Cantalisia
JF-Expert Member
- Sep 26, 2011
- 5,222
- 2,929
- Thread starter
- #61
Hapo tunatafuta njia ya kuairisha ndoa,ikishindikana hakuna jinsi ni bora aibu kuliko ndoa.Sasa anaoana na mtu ambaye hawawezi kukaa na kuongea nae kama kuna issue? Katika hili la yeye kuongea na mtu wake wazazi wanalizuiaje? Tatizo ni kama yeye mwenye hajiamini katika uamuzi anaotaka kuufanya.
Well, tuseme hakuna nafasi ya mazungumzo na wazazi na hata mwanaume...so anabakiwa na reasonable options mbili tu (zote ni za aibu!), moja ni kukimbia (kuna risk ya kutafutwa na kupatikana!) na nyingine ni kukataa (kwenda kwenye send off kama ipo, akishindwa atakataa kwenda kanisani, akishindwa anakataa kula kiapo cha ndoa (hili lipo kwenye uwezo wake hakuna wa kumlazimisha!) na kutia saidi cheti cha ndoa).