Kwanza, si busara hata kidogo kuihusisha CCM katika matukio hayo, kwani uchunguzi unaofanywa na vyombo vya dola umeshindwa mpaka sasa kuhusisha matukio hayo na siasa, badala ya kuyahusisha na makosa ya jinai ambayo hufanywa na watu kwa malengo tofauti na yale ambayo Ndg. Mbowe anataka kuwaaminisha watu.
Pili, CCM haijawai, haiwezi, na haitakuja fanya jambo lolote lenye lengo la kuvuruga Amani na Usalama wenye utulivu ndani ya taifa letu, hivyo uzushi na usingiziaji uliofanywa na Mtu Kama Ndg. Mbowe, si vema kuuacha kimya, badala yake nimetumia wasaa Huu muhimu Kujibu, na kutoa ufafanuzi ili Kuupa umma wa watanzania habari sahihi.
Ni aibu kwa Chama kama Chadema kujitahidi kwa nguvu zote kujaribu kuficha ukweli wa mauaji yanayotoa roho za watanzania wenzetu kwa kuyapa sura ya kisiasa. Hizi ni juhudi za makusudi za kutaka kuficha ukweli wa kinachotokea.
Ni aibu kwa chama kama Chadema kujaribu kutumia mauaji mabaya kama haya kutafuta mtaji wa kisiasa. Huku ni kuonyesha jinsi gani wamefilisika kisiasa mpaka wanafikia mahali pa kuamini kuwa wanaweza kutumia chochote kama mtaji wa kisiasa, vikiwemo vifo vya watanzania wenzetu. Huku si kufilisika tu ila kwakweli ni unyama unaotakiwa kulaaniwa na kila muungwana.
Nape Moses Nnauye
Chama Cha Mapinduzi
Ideology and Publicity Secretary
Si muda mrefu hawa tutawazika wazima wazima! It is just a matter of time! CCM siyo Mungu hata itawale milele. Vyama vyote vya siasa Africa vilivyo-take over baada ya wakoloni mwishoni mwa miaka ya 1950 na mwanzoni mwa miaka ya 1960 kusini mwa Sahara imebaki CCM tu. Very soon tutawazika wazima wazima. VERY VERY SOON!
Inashangaza kuona kada wa chama anatoa tamko linaloihusu jeshi la police,hv kinamanumba kz imewashinda.Sasa napata picha ni kweli policesisiem wanawaham wauwaji,ila kwakuwa jeshi le2 halipo huru ndo vile watoto wa mama kina nape wanadantia mambo.
Nape ni kilaza kweli hawezi kujenga hoja .Nape my young brother why are you unrealistic you can think hata kidogoNAPE kwisha kazi! Ni kelele za Mfa maji tu. CDM haiui kimwili mtu yeyote, inaua DHANA,MTAZAMO,FIKRA NA MAZOEA yote ya KIFISADI.Na hatimaye CCM itakufa.