Msalaba wa Urais

benzemah

JF-Expert Member
Nov 19, 2014
1,504
3,034
Na Ezekiel Kamwaga

Msalaba wa Urais Katika kipindi cha miaka 30 iliyopita, mmoja wa wanafamilia ya Rais aliye madarakani amekuwa akizushiwa tuhuma za rushwa na ufisadi.

Lakini tuhuma hizo hudumu wakati wa urais wa mume/baba/mke/mjomba na husahaulika anapoingia mwingine tuhuma hizo huyeyuka. Mara Nyingi huwa utajiri na ufisadi haujawahi kuonekana wala kuthibitishwa.

Wakati wa utawala wa Rais Mwinyi, tuliambiwa Mama Sitti ndiye kinara wa ufisadi na kwamba ameigeuza Ikulu kuwa pango la wezi na mafisadi. Kuna wakati alianza kufananishwa na Imelda Marcos wa Ufilipino.

TUHUMA
Alipoingia Benjamin Mkapa, Ikawa zamu ya Mama Anna Mkapa. Tukaambiwa Taasisi ya Fursa Sawa kwa Wote (EOTF) ilikuwa inanufaika na Urais na ni kichaka cha wapiga dili. Tukaambiwa Mama Anna ni tajiri wa kutupwa kwa sababu ya ufisadi wa taasisi hiyo.

Alipoingia Dkt Jakaya Kikwete

Ikawa zamu ya Ridhiwani Kikwete. Akiitwa Riz One wakati huo. Tukaambiwa kwamba anamiliki vituo vya mafuta na ana ukwasi usio na maelezo. Nchi nzima kulikuwa na nyumba, vituo vya mafuta na magari yake. JK alipotoka madarakani, utajiri wa mwanaye ukaishia hapo.

Alipoingia Dkt John Pombe Magufuli

Ikawa zamu ya Dotto James. Kila mradi mkubwa, kila uwekezaji na kila tajiri aliyeibuka, ilielezwa kuna mkono wa Dotto. Baada ya Magufuli, Dotto sasa hana shida. Na huo utajiri na ukwasi wake hauonekani popote.

Katika namna ileile ya Mwinyi, Mkapa, Kikwete na Magufuli, kwenye Urais wa Dkt Samia Suluhu

Naona sasa ‘jumba bovu’ linaanza kumwangukia mtoto wake Abdul. Staili ni ileile ya Mama Siti, Mama Anna, Ridhiwani na Dotto. Tuhuma nyingi bila ushahidi. Bila shaka Urais wa Samia ukiisha Tutahamia kwa mtoto/mke/mume/binamu/Kaka wa Rais mwingine atayekuja.

Sidhani kama huu ni utamaduni mzuri kuwa nao. Tunaharibu maisha na afya ya akili ya watu pasi na kujali. Wakati wazazi wao wakiwa marais, Ridhiwani na Abdul walikuwa vijana wadogo wenye umri chini ya miaka 30. Baadhi ya maneno na tuhuma wanazosikia kuwahusu zitawaachia makovu ya kudumu kwenye maisha yao.

Mimi ni mwandishi na nafahamu umuhimu wa kuwa na jamii iliyo tayari kufichua maovu. Hata hivyo, ni muhimu kutenda haki. Hii ‘kawaida yetu’ inaharibu maisha ya watu. Hakuna mtu aliyeomba kuzaliwa na fulani hapa duniani.

Nafahamu machungu ya baadhi ya watu waliowahi kutuhumiwa huko nyuma. Usiombe kupitishwa kwenye hicho kikombe. Leo kwa mwenzio, kesho kwako.

Siasa nyepesi sana hizi, kikubwa lazima watambue kwa nafasi walioko na ukaribu walioko na Rais ni rahisi sana kuzusha mambo kama hayo na kuaminika kirahisi. Hakuna haja ya kuibeba na kuiweka moyoni na kuacha makovu wachukulie ni sehemu ya maisha kwa watu wa karibu na Rais.

Ikulu.jpeg
 
Nchi hii ina watu wengi wanaopenda udaku na kuona wenzao wakifeli, hili kwa kiasi kikubwa ndio chanzo cha hayo
 
Hoja ijibiwe na hoja, awamu ya kwanza ya President Nyerere (rip),sio mke wake au mtoto wake aliyesemwa kwamba anajilimbikizia mali kifisadi, next President Mwinyi, huyu alikua na wake wawili rasmi sasa why why why mama sitti ahusishwe na sio mama Khadija?

Next President Mkapa (Mr.Clean), why mke wake Anna ahusishwe na ufisadi?wakati mme wake eti alikua anaendesha a clean government?(huyu alibinaifisha mashirika mengi ambayo President Nyerere aliyaanzisha)next president kikwete huyu ana mke mmoja rasmi na watoto kadhaa, why Jina la mtoto Riz lichomoke pekee kwenye ufisadi?

Then President Magufuli, mke wake mama Josephine Jina lake lilikua clean, watoto wake hata kujulikana hawakujulikana,binafsi nimesikia uwepo wao wakati wa mazishi ya baba yao except yule wa kike na issue ya masomo, but Jina la Dotto James likachomoza kifisadi, mtoa hoja hii sio rocket science, hao wote uliowataja kwa ufisadi ni mafisadi kweli, taasisi za utawala bora zinakuja na katiba mpya, yatajitokeza tu,tukipata judiciary huru, HRC huru, Press huru yenye waandishi wa kiuchunguzi, PP,DPP huru, then ukweli utaanikwa.
 
Hoja ijibiwe na hoja, awamu ya kwanza ya President Nyerere (rip),sio mke wake au mtoto wake aliyesemwa kwamba anajilimbikizia mali kifisadi, next President Mwinyi, huyu alikua na wake wawili rasmi sasa why why why mama sitti ahusishwe na sio mama Khadija?

Next President Mkapa (Mr.Clean), why mke wake Anna ahusishwe na ufisadi?wakati mme wake eti alikua anaendesha a clean government?(huyu alibinaifisha mashirika mengi ambayo President Nyerere aliyaanzisha)next president kikwete huyu ana mke mmoja rasmi na watoto kadhaa, why Jina la mtoto Riz lichomoke pekee kwenye ufisadi?

Then President Magufuli, mke wake mama Josephine Jina lake lilikua clean, watoto wake hata kujulikana hawakujulikana,binafsi nimesikia uwepo wao wakati wa mazishi ya baba yao except yule wa kike na issue ya masomo, but Jina la Dotto James likachomoza kifisadi, mtoa hoja hii sio rocket science, hao wote uliowataja kwa ufisadi ni mafisadi kweli, taasisi za utawala bora zinakuja na katiba mpya, yatajitokeza tu,tukipata judiciary huru, HRC huru, Press huru yenye waandishi wa kiuchunguzi, PP,DPP huru, then ukweli utaanikwa.
Well said, HOJA IJIBIWE KWA HOJA na mimi naongeza KWA FACTS.
Kwa ulichoandika "hao wote uliowataja kwa ufisadi ni mafisadi kweli" hebu thibitisha
 
Well said, HOJA IJIBIWE KWA HOJA na mimi naongeza KWA FACTS.
Kwa ulichoandika "hao wote uliowataja kwa ufisadi ni mafisadi kweli" hebu thibitisha
Unasema tuhuma hizo ni uzushi na hazijawahi thibituka,

Nami nikuulize, SHERIA ipi inaruhusu Rais aliyetoka madarakani aweza shtakiwa?

Tunadai KATIBA mpya itokanayo na Rasimu alosimamia Judge WARIOBA Ili Rais asiwe juu ya Katiba, awajibishwe Kwa Kila ovu akitenda kinyume na Katiba.

Aamen
 
Na Ezekiel Kamwaga

Msalaba wa Urais Katika kipindi cha miaka 30 iliyopita, mmoja wa wanafamilia ya Rais aliye madarakani amekuwa akizushiwa tuhuma za rushwa na ufisadi.

Lakini tuhuma hizo hudumu wakati wa urais wa mume/baba/mke/mjomba na husahaulika anapoingia mwingine tuhuma hizo huyeyuka. Mara Nyingi huwa utajiri na ufisadi haujawahi kuonekana wala kuthibitishwa.

Wakati wa utawala wa Rais Mwinyi, tuliambiwa Mama Sitti ndiye kinara wa ufisadi na kwamba ameigeuza Ikulu kuwa pango la wezi na mafisadi. Kuna wakati alianza kufananishwa na Imelda Marcos wa Ufilipino.

TUHUMA
Alipoingia Benjamin Mkapa, Ikawa zamu ya Mama Anna Mkapa. Tukaambiwa Taasisi ya Fursa Sawa kwa Wote (EOTF) ilikuwa inanufaika na Urais na ni kichaka cha wapiga dili. Tukaambiwa Mama Anna ni tajiri wa kutupwa kwa sababu ya ufisadi wa taasisi hiyo.

Alipoingia Dkt Jakaya Kikwete

Ikawa zamu ya Ridhiwani Kikwete. Akiitwa Riz One wakati huo. Tukaambiwa kwamba anamiliki vituo vya mafuta na ana ukwasi usio na maelezo. Nchi nzima kulikuwa na nyumba, vituo vya mafuta na magari yake. JK alipotoka madarakani, utajiri wa mwanaye ukaishia hapo.

Alipoingia Dkt John Pombe Magufuli

Ikawa zamu ya Dotto James. Kila mradi mkubwa, kila uwekezaji na kila tajiri aliyeibuka, ilielezwa kuna mkono wa Dotto. Baada ya Magufuli, Dotto sasa hana shida. Na huo utajiri na ukwasi wake hauonekani popote.

Katika namna ileile ya Mwinyi, Mkapa, Kikwete na Magufuli, kwenye Urais wa Dkt Samia Suluhu

Naona sasa ‘jumba bovu’ linaanza kumwangukia mtoto wake Abdul. Staili ni ileile ya Mama Siti, Mama Anna, Ridhiwani na Dotto. Tuhuma nyingi bila ushahidi. Bila shaka Urais wa Samia ukiisha Tutahamia kwa mtoto/mke/mume/binamu/Kaka wa Rais mwingine atayekuja.

Sidhani kama huu ni utamaduni mzuri kuwa nao. Tunaharibu maisha na afya ya akili ya watu pasi na kujali. Wakati wazazi wao wakiwa marais, Ridhiwani na Abdul walikuwa vijana wadogo wenye umri chini ya miaka 30. Baadhi ya maneno na tuhuma wanazosikia kuwahusu zitawaachia makovu ya kudumu kwenye maisha yao.

Mimi ni mwandishi na nafahamu umuhimu wa kuwa na jamii iliyo tayari kufichua maovu. Hata hivyo, ni muhimu kutenda haki. Hii ‘kawaida yetu’ inaharibu maisha ya watu. Hakuna mtu aliyeomba kuzaliwa na fulani hapa duniani.

Nafahamu machungu ya baadhi ya watu waliowahi kutuhumiwa huko nyuma. Usiombe kupitishwa kwenye hicho kikombe. Leo kwa mwenzio, kesho kwako.

Siasa nyepesi sana hizi, kikubwa lazima watambue kwa nafasi walioko na ukaribu walioko na Rais ni rahisi sana kuzusha mambo kama hayo na kuaminika kirahisi. Hakuna haja ya kuibeba na kuiweka moyoni na kuacha makovu wachukulie ni sehemu ya maisha kwa watu wa karibu na Rais.

View attachment 2484617
Kama Rais ana msalaba , atafutwe Harmonize ili aubebe huo msalaba, maana msalaba wa Kajala ameshautua.
 
Unasema tuhuma hizo ni uzushi na hazijawahi thibituka,

Nami nikuulize, SHERIA ipi inaruhusu Rais aliyetoka madarakani aweza shtakiwa?

Tunadai KATIBA mpya itokanayo na Rasimu alosimamia Judge WARIOBA Ili Rais asiwe juu ya Katiba, awajibishwe Kwa Kila ovu akitenda kinyume na Katiba.

Aamen
Kipengele hiki ndicho kinachofanya watu wanaowhabikia katiba Mpya wakati Samia akiwa madarakani kuwa ni wapuuzi! Hivi mnamuona Samia mpuuzi kiasi hicho! Ajinyonge ili ku afurahisha, thubutu! Cc Erythrocyte
 
Kipengele hiki ndicho kinachofanya watu wanaowhabikia katiba Mpya wakati Samia akiwa madarakani kuwa ni wapuuzi! Hivi mnamuona Samia mpuuzi kiasi hicho! Ajinyonge ili ku afurahisha, thubutu! Cc Erythrocyte
Ni Mapambano,

KATIBA mpya ni sasa.
 
Back
Top Bottom