Msaada tafadhali,binti kagundua mme mtarajiwa anaigiza ulokole, kumbe .......!

Sasa anaoana na mtu ambaye hawawezi kukaa na kuongea nae kama kuna issue? Katika hili la yeye kuongea na mtu wake wazazi wanalizuiaje? Tatizo ni kama yeye mwenye hajiamini katika uamuzi anaotaka kuufanya.

Well, tuseme hakuna nafasi ya mazungumzo na wazazi na hata mwanaume...so anabakiwa na reasonable options mbili tu (zote ni za aibu!), moja ni kukimbia (kuna risk ya kutafutwa na kupatikana!) na nyingine ni kukataa (kwenda kwenye send off kama ipo, akishindwa atakataa kwenda kanisani, akishindwa anakataa kula kiapo cha ndoa (hili lipo kwenye uwezo wake hakuna wa kumlazimisha!) na kutia saidi cheti cha ndoa).
Hapo tunatafuta njia ya kuairisha ndoa,ikishindikana hakuna jinsi ni bora aibu kuliko ndoa.
 
Mwenye pesa shetani makanisani kwa walokole anatengewa siti ya mbele kabisa ili iwe rahisi kutoa maburungutu ya sadaka.
Shetani wa pesa ana nguvu, si umeona wakwe wameng'ang'ania binti yao aolewe ili misaada ya shetani iendelee kumiminika
Sawa nakubali shetani yupo ila hawezi kushinda nguvu ya mungu hasa hasa anaijaribu tu,ndio maana mungu kamfunulia jen ubaya wa huyu mtu mapema kabla ya ndoa!
Na siku mungu akiamua kumuumbua shetani ndio km hv jamaa ukweli ukiwa wazi kazi yake kwisha!
 
Aisee mpe Jen pole sana.

Nikirudi baadaye ntamshauri cha kufanya.

Hamjamboni mabibi na mabwana?

Cantalasia mambo?
Shikamoo babu ODM!
Pole imefika,ila nakusubiri babu utoe andiko lako hapa lol!
 
No alimpenda kwa upendo wa kweli,baada ya kugundua jamaa kamdanganya kuwa kaokoka,kawadanganya wazazi,na hata kanisa pia na haya yote ni ili amuoe,kadanganya mpaka kazi yake,ndio maana jen hampendi tena!
Kwan hana imani naye tena inawezekana ana uovu mwingi nyuma ya pazia na hapo mapnzi yameisha.

Unafikiri huyo tajiri angemwambia jeni kuwa hajaokoka angempata jeni? na hakika asingempata na mabinti wa siku hizi ukimwambia ukweli tu anakukimbia mabinti wa siku hizi wanapenda kudanganywa jamaa nae amenitumia style hiyo
 
Mtandao wa Jinsia, TGNP, TAWLA nk wanasoma humu au wajulishwe mapema waingie kazini, namwonea huruma binti/dada yetu!
Nimekusoma na umenikumbusha kitu,ngoja kuna mtu niongee naye anahusika kbs!asante mkuu!
 
Unafikiri huyo tajiri angemwambia jeni kuwa hajaokoka angempata jeni? na hakika asingempata na mabinti wa siku hizi ukimwambia ukweli tu anakukimbia mabinti wa siku hizi wanapenda kudanganywa jamaa nae amenitumia style hiyo
Ndio ajiaandae kuumbuka,na ndio atajua mungu ni zaidi ya shetan na pesa zake!
 
Asante sisy,tatizo ni kwamba wale wazazi ulokole umewaingia kupita kiasi na jamaa alivyojidai ameokoka anahudhuria mpaka mikesha mbaya hapo ndio hata yy akamwamini, alfu kawa mdhamin wa familia anaprovide mahitaji yote.
Anataman kumwambia jamaa ukweli lkn je atakubali na keshatumia garama za kuandaa harusi na tayari wazazi wako upande wa jamaa itasaidia da husni?
Hapa labda hilo la kuugua au atoroke japo sina uhakika km atakuwa na ujasiri wa kutoroka!

HAYO NDO MADHARA YA WAZAZI WETU KUZAA WATOTO ILI WAJE WAWALETEE RETURNS(MAHELA) TOFAUTI NA WENZETU WA MBELE WANAZAA MTOTO kutokana mshiko wa kumlea na ku mprovidia mahitaji yake muhimu hatimaye wanamuacha ajiamulie akiwa huru kujiamulia mambo yake mwenyewe akiwa mkubwa.
 
Walikuwa hawajui bwana,unafikiri jamaa angekuwa mkweli jen angekubali?wala asingekubali na wasingefikia huku kote!

jeni si alikuwa anataka ndoa? na msimamo wa wadada wengi hata kama anatongozwa na chizi au mvuta bangi huwa inakuwa wanataka aende kwa wazazi kisha ndoa sasa jeni ni kigeu geu jamaa ametimiza yote leo anasema hamtaki kwa vile jamaa sio mlokole
 
HAYO NDO MADHARA YA WAZAZI WETU KUZAA WATOTO ILI WAJE WAWALETEE RETURNS(MAHELA) TOFAUTI NA WENZETU WA MBELE WANAZAA MTOTO kutokana mshiko wa kumlea na ku mprovidia mahitaji yake muhimu hatimaye wanamuacha ajiamulie akiwa huru kujiamulia mambo yake mwenyewe akiwa mkubwa.
Uko sahihi kbs mkuu!
Hela shetani.
 
Unafikiri huyo tajiri angemwambia jeni kuwa hajaokoka angempata jeni? na hakika asingempata na mabinti wa siku hizi ukimwambia ukweli tu anakukimbia mabinti wa siku hizi wanapenda kudanganywa jamaa nae amenitumia style hiyo
Wala jeni sio kigeu geu,tatizo ni uongo wa jamaa,kwann asingekuwa mkweli ili km jeni anamkubali, basi amkubali akiwa anajua ni mtu ambaye hajaokoka na nayeuza hayo mavitu kwan kungekuwa na shida gani?uongo ndio tatizo!
 
Wala jeni sio kigeu geu,tatizo ni uongo wa jamaa,kwann asingekuwa mkweli ili km jeni anamkubali, basi amkubali akiwa anajua ni mtu ambaye hajaokoka na nayeuza hayo mavitu kwan kungekuwa na shida gani?uongo ndio tatizo!

jen akaendelea kuwasiliana na jamaa na wakawa marafiki akamkaribisha kanisani kwao jamaa akawa anakuja mpaka naye akaokoka

Jeni aliamua kumbadilisha msimamo wa kidini jamaa mpaka akakubali na akaokoka na kubatizwa kwa maji mengi leo jeni anamgeuka na kumwona jamaa hafai sio mlokole kamili hivi kuna kipimo cha ulokole? jeni alimpa jamaa test afanye akachemka leo jeni anaconclude jamaa hafai kumwoa jeni? basi nyie marafiki zake mmemwonea wivu jeni na kumshauri vibaya apige teke bakuri la dhahabu
 
Jeni aliamua kumbadilisha msimamo wa kidini jamaa mpaka akakubali na akaokoka na kubatizwa kwa maji mengi leo jeni anamgeuka na kumwona jamaa hafai sio mlokole kamili hivi kuna kipimo cha ulokole? jeni alimpa jamaa test afanye akachemka leo jeni anaconclude jamaa hafai kumwoa jeni? basi nyie marafiki zake mmemwonea wivu jeni na kumshauri vibaya apige teke bakuri la dhahabu
Fidel80!!!!!!,ww haya,huyo jamaa ameongea mwenyewe kwenye simu kuwa karibia anamaliza kifungo cha ulokole feki,so alijikubalisha kuokoka kinafiki na kudanganya watu ndio maana jen amekasirika!
Mbona hakulazimishwa alijidai neno limemuingia na kukubali kmpokea yesu kumbe alikuwa anaigiza!
Hakuna wa kumtaka huyo mzungu wa unga tapeli,wala hana udhahabu wowote!
 
Inasikitisha .. Mwambie dada jenny ajaribu kuwa convince wazazi kwamba jamaa hafai.... pia mambo ya kulazimishana ndoa yameshapitwa na wakati..
 
Habari zenu wapendwa,,kuna binti flan nampa jina la Jen,huyu jen na familia yao yote ni walokole,jen elimu yake ni ya form four na ana miaka 20 kwa sasa,wazazi wake ni wakulima tu na wana elimu ya darasa la saba na yeye ndio mtoto wa kwanza ana wadogo zake wawili.

Mwezi wa pili mwaka huu alikutana na jamaa mmoja maeneo ya kibaha akiwa anatoka kanisani mida ya saa mbili usiku kwa vile mvua ilikuwa inanyesha yule jamaa akapaki gari na kumpa lifti ktk maongezi yao jamaa akasema ni mgen sehemu ile yeye anaishi dar ni mfanya biashara wakapeana contact alipofika anaposhuka karibu na kwao jamaa akamshusha na kuendelea na safari zake.

Basi tangu siku ile jen akaendelea kuwasiliana na jamaa na wakawa marafiki akamkaribisha kanisani kwao jamaa akawa anakuja mpaka naye akaokoka baada ya miezi km mitatu jamaa kwa vile alijiweka karibu na wazee wa kanisa na kuwa anatoa misaada na akawa anaheshimika pale kanisani basi akawajulisha wazee kuwa amempenda yule binti na anataka kumuoa kwani ameonna anamfaa,Basi wazee wakakubali na mipango ya uchumba ikaanza kwa taratibu za kilokole.

Katika harakati zote hizo aliwaleta baadhi ya ndugu wa binti na kuwatambulisha kwa watu aliodai ni dada zake maeneo ya magomen ambapo alisema anaishi nao wale ndugu pamoja na jen waliamini na akawa anaenda kuwatembelea mara chache na jamaa akampeleka kkoo kwenye kwenye duka la nguo ambalo alisema ndio ofic yake na yy ndio mmiliki so akaaminika na kila kitu kikaenda sawa.


Harusi imepangwa kufungwa jmosi ijayo,sas juzi jmosi jamaa akaenda kumchukua mchumba wake waje mjini kukamilisha kununua baadhi ya vitu amabvyo walikuwa hawajakamilisha kwa ajili ya harusi,kabla ya kwenda madukani akampeleka hotelin maeneo ya magomen jen hakuwa na wasiwasi akashangaa jamaa kachukua chumba na kumtaka waingie ana maongezi jen anasema alianza kupata hofu ila akaingia jamaa akaagiza vinywaji na vyakula na kuanza kuongea ambapo jamaa alimwambia jen anataka wafanye mapnz ikiwa ni sehemu ya kufahamiana na itakuwa ni siri kati yao na kwa vile wameshapima afya na arusi ni wiki ijayo haina shida,jen akakataa basi jamaa wala hakulazimisha akamwomba anywe wine jen hajui wine na hajawahi kunywa akabembelezwa mpaka akanywa na akawa najisikia km kulala akajiegesha na jamaa akawa anachati kwenye komyuta na kunywa wine.

Jamaa akajua jen kalala kumbe hajalala na anaona na kusikia kila kitu hata jamaa alipokuwa anaongea na simu,basi kuna wakati jamaa akavua shati jeni akaona na kushangaa jamaa mwili mzima umejaa tatuu!basi akiwa anavua shati simu ya jamaa ikaita akawa anaongea na watu kuhusu biashara ila ktk maongezi akawa haelewi ni aina gani ya biashara na gafla jamaa akatoka kwenda kuongelea nje ya chumba jen akasogea mlangoni akasikia jamaa akimwambia huyo mtu kuwa karibia atatoka kwenye kifungo cha ulokole feki kwan arusi ni jmosi na akishaoa basi na ulokole ndio mwisho.

Jen aliposikia hivyo akachanganyikiwa na zile tatuu ndio zikammaliza kbs,na kurudi kitandani jamaa aliporudi jen akamwambia anajisikia kuumwa anaomba waondoke jamaa akakaataa ila jen alipoanza kulia jamaa akakubali na wakarudi kibaha hawakwenda madukani tena,alipofika kwao akawaambia wazazi na ndugu zake hakuna aliyeamini na wote wanamtetea jamaa,na wanachofanya ni kumwombea jen wasema kaingiwa na pepo,badala ya kutafakari na kutafuta suluhisho la tataizo.

Jana jen akaja kwa rafiki yake ambaye ni jiran yangu akamsimulia huo mkasa,wakaamua kwenda kule magomen kwa wale wifi zake ikabidi awaeleze lile tatizo wale wadada wakaingiwa na huruma wakamwabia ukweli kuwa yule wala sio ndugu yao ni rafiki wa kaka yao anayeishi nje ya nchi na anatumia chumba cha kaka yao na nimuuza unga hata hilo duka analosema ndio oficn kwake ni uongo na walishindwa kumwambia mapema coz hakutaka kuwa karibu nao na walionekana wanapendana na wakamwomba vyovyote atakavyoamua asiwataje kwan atawagombanisha mpaka kwa kaka yao ambae ndio km mzazi wao ndio anawalea hapa mjin!

Hapo ndio jen akachanganyikiwa,wakaamua kwenda na kule kkoo bahati mbaya wakakuta duka limefungwa kumbe hawaji kazin cku za jpili.mpaka hapo anawasiliana na mchumba vizuri tu bila kumjulisha wala kuonyesha tofauti yoyote,jana jion wakautana na jamaa maeneo ya ubungo akamrudisha kibaha,usiku ameongea na wazazi na baadhi ya ndugu hakuna anayemuelewa wanamuona muongo na wanamtetea jamaa,mpaka wazazi wakaanzisha maombi wanamwombea jen eti kaingiwa na pepo na wamemkataza asiondoke hm tena mpaka siku ya arusi.

Leo asubuhi imebidi nimpigie jiran yangu anambie kinachoendelea akanambia jen kampigia analia amechanganyikiwa na hamtaki tena huyo bwana,wazazi hawamwelewi kinachofanyika ni maombi tu na jamaa kwa vile ana pesa kawashika wazazi vizuri wanamkubalia kila analosema huyo jamaa yani wanamthamini kuliko hata jen,na baba kasema lzm ndoa ifungwe,sasa jen anahitaji msaada wa mawazo afanyeje yy hataki kuolewa tena baada ya kugundua jamaa ni tapeli tu,na wazazi wanataka aolewe,nyumbani haruhusiwi tena kutoka sasa hajui la kufanya amechanganyikiwa jirani yangu ameiomba tushirikiane namna ya kumsaidia jen hata kimawazo nami nimeamua kuwaletea wana jamii tunaomba mawazo yenu kwan jen anasema ni bora afe kuliko kuolewa na huyo mtu,wazazi hawajali wanafanya maombi tu na wanataka aolewe.
Nawasilisha.

ndoa hailazimishwi hata siku moja. hakuna kufunga wala kuomba, kwani Mungu ameshaweka wazi kila kitu. Jeny aache kuwasiliana na huyu jamaa amkane kwa uwazi. hao wanaoendelea kumwombea jeni waendelee na maombi yao. siku ifkifika hawatamlazimisha kufanya agano la ndoa na huyo mjamaa.

onyo kwa Dada zetu:
msikubali lift ovyo na hata kuzoewa ovyo. mvua haiui, siku ile angenyeshewa tu hakuna tatizo kuliko hii njia panda aliyoingia sasa. wewe mtu humjui anakwambia upande gari yake wewe unapanda, hivi inawezekanaje?. Ashukuru amemvutia pumzi maana siku ileile angesha.... hata hii ya kubadilsihana contact na mtu humjui, ya nini? ivi duniani hapa watu unaowafahamu ni wachache sana kiasi cha kutaka contact mpya zisizo hata fahamika zitokako???. tujifunze kuwa sisi wenyewe. mara nyingi dada zetu huwapuuza watu ambao mnawafahamu, halafu mnaanguka kwa mijitu hata haifahamiki
 
Back
Top Bottom