Msaada tafadhali,binti kagundua mme mtarajiwa anaigiza ulokole, kumbe .......!

Hili la kusubiri mpaka siku itimie siliungi mkono; shetani na hila nyingi kama wazazi wameshindwa kumwelewa seuze kasisi wa kanisa.............hapana aise mwambir Jen aondoke sasa hivi wala asijikawize; Amani ya nafsi yake ni kitu muhimu zaidi ya vyote

Alafu siku ikitimia ukiona ana nyuki mbili sijui utamrudisha kanisani tena???
 
Wanawake huwa kinawaponza hiki siku zote
Mkuu ni kwamba hapa jen wala hizo hela hazijamchanganya ndio maana alipobain haya hataki tena kuolewa naye ila wazazi ndio wamechanganywa na hizo hela!
Na sio mabinti wote wanapagawishwa na hela au wanajitoa tu kwa sababu ya pesa.
 
... cha msingi ni kutafuta namna ya kutofungwa kwa ndoa hiyo jmos mpaka ukweli wa jambo upatikane.
Hapo ndio ninapopasema. Na ukweli huo ni lazima kumuhusisha mtuhumiwa ili atoe upande wake wa stori. Na sioni njia nyingine ya haraka kusimamisha shughuli zaidi ya kuzungumza na upande wa pili na hata kanisa pia. Anaweza kuamua ku boycott lakini hilo litaweka doa katika maisha ya binti ya baade (na hata familia)...kwa sababu ukweli kuhusu upande wa pili hautajulikana pasipo kuacha shaka na hivyo watu watabikia kuona binti ndiye tatizo na sio huyo mwanaume.
 
hilo ndo tatizo! Kinachowasumbua wazazi sio ulokole, bali 'udhamini' wanaopewa na huyo kijana ndo maana wapo tayari kumuuza binti yao. Huyo binti awe jasiri kusimamia uamuzi wake.

Asante sisy,tatizo ni kwamba wale wazazi ulokole umewaingia kupita kiasi na jamaa alivyojidai ameokoka anahudhuria mpaka mikesha mbaya hapo ndio hata yy akamwamini, alfu kawa mdhamin wa familia anaprovide mahitaji yote.
Anataman kumwambia jamaa ukweli lkn je atakubali na keshatumia garama za kuandaa harusi na tayari wazazi wako upande wa jamaa itasaidia da husni?
Hapa labda hilo la kuugua au atoroke japo sina uhakika km atakuwa na ujasiri wa kutoroka!
 
Mkuu ni kwamba hapa jen wala hizo hela hazijamchanganya ndio maana alipobain haya hataki tena kuolewa naye ila wazazi ndio wamechanganywa na hizo hela!
Na sio mabinti wote wanapagawishwa na hela au wanajitoa tu kwa sababu ya pesa.

Huyo jeni wako anajifanya sitaki nataka mabinti si ndo mlivyo
 
Sio hivyo mkuu_you got me bad,...nimesema niko busy hapa kijiweni na hivyo nikipata ka..muda ntarudi kusoma vizuri ili ni comment na mimi,..na kuhusu suala la mikataba sio kwamba hawasomi ni kwamba wanafanya makusudi wakiaahidiwa vijisent_....Mangungo was much more better kuliko hawa wa sasa ambao wanajua lakn wanafumba macho kuuza nchi...chief alisaini kwa kile alichokiamini

Sawa Mkuu, haina shida, nimekuelewa wote tunajenga nyumba moja.
 
Hapo ndio ninapopasema. Na ukweli huo ni lazima kumuhusisha mtuhumiwa ili atoe upande wake wa stori. Na sioni njia nyingine ya haraka kusimamisha shughuli zaidi ya kuzungumza na upande wa pili na hata kanisa pia. Anaweza kuamua ku boycott lakini hilo litaweka doa katika maisha ya binti ya baade (na hata familia)...kwa sababu ukweli kuhusu upande wa pili hautajulikana pasipo kuacha shaka na hivyo watu watabikia kuona binti ndiye tatizo na sio huyo mwanaume.
Hapo sasa binti bila kupata sapoti ya wazazi hiyo story ya upande wa pili itaongelewa vp? ila km akikataa kufunga ndoa au kusababisha ikaairishwa inaweza kusaidia wazazi wakastuka na kujaribu kumsikiliza mtoto na hata kuamua kumuita huyo bwana naye ajieleze.
Lkn kwa sasa hata wazazi hawaelwi wanataka ndoa ifungwe tu,ina maana hapo hakuna nafasi ya maongezi hata akimwambia jamaa bado hata kubali na wazazi watasema ana mapepo na kumlazimisha binti kuolewa!
 
  • Thanks
Reactions: SMU
Asubiri mpaka siku ya harusi.
Halafu ndo amkatae mbele ya umati

Utamwua Bwana arusi mtarajiwa kwa BP. Sio ushauri mzuri huo, hebu fikiria kukataliwa hadaharini mbele ya wazazi, ndugu, jamaa na marafiki. Unaweza anguka chini. Tena hapo watu watamwona Jen kama hakutumia akili, watauliza kwa ni asubiri hadi kanisani.
 
hilo ndo tatizo! Kinachowasumbua wazazi sio ulokole, bali 'udhamini' wanaopewa na huyo kijana ndo maana wapo tayari kumuuza binti yao. Huyo binti awe jasiri kusimamia uamuzi wake.
Haswaaaa,hapa shetan katumia njia ya pesa!naamini mungu atampa njia na shetan atashindwa!
 
Jen anajali furaha yake na sio pesa!
Labda mabinti unaokutana nao ww na sio wote tuko hivyo!

Tuseme jeni alikuwa anajipritent kwa huyo jamaa na jamaa ameamua kutangaza nia alafu jeni anachomoa wkt mara ya kwanza alimpenda sasa hivi jeni anagundua amependa pasipo penyewe
 
Hapo sasa binti bila kupata sapoti ya wazazi hiyo story ya upande wa pili itaongelewa vp? ila km akikataa kufunga ndoa au kusababisha ikaairishwa inaweza kusaidia wazazi wakastuka na kujaribu kumsikiliza mtoto na hata kuamua kumuita huyo bwana naye ajieleze.
Lkn kwa sasa hata wazazi hawaelwi wanataka ndoa ifungwe tu,ina maana hapo hakuna nafasi ya maongezi hata akimwambia jamaa bado hata kubali na wazazi watasema ana mapepo na kumlazimisha binti kuolewa!
Sasa anaoana na mtu ambaye hawawezi kukaa na kuongea nae kama kuna issue? Katika hili la yeye kuongea na mtu wake wazazi wanalizuiaje? Tatizo ni kama yeye mwenye hajiamini katika uamuzi anaotaka kuufanya.

Well, tuseme hakuna nafasi ya mazungumzo na wazazi na hata mwanaume...so anabakiwa na reasonable options mbili tu (zote ni za aibu!), moja ni kukimbia (kuna risk ya kutafutwa na kupatikana!) na nyingine ni kukataa (kwenda kwenye send off kama ipo, akishindwa atakataa kwenda kanisani, akishindwa anakataa kula kiapo cha ndoa (hili lipo kwenye uwezo wake hakuna wa kumlazimisha!) na kutia saidi cheti cha ndoa).
 
Hakuna mwenye uweza na nguvu km mungu,amin usiamini habari ndio hiyo!

Mwenye pesa shetani makanisani kwa walokole anatengewa siti ya mbele kabisa ili iwe rahisi kutoa maburungutu ya sadaka.
Shetani wa pesa ana nguvu, si umeona wakwe wameng'ang'ania binti yao aolewe ili misaada ya shetani iendelee kumiminika
 
Aisee mpe Jen pole sana.

Nikirudi baadaye ntamshauri cha kufanya.

Hamjamboni mabibi na mabwana?

Cantalasia mambo?
 
Tuseme jeni alikuwa anajipritent kwa huyo jamaa na jamaa ameamua kutangaza nia alafu jeni anachomoa wkt mara ya kwanza alimpenda sasa hivi jeni anagundua amependa pasipo penyewe
No alimpenda kwa upendo wa kweli,baada ya kugundua jamaa kamdanganya kuwa kaokoka,kawadanganya wazazi,na hata kanisa pia na haya yote ni ili amuoe,kadanganya mpaka kazi yake,ndio maana jen hampendi tena!
Kwan hana imani naye tena inawezekana ana uovu mwingi nyuma ya pazia na hapo mapnzi yameisha.
 
Mtandao wa Jinsia, TGNP, TAWLA nk wanasoma humu au wajulishwe mapema waingie kazini, namwonea huruma binti/dada yetu!
 
Back
Top Bottom