Msaada LAPF kuhusu fao la kujifungua

Red pen

Member
Mar 4, 2019
51
36
Habar zenu ndugu zangu?.Natokea wilaya ya Muleba, mkoani Kagera, naombeni msaada wa mawazo na muongozo kwa wale wanachama wa LAPF.

Nilijifungua mwaka Jana 10/8/2018 nilijaza fomu na kuweka viambatanisho vyote kudai fao la uzazi. Tarehe 5/9/2018 barua zangu zilipokelewa ofisi za LAPF mwanza maana huku hatuna ofisi.

Kinachoniuma mpaka Sasa sijalipwa hela yoyote, huku makato ya Kila mwezi yakiendelea.

Nimefatilia mpaka kutuma emails, kupiga simu n.k lakini Cha ajabu najibiwa bado nisubiri wanasubilia muongozo!!.

Nimeangaika kwenda ofisini kwa wakala wao aliyekuwepo nimekuta watu wengine wakanijibu Lapf haipo tena baada ya muungano wa mifuko kufanyika!

Nilimfatilia huyo kaka ananijibu nizidi kusubili!!!. Kinachoniuma zaidi na zaidi gharama zangu kwa maana huku hakuna ofisi zao kuprocess kila kitu mpaka miuli ya mwanasheria, na hela ya kutuma kwenye gari kuipeleka zilipo ofisi zao huko mwanza nilitoa 50,000/=!! Na hizo nilizikopa kwani sikuwa na hela ndo nimejifungua tena kwa opresheni!

Jamani jamani naombeni muongozo wa hili suala kama kuna anayejua nifanyeje na kama kuna muhusika labda ni mfanyakazi wa huo mfuko LAPF tafadhari naombeni mnisaidie nipitie wapi hadi nipatiwe haki yangu.

Nitashukuru Sana wadau.
 
Pole Sana mama huyo mtoto uliyezaa baba yake yupo au hayupo? Mbona unaonekana kuhangaika Sana peke yako?
 
Habar zenu ndugu zangu?.Natokea wilaya ya Muleba, mkoani Kagera, naombeni msaada wa mawazo na muongozo kwa wale wanachama wa LAPF.

Nilijifungua mwaka Jana 10/8/2018 nilijaza fomu na kuweka viambatanisho vyote kudai fao la uzazi. Tarehe 5/9/2018 barua zangu zilipokelewa ofisi za LAPF mwanza maana huku hatuna ofisi.

Kinachoniuma mpaka Sasa sijalipwa hela yoyote, huku makato ya Kila mwezi yakiendelea.

Nimefatilia mpaka kutuma emails, kupiga simu n.k lakini Cha ajabu najibiwa bado nisubiri wanasubilia muongozo!!.

Nimeangaika kwenda ofisini kwa wakala wao aliyekuwepo nimekuta watu wengine wakanijibu Lapf haipo tena baada ya muungano wa mifuko kufanyika!

Nilimfatilia huyo kaka ananijibu nizidi kusubili!!!. Kinachoniuma zaidi na zaidi gharama zangu kwa maana huku hakuna ofisi zao kuprocess kila kitu mpaka miuli ya mwanasheria, na hela ya kutuma kwenye gari kuipeleka zilipo ofisi zao huko mwanza nilitoa 50,000/=!! Na hizo nilizikopa kwani sikuwa na hela ndo nimejifungua tena kwa opresheni!

Jamani jamani naombeni muongozo wa hili suala kama kuna anayejua nifanyeje na kama kuna muhusika labda ni mfanyakazi wa huo mfuko LAPF tafadhari naombeni mnisaidie nipitie wapi hadi nipatiwe haki yangu.

Nitashukuru Sana wadau.
Pole sana, ni kweli utasubiri sana muongozo. Nimejaribu kufatilia orodha ya mafao yao lkn website yao inagoma sijajua shida.

Wewe angalia kwenye website yao kama wana fao la uzazi www.psssf.go.tz.

Kisha kama lipo basi piga hapa +255 26 2321952 kueleza malalamiko yako.

MUHIMU

Jua kwamba Sheria mpya ya PSSSF ilifuta sheria zoote za zazamani ikiwepo ya LAPF ambayo ilikua na fao la uzazi.

Sheria hii mpya imeanza kutumia tarehe 1/08/2019. Kwaiyo imefuta hizo sheria zazamani ambapo kwa uelewa wangu mimi ni kwamba, haya madai yako yalikua njiani kufanyiwa kazi sasa hayajafika mwisho ndio sheria mpya ikaja kazini.

Kwaiyo basi, huo muongozo wanaosubiri ni eidha uwe unatoa maelekezo wale ambao walijqza fomu zakuombea mafao yao lakini hawajapewa jee, walipwe au laa?

Kimatiki hapo huwezi kulipwa sababu sheria haina fao la kujitoa ( Kama fao lipo basi jaza fomu upya)

Wasalaam.
 
LAPF ,GEPF,PSPF NK.Imeunganishwa na Kuitwa PSSSF.
Kuna mabadiliko Makubwa ya Sheria Kwa waatumishi wa Kudumu,WA Muda Maalim na Watumishi wa Muda.
 
Pole Sana mama huyo mtoto uliyezaa baba yake yupo au hayupo? Mbona unaonekana kuhangaika Sana peke yako?
Asante, ninachokitafuta hapa ni kujua nifanyeje ili kupata fao langu la uzazi. Mim ndie muhusika na ninakatwa Kila mwezi.
 
Mmmh
Pole sana, ni kweli utasubiri sana muongozo. Nimejaribu kufatilia orodha ya mafao yao lkn website yao inagoma sijajua shida.

Wewe angalia kwenye website yao kama wana fao la uzazi www.psssf.go.tz.

Kisha kama lipo basi piga hapa +255 26 2321952 kueleza malalamiko yako.

MUHIMU

Jua kwamba Sheria mpya ya PSSSF ilifuta sheria zoote za zazamani ikiwepo ya LAPF ambayo ilikua na fao la uzazi.

Sheria hii mpya imeanza kutumia tarehe 1/08/2019. Kwaiyo imefuta hizo sheria zazamani ambapo kwa uelewa wangu mimi ni kwamba, haya madai yako yalikua njiani kufanyiwa kazi sasa hayajafika mwisho ndio sheria mpya ikaja kazini.

Kwaiyo basi, huo muongozo wanaosubiri ni eidha uwe unatoa maelekezo wale ambao walijqza fomu zakuombea mafao yao lakini hawajapewa jee, walipwe au laa?

Kimatiki hapo huwezi kulipwa sababu sheria haina fao la kujitoa ( Kama fao lipo basi jaza fomu upya)

Wasalaam.
Mmh! Asante.
 
Jua serikali yako imefirisika na kila sehemu imeharibu, hata wanaofatilia mafao yao wanapata tabu sana, kwa ushauri wangu japo unaweza usiuchukue ni kwamba wekeza nguvu zako kwenye jambo lingine na hesabu kuwa ushapoteza, hii itaokoa muda wako na kuwa na nafasi ya kujenga uchumi wako kuliko kupoteza na muda na hao wasioelewa kama ni LAPF au PSSSF.
 
Asante, ninachokitafuta hapa ni kujua nifanyeje ili kupata fao langu la uzazi. Mim ndie muhusika na ninakatwa Kila mwezi.
Unakatwa fao la uzazi? Mifuko imeunganishwa mfuko mpya waweza kuwa hauna Hilo fao uwe mpole tu.
 
Back
Top Bottom