Msingi wa Kuelewa Maadili ya Mgomo unaoendelea wa Madaktari Tanzania

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,476
39,995
Na. M. M. Mwanakijiji

Hakuna mgomo unaoitishwa na wafanyakazi ambao unawagawa wananchi mara moja tena kwa ukali kama mgomo wa madaktari. Mara moja mgomo wa madaktari unapoitishwa pande mbili zinazokinzana hujitokeza kwa haraka kama kufuatana kwa radi na ngurumo. Pande hizi zinakuwa na tofauti kubwa sana kiasi kwamba kwa haraka haraka ni vigumu kuona ni jinsi gani pande hizo mbili zinaweza kupatana au hata kukaribiana na kutafuta suluhu.

Upande mmoja kunakuwepo na wale ambao mara moja wanachukulia uamuzi wa madaktari kugoma kuwa ni mashambulizi dhidi ya afya za wagonjwa. Hawa huamini kuwa hakuna mazingira yanayoruhusu madaktari kugoma kwa sababu kufanya hivyo ni kupitisha sentensi ya kifo kwa wagonjwa ambao wanawategemea madaktari hao. Hivyo, upande huu mara nyingi hujenga hoja kuwa madaktari waendelee na kazi wakati “matatizo yao yanashughulikiwa” kwani kutofanya hivyo “ni kuhatarisha maisha ya wagonjwa na watu wasio na uwezo”.

Hoja ya hawa pia inaupande unaotokana na kile kinachoitwa “wito wa udaktari” yaani ni miongoni mwa kazi ambazo toka enzi na enzi zilionekana zina wito wa pekee. Miongoni mwa kazi nyingine zilizoonekana ni za wito ni zile za kidini, uwakili na ualimu. Kiongozi wa dini anatakiwa kutoa huduma ya kiroho bila kujali anayempatia huduma hiyo ni mtu wa namna gani, wakili anatakiwa amtetee mtu kwa uaminifu wa hali ya juu na mwalimu anatakiwa kumfundisha mtu mjinga na kumwondolea ujinga wake hata kama kufundishika kwa mtu huyo ni kugumu kupita kiasi.

Hata hivyo, tofauti na kazi hizo nyingine za wito ni kazi ya udaktari kwa namna ya pekee ambayo ina kitu kingine kinachokosekana kwenye hizi kazi nyingine – uhai na kifo. Madaktari wanahusika na afya za wagonjwa na hivyo maamuzi yao (mazuri au mabaya) yana matokeo ya moja kwa moja kwa mwanadamu mwingine au wanadamu wengine. Daktari akigoma kusaidia mama mja mzito anayejifungua ambaye mtoto wake amekabwa na kitovu (umbilical cord) mama na mtoto maisha yao yanaweza kuwa hatarini.

Wakili akikataa kumtetea mtu au akimtetea mtu vibaya kuna uwezekano uamuzi mbaya (adverse decision) kwa mtu huyo unaweza kugeuzwa katika rufaa na kumpa nafasi nyingine. Mtu aliyefundishwa na mwalimu mbaya ana uwezo wa baadaye kupata nafasi ya kufundishwa na mwalimu mzuri; mtu ambaye amechukizwa na mafundisho ya kiongozi wa dini yake anaweza akaamua kwenda na kukumbatia mafundisho ya dini nyingine. Mtu ambaye amekufa kwa sababu daktari ameshindwa kufanya kitu au amekifanya vibaya hana rufaa wala nafasi ya pili.

Ni kutokana na hili ndio maana watu wanaoamini katika kiapo cha Hippocriti wanaamini kabisa kuwa madaktari hawatakiwi kuchukua uamuzi wowote ambao utasababisha madhara kwa mgonjwa kwani ameapa “kutomsababishia madhara mgonjwa”. Hivyo, kwa msingi wa hoja hii mgomo wa madaktari ni mwiko kabisa na hakuna mazingira yoyote ambayo mgomo unaruhusiwa. Kwamba, hata kama madaktari wanafanya kazi katika hali mbaya kiasi gani, hata kama madaktari wana matatizo ya namna gani yanayotokana na maslahi yao, na hata kama madaktari wananyanyaswa vipi na mwajiri wao jukumu lao la kwanza ni kwa mgonjwa na wanatakiwa kufanya lolote lile kuhakikisha kuwa wagonjwa hawadhiriki. Mgomo unavunja utakatifu (the sacredness) wa kiapo chao.

SOMA ZAIDI KWENYE FIKRA PEVU


Au Download:
 

Attachments

  • MSINGI WA MAADILI YA MGOMO WA MADAKTARI.doc
    76.5 KB · Views: 173
Mgomo kama hatua ya mwisho
Wakati sekta nyingine wanaweza kuchukulia mgomo kama kitu cha kawaida cha kudai maslahi kwa daktari mgomo ni lazima uwe hatua ya mwisho na unapochukuliwa usiachiliwe kirahisi – kwani ukiachiliwa kirahisi ni rahisi kurudiwa tena baada ya muda mfupi. Mgomo wa madaktari ni lazima uwe na malengo ambayo yanaeleweka, yanayotimilizika na ambayo yanaweza kubadilisha hali yao kwa haraka. Hauwezi kuwa mgomo wa jumla wa kudai "maslahi" tu.

Ni kwa sababu hiyo madaktari wanapoamua kugoma hasa kwa nchi nzima basi ni lazima taifa lishtuke. Ni lazima wanasiasa na viongozi wajiulize imekuwaje tumefika mahali madaktari wa nchi nzima wanagoma. Kwamba, kuna kitu kimeshindikana kwa njia ya mazungumzo hilo ni dhahiri na kwamba watawala na wanasiasa wameshindwa kuweka uzito kwenye hoja za muda mrefu za madaktari nalo ni dhahiri. Madaktari wanapoitisha mgomo wa nchi nzima ni lazima watu wawajibishwe (heads must roll!).

Hii ni kwa sababu matokeo ya mgomo wa madaktari kwa muda mfupi ni msukumo (pressure) kwenye sekta ya afya ambayo kwa kweli haistahili kuwepo kwani matokeo yake mara zote ni makubwa sana. Mara nyingi matokeo ya mgomo wa madaktari hayaondoki mara moja. Nchini Malta mgomo wa madaktari uliwahi kudumu kwa miaka kumi! Huko New Zealand mgomo wa madaktari ulisababisha madhara ambayo hadi leo bado mwangwi wake unasikika katika huduma ya afya. Mgomo wa madaktari kinyume na migomo ya kada nyingi matokeo yake hudumu kwa muda mrefu ndio maana tunaposikia madaktari wamegoma tusichukulie kiurahisi – manake ni kuwa wamelazimika kugoma.

Madaktari wa Tanzania na migomo
Mwaka 2006 mgomo wa madaktari wa Muhimbili haukuungwa mkono kitaifa. Kwa kiasi kikubwa ulihusiana na ongezeko la posho na mishahara. Wakati ule kwa wanaokumbuka niliunga mkono upande wa serikali. Niliamini kwa serikali ambayo ilikuwa imeingia madarakani miezi michache nyuma yake ilikuwa siyo nafasi nzuri ya kudai ongezeko kubwa kabla serikali hiyo haijakaa chini kupitisha bajeti mpya. Hivyo, mgomo ule kwa kiwango kikubwa ulikuja wakati usiofaa.

Hata hivyo, leo hii miaka zaidi ya mitano baadaye ninaamini kabisa kuwa kama serikali yetu ingetaka kushughulikia tatizo la maslahi na mafao ya madaktari ingeweza kufanya hivyo. Hakuna tatizo ambalo linazungumzwa leo hii ambalo lilikuwa halijulikani miaka minne nyuma au miaka mitatu nyuma. Niruhusu kufafanua.

Mwaka 2008 utafiti ulichapwa katika Jarida la East African Journal of Public Health Volume 5 Number 1 April 2008 ukiwa na kichwa cha habari "Motivation of Health Care Workers in Tanzania: A Case Study of Muhimbili National Hospital". Katika utafiti huo mambo mbalimbali yalionekana ambayo naamini yatupasa tuyafikirie kidogo kabla hatujaamua kuchukua upande mmoja au mwingine katika mjadala wa mgomo huu unaoendelea.

Utafiti huu ulifanyika kati ya 2003-2004 ukihusisha watumishi 462 walihusishwa katika pool ya watumishi wapatao 2310. Watafiti waligundua mambo yafuatayo (kati ya mengine mengi)

  • Asilimia 88 ya watumishi waliamini kuwa mwajiri wao hawajali (kati yao madaktari asilimia 82.4, Manesi asilimia 90.7 na Watumishi wengine 87.9)
  • Asilimia 63.3 ya madaktari walionesha kutoridhika na mishahara yao huku kwa manesi ikiwa ni asilimia 66.7
  • Sababu tatu kubwa zilizoonekana kuwafanya watumishi hao kutokuwa na motisha mzuri wa kazi – kwa mfuatano wa uzito wake – ni mishahara, mazingira ya kazi, na vifaa duni vya kazi.
  • Karibu asilimia 30 ya manesi walikuwa hawajaridhika na kazi zao kiasi cha kutaka kuacha kazi hizo. Kwa madaktari ni asilimia 29
Je, kuna jambo lolote ambalo tunaweza kusema leo katika mgomo huu halikuwa likijulikana?

Ufisadi na maslahi ya madaktari
Mojawapo ya mambo ambayo labda Watanzania hatujakaa chini na kuyahusisha na matatizo mengi tunayoyaona kwenye sekta za elimu, afya, maji na nishati ni suala la ufisadi. Nimewahi kuandika huko nyuma kuwa ufisadi una gharama na gharama yake kubwa hulipwa na maskini! Kinyume na watu wengi wanavyofikiria matajiri na wale wenye uwezo hulipa gharama ya ufisadi lakini wanailipa kwa sababu wanaimudu. Mtu tajiri au mwenye uwezo akiumwa kichwa anakimbilia India; mbunge amejitengenezea sheria inayompa haki ya kufanyiwa uchunguzi nje ya nchi kila mwaka; Rais amepewa haki hiyo kwa maisha yake yote hata akitoka kwenye cheo chake. Maskini hata hivyo mpaka vikao vifanyike na apitie uchunguzi mrefu ndio atapatiwa nafasi ya kwenda kwenye hospitali ambayo imeteuliwa na watu wengine!

Maskini ambaye hatopata nafasi hiyo anajikuta anahangaika na hospitali za humu humu nchini au mambo yakiwa magumu zaidi huishia kwenda kunywa kikombe, kupiga ndumba na ramli au kuishia kwenye imani za kidini. Tajiri atatafuta vitu hivyo vingine pale ambapo fedha zake zimeshindwa kumsaidia! Wakati kwa maskini ramli, ndumba na ibada ni vitu vya kwanza kwa tajiri ni vya mwisho (ukiondoa wale ambao wanachanganya mumo kwa mumo).

Kwenye taifa kama la kwetu ambapo ufisadi umetamalaki matokeo yake ni makubwa zaidi. Leo hii serikali inaweza kusimama na kusema kuwa haina uwezo wa kuboresha maslahi ya madaktari au kununua vifaa au kuhakikisha vifaa vinafanya kazi. Kwa kawaida hili linaweza kuwa kweli kama wananchi wangekuwa hawasikii kashfa mbalimbali za ufisadi na upotevu wa mabilioni ya fedha za umma. Siyo kwenye sekta nyingine tu bali pia kwenye sekta ya afya yenyewe.

Katika mwaka wa fedha ulioishia Juni 2010 Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu aligundua kati ya mambo mengine mengi kuhusiana na wizara ya Afya

  • Kiasi cha sh 1,895,253,371 kililipwa kwa wazabuni kabla ya kupokea vifaa. Hata hivyo, ukaguzi uliofanyika katika idara za Wizara umebaini kwamba vifaa vya thamani ya sh 1,648,407,271 vilikuwa havijaletwa.
  • Kanuni 198 ya sheria ya fedha za umma ya mwaka 2001 inasema kwamba vifaa vyote vilivyonunuliwa lazima viandikwe kwenye daftari la vifaa. Kinyume na kanuni hii Wizara haikuandika kwenye daftari vifaa vya thamani ya Sh 148,293,950
  • Taarifa ya upotevu ilionyesha upotevu wa kiasi cha sh 4,709,461,863.63 ikihusisha upotevu wa vifaa kiasi cha sh. 2,383,792.63 na madawa yaliyopitwa na wakati kiasi cha Sh.4,707,078,078,071 kwenye Idara ya Bohari Kuu ya Madawa katika mikoa mbalimbali.Upotevu huu ni wa tangu mwaka 2003/2004
  • Wizara ya Afya na Usitawi wa Jamii hupeleka fedha katika bohari ya madawa kwa ajili ya hospitali ya mkoa ili kununua madawa na vifaa vya hospitali. Ukaguzi ulibaini kwamba hospitali ya mkoa wa Singida haikuwa na kumbukumbu za fedha zilizoletwa na Wizara ya Afya na Usitawi wa Jamii kwenda hospitali ya mkoa kununua madawa na vifaa vya hospitali ingawa bohari ya madawa ilionyesha kiasi cha 248,990,169 katika taarifa za fedha.
  • Ilionekana kuwa malipo yaliyofanyika kununulia kemikali katika mwaka huu yaliongezeka kufikia Shilingi bilioni 6.7 kutoka shilingi bilioni 2.3 za mwaka uliopita ikiwa ni ongezeko la asilimia 200. Hali hii inaonyesha kuwa ongezeko limetokana na kutokuwepo udhibiti mzuri wa Kemikali hizo. Kutokuwepo kwa udhibiti wa kemikali za maabara kutoka stoo za hospitali hupelekea Hospital ya Muhimbili kuingia gharama za ziada kununua kemikali ambazo mara nyingi zinatumiwa isivyopaswa.
  • Ukaguzi ulibaini kuwepo kwa tofauti kati ya mishahara inayotoka Hazina na ile inayoandaliwa na baadhi ya Mashirika ya Umma. Katika Hospitali ya Muhimbili, Tume ya Ushindani wa Biashara (FCC) na Chuo Kikuu cha Dodoma ambapo mishahara ilikuwa inalipwa tofauti na ile inayotoka Hazina. Hali hii inaweza kupelekea udanganyifu kwenye malipo ya mishahara ikiwa ni pamoja na kulipwa kwa mishahara hewa.
Hiyo ni mifano michache tu ya kuonesha kuwa Wizara ya Afya yenyewe ina matatizo mengi ya msingi ambayo yanajulikana vile vile ambayo gharama yake bila ya shaka inalipwa na hali mbaya ya maslahi ya madaktari.

Mgomo ni lazima uwe na matokeo ya kuboresha afya za wananchi
Mgomo huu hauwezi kuwa ni mgomo wa maslahi ya madaktari tu na ndio maana binafsi siamini kuwa unapaswa kumalizika kwa "serikali kukubali kutoa nyongeza" kwani kufanya hivyo ni kujiandaa kwa matatizo mengine. Kuna mambo au vitu ambavyo vinatakiwa kukubaliwa na serikali sasa hivi pamoja na hilo suala la maslahi. Serikali ni lazima iwe tayari kuweka ahadi na kutenga fedha mara moja kwa ajili ya kushughulikia baadhi ya matatizo sugu yanayokabili hospitali zetu.

Mgomo huu utakuwa wa manufaa katika matokeo yake endapo tu:

Serikali itakubali kuweka viwango vya ubora wa huduma inayotakiwa kutolewa katika hospital zetu, viwango ambavyo wananchi watatarajia kuviona. Je, Mtanzania atakapoenda kwenye hospitali baada ya mgomo huu ataona nini tofauti katika huduma inayotolewa kwake kama mwananchi, mlipa kodi na mteja? Ni lazima kuwe na tofauti.
Vifaa vya msingi kwa huduma ya hospitali vinaanza kupatikana. Iwe mwiko kwa mwananchi kwenda na glovu yake au sindano yake kwenye hospitali. Wananchi wanatarajia kuona kuwa vitu vya kawaida kwa huduma hospitali vinapatikana kama sehemu ya matibabu. Daktari au muuguzi ni lazima awe na vifaa vya msingi tena vya kisasa ambavyo vitamsaidia kutoa huduma kwa mgonjwa. Haiwezekani nesi anapoenda kazini awe amebeba na box la glovu au bandeji!

Madaktari pamoja na wauguzi wanapatiwa afueni ya msingi ikiwemo kwenye kodi zao na mishahara yao. Ni lazima tuwape motisha ili kwamba tukitaka daktari aache usingizi na kukimbia kumhudumia mgonjwa asitusonye! Tusimfanye daktari achague kati ya kwenda kusimamia baa yake au kwenda kuhudumia wagonjwa. Wauguzi wasilipe kodi ya mapato!

Serikali iamue mara moja kuwekeza katika ujenzi wa nyumba za madaktari katika maeneo yaliyo karibu na mahospitali. Habari kuwa ati katika nchi nzima serikali imeamua kujenga nyumba nane za madaktari ni kuchezea akili za Watanzania! Kwanini hawakujenga nyumba mbili za mawaziri kama majaribio au ofisi moja ya TAKUKURU kama mfano? Kwanini JWTZ au JKT wasihusishwe katika kujenga nyumba za kisasa (flats au bungalows) kwa ajili ya madaktari kutokana na hadhi zao? Binafsi naamini pa kuanzia tu serikali ijicommit katika kujenga nyumba zisizopungua 100 za madaktari mikoani kwa mwaka huu na kabla ya 2015 zifikie nyumba zisizopungua 1000! Kama tumeweza kujenga nyumba ya Gavana kwa bilioni 3 kwa mtu mmoja na nyumba ya Spika na za wabunge nina uhakika serikali inaweza kabisa kuanza ujenzi wa nyumba za madaktari.
Serikali ianze kutekeleza mpango wa kujiondoa kwenye uendeshaji wa baadhi ya hospitali na kuziachilia zianze kuwa hospitali binafsi au zenye ushiriki wa umma. Kwa mfano, miji au halmashauri ziachiliwe ziwe na udhibiti kamili wa hospitali zao (kuanzia ajira, mafao n.k). Serikali yetu imekuwa kubwa sana (inasimamia polisi, walimu, afya, jeshi n.k) kuna mambo mengine yanaweza kufanywa na serikali za mitaa au halmashauri au sekta binafsi.

Serikali ifanya haraka kutengeneza ilipoharibu
Mgomo huu unaweza kuisha mara moja na ukaisha vizuri. Lakini, ninaamini hauwezi kwisha bila kumalizika. Hauwezi kumalizika kama ulivyolazimishwa ule wa 2006 ambapo serikali iliamua kuwatimua madaktari kwani tofauti na wa wakati ule huu wa sasa umeenea nchi nzima na tukio lolote la kutishia kuwafukuza madaktari (walioanzisha au walioshiriki) linaweza kuwafanya madaktari kuwa na msimamo mkali ziaid.

Serikali ikubali kuwa imefanya makosa mengi kwenye sekta ya afya na kuwa wakati umefika wa kupitia sera yake ili kufanyia mabadiliko na iwaahidi Watanzania kuwa inapokuja bajeti mpya mabadiliko makubwa yanakuja. Kama serikali haina watu wenye uwezo wa kufikiria sera bora za afya basi iajiri watu ambao watasaidia kuwapa mawazo mapya nje ya yale waliyoyazoea – mimi niko tayari kuwasaidia hapo.

Kitu pekee ambacho serikali isifanye ni kupuuzia kwa sababu wasiposhughulikia kwa ukamilifu wake vyanzo vya mgomo huu na kutengeneza pale ambapo wao serikali wameharibu wajue kabisa kuwa mgomo huu hautakuwa wa mwisho na utazidisha chuki ambacho wananchi wameanza kuwa nayo dhidi ya serikali yao. Chuki ya namna hii mara zote inasababisha watu kuchukia chama tawala kinachounda serikali hiyo na hatimaye kukikataa kwenye sanduku la kura. Sasa hivi, inaonekana serikali inajaribisha uvumilivu wa wananchi. Uvumilivu una kikomo.

SOURCE : FIKRA PEVU
 
HILI NDIO KUNDI NTASIMAMA NALO MPAKA MWISHO NA HUU NDIO UKWELI
"Upande mwingine hata hivyo, wapo wale ambao wanaona kuwa madaktari nao kama wanadamu wengine wanaishi kwa kutegemea jasho lao. Kwamba, madaktari licha ya kwamba wanashughulikia afya wanatarajia kuwa na wao waweze kuishi maisha yanayoendana na utu na kutegemea ujuzi wao. Lakini vile vile madaktari wanatarajiwa kuwa katika hali inayowafanya waweze kufanya kazi yao kwa ufanisi bila kuwa na sababu ya kutokuwa makini."
 
for me not to do harm to my patient i have to be @ peace with my body and soul.how can i attain that peace kwa mazingira na usumbufu uliopo hospitalin mwetu?ntatibuje kama sijalipwa??ni bora nigome kuliko kumuattend mgonjwa unfairly
 
NI bora madaktari wagome leo ili kesho wawe wanatoa huduma bora zaidi!!! it is a painful stage we have to pass through:poa
 
for me not to do harm to my patient i have to be @ peace with my body and soul.how can i attain that peace kwa mazingira na usumbufu uliopo hospitalin mwetu?ntatibuje kama sijalipwa??ni bora nigome kuliko kumuattend mgonjwa unfairly
gomeni tu wanasiasa hawana heshima na taaluma za watu
 
Tatizo ni tafsiri ya kiapo, hakuna haki bila wajibu, anayetafuta haki ya kutibiwa awajibike na kuandaa mazingira. Mfumo wetu unalazimisha taaluma hii isimamiwe na wanasiasa, Madaktari ni washauri tu wa mazingira yao ya kazi, wanasiasa ndio waamuzi wa kila kitu. Si ajabu kukuta dharau juu ya haki za madaktari inatolewa na kisingizio cha kiapo. Tuangalie kwa upana juu ya weledi wa taaluma unakuzwa na mazingira yepi iwapo kutwa ni udhalilishaji wa siasa, ukabila na mengineyo. Tuwe wakweli, sakata lote la udhalilishaji huu linaanzia kwa Luahnjo kujenga tabaka la wakwetu pale MoHSW. Blandina na Mtasiwa wako nyuma ya sakata hili, wawe wakweli kwa nini hawaendi kuzungumza na madaktari, badala yake kutoa mipasho kupitia vyombo vya habari. Hoja ni muktadha wa uwajibikaji zaidi kuliko maslahi. Hili la ubaguzi lina implication kwenye utawala wa Wizara hii. Pole Mponda, umedandia Meli sijui kama unajua. Kumbuka wewe ni mteule wa wananchi, huwajibiki kwa Wizara, waache hao wafanyakazi watekeleze wajibu wao, wewe fanya kazi ya kuwasimamia na kukemea uzembe wao, wacha wajisemee wao.
 
Ahsante sana mkuu,

Jamii forums inagreatthinkers wazuur sana. Hii inathibitisha kuwa iwapo CCM itang'oka nchi yetu inaweza pia kubadilika.
Daktari afanye upasuaji apewe allowance 10,000-mbunge anachapa usingizi wala hatoi mchango wowote mjengeno alipwe 200,000 allowance!!!!!!!!!!!!!!!!

To hell-Endeleeeni kugoma. Kada zingine nazo ziunge tela ikiwezekana.
 
Mzee Mwanakijiji,

Unaonaje ubabe unaofanywa na wizara kwa hawa madaktari? Kumbuka ni wanadamu, wana shida kama za kwangu na zako, wanafamilia, wanatakiwa walipie pango, usafiri n.k. Je wasipopata haki yao watatoaje huduma hii kwa wagonjwa? Hapa serikali lazima iwajibike na kuheshimu taaluma ya udaktari.
 
Asante sana kwa kuileta hapa!!

hii nimeipenda,ila kwenye hippocrit oath kuna kipengele kinazungumzia kwamba na maisha ya daktari yawe ya amani,upendo na utulivu nyumbani na kazini. Pia afya yake na ndugu zake ijaliwe. Unaposhindwa kuboresha mazingira ya kazi ni kumkosesha vitu hivyo akiwa kazini.

Kumpa mshahara kidogo na marupurupu duni ni kumkosesha vitu hivyo nyumbani na kazini. Mungu wabariki watanzania wote wanaounga mkono mageuzi yanayokuja maana yatanufaisha hata wale wanaopinga kwa wakati huu. Dodoma wamefunga hospitali kabisa leo!
 
jamii lazima ielewe kwamba haya madai sio kwa faida ya madaktari tu ni kwa faida ya jamii nzima ya watanzania.Killa mtanzania anastahili huduma bora.ni hizi huduma zinakuwa insured na serilkali kwa sababu ndo inakusanya kodi na kusimamia vyanzo vingine vya mapato kwa ajili ya kumuhudumia mtanzania.Upatikanaji wa huduma bora unaendana na upatikanaji wa vifaa tiba,madawa na watoa huduma waliowezeshwa(haya ndo madai ya madaktari wanayopigania).Haya yakifanikiwa kila mtanzania atafaidika.Kila mtanzania atakuwa na uhakika kuwa akiumwa akapelekwa hospitalini atapata vipimo vyote vinavyohitajika na atahudumiwa na mtu ambaye hajaelemewa na stress zake,wala hatakuwa na zazo kwamba mpaka utoe chochote au au umfahamu mhudumu wa afya ndipo utakapohudumiwa.Movement ya madaktari ni kwa faida ya watanzania wote.Kila mtanzania mwenye upeo hana budi kuwaunga mkono
 
sina cha kuchangia umemaliza vyote, lakini mwalimu ndicho chanzo kikuu cha kuwa uwezo wa kutambua kitu lakini ndiyo taluma inayonewa sana duniani
 
Baada ya kusoma hoja zilizopo kwenye mada yako, Maswali haya yananitatiza:-
1. Ni kweli kwamba unaweza kulipeleka jeshi vitani bila silaha kwa kuwa tu limekula kiapo kulinda nchi hadi kifo?
2. Hivi tutamtafsiri vipi daktari asiyekuwa na fedha ya kutosha kisha kula chakula kichafu na kupata kipindupindu au kichocho au kuhara?
3. Mbunge anayeomba aongezwe posho ili akasimame kwenye TV kutoa msaada wa magunia ishirini ya mahindi akijinadi anaguswa na maisha magumu ya wananchi unamtafsiri vipi?
KUNA WAKTI INABIDI BAADHI YA WATU WAUMIE ILI KUREKEBISHA TATIZO!!
 
na hawa watu wanaendelea kutupumbaza kuwa "serikali haina pesa", "serikali inalishughulikia suala la madaktari", nk wakati huku nyuma wanatwambia uchumi unakua kwa 7.8%!!!

Na hawa wabunge kama wanadai haya basi ni bora wangepewa kitu kama performance contract ili anayefika bungeni na kufikisha alichotumwa na wananchi wake (matatizo ya madaktari) ndipo apate hiyo posho na sio kuipata kwa kulala (kusinzia fofofo), Madaktari wakiamua nao kuwa wanaenda kazini wanasinzi fikiria itakuwaje!?
Ahsante sana mkuu,

Jamii forums inagreatthinkers wazuur sana. Hii inathibitisha kuwa iwapo CCM itang'oka nchi yetu inaweza pia kubadilika.
Daktari afanye upasuaji apewe allowance 10,000-mbunge anachapa usingizi wala hatoi mchango wowote mjengeno alipwe 200,000 allowance!!!!!!!!!!!!!!!!

To hell-Endeleeeni kugoma. Kada zingine nazo ziunge tela ikiwezekana.
 
Ndugu M.M Mwanakijiji,

Nadhani unakumbukumbu nzuri kuwa mimi ni mmoja wa watu tunaokubaliana na mgomo huu kwa namna yeyote tokea Lula Mwananzela alipoandika. Ndugu yangu hii piece ni best justification ever written ikiweka na kutumia ushaidi uliowazi kutoka ndani ya serikali ya CCM inayoongoza nchi kwa miaka 50 tokea uhuru. Tutagoma lakini tatizo/failure ni CCM political ruling elite ambao wanadictate priority za sera zote. Tunaongozwa na sera za CCM na hizo ndizo utekelezaji wake umetufikisha hapa. Binafsi naamini demands za madaktari kidogo zimemiss goal posts. Hasa sababu ya kusema Blandina Nyoni, Mtasiwa, Nkya, Mponda etc wajiuzulu sio solution kwani wao ni sehemu ndogo. Kuwashutumu hao bila kuijumuisha Ikulu "magogoni" na kiongozi wake JK kwenye sentensi moja ni kukwepa ukweli na kitendo cha kuonyesha uoga/weakness mbele ya adui wa afya zetu. Inatubidi kusema "spade a spade rather than shovel"
 
Ndugu M.M Mwanakijiji,

Nadhani unakumbukumbu nzuri kuwa mimi ni mmoja wa watu tunaokubaliana na mgomo huu kwa namna yeyote tokea Lula Mwananzela alipoandika. Ndugu yangu hii piece ni best justification ever written ikiweka na kutumia ushaidi uliowazi kutoka ndani ya serikali ya CCM inayoongoza nchi kwa miaka 50 tokea uhuru. Tutagoma lakini tatizo/failure ni CCM political ruling elite ambao wanadictate priority za sera zote. Tunaongozwa na sera za CCM na hizo ndizo utekelezaji wake umetufikisha hapa. Binafsi naamini demands za madaktari kidogo zimemiss goal posts. Hasa sababu ya kusema Blandina Nyoni, Mtasiwa, Nkya, Mponda etc wajiuzulu sio solution kwani wao ni sehemu ndogo. Kuwashutumu hao bila kuijumuisha Ikulu "magogoni" na kiongozi wake JK kwenye sentensi moja ni kukwepa ukweli na kitendo cha kuonyesha uoga/weakness mbele ya adui wa afya zetu. Inatubidi kusema "spade a spade rather than shovel"

Kujiuzulu kwa viongozi hao wa wizara mwanzoni ingekuwa ni nje kidogo ya hoja ya madaktari lakini kwa kuendelea kwa mgomo kwa zaidi ya siku nne sasa kunahalalisha watu hawa kuachilia nafasi zao. Kwa sababu, kwanza wangeweza kabisa kuzuia mgomo huu - japo wanaweza kujitetea kuwa wanatekeleza sera tu zilizoamriwa toka juu - na pili dalili za mgomo zilipoanza kuja wangefanya kila liwezako kuuepuka. Bahati mbaya hawakufanya hilo la pili.

Mgomo huu lazima uondoke na hawa watu wizarani hatuwezi kuwa na miungu kwenye utumishi wa umma!
 
Back
Top Bottom