MSAADA: Michakato na hatua za ndoa mpaka kukamilika

braity

JF-Expert Member
May 24, 2020
354
443
Habari ya Uzima wanajamvi. Natumai wengi wetu, Mungu wetu wa Rehema ametuvusha Salama kufika mwaka 2023. Jambo la Kumshukuru sana Mungu.

Nijikite sasa kwenye Mada yetu husika wanajamvi. Kama ilivyoada kila mwanadamu huwa ana malengo yake husika ndani ya Mwaka mzima ili kujiweka juu zaidi katika maendeleo yake.

Mwaka 2023 ni mwaka ambao nimejishuhudia kabsa kwamba, miongo 3 kamili inatosha sasa kwa Kijana Mimi kuishi maisha ya Mume na Mke na kupunguza au kuacha kabisa tabia za uzinzi.

Ninamshukuru Mungu mchumba amenipatia na Hatua zote za awali zilikamilika mwishoni mwa mwaka 2022 (posa na Mahali) na Sasa kilichosalia ni Ndoa ili kusudi familia ya mke wangu mtarajiwa wanikabidhi Mke rasmi.

Ombi langu sasa, Ninaomba Ushauri wenu wa mawazo kwa wale ambao wamefanikiwa kufunga ndoa: Ni hatua gani napaswa kuzifuata sasa ili michakato yote iweze kwenda sawa? Mpaka sasa sijajua wapi naanzia na wapi namalizia!

List ya wanakamati watakaonisaidia hili swala ninayo kichwani na bila shaka hakuna atakayenigomea kwa hao wote.

Swala la kadi za harusi sijajua naliandaaje, je ni kwamba nikaripoti kanisani kwanza ili nijue muda wa harusi ndipo niandae kadi za harusi au niandae kwanza kwa utashi wangu na kuzigawa kwa watu watakaonishika mkono kwa hilo?

Najikuta nachanganyikiwa sana Tafadhali kwa mliofunga ndoa hivi karibuni na mnafahamu hatua zote mlizopitia naomba tusaidieni kimawazo ili kusudi sisi wageni tupate kunufaika katk Hili na tuje kuwasaidia wengine.

Tusaidiane ili kasherehe kawe kazuri nisije nikamuaibisha Muhaya wangu na familia yake.

NB: Ndoa kwa mipango yangu ni mwezi wa sita (6).
 
Mahali tayri ila tu wazazi hawako tayari binti yao atoke pasi harsi

Kwani harusi NI yakwao?
Wao kama wanataka kumtoa Binti Yao na sherehe wamtoe si ndio inaitwa Sendoff,
Waache upumbavu na upuuzi!

Ninyi upande wa kiumeni ndio mnahiyari ya kufanya sherehe ya kumpokea mwali ambayo huitwa Harusi.

Hao Wakwe zako masharti Yao yanaishia kwenye Mambo ya Mahari, ukishatoa Mahari tayari huyo ni Mkeo.
Hizo zingine ni mbwembwe!

Wasikuchanganye!
Kama hawawezi waambie warudishe Mahari tafuta Mwanamke mwingine, wapo wengi ambao unaweza kuwaoa tena pasipo hayo makitu ya Mahari na harusi
 
Mahali tayri ila tu wazazi hawako tayari binti yao atoke pasi harsi
Kwa kukusaidia kwanza tofautisha baina ya.
  • Kufunga ndoa kanisani.
  • Na sherehe baada ya ndoa.
Bila shaka wazazi wa binti wnataka zaidi ndoa , na sio sherehe.

Ndoa yaweza kufungwa kanisani, na ikahudhuriwa na ndugu wachache wa pande zote mbili, hapo rasmi umekabidhiwa mke, then swala la harusi/ yaani Sherehe ikawa wakati mwingine utakaokuwa umejipanga kiuchumi. Ni swala la wewe kukubaliana na binti nini mfanye. Ila epuka kufanya maamuzi kwa shinikizo.
 
Kwa kukusaidia kwanza tofautisha baina ya.
  • Kufunga ndoa kanisani.
  • Na sherehe baada ya ndoa.
Bila shaka wazazi wa binti wnataka zaidi ndoa , na sio sherehe.

Ndoa yaweza kufungwa kanisani, na ikahudhuriwa na ndugu wachache wa pande zote mbili, hapo rasmi umekabidhiwa mke, then swala la harusi/ yaani Sherehe ikawa wakati mwingine utakaokuwa umejipanga kiuchumi. Ni swala la wewe kukubaliana na binti nini mfanye. Ila epuka kufanya maamuzi kwa shinikizo.
Duuh nimekupata
 
Kwani harusi NI yakwao?
Wao kama wanataka kumtoa Binti Yao na sherehe wamtoe si ndio inaitwa Sendoff,
Waache upumbavu na upuuzi!

Ninyi upande wa kiumeni ndio mnahiyari ya kufanya sherehe ya kumpokea mwali ambayo huitwa Harusi.

Hao Wakwe zako masharti Yao yanaishia kwenye Mambo ya Mahari, ukishatoa Mahari tayari huyo ni Mkeo.
Hizo zingine ni mbwembwe!

Wasikuchanganye!
Kama hawawezi waambie warudishe Mahari tafuta Mwanamke mwingine, wapo wengi ambao unaweza kuwaoa tena pasipo hayo makitu ya Mahari na harusi
Nimekupata mkuu
 
Habari ya Uzima wanajamvi. Natumai wengi wetu, Mungu wetu wa Rehema ametuvusha Salama kufika mwaka 2023. Jambo la Kumshukuru sana Mungu.

Nijikite sasa kwenye Mada yetu husika wanajamvi. Kama ilivyoada kila mwanadamu huwa ana malengo yake husika ndani ya Mwaka mzima ili kujiweka juu zaidi katika maendeleo yake.

Mwaka 2023 ni mwaka ambao nimejishuhudia kabsa kwamba, miongo 3 kamili inatosha sasa kwa Kijana Mimi kuishi maisha ya Mume na Mke na kupunguza au kuacha kabisa tabia za uzinzi.

Ninamshukuru Mungu mchumba amenipatia na Hatua zote za awali zilikamilika mwishoni mwa mwaka 2022 (posa na Mahali) na Sasa kilichosalia ni Ndoa ili kusudi familia ya mke wangu mtarajiwa wanikabidhi Mke rasmi.

Ombi langu sasa, Ninaomba Ushauri wenu wa mawazo kwa wale ambao wamefanikiwa kufunga ndoa: Ni hatua gani napaswa kuzifuata sasa ili michakato yote iweze kwenda sawa? Mpaka sasa sijajua wapi naanzia na wapi namalizia!

List ya wanakamati watakaonisaidia hili swala ninayo kichwani na bila shaka hakuna atakayenigomea kwa hao wote.

Swala la kadi za harusi sijajua naliandaaje, je ni kwamba nikaripoti kanisani kwanza ili nijue muda wa harusi ndipo niandae kadi za harusi au niandae kwanza kwa utashi wangu na kuzigawa kwa watu watakaonishika mkono kwa hilo?

Najikuta nachanganyikiwa sana Tafadhali kwa mliofunga ndoa hivi karibuni na mnafahamu hatua zote mlizopitia naomba tusaidieni kimawazo ili kusudi sisi wageni tupate kunufaika katk Hili na tuje kuwasaidia wengine.

Tusaidiane ili kasherehe kawe kazuri nisije nikamuaibisha Muhaya wangu na familia yake.

NB: Ndoa kwa mipango yangu ni mwezi wa sita (6).

Kwanza jipange kifedha aff mengine yatakaa kwenye mstari
 
Njoo naye nikufungishe hiyo ndoa kibabe,kilichobakia nenda kanisani kwako mtafute kiongozi wa kiroho umalize,harusi Ni hiyari
 
Back
Top Bottom