Msichana wa Kazi anatafutwa

Teh teh teh! Mshikaji hatafuti mchumba, anatafuta HG!
Kweli mkuu mbona kuna site nyingi sana za kutafutia wachumba? Kwi kwi Jamaa ameamua kunimwaga tu, Kumtoa mtu out ukampe maneno inacost kiasi gani mpaka uingie kwa gia za kutafuta mhudumu wa nyumbani khaa
 
Msichana wa kazi anatafutwa kwa kazi za ndani kijijini kwa mkataba wa miezi Mitatu kwanza kuanzia Dec 15 akifanya vizuri mkataba unaweza kuongezwa.
SIFA
Umri - wowote
Msafi
Elimu angalau Form IV

Job Discription:
Kufanya shughuri zote za ndani ikiwemo kupika, usafi wa nyumba kwa familia ndogo.Mshahara - Kima cha chini cha serikali
Kwa mwenye Interrest au anajua mtu anayetaka hiyo kazi aniandikie mbogela@jamiiforums.com au Pm
Asanten

Familia ndogo kiasi gani?
 
Kweli mkuu mbona kuna site nyingi sana za kutafutia wachumba? Kwi kwi Jamaa ameamua kunimwaga tu, Kumtoa mtu out ukampe maneno inacost kiasi gani mpaka uingie kwa gia za kutafuta mhudumu wa nyumbani khaa

Taratibu mkuu, akikuchenjia mimi simo! Mimi naamini kweli anatafuta HG, tumsaidie tu mkuu. Si unacheki kwenye sifa hajainclude figure, sura, urefu n.k?
 
Taratibu mkuu, akikuchenjia mimi simo! Mimi naamini kweli anatafuta HG, tumsaidie tu mkuu. Si unacheki kwenye sifa hajainclude figure, sura, urefu n.k?

Mkuu ilikuwa sentensi yangu mwajiri, Nilikuwa nafafanua kuwa nikihitaji mchumba au demu sijui mbona kuna site nyingi na wapo wengi wanatafuta watu wawatoe out alafu wakawape maneno ha ha ha
 
Mkuu ilikuwa sentensi yangu mwajiri, Nilikuwa nafafanua kuwa nikihitaji mchumba au demu sijui mbona kuna site nyingi na wapo wengi wanatafuta watu wawatoe out alafu wakawape maneno ha ha ha

Oh, sorry mkuu nimejimix. Sasa hiyo familia ndogo kiasi gani? Unajua kwa wengine familia ndogo ni watu wawili wakati kwa wengine ni 8!
 
we vipi mtu ataenda kununua cheti ili awe hausgal
fikiria kidogo
Tutakapofikia hali hiyo basi wanafunzi wa vyuo vikuu watakuwa wanatuhudumia kwenye mabaa, wakulima wetu wa monelemango watakuwa wanasoma Makaubaliano ya Marais juu ya mazao ya chakula kwenye mikutano yao ya WTO
 
Tutakapofikia hali hiyo basi wanafunzi wa vyuo vikuu watakuwa wanatuhudumia kwenye mabaa, wakulima wetu wa monelemango watakuwa wanasoma Makaubaliano ya Marais juu ya mazao ya chakula kwenye mikutano yao ya WTO

dada ulaya wanafunzi wa vyuo vikuu wanafanya kazi kwenye bar/madukani nk, hawaoni tatizo lolote
kwani wanafunzi wa bongo wakifanya kazi kwenye bar kuna tatizo gani????
 
Ataishi kwangu, lakini akimua kuishi kwake haitakuwa tabu lakini kumbuka ni kijijini. Ajira inapatika wilayani Makete


makete ipo iringa..
na iringa ndio inaongoza kwa kutoa ma house girl nchini.
so maybe muanzie huko kwanza.
 
Back
Top Bottom