Nyerere aliweza kukilazimisha chama chake kiangalie upya suala la utanganyika au OIC basi alikuwa msemaji wa chama! Chama kilikuwa na uwezo wa kumkana na asingeweza kufanya lolote nje ya kulalamika nje na kuwashawishi watanzania wasikipigie kura safari ijayo! Mtei hivyo hivyo. Chama chake kinaweza kupuuza maneno yake na yeye asiwafanye kitu. Alichokisema Mtei ni kile ambacho wamisheni wengi wanakisema wanapokuwa wenyewe au hata wanapokuwa makanisani mwao. Wanachokisema wakina Mkandara ni kile ambacho waislamu wengi wanakisema wanapokuwa wenyewe au wakiwa kwenye misikiti yao. Hizi si zama za Nyerere. Dini imeingia na inatumiwa vibaya na wengi wetu. Badala ya kujaribu kukificha kidonda ni heri tukiache wazi ili tiba iweze kupatikana. Mtei apingwe kwa hoja na si kwa vitisho na shutuma.

Amandla.......
 
Kaongea na Jambo leo tu au ndo habari na mwandishi wetu

ndugu yangu hawa mijamaa ya jamba leo ni mapuuzi sana, yani yanakuza mambo kishenzi, yani baada ya rais kutangaza tume, kila mtu alitoa maoni yake kwa namna anavyo jua yeye, siku hiyo ndo zitto kaandika kwenye ukurasa wake wa tweeter kuwa yeyote atakayepinga tume iliyo tangazwa na rais kwa misingi ya dini, kabila au ukanda amefilisika mawazo, sina hakika kama wakati mtei alishatoa maoni yake wakati huo, wanachofanya jamba leo ni kumchonganisha mzee mtei na zitto wapate cha kuandika wawafurahishe mijamaa fulani.
 
Hayo maneno ya mtei angekuwa kaongea sheikh kuhusu wakristo ungesikia hawa wanapenda udini wasubiri wakale ubwabwa kwa vile ni baba mkwe yanakuwa ni mawazo yake binafsi sasa ndio mtajua udini upo au haupo chafya ikija huwezi izuia

kwani mzee ana kosa gani? kwani ni uongo kuwa waislamu ni wengi (23, wakristu 11?). Hawaendi kuswalisha lakini hata kama mtei asingeongea mapema wengine wangeyaona baadae tu. Tulitaka tume iwe na usawa so mtu akiona huo uwiano lzma atajihoji maswali 2.
 
Bado nasisitiza hoja yangu. Baada ya mtu yeyote kufikisha umri wa miaka 70 apumzike SIASA za hadharani. Mzee Mtei na wazee wengine nchi hii wangepumzika sasa. Wabaki kuwa washauri wa ndani tu kwa watakaohitaji ushauri wao. Wamechoka. Wamefanya na kusema mengi mazuri tu kwa nchi hii. Wakiendelea kung'ang'ana kufanya SIASA watakuwa kama kale kazee ka Senegal.
Nilimshangaa sana Rais wangu JMK kuteua wazee sana akina Warioba kuongoza tume ya Katiba ya Mpya ambayo wazee hawa hawataishi kwa miaka angalau kumi kuiona ikifanyakazi. Kwa umri wa Warioba, SAS, Mtei, Augustino Ramadhani, Butiko,..., wanasimamia mchakato ambao hauwahusu kabisa. Jirani zetu hapa Kenya waliosimamia mchakato huu ni vijana sana. Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi ya Kenya ni kijana mdogo mwenye asili ya Kisomali.
 
Mkuu wangu nitakukumbusha kitu kimoja muhimu sana ufahamu. Viongozi wa Palestine waliwahi kusema kwamba wataizamisha Israel ndani ya bahari wakiwa na maana kuuondoa utawala wa kukoloniwa madarakani.. Huu ni msemo ulotumiwa na kina Che, Castro, Mao Tse Tung na hata Mandela South Afrika enzi za makaburu lakini nini kimewakuta Wapalestina?
Dunia nzima wanaamini kwamba lengo la nchi za kiarabu ni kuipiga mabomu Israel hadi izamishwe baharini.. Maneno haya yamewaponza Wapalestina badala ya kuwanufaisha kama waliotangulia..Sasa jiulize kama Wapestine wana nia hiyo, wakiisha izamisha Israel baharini wao wataishi wapi?..haiingi akilini lakini ndio walishasema maana siku hizi mpigania Uhuru huitwa gaidi..

Kwa hiyo kauli yoyote ile inaweza kuwa na ukweli wala sii uongo, lakini inategemea na itakavyo tafsirika na muhimu sana kutumia busara ktk maswala mazito kama haya maana inaweza kabisa kula kwako. Mzee Mtei alikosea na tumkosoe kama alivyokosolewa Malecela ktk swala la Muungano japokuwa alisema kweli. Ifahamike tu kwamba kuwepo kwa serikali tatu kama tunavyodai baadhi yetu kuna athari zake.

Kuwa na serikali tatu kwa jinsi sisi tulivyo na ktk mazingira yetu ni hatua moja karibu kuvunja muungano kuliko kuuimarisha muungano amini maneno yangu. Na maadam binafsi yangu sintojali mojawapo nayapokea kama yalivyo lakini najua fika serikali tatu itakuwa mwanzo wa kuvunja muungano. Kama leo tupo radhi kumkosoa rais wetu JK, tupo radhi kumkosoa mwenyekiti Mbowe, katibu mkuu Dr.Slaa na naibu katibu mkuu wa chama Zitto tunashindwa vipi kumkosoa Mzee Mtei..

nimekusikia mkuu. awali ya yote, na-declare position yangu kwenye hii debate..... mimi ni mkristo.

the irony behind my earlier post ni kwamba kuna mambo ambayo kwenye mchakato huu wa katiba mpya kama hatutayapekenyua to the finest details (inside-out, upside-down, back n forth, black n white), kuna uwezekano wa kupata katiba yenye mizizi ya kinafiki. so, let's put everything on the table now and chew it to the last bit.

uchokonozi aliouanzisha mtei usinge-attract a heated and intense debate like this kama uchokonozi huu ungekuwa umeanzishwa na a nobody like "m-mbabe". that's why nimependezewa sana kwamba ni mtei (or hata kama ingekuwa equivalent dignitaries like mkapa, lipumba, mwinyi, etc) ndiye aliyechokoza mada hii.

otherwise, arguments zako katika huu mjadala kuhusu position ya uislam ni more than valid.
 
CHADEMA WAWE MAKINI SANA NA ZITTO. Sijawahi kupenda jinsi Zitto anavyoshughulikia mambo. Amekuwa akijitafutia sifa peke yake, masuala mengi anayoyasema ni kama anafanyakazi independently na hakitakii mema chama hata siku moja
 
Simu ya lulu iliyomuua STEVEN KANUMBA usiku wa manane alikuwa anachati na Mheshimiwa Zitto Zuberi Kabwe.
Kanumba alipata mshtuko na kupata hasira baada ya kusikia LULU akisema Mh. Zitto I Love you than any body TAKE A KISSY MWAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAA
 
Kama huamini Zitto ametafuta mawakili wa kumtetea LULU ili akitoka amuoe. Pia kafanya mpango wa kufoji cheti cha kuzaliwa LULU aonekane ana miaka 17 wakati mwenyewe siku ya Birthday yake alionesha cheti cha miaka 18. Je ZITTO ana maaana gani kudanganya umma umri wa lulu. Pia LULU akihojiwa na SALAMA Kwenye EAT TV alikiri KUTIMIZA MIAKA 18
 
iyo katiba mpya kuliko kushuudia mahakama ya kadhi na nchi inaingizwa oic..bora tumwagane damu kupigania iman zetu ili tuone Jesus na mwamedi nani kamanda.

Ma2mbo,
I love your consistency. But this time, please call a spade a spade.

Kama nchi inaingia OIC kupitia referundum tatizo liko wapi?mahakama ya kadhi inawakera nini? Mbona tuna uhusiano wa kidiplomasia na vatican? Mimi ni mkristu,ila natanguliza utaifa wangu mbele ya itikadi za kidini na kikabila.Kwa kweli dini ikipokelewa vibaya inaweza kugeuka kuwa uchawi mbaya kuliko ushirikina wowote ule

Kwa vijana,tuache kuunga mkono watu hata kama wamekosea.picha ninayopata hapa ni kwamba tunaandaa taifa la ovyo
 
Simu ya lulu iliyomuua STEVEN KANUMBA usiku wa manane alikuwa anachati na Mheshimiwa Zitto Zuberi Kabwe.
Kanumba alipata mshtuko na kupata hasira baada ya kusikia LULU akisema Mh. Zitto I Love you than any body TAKE A KISSY MWAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAA

Kama huamini Zitto ametafuta mawakili wa kumtetea LULU ili akitoka amuoe. Pia kafanya mpango wa kufoji cheti cha kuzaliwa LULU aonekane ana miaka 17 wakati mwenyewe siku ya Birthday yake alionesha cheti cha miaka 18. Je ZITTO ana maaana gani kudanganya umma umri wa lulu. Pia LULU akihojiwa na SALAMA Kwenye EAT TV alikiri KUTIMIZA MIAKA 18


UMMATI,

Una uhakika na hili unalosema?imekuwa ni tabia kwa watu kutumia ID fake kuchafua wengine kwa maslahi binafsi.Kama haya unayosema ni kweli katoe ushahidi polisi ili haki itendeke.Vinginevyo huu ni mwendelezo wa hila za kuchafua watu kwa nguvu zote kukidhi matakwa binafsi,na mwendelezo huu ni wa kushusha hadhi ya JF

Steve Kanumba ametangulia mbele za haki.Tumuache apumzike tuache kutumia kifo chake kukidhi matakwa binafsi ya kisiasa ai ya kiitikadi kwa maslahi binafsi.Hebu tuwe wastaarabu,tuwe na ubinadamu hata kama tunatumia ID fake

Besides,Zitto kama anatumia mawakili kumtetea Lulu kuna kosa gani? Tuna tatizo la kutoa hukumu bila kufikiria.Haki itendeke na ndicho kinachotakiwa katika kujenga taifa lenye kuzingatia utawala wa sheria.Mtuhumiwa yeyote ana haki ya kusaidiwa kisheria.Tuache ubinafsi,tuache matamanio binafsi na mihemko(emotions)
 
Tusibishe kitu bila kuchunguza kwa makini. Jamani kuna neno Mtei kasema si la kweli? Kweli tume ndio ilivyo kwanini tubishe. Pia mzee anauzoefu kaona tume nyingi na zilizopita na changamoto zake.
 
Simu ya lulu iliyomuua STEVEN KANUMBA usiku wa manane alikuwa anachati na Mheshimiwa Zitto Zuberi Kabwe.
Kanumba alipata mshtuko na kupata hasira baada ya kusikia LULU akisema Mh. Zitto I Love you than any body TAKE A KISSY MWAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAA

Hivi,

Wewe unajua kutumia fake id sio kigezo cha kuficha identity yako. Ningelikuwa moderator au nafanya kazi usalama wa taifa nina uwezo kukujua wewe nani na usiombe mungu kama unatumia computer au simu yenye camera kwani ningeliweza hata kupata picha yako. Usifikiri kuna kujificha katika ulimwengu wa utandawazi jaribu kutumia akili sometimes. Kama una evidence nenda zako pale Salender ukatoe vithibitisho vyako na sio kuwa unabwata bwata kama kuku hapa JF. Kapish!!!
 
Ma2mbo,
I love your consistency. But this time, please call a spade a spade.

Kama nchi inaingia OIC kupitia referundum tatizo liko wapi?mahakama ya kadhi inawakera nini? Mbona tuna uhusiano wa kidiplomasia na vatican? Mimi ni mkristu,ila natanguliza utaifa wangu mbele ya itikadi za kidini na kikabila.Kwa kweli dini ikipokelewa vibaya inaweza kugeuka kuwa uchawi mbaya kuliko ushirikina wowote ule

Kwa vijana,tuache kuunga mkono watu hata kama wamekosea.picha ninayopata hapa ni kwamba tunaandaa taifa la ovyo

wewe kama hauoni tatizo kwa nchi kuingia oic na kuwa nchi ya kiislamu,mimi siwezi kukubali hii kitu niishudie kwa macho yangu ikibidi ata kumwaga damu yangu kuzuia hii movement ya kuibadili nchi yetu kuwa ya kiislamu...kama jk ameteua masheikh wenzake kutimiza azma inayoubiriwa kila siku na redio iman basi ajue amechemsha..tutapambana mpaka cell ya mwisho..

Ben achana na Zitto uyo,hana lengo zuri tizama ata watu wanaomuunga mkono,alafu ufikirie mara mbilimbili..
 
wewe kama hauoni tatizo kwa nchi kuingia oic na kuwa nchi ya kiislamu,mimi siwezi kukubali hii kitu niishudie kwa macho yangu ikibidi ata kumwaga damu yangu kuzuia hii movement ya kuibadili nchi yetu kuwa ya kiislamu...kama jk ameteua masheikh wenzake kutimiza azma inayoubiriwa kila siku na redio iman basi ajue amechemsha..tutapambana mpaka cell ya mwisho..

Ben achana na Zitto uyo,hana lengo zuri tizama ata watu wanaomuunga mkono,alafu ufikirie mara mbilimbili..

Acha kutisha watu wewe,

Na sisi waislamu hatutaki kuendelea kuwa nchi inayotumika na kanisa. Hii ni nchi yetu sote tutapambana na wewe hadi tone la mwisho la damu yetu. Fikiria mara mbili kauli zako hizo. Nimewauliza katika thread ya mahakama ya kadhi na OIC nipeni hasara za OIC hamna? Nimewauliza mbona Uganda na Nigeria wapo OIC nyie kinawazuia nini? Mbona wamarekani wameomba kuwa observatory member nyie kisebusebu cha nini???

Tuondoleee ujinga wako hapa hii tanzania yetu sote tutapambana na wewe hadi cell ya mwisho.
 
Uwongo kwani!!! Zitto nadhani ana lake jambo hapo. Au naye ni mwislam? Unajua linapokujaga suala la kutetea dini ya mtu uwezo wa kufikiri na kutambua HUZAMA nadni ya CHOO cha shimo na kufukiwa!!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom