Mtanzania kama hujawahi kufika South Africa, Europe au USA wewe ni mshamba tu

mdukuzi

JF-Expert Member
Jan 4, 2014
16,053
35,951
Godbless Lema alikuwa hajawahi kutoka nje ya East Africa, aliishia Nairobi tu, siku alipotoka nje ya Afrika ndio akagundua kumbe sisi hatuishi tunadumu. Ndio maana anaropoka tu, asamehewe, mashikolo mageni..

Nelson Mandela baada ya kutoka gerezani alikokaa kwa miaka zaidi ya 26 alikuta south Africa inawaka akawa anashangaa tu magorofa na mabarabara.

Kombe la dunia 2010 nchini South Africa loliwaacha wazungu midomo wazi,jiji kama Capw Town hata ulaya kuna majiji hayafikii uzuri wake

Kuna dada wakazi mmoja toka Iringa siku anaambiwa anaenda kufanya kazi Dar usiku hakulala.

Akapakizwa basi akashuka Magufuli stand then akapokelewa na mwenyeji wake mpaka Malamba mawili, baada ya miezi sita wakazinguana akarudi kijijini, ilikuwa ni kuponda jiji la Dar kuwa ni kubaya bora Iringa, kumbe hakuwahi kufika Kariakoo wala posta, Mbezi beach, Masaki, Oysterbay, Kigamboni, Msasani, Mikocheni, Mbweni nk.

Kuna watu wakiwa Dar wanajiona wajanja sana ila ni washamba.

South Africa ina vitu vya kushangaza, Europe na USA hali kadhalika.

Jambo ka kushangaza watanzania hatupendi kusafiri sijui kwa nini. Yaani ukienda nchi za watu utakuta wakenya na watu wa West Africa tu, watanzania ni wa kuhesabu. Hii inasababisha ushamba na uwezo mdogo wa kufikiri na ndio mtaji wa viongozi wetu ili watutawale.

Idara ya uhamiaji nayo ni kama imepewa maelekezo kunyima watu passport bila sababu za msingi.

Amin amin nawaambia bila kuusafiri nchi za wenzetu hatutobi. Akina Vasvo da Gama na Collumbus hawakuwa wajinga, Nyerere na Karume wakishasafiri kabla ya kuongoza nchi.

Nimeandika haya baada ya kukuta mzee mmoja huku Nzega hajawahi kufika Tabora mjini Tangu azaliwe halafu anakwambia Chama noma sijui CCM baba lao.

Kama hausafiri wewe ni mshamba,kusafiri ni elimu tosha
 
Back
Top Bottom