Mtaalamu wa Dawa na Tiba: Ninakaribisha maswali kuhusu Magonjwa, Tiba na Dawa

DR. mamaangu jicho moja haoni lina mtoto wa jicho na nimejaribu kwendanae hospital wanasema amechelewa kutibu hivyo hataweza kuona tafadhal naomba ushauri wako daktari
 
Naomba msaada wako doct kwamba mm kila nikiogea brashi basi mapaja yangu yanawasha kwa muda wa DKK(10). Ni kwa muda mrefu SAS hicho kitu kinanitokea mpaka Leo. Yaan naogopa hata kuoga doct.
 
KISUKARI NAMNA YA KU-CONTROL SUGAR

Hutokea mara moja moja kuamka sukari iko juu(8-10) nina 55yrs

Aidha kwa sbb zisizoeleweka(Malaria) au kubadilika muda wa kula au chakula hasa matunda/juice au hata kiwango cha chakula .

Hii hutokana na mazingira ya kazi yangu(safari n.k),

Dawa natumia Amarly M2 au Gema 2 asubuhi baada ya breakfast na usk baada Dinner.

Swali langu : je ukijikuta asb mfano sugar iko 9 na unasikia njaa na unahisi mwili uko weak unahitaji kula vizur na ushibe vzr, ni nini cha kufanya ?

1. Kuongeza dawa ? yaani badala x2 unywe x3 ?

2. Kuongeza dawa ? yaani badala 1 tab unywe kidonge 1na nusu x2 tu ?



Tafadhali naombeni USHAURI WENU Dr's na hata wagonjwa wenzangu.
 

Inabidi umpelekee kwa General Surgeon wamtizame kama anatatizo anatomically kwaajili ya tukio hilo.
 
Dr. sometimes ninapoenda kujisaidia haja ndogo mara nyingi nyakati za usiku ninapotokea usingizini hasa kama nimekunywa maji mengi, nahisi kama simalizi mkojo wangu, yaani nahisi kama umebaki ndani, aidha nikae muda mrefu nijaribu kuulazimisha au nirudi kulala halafu naweza kurudi tena kukojoa tena baada ya muda nakuta ndipo mkojo wote unatoka. Hali hii hunitokea nyakati za usiku tu nikitokea usingizini sio mchana, sina wala sisikii maumivu. Hii ni hali gani na huenda inasababishwa na nini?

Hii tatizo inaitwa "Impaired Bladder Emptying" na inaweza kutokana na infection au kama kuna blockage kwenye mirija ya kukojoa au kama mtu anatatizo ya prostate na kadhalika. Lakini tatizo yako inatokea usiku tu. Kuna wakati mwingine mtu anakuwa hayupo relaxed au anayo anxiety na hii tatizo linatokea. Jaribu kuvuta pumzi mara tatu (Deep breaths) kabla kukojoa. relax kidogo alafu maliza haja yako. Nipe mrejesho.
 
KISUKARI NAMNA YA KU-CONTROL SUGAR

Hutokea mara moja moja kuamka sukari iko juu(8-10) nina 55yrs

Aidha kwa sbb zisizoeleweka(Malaria) au kubadilika muda wa kula au chakula hasa matunda/juice au hata kiwango cha chakula .

Hii hutokana na mazingira ya kazi yangu(safari n.k),

Dawa natumia Amarly M2 au Gema 2 asubuhi baada ya breakfast na usk baada Dinner.

Swali langu : je ukijikuta asb mfano sugar iko 9 na unasikia njaa na unahisi mwili uko weak unahitaji kula vizur na ushibe vzr, ni nini cha kufanya ?

1. Kuongeza dawa ? yaani badala x2 unywe x3 ?

2. Kuongeza dawa ? yaani badala 1 tab unywe kidonge 1na nusu x2 tu ?

Tafadhali naombeni USHAURI WENU Dr's na hata wagonjwa wenzangu.


Kawaida huwa wanaongeza idadi ya dawa na siyo muda. Lakini ni vizuri ukwende kituo cha afya ili wapime HbA1C yako. Kipimo hiki litamsaidia daktari kukubadilishia dose. Vile vile, anaweza kuongeza dawa inaoitwa "Acarbose". Dawa hii inatumika nusu saa kabla ya kula chakula, inapunguza sukari inayochukuliwa na mwili. Ningekushauri pia ule chakula usiku kwa makini sana. Usile vyakula vyenye sukari au starch nyingi. Punguza viazi, wali, viazi tamu, mohogo, mahindi nk.
 
DR. mamaangu jicho moja haoni lina mtoto wa jicho na nimejaribu kwendanae hospital wanasema amechelewa kutibu hivyo hataweza kuona tafadhal naomba ushauri wako daktari

Mkuu, kwa hilo inabidi umuone daktai bingwa wa macho. Ampime na kutoa ushauri bora. Inabidi umuone "Opthalmologist".
 
Mtoto wangu ana miaka 2 sasa, akiwa na miezi 8-9 alianza kusumbuliwa na matatizo ya ngozi(ngozi kubabuka) hasa mgongoni na sehemu za joints, nikaambiwa hospital tatizo la joto(hali ya hewa),. lakini nilikaa kwa mda kama miezi miwili hali ikawa mbaya nikafanya vipimo vya allergy nikaambiwa asitumie vitu kama jamii ya samaki, karanga na maziwa ya kopo. nimezingatia lakini hali ilipungua kidogo. kuanzia mwezi 4/2016 hadi leo hali sio nzuri na imeanza kuzidi sana hasa 7/2016 yaani mtoto anajikuna hadi mgongo unakuwa mwekundu. kwenye mikono vinatoka viupele vyenye majimaji na kupasuka. sasa nimepita haspitali mbalimbali hadi wananichanganya hasa ni nini tatizo maana kila dr amekuwa akitaja ugonjwa tofauti na dr mwingine. Natanguliza shukrani kwa msaada wako.

Hii inaonekana kuwa heat rash. Inabidi nguo za mtoto zisimbane sana. Badilisha sabuni unaotunia kumuogesha. Jaribu kutumia sabuni special kwaajili ya watoto. Hakikisha nguo zake hazina unyevunyevu. Tumia hydrocortisone cream mgongoni. Inabidi upakae kidogo usiku kwa siku 3. Naomba unipe mrejesho.
 
Dr nina tatizo la sikio yapata miaka 3 sasa, sikio la kulia linapiga kelele ya mluzi mfululizo, ila haliumi wala halitoi uchafu, na sasa kuna uvimbe umetokea chini ya hilo sikio karibu na taya nao hauna maumivu, nimekwenda muhimbili nimepima kipimo cha uvimbe wa kansa majibu sio, sasa naona na upande wa kushoto napo pembeni ya sikio kunavimba. Tafadhali dr hizi ni sadaka kwako

Tafadhali tumia dawa hii, Dexamethasone + Gentamicin Ear Drops. Weka Drops 3 kutwa mara tatu kwa muda wa siku 10.
 
Doctor Dr. Sajjad Fazel naomba kuuliza kitu
mimi ni kijana wa kiume huwa nahisi ndani ya mwili wangu muscles zinakuwa zinachezacheza tena ni mwili mzima je tatizo linaweza kuwa ni nin na nin tiba yake
natanguliza shukran

Mkuu, tafadhali fafanua tatizo lako. Na je ukisema muscles zinacheza inakupa tatizo gani au unahisi vipi? Na pia unayo dalili yeyot kingine? Je unatumia dawa yeyote?
 
Hivi kwa nini mbu hawezi kueneza ukimwi hali ya kuwa anaweza akamnyonya damu mwenye ukimwi at the same time akunyonya na wewe lakini maambukizi usipate.

Mkuu, Umeuliza swali nzuri sana. Hizi hapa jibu:

  1. Mbu anatumia mirija tofauti kunyonya damu na kuingiza mate yake kwenye mwili wa binadamu. Vimelea vya malaria vinakuwa kwenye mate wake lakini virusi vya ukimwi vinakwenda tumboni na anaponyonya tena hizo virusi hazitoki tena.
  2. Tumbo la mbu linaua hizo virusi vya HIV.
  3. Mbu anachukua idadi ndogo sana ya damu.
 
Back
Top Bottom