Wanajamii tumekuwa tukilalamika sana juu ya ufaulu wa wanafunzi juu ya hasa masomo ya sayansi bila kutoa suluhisho la tatizo hilo hasa kwa shule za kata. Sisi hapa Ngara mkoa wa kagera kama vijana tumejinga pamoja chini ya mwavuli wa cbo yetu nakufikiri kuanzisha maabara ya masomo ya sayansi kwa wanafunzi wanaosoma masomo hayo huku wakitokea majumbani mwao ili wakiwa na muda wao wa ziada waweze kutumia center hiyo kujiongezea maarifa zaidi kwani vifaa vya practical havipatikani kwenye shule zao na hivyo waweze kutumia kituo hicho ili waweze kufanya mitihani yao kutumia kituo hicho. kituo hicho pia kitakuwa na huduma ya maktaba kwa vitabu vya sayansi kwani hapa ngara hakuna community library. kwa yeyote ambaye anaweza kutusaidia ili tupate vifaa( chemicals and apparatus) tungekaribisha msaada huo napia tutaweza kumtumia project plan yetu na mahitaji yetu kwa ujumla. tunaweza kuwasiliana kwa email mwijagejr@gmail.com.
tunatanguliza shukrani ili tuweze kuwakwamua vijana wetu pia kuwa na wanasayansi imara.
tunatanguliza shukrani ili tuweze kuwakwamua vijana wetu pia kuwa na wanasayansi imara.