Wanajamii ninaomba msaada wa kibiashara nina milion hizo nashindwa nifanye biashara gani kwa wale wataalamu wa biashara wanishauri
yaani sijajua nifanye biashara gani kwani tangu nianze kani sijawai fanya biashara aina yeyote! ila kutokana na maisha yanavyozidi kuwa magumu imenibidi niwe na wazo la biashara
Wewe binafsi unapenda nini?
Una uwezo kufanya nini?
Ukishajua hayo..nenda hatua mbele zaidi kuangalia je hicho unachotaka kufanya na una uwezo kukifanya ni kitu kitakacho"uzika" ?Maana biashara siyo sadaka.Unataka ufanye faida.
Hayo ni ya msingi kujua kabla ya kuangalia pesa.
Usianze na " nina sh. million 5..nifanye nini" Hii ni sawa na kuanza na mkokoteni mbele ya punda au farasi. Halitaenda.
nunua mawese uwe unapeleka hapo ng'ambo Burundi.vilevile unaweza kufanya biashara ya dagaa kutoka kigoma kwenda mikoa mingine kama mwanza ,shinyanga,hasa geita.