Bengoldstar
Member
- Apr 24, 2022
- 67
- 46
- Thread starter
- #21
Ahsante sana kwa somo hili hakika nalichukua kwa mikono miwili na nitalifanyia kazi nitafute watu wa kufanya kisomo nadhan nitakuwa sawa boss.Hii ndoto ya kuota upo shule ni maarufu sana ila watu wengi wanaichukulia poa. Unaota upo darasa la saba wakati na wenzako wakati ulimaliza la saba miaka 20 iliyopita. Unaota upo shule unafanya mitihani na una hofu kubwa kwani hujasoma na mtihani ndio huo kesho.
Kwa kifupi tu ndoto hii inaashiria kurudishwa nyuma katika ulimwengu wa roho. Maendeleo yako yamekwamishwa kiroho kwa njia za kichawi. Shukuru kwamba umeota hivyo na haitakuwa mwisho hadi utatue tatizo lililopo katika ulimwengu wa roho.
Mara nyingi ni uchawi wa kumkwamisha mtu, roho ya konokono, roho ya kobe au ya kinyonga. Hizi ni roho za kukufanya usiende mbele kimaendeleo kwa kasi yako. Mara nyingi pia ni mtu anatumia nyota yako kichawi. Kifupi umepigwa stop.
Wengi hupatwa na roho hiyo pia kutokana na kuibiwa nyota kunakotokana na kulala na wanawake wanaotumika kama maagenti wa kuiba nyota za watu kupitia kujamiiana. Ni wengi mno huibiwa kwa njia hii.
Unapaswa kuondoa makwazo hayo katika ulimwengu wa roho. Nakushauri mtafute mtu wa kweli wa Mungu, mwombeaji hodari mwenye nguvu za Mungu wa Kweli akuombee.