Msaada wa kunifikisha mkutano wa vijana zurich!

kijanamakini

Senior Member
Nov 2, 2010
116
13
Habari kwa wanajamii forums wote!
Mimi ni kijana wa kitanzania ninaye amini katika mabadiliko na maendeleo. Naimani kama tunataka kujenga taifa la kisasa na lenye mitazamo ya kisasa katika masuala yote ya kijamii, kama siasa, uchumi, mazingira na teknolojia then tunaitaji vijana wenye mtazamo wa kisasa na waliopevuka katika nyanja za kimataifa na wenye mtazamo mpana.
Kuja katika point ya mzingi ni kwamba nimebaatika kuwa accepted kuiwakirisha Tanzania katika mkutano wa kimataifa utakaofanyika jijini Zurich mwezi wa tisa mwaka huu. Ila naitaji sponsor wa kunisaidia kulipa gharama, kiasi chochote kinakaribishwa. Tupo vijana sita kutoka Tanzania ila ushiriki wa kila mmoja wetu utategemea mchango tunaoweza kuchangia kufikia goal la 3000Euros per candidate/delegate. Pesa hizo sitazishika mimi bali mtu yeyote au kupitia kampuni itakayokuwa tayari kunisaidia nitatuma official mail kwanu yenye contacts za One Young World organisation ili malipo yafanyike kati yenu. Mambo yakikamilika wao ndio watakaonilipia ticket na kila kitu kwa siku 4-6 za mkutano huo.

Tunategemea kukutana vijana 1500, 300 from Africa. Walezi wa mkutano huu inawajumuisha Kofi Annan na Desmond Tutu, theme ni kujenga viongozi wapya kutoka kwa vijana.Nimechagua kushiriki kwenye panel za Environment, Leadership, Health and Media. Kwa kuwa Instructitions aziruhusu kuweka links hapa sitaweza fanya hivyo. Ila kama kuna mtu yupo tayari kunisaidia nitashukuru sana namba yangu ya simu ni 0717790034, ukiwasiliana nami nitakupa profile link yangu ya One Young World ili uweze kunifahamu zaidi, twitter napatikana kama 'stevpm'.

Asanteni sana!
Stev
 
Kwahiyo unaleta mambo ya siri siri kama ccm? weka link hapa tujuwe kama kweli kuna hiyo event, na tujiridhishe kama hiyo event haikugharamii kila kitu, hapa ni open forum na tunazungumzia swala la cash, kwahiyo hakuna kazi ya kutoa cash pasipo kujiridhisha.
 
Back
Top Bottom