Msiba Wa Mwana JF

RIP Mpenzi wa Islam
Pole kwa msiba huu mzito X-Paster tuko pamoja.
 
SAD NEWS... Mwenyezi Mungu ampe pumziko la amani.

Nasikitika kuondokewa na mwenzetu lakini hii ni ishara tosha kuwa sote tu wa njia moja!

Kwaheri Mpenzi wa Islam, hapa JF tutakukumbuka daima
 
ooh!
r.i.p mpenzi wa islam

LAKINI.........
MBONA TAARIFA IMEKUJA KWA KUCHELEWA SANA?
Taarifa imechelewa kwa sababu Marehemu alikuwa anaishi Dar ES salaam na mimi naishi nje ya bara la Afrika, ilikuwa kama bahati tu, baada ya kuona kwenye MSN kuwa yupo online, baada ya kuulizia kumbe alikuwa Binti yake na ndiye aliyenipa taarifa ya msiba.
 
Inna Lillahi wa Inna ilayhi Raj'oon

Verily to Allah we belong & to him we shall return

Taarifa ya Msiba wa MwanaJF


Kwa niaba ya Familia ya Ndugu yetu na mwanachama mwenzetu Aliyekuwa akijulikana kwa jina la Mpenzi wa Islam, wanasikitika kutangaza kifo cha ndugu yetu Mpenzi wa Islam Kilichotokea tarehe 19th - March - 2010.

Marehemu aliuguwa ghafla moyo na akafariki na kuzikwa siku hiyo hiyo, mjini Dar es salaam. Taarifa hizi nimeletewa na Binti yake na Marehemu.

Marehemu alikuwa si Swahibu yangu tu, ila alikuwa ni ndugu yangu na mshauri wangu wa karibu sana. Huu ni msiba mkubwa kwa kweli.
_____________

"Surely Allah takes what is His, and what He gives is His, and to all things He has appointed a time...so have patience and be rewarded." [Bukhari] -
Dhikr & Patience are the most befitting Remedy

X-PASTER yaani huu msiba umenigusa sana. Mpenzi wa Islam nilitokea kumuheshimu sana katika mijadala ambayo alikuwa anashiriki hasa ya kidini ambapo siku zote alikuwa haonyeshi jazba, au kutumia lugha kali kama wachangiaji wengine.

Nilimuona kama ndugu yangu na katika watu katika ukumbi huu ambao nilipenda sana kukutana nao uso kwa uso yeye ni mmoja wao ukiwemo na wewe pia na wote niliwataarihu kuhusu nia yangu hiyo. Kweli wema hawaishi maisha marefu.

Sitaweza tena kutimiza nia yangu ya kukutana na huyu mtu ambaye nilimuona alikuwa na kipaji cha ajabu katika ustahimilivu mkubwa sana. Kwaheri rafiki yangu ukapumzike pumziko la milele lililojaa amani.

Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi na awape nguvu wafiwa katika kipindi hiki kigumu sana kwao~AMEN
 
OH NO!
I will be in denial but death is unavoidable.
M.W.I . will be remembered by many as a defender of the defenceless.Binafsi nitakukumbuka sana na RIP!
 
Eeh mola uilaze roho ya marehemu pema peponi
Inna Lillahi wa Inna ilayhi Raj'oon

Sote ni wa Mola na kwake turarejea!
 
X-PASTER, wanafamilia na wana JF poleni kwa kuondokewa na mpiganaji. Mungu Ailaze mahali pema peponi roho ya marehemu kama kweli anastahili. Je katika mazingira kwamba mwana JF sio hai tena kuna haja ya kuendelea kuficha identity yake halisi? Ningependekeza jina lake halisi litajwe kwani hakuna madhara yoyote yatakayomkuta katika mazingira kwamba hayupo pamoja nasi tena hapa duniani.

Tiba
 
Pole sana wafiwa
Mungu awape moyo wa uvumilivu
.....Mungu na ashukuriwe zaidi maana yote ni katika yeye....
R.I.P Mpenzi wa uislam
 
X-PASTER, wanafamilia na wana JF poleni kwa kuondokewa na mpiganaji. Mungu Ailaze mahali pema peponi roho ya marehemu kama kweli anastahili. Je katika mazingira kwamba mwana JF sio hai tena kuna haja ya kuendelea kuficha identity yake halisi? Ningependekeza jina lake halisi litajwe kwani hakuna madhara yoyote yatakayomkuta katika mazingira kwamba hayupo pamoja nasi tena hapa duniani.

Tiba
Mkuu Tiba, ni kweli maneo yako, lakini kwa kuzingatia kuwa yeye mwenyewe (Marehemu), tangia uhai wake hakuweza kuweka bayana Jina lake halisi wala nasaba yake basi itakuwa si haki kuliweka hapa jina lake na nasaba yake. Kwa kweli itakuwa si kumtendea haki marehemu. Naomba turidhike kama mlivyo ridhika kulikubali jina lake la kupanga.
 
Mkuu Tiba, ni kweli maneo yako, lakini kwa kuzingatia kuwa yeye mwenyewe (Marehemu), tangia uhai wake hakuweza kuweka bayana Jina lake halisi wala nasaba yake basi itakuwa si haki kuliweka hapa jina lake na nasaba yake. Kwa kweli itakuwa si kumtendea haki marehemu. Naomba turidhike kama mlivyo ridhika kulikubali jina lake la kupanga.


Mkuu X-PASTER nakubaliana kabisa na uamuzi wako wa kutoliweka jina la marehemu hapa jukwaani. Yeye mwenyewe alipokuwa hai hakupenda kufanya hivyo, hivyo kuliweka jina hilo sasa hivi itakuwa si kumtendea haki marehehemu, ndugu, jamaa na marafiki zake.

Niliwahi kuwa na mazungumzo na mtu hapa jukwaani ambaye tunafahamiana kwa miaka mingi tu, basi ikaja hii topic ya kufariki from nowhere akaniuliza nikifariki utawaambia Jamii kama nimefariki au la? Je, utatumia jina langu la kwenye forum au jina langu la kweli? Basi tukajadili kwa kirefu na hatimaye tukafikia makubaliano kwamba ni bora tu kutumia jina la kwenye forum ili kuwatendea haki ndugu, jamaa na marafiki zake akiwamo na yeye mwenyewe. Hakuwa mgonjwa wala nini ni mazungumzo tu yalifuata mkondo ambao sisi wala hatukuupanga uelekee kwenye topic hiyo ya kufariki.
 
RIP Mpenzi wa Islam.

Poleni sana wafiwa, pole sana X-PASTER!
 
Back
Top Bottom