Mtei alipotofautiana na Mwalimu Nyerere

Kama huyu jamaa amepewa kazi rasmi ya kuzusha majungu hapa CCM wamechemka. Maana jamaa anajua kutembeza kalamu lakini siyo kujenga hoja. Hakuna mahali popote alipotoa ushahidi kulinda hoja zake bali anajaribu kuunganisha mambo na matukio yasiyo na uhusiano. Kwa mfano hakuna popote anapoonyesha kwamba kweli Nyerere alikuwa na chuki na Mtei. Angewezaje basi amfanye Gavana wa Benki Kuu, Katibu Mkuu, Waziri, Katibu Mkuu wa EAC na baadaye (baada ya kuacha Ugavana) kumfanya mwakilishi wa Kanda ya Afrika kwenye IMF? Kwangu hii inaonyesha imani badala ya chuki. Ni watu wajinga sana wanaoweza kuamini upuuzi wake.

Mtu mjinga hawezi kujua contradiction ipo wapi...anaangaika tu kuunganisha ili na lile na kujenga sababu kama vile za ajira ya Mtei iliwezekana kwa vile hawakuwepo wasomi (This is a credit to Mtei, by the way)
 
Ni wazi kuwa Edwin Mtei hakufanya uamuzi sahihi kumpa ushauri mbovu kama ule Mwl Nyerere and good enough Nyerere alikuwa anaona mbalimbali alishasoma alama za nyakati akakataa lakini kinachonisikitisha ni baadhi ya watanzania ambao kwa sababu zao za kisiasa wanataka kirahisirahisi kwa hoja dhaiu kutushawishi kuwa Mtei alkuwa sahihi lakini ni uongo tu.
 
Kuna maswali ya msingi umeulizwa hujajibu kama kweli kuna hoja katika hili@Ernesto Angalia na usome vizuri tena jamiiforum! pili Mtei Hahusiani kabisaa na nini watanzania wanachotaka kwa sasa Naamini Chadema inaendeshwa kwa kufuata sheria na katiba yake kama sivyo serikali ingeifuta siku nyingi tuu kwenye ramani ya vyama vingi msingi mkubwa umejengwa, nasi tunasonga mbele kama taifa hakuna haja ya kurudi nyuma kwa visingizio vya maisha binafsi ya viongozi waliopita.kama hoja ni historia nadhani inajieleza yenyewe wewe Ernesto hujapewa kazi na watanzania uunganishe vipande vya maelezo yako eti tuamini kama ni historia hiyo. pia ndugu zangu kufanikiwa au kutofanikiwa kwa sera za Mtei nadhani angehukumiwa zaidi kama zingezingatiwa chini yake kama zilifuatwa baada ya yeye kuwa nje ya serikali hawezi kulaumiwa kwa matokeo yeyote kwa sasa huwezi toa lawama ya kutofanikiwa kwa mradi ambao muanzirishi wake hakuwepo kazini katika utekelezaji wake.
 
..........kwangu mimi nikihusanisha hoja kama Edwin Mtei ni muanzilishi wa CHADEMA halafu kaboronga basi hili lina athari kwa CHADEMA yote kwa maana hata samaki akioza basi wote wameoza kwanza CHADEMA ijisafishe kwa hili...........

....................Amin's limited education could not fathoom the consequenses of his acts............yoweri museveni(sowing a mustard seed in uganda a struggle for freedom and democracy published in 2004)
 
kanda2,

..kwa mtizamo wangu tulipaswa kuchukua ushauri wa Mtei kabla hali ya uchumi haijaharibika kabisa. tungechukua hatua zile mapema basi tungekuwa na leverage zaidi ktk ku-neogotiate na IMF/WB.

Sikubaliani na yale maaeneo ya mjadala huu yanayotaka tuamini eti UCHAGA wa CHADEMA ni mkakati wa kichama na sio ujinga wa watu wachache ambao wanadhani kuwa hilo litasaidia katika kufanikisha matamanio yao na wala sikubaliani kuwa Mzee Mtei ni mmoja wa waumini wa ujinga huo kwani hata hivi majuzi yeye ndiye alikuwa mstari wa mbele katika kupigia debe umuhimu wa kupanua chama na kumzuia Freeman kulazimisha watu wake wapewe nafasi za juu katika nafasi za viti maalum.

Naweza kupishana na Mzee Mtei Kifalsafa na kiitikadi lakini sio uzalendo wake kwa Tanzania.

Lakini, ktika suala hili la Mzee Mtei na WB/IMF nina haya yafuatayo;

Hivi katika enzi zile za Reaganate and Thatchirite exterem right resurgence kulikuwa na uwezekano wowote kwa ka-Tanzania ketu kuwa na leverage ya kunegotiate na IMF and WB ambao walichukua kila ushauri wafuasi wa hawa Makaburu walioapa kuimaliza third world yote kama haitafuata na kuunga mkono aina ya dunia waliyokuwa wakiitaka wao. Hivi mnajua lugha waliyokuwa wakiitumia hawa ECONOMIC HITMEN waliokuja kumlazimisha Mwalimu kukubali matakwa yao na kuweza kupata support kwa Mzee Mtei?

Na unawezaje kuwa na leverages za kunegotiate na WB na IMF wakati ndio kwanza umetoka vitani hohehahe....

Hujui kuwa imechukua hadi miaka ya 2000 ndipo angalao Mkapa akaweza kujenga mazingira ya katusaidia kuanza kutofuata kila kilichomo katika blueprint za Washington na kujaribu kuja na kitu ambacho kina angalao kiasi fulani cha input yetu kwa jina la MKUKUTA?

Na kwa wale wanaodhani kuwa tungefuata huo ushauri wa Mtei tukafuata hizo dozi za IMF tokea wakati huo, huu mgawanyiko wa kipato/kitabaka uliopo sasa ambao ni moja kwa moja ni zao la sera za WB/IMF si ungeshafika kileleni ambako hata mimi na wewe tusingeweza kuvumiliana?
 
Uzuri ni kwamba Nyerere mwenyewe alikiri kwamba serikali yake iliboronga....na akawasihi successors wake wasiige yale ya kipumbavu waliofanya wao... bali wachukue ya maana tu!!!!

Ila hilo halipunguzi hata kidogo utumishi uliotukuka wa Nyerere kwa Tanzania.... He was a legend... a political icon that was so admirable.... Aliwapenda watu wake kutoka moyoni... and this is perhaps why everything that was tabled in his office could only be approved if and only if it complied with the interests of the majority, not minority. Infact, IMF requirements alizokuwa anatetea Mtei zilikuwa haziepukiki by then(that's why zilikuja kutekelezwa na Raisi Mwinyi baadae) ila Nyerere alizikataa due to its impact to Tanzanians.... It is true tha Devaluation is usually undertaken as a means of correcting a deficit in the balance of payments. Some analyst are of the view that weakening the value of currency could actually be good for the economy – since a weaker currency will boost exports, which in turn will lift employment and all this will set in motion economic growth and keep the economy going.

But Nyerere refused currency devaluation on the ground that it makes imports more expensive and at the same time exports are made cheaper....Kwa tafsiri ambayo aliitoa Nyerere mwenyewe katika moja ya hotuba zake aliitafsiri dhana hii kwamba "kama kabla ya kupunguza thamani ya shilingi ulikuwa na uwezo wa kununua matrekta 10 kwa kuuza nje ya nchi magunia 10 ya kahawa...basi ujue kwamba baada ya kushusha thamani ya shilingi itabidi ununue matrekta hayohayo kumi kwa kuuza magunia 15 ya kahawa"(kwa sababu kushusha shilingi thamani kunafanya mauzo ya nje yawe rahisi wakati huohuo manunuzi kutoka nje yanakuwa ghali).... Hii pia inamaanisha kwamba kwasabu Tanzania ni nchi changa kiviwanda, manunuzi kutoka nje yangekuwa ya thamani kubwa(i.e., ya bei ghali sana) na wakati huohuo mauzo yetu yangekua zaidi ya malighafi(i.e., ya bei rahisi sana)..... Hii ina maana kwamba mfumuko wa bei usingeepukika na kwahiyo maisha kwa mtanzania wa kawaida(maskini) yangekuwa ya ghali kila uchao......

 
nimefanya hivyo makusudi, mimi ni mtu mabadiliko, sikuta kutumia account yangu ya siku zote, nimeleta hapa ili tujue jinsi ya kukabiliana na hizi smears, kwana wataanza kuzituma kwenye email soon sasa msiwe na fikra potofu kama mimi nahusika na huu upuuzi, tembelea kwenye wall ya huyo mpuuzi hapo juu ndo mtajua kuwa ni nani mbona niweka kila kitu hapo juu hebu tusianze kupakaziana wenyewe kwa wenyewe pls, hizi smears inabidi tuzikabili

Hivi alichofanya huyu jamaa na anachokifanya Mzee Mwanakijiji na wenzake miaka yote hii kuna tofauti gani. Yaani mngelipenda watu wandike yale mnayopenda ninyi tu lakini wengine wakindika ni sumu. Hivi hashukuru kuwa angalao sasa tunaona propaganda zinazoenda shule kuliko zile tulizoanza kuzizoea hapa ambazo zaidi ya mipasho, vijembe na kauli mbiu zilizojaa mbegu za chuki?

Tusiwe maadui wa rationality for the sake of FUNIKA KOMBE MWANAHARAMU APITE......Kudadisi mambo ni msingi wa Uzalendo Makini......

Na huu utamaduni wa kukimbilia kuwakashifu, kuwatukana ama kuwatisha watu wanaoanzisha hoja msizotaka zisikike hauna tofauti na utamduni wa wanamtandao ambao mnadai ndio waliolifikiha taifa hapa tulipo
 
Uzuri ni kwamba Nyerere mwenyewe alikiri kwamba serikali yake iliboronga....na akawasihi successors wake wasiige yale ya kipumbavu waliofanya wao... bali wachukue ya maana tu!!!!

Nijuavyo sio kuwa alikubali kila kosa ambalo makuwadi wa soko huria walikuwa wakidai. Hata sera za ujamaa kwa ujumla wake aliendelea kuamani zilikuwa muhimu na bado zina nafasi na zinaweza kufanikiwa....alikubali machache na likiwemo la kunationalize mashamba ya mkonge...sasa kama kuna mengine aliyokubali naomba tuhabarishane lakini tuache kugeneralize mambo kama wale wahubiri wa mihadhara ya mitaani....
 
The Moment Of Truth:The Complete Text.(What Every Tanzanian Should Read)



by Ernesto Sheka on Thursday, October 21, 2010 at 8:19am



Tarehe 17 Oktoba nilieleza kijuujuu kwamba inawezekana mwaka 1979 Mwalimu Julius Nyerere alipomsimamisha kazi Edwin Mtei(gavana wa BoT wakati huo),kinyongo kiliendelea.Ulikuwepo msuguano mkubwa kati ya Mwalimu na Mtei kuhusu utekelezaji wa sera za IMF nchini Tanzania na katika moja ya mambo ambayo Mwalimu hakutaka hata kuyasikia lilikuwa suala la kushusha thamani shilingi yetu dhidi ya fedha za nchi za kigeni (devaluation) tulizokuwa tunafanya nazo biashara.Katika moja ya hotuba za Mwalimu alishaliongelea hili.1979 haukuwa mwaka mzuri kwa Edwin Mtei ila alipata kazi katika shirika la fedha IMF na kuhamia Marekani ambapo wanawe walipata elimu yao huku akiwepo Lilian Mtei ambaye baadaye alikuja kuolewa na Freeman Aikaeli Mbowe.
Historia haionyeshi kama Edwin Mtei,mtu aliyepata ugavana wa benki kuu akiwa na umri wa miaka 33 tu mwaka kwamba alimsamehe Mwalimu kwa fedheha hii.Najua wengi watasema kwamba haya yaliisha.Lakini tukumbuke kuwa maisha ya binadamu yanaathiriwa na matukio yanayoyazunguka.(Dacher Keltner,"The Compassionate Instinct: The Science of Human Goodness" uk.234-249).Kisasi hasa kwa mtu mwenye madaraka kushushiwa heshima yake kwa kile ambacho Edwin Mtei alikiamini ni sahihi ni jambo lisilopingika.Kwa hiyo toka mwaka 1979 (pengine mapema kabla ya hapo,nitaeleza zaidi mbele) Edwin Mtei tayari alishaanza kufikiri jinsi ya kupata sehemu yake,kurudisha heshima yake iliyopotea kama moja ya wasomi wa wakati huo lakini pia kumuonyesha Mwalimu kwamba alifanya kosa kumsimamisha kazi.Bahati haikuwa yake mapema na ilimpasa kusubiri kwa miaka takribani 13 hadi mwaka 1992 mfumo wa vyama vingi ulipoanzishwa huku mfumo wa kibepari ambao Mtei amekuwa moja ya makuwadi wake akiwa IMF ukishika mizizi na jamii nyingi za Kikomunisti za wakati huo zikirudi kwenye ubepari.Katika yote hayo ndoto yake ilikuwa inaendelea."Lazima niwaadabishe Nyerere na wote waliomsapoti".Tukumbuke kuwa ilikuwa ngumu hata kwa Lilian Mbowe ambaye alisoma chuo kikuu cha Maryland kupata kazi Tanzania wakati huo.Yote haya yalimzidishia Edwin Mtei uchungu huku akiamini kuwa familia yake ilikuwa na haki zaidi kuliko nyingine.Kwa hiyo mwaka 1992 ulipofika Chadema ikasajiliwa moja kwa moja.(Ndugu,jiulize utaratibu wote uliandaliwa lini,kwa nani na kwa faida ya nani?).Kushiriki siasa kwa Edwin Mtei huku Nyerere akiwa hai halikuwa jambo la busara sana,mzee huyu (ambaye kwa aina ya masterplan yake) naamini kwamba ni mwerevu sana akamuweka Bob Makani,huyu alipaswa kukipasha kiti moto kwa muda kabla Freeman Mbowe ambaye amemuoa Lilian Mtei (mtoto wa Mtei) kukabidhiwa mikoba ya kuendeleza plan yake.




Kuna maswali mnajiuliza:
Je, ni nani hasa Edwin Mtei?
Je,ilikuwaje Mbowe akashinda uenyekiti na si Zitto Kabwe?
Ni ipi hasa master plan ya mzee huyu aliyechekeana kinafiki na Nyerere?
Imefanikiwa kiasi gani?
Je,anawatumia watu gani?Mimi naweza kuwa natumiwa bila kujua?
Vipi Wangwe?Melo?
Ni nani Deus Mallya na kina nani walimlipia mafunzo ya Kijajusi ughaibuni?(sasa ni mpiga picha wa Chadema)
Ni kweli Chadema walifuja dola milioni mbili kama msaada toka chama cha Conservative cha Uingereza?
Saed Kubenea,Jenerali Ulimwengu,Philemon Ndesamburo,Absolum Kibanda ni kina nani na wanahusika vipi na grand plan ya Mtei?
Nini maana ya "M.Z.M.S" katika Chadema na ilikuwaje Mtei akairushusu na ameiruhusu kufanya kazi katika mlolongo upi na nani yujo juu ya sheria ndani ya Chadema na kwa nini?



Tarehe 17 June mwaka 1972 watu watano waliingia kwa siri katika makao makuu ya chama cha Democrats kwenye jengo la Watergate jijini Washington nchini Marekani.Mbali na kuchukua nyaraka za siri ambazo lengo kubwa lilikuwa kumlinda Richard Nixon pia waliharibu baadhi ya nyaraka.FBI walikuja kuugundua mchezo.Wakawakamata wahusika na Agosti 9, 1974,Richard Nixon alijiuzulu kama rais wa Marekani kutokana na kashfa hiyo huku ikibainishwa kuwa alikuwa na kifaa cha siri kilichorekodi sauti ndani ya ofisi hiyo na kila kitu kilichokuwa kinazungumziwa katika ofisi hiyo alikuwa akikifahamu.Nimeanza kwa mfano huu kujenga picha kwamba wanasiasa huwa wana malengo ambayo huwa nayo daima hadi kufa kwao.Edwin Mtei akiwa mmoja wapo kama nilivyosema katika sehemu iliyopita.

Swali kwa vijana wengi ni kwamba je Edwin Mtei ni nani limekuwa gumu wiki hii.Zaidi ya ugavana,uwaziri na ukulima wa kahawa hakuna wanaojua nini kipo nyuma ya pazia hili la Godfather.Mimi naanza kwa kuchambua huyu mtu ni nani na kila aya nasisitiza hatari yake kwa taifa letu na watu ambao ni ngazi zake muhimu.Hili ni jicho linalokutazama mtanzania kila hatua unayopiga na kuonyesha kwamba ni plan makini sana limefanyika kila linalowezekana kumuweka mbali na vyombo vya habari huku ukweli wa binti yake (ambaye ni mke wa Mbowe) kujihusisha na kuajiri mabinti wadogo na kisha kuwadhulumu katika Club yao ya usiku ya Bilicanas ukifichwa kwa kila nguvu na waandishi wa habari wanaolipwa na Edwin Mtei mwenyewe akiwamo mhariri wa gazeti la Tanzania Daima (mali ya Edwin Mtei kwa jina la Freeman Mbowe).Akiishi katika shamba lake Arusha,huku akijiita mkulima wa kahawa asiyependa makuu mzee huyu ni kama walowezi wa Zimbabwe.Kwa waliofika shambani kwake wanatambua naongea nini.(Inawezekana hili la kuwa setla alilianza mwaka1955 hadi 1959 alipokuwa Kenya akifanya kazi kampuni ya tumbaku ya Afrika Mashariki?Nitalichambua kwa hoja baadaye).

Ametoka wapi?Alizaliwa mwaka 1932 mkoani Kilimanjaro,mwaka 1946 alipata skolashipu toka Chagga Council (Waliompatia skolashipu hii wajukuu zao wengi wako katika kampuni zake kama wafanyakazi huku wengine wakishirikiana na vijana mbalimbali ambao hawajui lolote katika chadema kuifikia "ndoto").1953 alitoka Makerere na kuingia nchini Kenya katika kampuni ya tumbaku ya Afrika Mashariki.Itambulike kwamba wakati huu ulikuwa wakati wa vuguvugu la kudai haki ya mtu mweusi Tanzania na miaka minne baadaye TANU ilianzishwa.Huku mtu huyu akiwa Kenya,akifanya kazi katika serikali ya wazungu huku Mwalimu na wenzake walikuwa wakiendesha baiskeli toka Pugu hadi Kariakoo na Upanga kutimiza ndoto ya watanzania.Mtei yeye alikuwa bize Kenya akiwa na girlfriend wake ambaye alimuoa miaka michache baadaye.Hapa tuanaona USALITI wa aina yake.Huku Mwalimu na wanaharakati wengine kama Bibi Titi,Mzee Mwinyimadi Tambaza,Sykes na wengineo wakichomwa jua Dar es salaam,Mtei na elimu yake ya Makerere alikuwa busy akifurahia maisha Nairobi hadi mwaka 1959 aliporudi Tanzania.Miaka 33 baadaye(1992) alitoa wapi kifua cha kujiita mwanamabadiliko???Tuendelee.

Tarehe 20 Januari 1959 alirudi nyumbani akaenda kwao Marangu na baadaye tarehe 9 Februari akafika Dar na akarudia kosa lile lile la kujitenga na wanaharakati wenzake.(Ukisoma katika kitabu chake ambako amejitahidi kwa nguvu zote kuupindisha ukweli utagundua kwamba hili alilipanga tangu akiwa Kenya).Akaenda kuomba kazi katika serikali ya kikoloni na kuajiriwa katika Central Secretariat of the Tanganyika Civil Service.Huu ni mwaka mmoja tu kabla ya uhuru!Kama gwiji wa mitandao ya kijamii (social networks),Mark Zuckerberg anavyosema,"this is a man who never believed and supported other people's dreams." Hii ni sifa kubwa ya watu wabinafsi na waroho wa madaraka.(Ayn Rand,The Virtue Of Selfishness,uk 117 -129).(Kama kuna mtu anabisha hili mfuateni mkamuulize mtarudi na jibu kuwa alikuwa mbinafsi na msomi asiye mtu wa watu toka akiwa Makerere).HUYU NDIYE ANAYETAKA KUWA BABA WA TAIFA KWA GHARAMA YOYOTE ILE.Tuendelee.

Mwaka 1961 Tanganyika ilipata uhuru wake na katika kusherehekea siku hiyo mzee huyu anajigamba akionyesha wazi hulka yake ya ubinafsi na kujali nafasi aliyo nayo akisema,"...and I remember celebrating that event very hard because I was newly married and in a newly created country,enjoying my job in a fairly senior position at the Secretariat."That's him pouring rubbish.

Mwaka 1963 akaajiriwa tena EACSO akarudi Nairobi.(Je,alishaanza kuota ndoto ya kuwa bepari?Tafakari).Alidumu kwa mwaka mmoja tu na Mwalimu (naamini 100% kwa kukosa wasomi wa kutosha) akamuita nyumbani aje kuwa katibu mkuu wa wizara ya fedha.Kutokana na ufinyu wa muda kuna mambo mazito ambayo nitawaeleza kwa kifupi sana na kuwaacha muone ni jinsi gani mtu huyu ambaye anajificha nyuma ya pazia pamoja na vibaraka wake kama mkwewe Mbowe na Slaa wanajaribu kuufanya umma wa watanzania vihiyo_Oktoba mwaka 1965 kibaraka huyu wa faida binafsi akafanywa gavana mteule na Mwalimu Nyerere(narudia tena kwa jinsi hali inavyofuata huku mbele utaona kuwa alipewa nafasi hii kutokana na upungufu wa wataalamu na Mwalimu alim-doubt toka siku ya kwanza na daima alimuangalia kila hatua alizopiga).

Asubuhi ya Alhamis tarehe 6 Januari 1966 Edwin Mtei akiwa na umri wa miaka 34 alifanywa gavana rasmi wa benki kuu ya Tanzania na miezi michache baadaye (Tarehe 14 Juni 1966 ) shilingi ilianza kutumika rasmi.Hali haikuwa shwari kama ambavyo nimejaribu kueleza awali,mtu huyu hakuwa anaaminika na Mwalimu na ni sababu tosha kwa nini Mwalimu hakumpa nafasi ya kufanya maamuzi mengi.Utete wa hali hii ukazidi na Mwalimu kwa busara zake akampendekeza kuwa Katibu Mkuu wa EAC wakati huo.Hii ilikuwa mwezi Aprili mwaka 1974,kwa hiyo akatoka katika ugavana na kwenda EAC.Mwaka 1977 (miaka mitatu tu baada ya huyu Godfather kwenda pale),EAC ikavunjika.Kama mchumi hakuona dalili,akashindwa kutoa maono yake kwa usafi na nadiriki kusema anajua kwa nini watanzania wengi ambao leo ni wazee wa rika lake hawajalipwa na EAC.(anajua yeye ni sehemu ya tatizo hilo kwani watanzania wengi walibaki kama vibarua huku wengine wa Kenya wakipewa ajira na mkuu akiwa Edwin Mtei!!!!!!!!).Nitawaachia ninyi muamue.Baada ya hapo Mwalimu akamrudisha nyumbani tena,akamweka awe waziri wa Uchumi na Mipango mwaka 1977.Kauli zake kupokea nafasi hiyo zilikuwa za majivuno na kebehi na kuna mahali alijisahau na kusema,"…..although I held views critical of the general trend of things,I accepted to serve as Minister in 1977 in a spirit of constructive engagement, believing that I could play a part in improving matters whilst in rather than out."Nadhani alitamani Mwalimu afeli kabisa(rejea kujitenga kwake na wapigania uhuru na kujikomba kuomba kazi kwa wazungu) atimize ndoto yake.Nitaeleza kwa upana mbele.Tuendelee.

Hebu turudi nyuma kidogo.Jumapili tarehe 5 Februari 1967.Siku hii katika kikao kikuu cha kujadilia Azimio laArusha,Mwalimu alimruhusu afike kama observer tu!!!!Jiulize inaingiaje akili mtu mkubwa kama gavana wa benki kuu awe tu msikilizaji wa kawaida katika kikao kikubwa kama kile???(Muulizeni mkwe wake au yeye kama ana jibu.Believe me,hakuna mwenye kujua haya ninayoyaandika katika Chadema tunayoiona kama system yao ni kuokota ndege wanaokaribia kufa njiani na kuwafuga wakiwaita ndege bora.How does a political party that doesn't understand it's own history and motives behind it's founders move forward?It's a hoax.Political abracadabra.(Daniel Posner,Institutions and Ethnic Politics in Africa:political Economy of Institutions and Decisions,uk.36-59).Mwenye macho haambiwi tazama.Naendelea.

Kitendo cha Mtei kuambiwa na Mwalimu akae kama msikilizaji tu kilimuuma sana,kumbuka huyu ni waziri na gavana wa kwanza wa benki kuu ya Tanzania.(connect the dots ujue Slaa huwa anapata wapi documents za BoT,na kwa nini anazipata leo na si jana,kuna mtu anakutazama).Mwenyewe anakubali katika baadhi ya maandiko yake kwa masikitiko kama pale alipopinga mambo makuu mawili.Villagisation mwaka 1971 hadi 1973 na kutishia kuhusu Capital flight kama Mwalimu angeamua kuingia katika Azimio la Arusha.Kuonyesha kwamba Mwalimu alishamuona si lolote tangu 1953 alipotoka Makerere na kuishi Nairobi miaka 6 huku wanaharakati wa kweli wakiwa Tanganyika,Mwalimu alimpuuza.(Iko wazi kwamba Mtei aliona hathaminiki na ndoto zake za ubepari zilikuwa wazi,tunaweza kusema kwa waziwazi wazo lake la kuasi serikali ya Mwalimu alikuwa nalo toka mwaka 1967,nitaeleza kwa nini).This is a man who believed in capitalism from day one na Mwalimu alijua hivyo kwa hiyo hakumweka katika maamuzi makubwa in reality,alimwacha aelee na kumwangalia kwa karibu.

Hali ikazidi kuwa mbaya,1979 Mwalimu akamtimua huku yeye akisema aliachia ngazi mwenyewe (Jiulize kwa nini na ilikuwaje akatoa kitabu cha historia ya maisha yake baada ya kifo cha Mwalimu.Connect the dots,it makes a click.).Naamini kama Mwalimu angekuwa na intelijensia bora,Mtei angekuwa wa kwanza kuihama Tanzania kabla ya marehemu Oscar Kambona.Katika moja ya maandishi yake anaeleza kwa kujificha sana kwamba alikuwa mtu safi huku akificha ukweli kwamba katika sera kama devaluation na reconstruction ya mashirika ya umma si sahihi kufuata tu oda za IMF bali pia kuangalia muda husika!Aibu sana.This is him.
“The IMF therefore required us to devalue the Tsh and to review the management of our parastatals before they could give us balance-of-payments support. In the negotiations, I was able to get the IMF to scale down their demands on devaluation and make them accept that we would examine individual public corporations to see how they could be restructured to perform better.When I explained this approach to the President he was quite categorical that he would not accept any devaluation and that he would review the parastatals onlyat his own timing. He implied that he would not be dictated to from Washington..." Anajaribu kusemaje?Mwalimu was stupid?How on earth do you restructure your parastatals when you don't have enough natives educated to take over and work with highly qualified foreigners?Ni simple economics.!Mtei alifumba macho na Mwalimu alipojiridhisha kwamba amembeba kiasi cha kutosha ila habebeki,akamtimua.Safari ya Marekani ikanukia na akaenda zake Washington.(The only reason he was never exiled ni kwa sababu tayari alijua mengi sana kuhusu intelijensia ya nchi.Je,aliwafuata marafiki zake?).Tuendelee.

Novemba 1986 akarudi nyumbani.(Angalia timing!Just a year after Mwalimu has resigned!!)Huku nako mambo hayakuwa sawa,ujamaa ulishindikana.(si tu kwa sababu duniani haukufanikiwa lakini pia kwa sababu watu ambao Mwalimu alitegemea wangempa sapoti kama Mtei na Kambona walijifanya majuha wakataka waishi ndoto zao ndani ya sekunde).Moja ya watu waliopata masahibu ya Mwalimu ni Jenarali Ulimwengu ambaye alisimamishwa ubunge baada ya sakata la G55.Huyu akiamini kabisa kwamba yeye ni bora kuliko Jakaya Kikwete na Maalim Seif ambao walikuwa vijana wapenzi wa Mwalimu kipindi hicho akajikita katika habari huku naye akiwa na ndoto zake).

Ndoto na chuki zaja hadharani sasa;
Baada ya miaka takribani 26,Julai 1992 mfumo wa vyama vingi ukaanza.The same year Mtei akaanzisha Chadema na mpaka ninapoandika hili,in practical terms yeye ni mwenyekiti wa Chadema,kwake yeye ile ni fimbo maalumu ya kumchapa Mwalimu Nyerere siku akifanikiwa japo kila mara anakosea mahesabu huku jamii ikizidi kuamka na kujua historia ya taifa na kuchambua mambo hatua kwa hatua.Uzee wake umekuwa wa mashaka na wasiwasi.Ni dhahiri kuwa masterplan ya kuanza kwa Chadema ilianza kuandikwa Nairobi na baadaye Washington huku ikiuwaza ubepari na Ikulu kabla hata ya usajili.Lilian Mbowe ni mtoto wa kike wa Edwin Mtei ambaye aliolewa na Mbowe.Ni daktari ambaye kama nilivyosema awali anajishughulisha na kuendesha club ya usiku katikati ya jiji la Dar es salaam mtaa wa Mkwepu.Nyumba zao hutumika kukusanya vijana na wengi wana upofu na historia ya Chadema,wanaogundua huondoka mara moja.(Mtafuteni David Kafulila atawahadithia sehemu hii).


Je,ilikuwaje Mbowe akashinda uenyekiti na si Zitto Kabwe?
Edwin Mtei namnukuu akisema,"we can't give this position to a man from nowhere" akimaanisha Zitto Kabwe,Zitto alitaka kuondoka ila alibaki kwa sababu zake.Tafakari hiyo kauli ya Mtei.Who's a man from nowhere and who's a man from somewhere??Ni ipi hasa masterplan ya mzee huyu aliyechekeana kinafiki na Nyerere?To revenge and take back his dignity and self interests.Ni ndoto yake ya ujanani na anaomba Watz tumsaidie aitimize.

Imefanikiwa kiasi gani?
Hali ni ngumu,ukabila bado umekuwa tatizo.Kifo cha Wangwe,maneno kuhusu viti maalumu,uwepo wa Deus Mallya aliyevuruga mpango wa kufunika sakata la kula pound za waingereza kama ruzuku kwa chama na baadaye kufoji risiti .(John Mnyika alikuwa kinara wa shughuli hii ya kuchakachua risiti).Wangwe's head had a price but Deus Mallya made a noise and Chadema let him went down and come up alone(sifa kubwa ya majasusi unapoharibu mpango wa kazi na ukapata tatizo).Ninapoandika hili,Deus Mallya ni mpiga picha na designer rasmi wa Chadema huku mifupa na damu ya Chacha Zakayo Wangwe ikilala udongoni kule Tarime.

Je,anawatumia watu gani?Mimi naweza kuwa natumiwa bila kujua?
Anawatumia watu ambao mkwewe,Freeman Mbowe humpelekea.Hakuna details zozote kuonyesha kama Slaa,Zitto na Mtei walikuwa na uhusiano wa karibu miaka saba nyuma!Wachezaji waliokaa pamoja siku mbili wanataka kuomba mechi.Sick jokes.Jenerali Ulimwengu,Saed Kubenea,Maxence Melo,Mike Mushi (huyu baadaye alikimbia).Kuchafua nchi mtandaoni kwa kutumia mtandao wa Maxence Melo ambao una mahusiano ya karibu na baadhi ya watu waliko Houston,Texas.Absalom Kibanda (ni mwandishi na mhariri wa Tanzania Daima ambaye anatembea juu ya ukanjanja wa kutupwa).Unaweza kutumika bila kujua kama hutasikiliza na kutafakari na kuhoji.Sote tunakubaliana huwezi kuacha kutumia gari lako zima ukaamua kuazima gari la jirani yako ambalo lina taa mbovu,tairi mbili mbovu na mafuta hakuna.

Nini maana ya "M.Z.M.S" katika Chadema na ilikuwaje Mtei akairushusu na ameiruhusu kufanya kazi katika mlolongo upi na nani yujo juu ya sheria ndani ya Chadema na kwa nini?M.Z.M.S ni ufupisho wa watu wenye veto power ndani ya Chadema japo zinatofautiona uzito.(Mama Shida Salum,mama mzazi wa Zitto anajua hili).Mbowe,Zitto,Mnyika na Slaa.Uzito wa kura uko kama nilivyoorodhesha majina toka juu kwenda chini.Kama mtu sijamtaja hapo ujue hata Mtei hataka kujua undani wako.(Kasoro Philemon Ndesamburo na familia yake).

Hitimisho:
Nashukuru kwa kuisoma,je utamsaidia Mtei kumchapa Mwalimu Nyerere bakora kisha alete ilani yake?Si ile inayonadiwa.Je,unajua undani kwa nini moja ya sera za Chadema ni kuigawa nchi katika zones?(majimbo)?Ni nani wanakusudia wawe magavana,majimbo hayo ni yapi na kwa nini?

Muda umeniishia ila tafakari na amua mwenyewe.
Mungu Ibariki Tanzania.
Ernesto Sheka.
Oktoba 20,2010
Butiama,Musoma, Tanzania.

NAJUA MENGI YATASEMWA,KWA MFANO WHY NOW?WELL,THERE'S A SEASON & A REASON FOR EVERYTHING.TUMUULIZE MTEI KWA NINI ALIZINDUA KITABU CHAKE BAADA YA KIFO CHA MWALIMU PIA AMA?WATU WAJINGA KABISA.

 
The Moment Of Truth:The Complete Text.(What Every Tanzanian Should Read)



by Ernesto Sheka on Thursday, October 21, 2010 at 8:19am



Tarehe 17 Oktoba nilieleza kijuujuu kwamba inawezekana mwaka 1979 Mwalimu Julius Nyerere alipomsimamisha kazi Edwin Mtei(gavana wa BoT wakati huo),kinyongo kiliendelea.Ulikuwepo msuguano mkubwa kati ya Mwalimu na Mtei kuhusu utekelezaji wa sera za IMF nchini Tanzania na katika moja ya mambo ambayo Mwalimu hakutaka hata kuyasikia lilikuwa suala la kushusha thamani shilingi yetu dhidi ya fedha za nchi za kigeni (devaluation) tulizokuwa tunafanya nazo biashara.Katika moja ya hotuba za Mwalimu alishaliongelea hili.1979 haukuwa mwaka mzuri kwa Edwin Mtei ila alipata kazi katika shirika la fedha IMF na kuhamia Marekani ambapo wanawe walipata elimu yao huku akiwepo Lilian Mtei ambaye baadaye alikuja kuolewa na Freeman Aikaeli Mbowe.
Historia haionyeshi kama Edwin Mtei,mtu aliyepata ugavana wa benki kuu akiwa na umri wa miaka 33 tu mwaka kwamba alimsamehe Mwalimu kwa fedheha hii.Najua wengi watasema kwamba haya yaliisha.Lakini tukumbuke kuwa maisha ya binadamu yanaathiriwa na matukio yanayoyazunguka.(Dacher Keltner,"The Compassionate Instinct: The Science of Human Goodness" uk.234-249).Kisasi hasa kwa mtu mwenye madaraka kushushiwa heshima yake kwa kile ambacho Edwin Mtei alikiamini ni sahihi ni jambo lisilopingika.Kwa hiyo toka mwaka 1979 (pengine mapema kabla ya hapo,nitaeleza zaidi mbele) Edwin Mtei tayari alishaanza kufikiri jinsi ya kupata sehemu yake,kurudisha heshima yake iliyopotea kama moja ya wasomi wa wakati huo lakini pia kumuonyesha Mwalimu kwamba alifanya kosa kumsimamisha kazi.Bahati haikuwa yake mapema na ilimpasa kusubiri kwa miaka takribani 13 hadi mwaka 1992 mfumo wa vyama vingi ulipoanzishwa huku mfumo wa kibepari ambao Mtei amekuwa moja ya makuwadi wake akiwa IMF ukishika mizizi na jamii nyingi za Kikomunisti za wakati huo zikirudi kwenye ubepari.Katika yote hayo ndoto yake ilikuwa inaendelea."Lazima niwaadabishe Nyerere na wote waliomsapoti".Tukumbuke kuwa ilikuwa ngumu hata kwa Lilian Mbowe ambaye alisoma chuo kikuu cha Maryland kupata kazi Tanzania wakati huo.Yote haya yalimzidishia Edwin Mtei uchungu huku akiamini kuwa familia yake ilikuwa na haki zaidi kuliko nyingine.Kwa hiyo mwaka 1992 ulipofika Chadema ikasajiliwa moja kwa moja.(Ndugu,jiulize utaratibu wote uliandaliwa lini,kwa nani na kwa faida ya nani?).Kushiriki siasa kwa Edwin Mtei huku Nyerere akiwa hai halikuwa jambo la busara sana,mzee huyu (ambaye kwa aina ya masterplan yake) naamini kwamba ni mwerevu sana akamuweka Bob Makani,huyu alipaswa kukipasha kiti moto kwa muda kabla Freeman Mbowe ambaye amemuoa Lilian Mtei (mtoto wa Mtei) kukabidhiwa mikoba ya kuendeleza plan yake.




Kuna maswali mnajiuliza:
Je, ni nani hasa Edwin Mtei?
Je,ilikuwaje Mbowe akashinda uenyekiti na si Zitto Kabwe?
Ni ipi hasa master plan ya mzee huyu aliyechekeana kinafiki na Nyerere?
Imefanikiwa kiasi gani?
Je,anawatumia watu gani?Mimi naweza kuwa natumiwa bila kujua?
Vipi Wangwe?Melo?
Ni nani Deus Mallya na kina nani walimlipia mafunzo ya Kijajusi ughaibuni?(sasa ni mpiga picha wa Chadema)
Ni kweli Chadema walifuja dola milioni mbili kama msaada toka chama cha Conservative cha Uingereza?
Saed Kubenea,Jenerali Ulimwengu,Philemon Ndesamburo,Absolum Kibanda ni kina nani na wanahusika vipi na grand plan ya Mtei?
Nini maana ya "M.Z.M.S" katika Chadema na ilikuwaje Mtei akairushusu na ameiruhusu kufanya kazi katika mlolongo upi na nani yujo juu ya sheria ndani ya Chadema na kwa nini?



Tarehe 17 June mwaka 1972 watu watano waliingia kwa siri katika makao makuu ya chama cha Democrats kwenye jengo la Watergate jijini Washington nchini Marekani.Mbali na kuchukua nyaraka za siri ambazo lengo kubwa lilikuwa kumlinda Richard Nixon pia waliharibu baadhi ya nyaraka.FBI walikuja kuugundua mchezo.Wakawakamata wahusika na Agosti 9, 1974,Richard Nixon alijiuzulu kama rais wa Marekani kutokana na kashfa hiyo huku ikibainishwa kuwa alikuwa na kifaa cha siri kilichorekodi sauti ndani ya ofisi hiyo na kila kitu kilichokuwa kinazungumziwa katika ofisi hiyo alikuwa akikifahamu.Nimeanza kwa mfano huu kujenga picha kwamba wanasiasa huwa wana malengo ambayo huwa nayo daima hadi kufa kwao.Edwin Mtei akiwa mmoja wapo kama nilivyosema katika sehemu iliyopita.

Swali kwa vijana wengi ni kwamba je Edwin Mtei ni nani limekuwa gumu wiki hii.Zaidi ya ugavana,uwaziri na ukulima wa kahawa hakuna wanaojua nini kipo nyuma ya pazia hili la Godfather.Mimi naanza kwa kuchambua huyu mtu ni nani na kila aya nasisitiza hatari yake kwa taifa letu na watu ambao ni ngazi zake muhimu.Hili ni jicho linalokutazama mtanzania kila hatua unayopiga na kuonyesha kwamba ni plan makini sana limefanyika kila linalowezekana kumuweka mbali na vyombo vya habari huku ukweli wa binti yake (ambaye ni mke wa Mbowe) kujihusisha na kuajiri mabinti wadogo na kisha kuwadhulumu katika Club yao ya usiku ya Bilicanas ukifichwa kwa kila nguvu na waandishi wa habari wanaolipwa na Edwin Mtei mwenyewe akiwamo mhariri wa gazeti la Tanzania Daima (mali ya Edwin Mtei kwa jina la Freeman Mbowe).Akiishi katika shamba lake Arusha,huku akijiita mkulima wa kahawa asiyependa makuu mzee huyu ni kama walowezi wa Zimbabwe.Kwa waliofika shambani kwake wanatambua naongea nini.(Inawezekana hili la kuwa setla alilianza mwaka1955 hadi 1959 alipokuwa Kenya akifanya kazi kampuni ya tumbaku ya Afrika Mashariki?Nitalichambua kwa hoja baadaye).

Ametoka wapi?Alizaliwa mwaka 1932 mkoani Kilimanjaro,mwaka 1946 alipata skolashipu toka Chagga Council (Waliompatia skolashipu hii wajukuu zao wengi wako katika kampuni zake kama wafanyakazi huku wengine wakishirikiana na vijana mbalimbali ambao hawajui lolote katika chadema kuifikia "ndoto").1953 alitoka Makerere na kuingia nchini Kenya katika kampuni ya tumbaku ya Afrika Mashariki.Itambulike kwamba wakati huu ulikuwa wakati wa vuguvugu la kudai haki ya mtu mweusi Tanzania na miaka minne baadaye TANU ilianzishwa.Huku mtu huyu akiwa Kenya,akifanya kazi katika serikali ya wazungu huku Mwalimu na wenzake walikuwa wakiendesha baiskeli toka Pugu hadi Kariakoo na Upanga kutimiza ndoto ya watanzania.Mtei yeye alikuwa bize Kenya akiwa na girlfriend wake ambaye alimuoa miaka michache baadaye.Hapa tuanaona USALITI wa aina yake.Huku Mwalimu na wanaharakati wengine kama Bibi Titi,Mzee Mwinyimadi Tambaza,Sykes na wengineo wakichomwa jua Dar es salaam,Mtei na elimu yake ya Makerere alikuwa busy akifurahia maisha Nairobi hadi mwaka 1959 aliporudi Tanzania.Miaka 33 baadaye(1992) alitoa wapi kifua cha kujiita mwanamabadiliko???Tuendelee.

Tarehe 20 Januari 1959 alirudi nyumbani akaenda kwao Marangu na baadaye tarehe 9 Februari akafika Dar na akarudia kosa lile lile la kujitenga na wanaharakati wenzake.(Ukisoma katika kitabu chake ambako amejitahidi kwa nguvu zote kuupindisha ukweli utagundua kwamba hili alilipanga tangu akiwa Kenya).Akaenda kuomba kazi katika serikali ya kikoloni na kuajiriwa katika Central Secretariat of the Tanganyika Civil Service.Huu ni mwaka mmoja tu kabla ya uhuru!Kama gwiji wa mitandao ya kijamii (social networks),Mark Zuckerberg anavyosema,"this is a man who never believed and supported other people's dreams." Hii ni sifa kubwa ya watu wabinafsi na waroho wa madaraka.(Ayn Rand,The Virtue Of Selfishness,uk 117 -129).(Kama kuna mtu anabisha hili mfuateni mkamuulize mtarudi na jibu kuwa alikuwa mbinafsi na msomi asiye mtu wa watu toka akiwa Makerere).HUYU NDIYE ANAYETAKA KUWA BABA WA TAIFA KWA GHARAMA YOYOTE ILE.Tuendelee.

Mwaka 1961 Tanganyika ilipata uhuru wake na katika kusherehekea siku hiyo mzee huyu anajigamba akionyesha wazi hulka yake ya ubinafsi na kujali nafasi aliyo nayo akisema,"...and I remember celebrating that event very hard because I was newly married and in a newly created country,enjoying my job in a fairly senior position at the Secretariat."That's him pouring rubbish.

Mwaka 1963 akaajiriwa tena EACSO akarudi Nairobi.(Je,alishaanza kuota ndoto ya kuwa bepari?Tafakari).Alidumu kwa mwaka mmoja tu na Mwalimu (naamini 100% kwa kukosa wasomi wa kutosha) akamuita nyumbani aje kuwa katibu mkuu wa wizara ya fedha.Kutokana na ufinyu wa muda kuna mambo mazito ambayo nitawaeleza kwa kifupi sana na kuwaacha muone ni jinsi gani mtu huyu ambaye anajificha nyuma ya pazia pamoja na vibaraka wake kama mkwewe Mbowe na Slaa wanajaribu kuufanya umma wa watanzania vihiyo_Oktoba mwaka 1965 kibaraka huyu wa faida binafsi akafanywa gavana mteule na Mwalimu Nyerere(narudia tena kwa jinsi hali inavyofuata huku mbele utaona kuwa alipewa nafasi hii kutokana na upungufu wa wataalamu na Mwalimu alim-doubt toka siku ya kwanza na daima alimuangalia kila hatua alizopiga).

Asubuhi ya Alhamis tarehe 6 Januari 1966 Edwin Mtei akiwa na umri wa miaka 34 alifanywa gavana rasmi wa benki kuu ya Tanzania na miezi michache baadaye (Tarehe 14 Juni 1966 ) shilingi ilianza kutumika rasmi.Hali haikuwa shwari kama ambavyo nimejaribu kueleza awali,mtu huyu hakuwa anaaminika na Mwalimu na ni sababu tosha kwa nini Mwalimu hakumpa nafasi ya kufanya maamuzi mengi.Utete wa hali hii ukazidi na Mwalimu kwa busara zake akampendekeza kuwa Katibu Mkuu wa EAC wakati huo.Hii ilikuwa mwezi Aprili mwaka 1974,kwa hiyo akatoka katika ugavana na kwenda EAC.Mwaka 1977 (miaka mitatu tu baada ya huyu Godfather kwenda pale),EAC ikavunjika.Kama mchumi hakuona dalili,akashindwa kutoa maono yake kwa usafi na nadiriki kusema anajua kwa nini watanzania wengi ambao leo ni wazee wa rika lake hawajalipwa na EAC.(anajua yeye ni sehemu ya tatizo hilo kwani watanzania wengi walibaki kama vibarua huku wengine wa Kenya wakipewa ajira na mkuu akiwa Edwin Mtei!!!!!!!!).Nitawaachia ninyi muamue.Baada ya hapo Mwalimu akamrudisha nyumbani tena,akamweka awe waziri wa Uchumi na Mipango mwaka 1977.Kauli zake kupokea nafasi hiyo zilikuwa za majivuno na kebehi na kuna mahali alijisahau na kusema,"…..although I held views critical of the general trend of things,I accepted to serve as Minister in 1977 in a spirit of constructive engagement, believing that I could play a part in improving matters whilst in rather than out."Nadhani alitamani Mwalimu afeli kabisa(rejea kujitenga kwake na wapigania uhuru na kujikomba kuomba kazi kwa wazungu) atimize ndoto yake.Nitaeleza kwa upana mbele.Tuendelee.

Hebu turudi nyuma kidogo.Jumapili tarehe 5 Februari 1967.Siku hii katika kikao kikuu cha kujadilia Azimio laArusha,Mwalimu alimruhusu afike kama observer tu!!!!Jiulize inaingiaje akili mtu mkubwa kama gavana wa benki kuu awe tu msikilizaji wa kawaida katika kikao kikubwa kama kile???(Muulizeni mkwe wake au yeye kama ana jibu.Believe me,hakuna mwenye kujua haya ninayoyaandika katika Chadema tunayoiona kama system yao ni kuokota ndege wanaokaribia kufa njiani na kuwafuga wakiwaita ndege bora.How does a political party that doesn't understand it's own history and motives behind it's founders move forward?It's a hoax.Political abracadabra.(Daniel Posner,Institutions and Ethnic Politics in Africa:political Economy of Institutions and Decisions,uk.36-59).Mwenye macho haambiwi tazama.Naendelea.

Kitendo cha Mtei kuambiwa na Mwalimu akae kama msikilizaji tu kilimuuma sana,kumbuka huyu ni waziri na gavana wa kwanza wa benki kuu ya Tanzania.(connect the dots ujue Slaa huwa anapata wapi documents za BoT,na kwa nini anazipata leo na si jana,kuna mtu anakutazama).Mwenyewe anakubali katika baadhi ya maandiko yake kwa masikitiko kama pale alipopinga mambo makuu mawili.Villagisation mwaka 1971 hadi 1973 na kutishia kuhusu Capital flight kama Mwalimu angeamua kuingia katika Azimio la Arusha.Kuonyesha kwamba Mwalimu alishamuona si lolote tangu 1953 alipotoka Makerere na kuishi Nairobi miaka 6 huku wanaharakati wa kweli wakiwa Tanganyika,Mwalimu alimpuuza.(Iko wazi kwamba Mtei aliona hathaminiki na ndoto zake za ubepari zilikuwa wazi,tunaweza kusema kwa waziwazi wazo lake la kuasi serikali ya Mwalimu alikuwa nalo toka mwaka 1967,nitaeleza kwa nini).This is a man who believed in capitalism from day one na Mwalimu alijua hivyo kwa hiyo hakumweka katika maamuzi makubwa in reality,alimwacha aelee na kumwangalia kwa karibu.

Hali ikazidi kuwa mbaya,1979 Mwalimu akamtimua huku yeye akisema aliachia ngazi mwenyewe (Jiulize kwa nini na ilikuwaje akatoa kitabu cha historia ya maisha yake baada ya kifo cha Mwalimu.Connect the dots,it makes a click.).Naamini kama Mwalimu angekuwa na intelijensia bora,Mtei angekuwa wa kwanza kuihama Tanzania kabla ya marehemu Oscar Kambona.Katika moja ya maandishi yake anaeleza kwa kujificha sana kwamba alikuwa mtu safi huku akificha ukweli kwamba katika sera kama devaluation na reconstruction ya mashirika ya umma si sahihi kufuata tu oda za IMF bali pia kuangalia muda husika!Aibu sana.This is him.
"The IMF therefore required us to devalue the Tsh and to review the management of our parastatals before they could give us balance-of-payments support. In the negotiations, I was able to get the IMF to scale down their demands on devaluation and make them accept that we would examine individual public corporations to see how they could be restructured to perform better.When I explained this approach to the President he was quite categorical that he would not accept any devaluation and that he would review the parastatals onlyat his own timing. He implied that he would not be dictated to from Washington..." Anajaribu kusemaje?Mwalimu was stupid?How on earth do you restructure your parastatals when you don't have enough natives educated to take over and work with highly qualified foreigners?Ni simple economics.!Mtei alifumba macho na Mwalimu alipojiridhisha kwamba amembeba kiasi cha kutosha ila habebeki,akamtimua.Safari ya Marekani ikanukia na akaenda zake Washington.(The only reason he was never exiled ni kwa sababu tayari alijua mengi sana kuhusu intelijensia ya nchi.Je,aliwafuata marafiki zake?).Tuendelee.

Novemba 1986 akarudi nyumbani.(Angalia timing!Just a year after Mwalimu has resigned!!)Huku nako mambo hayakuwa sawa,ujamaa ulishindikana.(si tu kwa sababu duniani haukufanikiwa lakini pia kwa sababu watu ambao Mwalimu alitegemea wangempa sapoti kama Mtei na Kambona walijifanya majuha wakataka waishi ndoto zao ndani ya sekunde).Moja ya watu waliopata masahibu ya Mwalimu ni Jenarali Ulimwengu ambaye alisimamishwa ubunge baada ya sakata la G55.Huyu akiamini kabisa kwamba yeye ni bora kuliko Jakaya Kikwete na Maalim Seif ambao walikuwa vijana wapenzi wa Mwalimu kipindi hicho akajikita katika habari huku naye akiwa na ndoto zake).

Ndoto na chuki zaja hadharani sasa;
Baada ya miaka takribani 26,Julai 1992 mfumo wa vyama vingi ukaanza.The same year Mtei akaanzisha Chadema na mpaka ninapoandika hili,in practical terms yeye ni mwenyekiti wa Chadema,kwake yeye ile ni fimbo maalumu ya kumchapa Mwalimu Nyerere siku akifanikiwa japo kila mara anakosea mahesabu huku jamii ikizidi kuamka na kujua historia ya taifa na kuchambua mambo hatua kwa hatua.Uzee wake umekuwa wa mashaka na wasiwasi.Ni dhahiri kuwa masterplan ya kuanza kwa Chadema ilianza kuandikwa Nairobi na baadaye Washington huku ikiuwaza ubepari na Ikulu kabla hata ya usajili.Lilian Mbowe ni mtoto wa kike wa Edwin Mtei ambaye aliolewa na Mbowe.Ni daktari ambaye kama nilivyosema awali anajishughulisha na kuendesha club ya usiku katikati ya jiji la Dar es salaam mtaa wa Mkwepu.Nyumba zao hutumika kukusanya vijana na wengi wana upofu na historia ya Chadema,wanaogundua huondoka mara moja.(Mtafuteni David Kafulila atawahadithia sehemu hii).


Je,ilikuwaje Mbowe akashinda uenyekiti na si Zitto Kabwe?
Edwin Mtei namnukuu akisema,"we can't give this position to a man from nowhere" akimaanisha Zitto Kabwe,Zitto alitaka kuondoka ila alibaki kwa sababu zake.Tafakari hiyo kauli ya Mtei.Who's a man from nowhere and who's a man from somewhere??Ni ipi hasa masterplan ya mzee huyu aliyechekeana kinafiki na Nyerere?To revenge and take back his dignity and self interests.Ni ndoto yake ya ujanani na anaomba Watz tumsaidie aitimize.

Imefanikiwa kiasi gani?
Hali ni ngumu,ukabila bado umekuwa tatizo.Kifo cha Wangwe,maneno kuhusu viti maalumu,uwepo wa Deus Mallya aliyevuruga mpango wa kufunika sakata la kula pound za waingereza kama ruzuku kwa chama na baadaye kufoji risiti .(John Mnyika alikuwa kinara wa shughuli hii ya kuchakachua risiti).Wangwe's head had a price but Deus Mallya made a noise and Chadema let him went down and come up alone(sifa kubwa ya majasusi unapoharibu mpango wa kazi na ukapata tatizo).Ninapoandika hili,Deus Mallya ni mpiga picha na designer rasmi wa Chadema huku mifupa na damu ya Chacha Zakayo Wangwe ikilala udongoni kule Tarime.

Je,anawatumia watu gani?Mimi naweza kuwa natumiwa bila kujua?
Anawatumia watu ambao mkwewe,Freeman Mbowe humpelekea.Hakuna details zozote kuonyesha kama Slaa,Zitto na Mtei walikuwa na uhusiano wa karibu miaka saba nyuma!Wachezaji waliokaa pamoja siku mbili wanataka kuomba mechi.Sick jokes.Jenerali Ulimwengu,Saed Kubenea,Maxence Melo,Mike Mushi (huyu baadaye alikimbia).Kuchafua nchi mtandaoni kwa kutumia mtandao wa Maxence Melo ambao una mahusiano ya karibu na baadhi ya watu waliko Houston,Texas.Absalom Kibanda (ni mwandishi na mhariri wa Tanzania Daima ambaye anatembea juu ya ukanjanja wa kutupwa).Unaweza kutumika bila kujua kama hutasikiliza na kutafakari na kuhoji.Sote tunakubaliana huwezi kuacha kutumia gari lako zima ukaamua kuazima gari la jirani yako ambalo lina taa mbovu,tairi mbili mbovu na mafuta hakuna.

Nini maana ya "M.Z.M.S" katika Chadema na ilikuwaje Mtei akairushusu na ameiruhusu kufanya kazi katika mlolongo upi na nani yujo juu ya sheria ndani ya Chadema na kwa nini?M.Z.M.S ni ufupisho wa watu wenye veto power ndani ya Chadema japo zinatofautiona uzito.(Mama Shida Salum,mama mzazi wa Zitto anajua hili).Mbowe,Zitto,Mnyika na Slaa.Uzito wa kura uko kama nilivyoorodhesha majina toka juu kwenda chini.Kama mtu sijamtaja hapo ujue hata Mtei hataka kujua undani wako.(Kasoro Philemon Ndesamburo na familia yake).

Hitimisho:
Nashukuru kwa kuisoma,je utamsaidia Mtei kumchapa Mwalimu Nyerere bakora kisha alete ilani yake?Si ile inayonadiwa.Je,unajua undani kwa nini moja ya sera za Chadema ni kuigawa nchi katika zones?(majimbo)?Ni nani wanakusudia wawe magavana,majimbo hayo ni yapi na kwa nini?

Muda umeniishia ila tafakari na amua mwenyewe.
Mungu Ibariki Tanzania.
Ernesto Sheka.
Oktoba 20,2010
Butiama,Musoma, Tanzania.

NAJUA MENGI YATASEMWA,KWA MFANO WHY NOW?WELL,THERE'S A SEASON & A REASON FOR EVERYTHING.TUMUULIZE MTEI KWA NINI ALIZINDUA KITABU CHAKE BAADA YA KIFO CHA MWALIMU PIA AMA?WATU WAJINGA KABISA.


Watafuta hii.
 
Kwanza na mpongeza sana mzee mtei, kwakuwa na msimamo na uwezo wa kujenga na kusimamia hoja zake. Binadamu wote na hasa watanzania tungejaliwa uwezo kama wa mtei tunge songambele. Wapo wengi sana ndani ya serikali, makanisani, kwenye vyama vya siasa, wao kazi ni ndio mzee. Sasa hivi hata ndani ya vyama vikubwa hakuna hitifaki, vikao vinafanywa nyumbani familia inasmaba nchi nzima kupiga kameni, hakuna hata mtu mmoja anauliza ni kwa mamuzi ya kikao gani, na kwa wadhifa gani mtu anafanya mambo gani. Kwa wanomfahamu baba wa taifa wanajua alikuwa si mtu mchezo, kwa mtei kumwambia vision yake na kuisimamia na kukubali kupokwa ugavana, na kujipanga kuonyesha kwamba vision yake ni sahihi ni haki yake hasa anapoonyesha kwa hoja sioni ubaya, yamoni ni mungu tu, ndiyo anajua kama nani anakinyongo au kasamehe.
Viva mtei viva.
 
Hii imeshakuwa posted
Mods waunganishe.

CCM wanakaribia kukata roho. Naona wanajaribu kufurukuta...

Siasa za maji taka zinawaponza CCM bado hajajifunza tu!

Mzee Mtei ametoa kitabu kinachoongelea maisha yake na moja ya vitu alivyoongelea ni kwanini alijiuzuru Uwaziri wa fedha kipindi cha Nyerere. Na baadae Nyerere akamteua akatuwakilishe IMF

Mwaka huu wananchi hatudanganyiki!
 
Hii imeshakuwa posted
Mods waunganishe.

CCM wanakaribia kukata roho. Naona wanajaribu kufurukuta...

Siasa za maji taka zinawaponza CCM bado hajajifunza tu!

Mzee Mtei ametoa kitabu kinachoongelea maisha yake na moja ya vitu alivyoongelea ni kwanini alijiuzuru Uwaziri wa fedha kipindi cha Nyerere. Na baadae Nyerere akamteua akatuwakilishe IMF

Mwaka huu wananchi hatudanganyiki!

kuna ubaya gani kuwa against na nyerere? last time i checked he was a man just like any other
VIVA CHADEMA VIVAAAAAAAAAAAA
 
Here comes October 31 2010 suka ama nyoa chagua mwenyewe kwa upeo wako kati ya;

CHADEMA = CHAGGA DEVELOPMENT MANIFESTO and CCM = CHAMA CHA MAFISADI
 
Ndugu zanguni wana JF hoja siku zote hujibiwa na hoja. Wanaosema kwa nini Mzee Mtei kaandika kitabu leo, wanasahau kwamba kuandika kitabu ni haki yake ya msingi mzee Mtei. Prof.Babu aliandika kitabu chake wakati yupo jela, mpaka leo kuna baadhi ya Vyuo vinarecommend hicho kitabu.

Pili, ni vyema tusikilize pande zote mbili then tumia uwezo na upeo wako kujudge based on the facts presented. Na sio kusimama na kulalawa why now, why and why? Think kwanza then analyze.

Nikiwa kama mpenda uchumi, nimesoma vitabu vingi sana kuhusu IMF and World Bank na umafia wao. Kuna valid arguments ambazo tunaweza kujifunza kutoka kwa Mzee Mtei, jee walipo kubali kudevaluate the currency baada ya mwaka 1985 then what happened? Did we achieved what IMF recommended? Why IMF waliondoka kutoka kwenye SAP and introduce PRSP? Akiwa Washington DC jee ni kwa ukubwa gani policies IMF zilikuwa zina reflect policy za Ronald Reagan and Thatcher za free market, small government and no intervation? Jee kwa umasikini wa asilimia 70 ni kweli tungeweza kushindana katika soko huria na kushinda?

Kusema kweli argument za Sheka zimebase kwenye chuki kati ya Capitalism and Socialism ndio maana kwa asilimia kubwa naona hazijengi bali zinaboa. Sababu badala ya kutoa maono yake concern policy alizopresent Mzee Mtei kwa Mwalim ana present personal attack. Hii inaonyesha jinsi gani bwana Sheka alivyokuwa hana sera, bali ni chuki.

Kwa wale ambao hawajajikita sana kwenye uchumi, labda niseme kwamba Sera za IMF and WB ndio zinaongoza dunia ya tatu kwa kiasi kikubwa. Na ukweli ulio wazi IMF hawana nchi hata mmoja ambao wataweza kusema wale wamefuata recommendation zetu na wamefananikiwa. Nionyesheni moja kama kuna mtu anafahamu.

Upande mwingine, nimesoma na kuresearch policy za Mwalim kwa muda sasa. Nimeongea na good economist mbalimbali kuhusu what was inside mwalim brain. Kusema kweli out of honest Nyerere policy was based on idealogy and not scietific facts, however it can be defended. As one fellow at Wall Street magazine said “Dr. Nyerere may have been poor economist but he was skillful nation builder. He fused Tanzanian’s 120 tribes into a cohesive state, preventing tribal conflicts plaguing so much of Africa”
 
Ndugu zanguni wana JF hoja siku zote hujibiwa na hoja. Wanaosema kwa nini Mzee Mtei kaandika kitabu leo, wanasahau kwamba kuandika kitabu ni haki yake ya msingi mzee Mtei. Prof.Babu aliandika kitabu chake wakati yupo jela, mpaka leo kuna baadhi ya Vyuo vinarecommend hicho kitabu.

Pili, ni vyema tusikilize pande zote mbili then tumia uwezo na upeo wako kujudge based on the facts presented. Na sio kusimama na kulalawa why now, why and why? Think kwanza then analyze.

Nikiwa kama mpenda uchumi, nimesoma vitabu vingi sana kuhusu IMF and World Bank na umafia wao. Kuna valid arguments ambazo tunaweza kujifunza kutoka kwa Mzee Mtei, jee walipo kubali kudevaluate the currency baada ya mwaka 1985 then what happened? Did we achieved what IMF recommended? Why IMF waliondoka kutoka kwenye SAP and introduce PRSP? Akiwa Washington DC jee ni kwa ukubwa gani policies IMF zilikuwa zina reflect policy za Ronald Reagan and Thatcher za free market, small government and no intervation? Jee kwa umasikini wa asilimia 70 ni kweli tungeweza kushindana katika soko huria na kushinda?

Kusema kweli argument za Sheka zimebase kwenye chuki kati ya Capitalism and Socialism ndio maana kwa asilimia kubwa naona hazijengi bali zinaboa. Sababu badala ya kutoa maono yake concern policy alizopresent Mzee Mtei kwa Mwalim ana present personal attack. Hii inaonyesha jinsi gani bwana Sheka alivyokuwa hana sera, bali ni chuki.

Kwa wale ambao hawajajikita sana kwenye uchumi, labda niseme kwamba Sera za IMF and WB ndio zinaongoza dunia ya tatu kwa kiasi kikubwa. Na ukweli ulio wazi IMF hawana nchi hata mmoja ambao wataweza kusema wale wamefuata recommendation zetu na wamefananikiwa. Nionyesheni moja kama kuna mtu anafahamu.

Upande mwingine, nimesoma na kuresearch policy za Mwalim kwa muda sasa. Nimeongea na good economist mbalimbali kuhusu what was inside mwalim brain. Kusema kweli out of honest Nyerere policy was based on idealogy and not scietific facts, however it can be defended. As one fellow at Wall Street magazine said “Dr. Nyerere may have been poor economist but he was skillful nation builder. He fused Tanzanian’s 120 tribes into a cohesive state, preventing tribal conflicts plaguing so much of Africa”


Mtanganyika:

Itabidi nijitoe. Maana naona mada ya Mtei ime-merged na mada zingine na kuwa thread moja.
 
Omarilyas said:
Lakini, ktika suala hili la Mzee Mtei na WB/IMF nina haya yafuatayo;

Hivi katika enzi zile za Reaganate and Thatchirite exterem right resurgence kulikuwa na uwezekano wowote kwa ka-Tanzania ketu kuwa na leverage ya kunegotiate na IMF and WB ambao walichukua kila ushauri wafuasi wa hawa Makaburu walioapa kuimaliza third world yote kama haitafuata na kuunga mkono aina ya dunia waliyokuwa wakiitaka wao. Hivi mnajua lugha waliyokuwa wakiitumia hawa ECONOMIC HITMEN waliokuja kumlazimisha Mwalimu kukubali matakwa yao na kuweza kupata support kwa Mzee Mtei?

Na unawezaje kuwa na leverages za kunegotiate na WB na IMF wakati ndio kwanza umetoka vitani hohehahe....

Hujui kuwa imechukua hadi miaka ya 2000 ndipo angalao Mkapa akaweza kujenga mazingira ya katusaidia kuanza kutofuata kila kilichomo katika blueprint za Washington na kujaribu kuja na kitu ambacho kina angalao kiasi fulani cha input yetu kwa jina la MKUKUTA?

Na kwa wale wanaodhani kuwa tungefuata huo ushauri wa Mtei tukafuata hizo dozi za IMF tokea wakati huo, huu mgawanyiko wa kipato/kitabaka uliopo sasa ambao ni moja kwa moja ni zao la sera za WB/IMF si ungeshafika kileleni ambako hata mimi na wewe tusingeweza kuvumiliana?


Omarilyas,

..tatizo lenu wengi mmesikiliza a one sided story for a very very long time.

..Mzee Mtei ameeleza sababu zilizompelekea kutoa mapendekezo yale kwa Mwalimu ktk kitabu chake.

..hata suala la devaluation amelielezea vizuri sana,tena kwa lugha rahisi kabisa, na sababu zake. kutokana na Mwalimu kuwa na mashaka na suala la devaluation, Mtei alipendekeza kuwe na gradual devaluation.

..of course we had very little leverage kutokana na matatizo ya uchumi ambayo tuliyasababisha sisi wenyewe. lakini vilevile leverage hiyo ndogo ilikuwa inaendelea kupungua jinsi tulivyokuwa tunasuasua kuchukua hatua za haraka kurekebisha uchumi wetu.

..matatizo ya kiuchumi yanafanana na maradhi ya binadamu. ukiyashughulikia mapema, basi unajiongezea probability ya kupona.

..Mkapa ameweza kuleta hiyo mkukuta kwasababu Mwalimu na Mzee Mwinyi walikubali ushauri wa kurekebisha uchumi miaka ya 80 na 90.

..wengine tume-experience matatizo yale, na nakuhakikishia sizingechukuliwa hatua za kuyarekebisha sijui tungekuwa wapi leo hii.

NB:

..kama Mtei alikuwa ni mtu mbaya aliyetoa mapendekezo ya kuangamiza uchumi wetu, mbona aliendelea kuwa na access hata na Mwalimu Nyerere?

..mbona ni serikali hiyo hiyo ya Mwalimu Nyerere iliyopendekeza Mtei aende kuongoza idara ya Afrika IMF?

..mbona Mtei aliporudi nchini Mzee Mwinyi alimteua kuongoza Tume ya kurekebisha idara zetu ya mapato na forodha. mapendekeo ya Tume ya Mtei ndiyo yaliyopelekea kuundwa kwa TRA.
 
Hii thread imebadilika ghafla sana. Nilivyoiacha jana siyo kama ilivyo leo; nashindwa kupata materials ya jamaa zangu tuliokuwa tuanbadilishana uchambuizi wa hali ya halisi ya wakati huo, badala yake imejaa upuuzi mtupu.

Ndugu zangu Zakumi, Mkandara, Jasusi, Waberoya, na Jokakuu; samahani kwa kupotezana kiasi kuwa sasa sijui nianzie wapi tena. Nadhani huu uvundo wa kulazimishana kuwapenda wanasiasa ukiisha tutairudia tena mada hii.
 
Here comes October 31 2010 suka ama nyoa chagua mwenyewe kwa upeo wako kati ya;

CHADEMA = CHAGGA DEVELOPMENT MANIFESTO and CCM = CHAMA CHA MAFISADI

Ndugu Mfunyukuzi,

Mimi binafsi napenda na kuheshimu sana watu wachapa kazi na wabunifu. Lakini kama CHADEMA ni CHAgga DEvelopment MAnifesto, napendekeza ufanye utafiti kidogo kuhusu uongozi wa hiki chama kilipoasisiwa 1992, ukilinganisha na uongozi wa sasa.

Mimi nilichaguliwa Mwenyekiti, 1992 Makamu wangu alikuwa Brown Ngwilulupi wa Tukuyu, Mbeya. Katibu Mkuu alikuwa Bob N. Makani wa Shinyanga na Makamu wake alikuwa Erick Mchatta wa Mtwara.

Uongozi wa sasa: Freeman Mbowe, Mwenyekiti, Makamu wake ni Said Arfi wa Mpanda, Mkoa wa Rukwa; Katibu Mkuu ni Dk. Willibrod Slaa wa Karatu na Makamu wake ni Zitto Kabwe wa Kigoma.

Kabla ya uongozi wa sasa, Mwenyekiti alikuwa Bob N. Makani na Makamu wake alikuwa ni Dk. Willibrod Slaa. Katibu Mkuu alikuwa Dk. Amaan W. Kabourou wa Kigoma.

Najivunia Chama nilichoshiriki ktk kukiasisi kwamba kinaendelea kuzingatia kuwa na uongozi wa kitaifa na papo hapo kusisitiza umahiri ktk uchambuzi wa masuala ya kitaifa wakiwa wazalendo waadilifu. Hakuna Uchagga ktk uongozi wake, bali labda pale watu wananuia kuwabagua.
 
Back
Top Bottom