Msaada biashara ya Tractor

Cholemasaki

Member
Mar 26, 2013
61
13
Ninaomba msaada wa mawazo ya biashara nnayoweza kufanya na trekta.

Awali nilikua kwenye kilimo cha mpunga lakini nimeona hakinilipi na trekta lilikua linaharibika mara kwa mara na kunigharimu sana.

Pia kwakua nipo mjini, trekta lipo mkoani, ufuatiliaji ulikua mgumu.

Ninaomba ushauri wa biashara nyingine ninayoweza kufanya na trekta, ambayo itanilipa, ukiacha kilimo.

Pia ningependelea zaidi mawazo ya biashara ambayo naweza kuifanya not far from mjini ambayo ufuatiliaji wake utakua si mgumu na utafanya less damage kwa trekta langu.

Natanguliza Shukrani.
 
hahahah.... sasa mkuu unataka trekta utumie mjini hivi kwel inaezekana, ushakutana na trekta posta kwel!?? wakati unanunua ulifikiria nini....

mbona trekta zinalipa vizuri sana na zipo vijijini, sema we hujawekeza.... jaribu hili:
tafuta kiasi cha pesa kwa ajiri ya matengenezo kwanza ya trekta yako sababu umesema linaharibika, nunua vifaa genuine.....
funga gprs kwenye trekta yako utakua unaona kupitia sim au kompyuta sehemu yoyote hilo trekta lilipo, dereva hakudanganyi kitu(usimwambie kama umeweka gprs, atachakachua).....
tafuta location nzuri yenye shughuri za kilimo kwa wingi....
baada ya hapo utanyanyua miguu usubirie faida tu!!!!!
 
hahahah.... sasa mkuu unataka trekta utumie mjini hivi kwel inaezekana, ushakutana na trekta posta kwel!?? wakati unanunua ulifikiria nini....

mbona trekta zinalipa vizuri sana na zipo vijijini, sema we hujawekeza.... jaribu hili:
tafuta kiasi cha pesa kwa ajiri ya matengenezo kwanza ya trekta yako sababu umesema linaharibika, nunua vifaa genuine.....
funga gprs kwenye trekta yako utakua unaona kupitia sim au kompyuta sehemu yoyote hilo trekta lilipo, dereva hakudanganyi kitu(usimwambie kama umeweka gprs, atachakachua).....
tafuta location nzuri yenye shughuri za kilimo kwa wingi....
baada ya hapo utanyanyua miguu usubirie faida tu!!!!!

Noted mkuu... Asante sana
 
Pole kwa kushindwa kupatiwa ushauri mzuri, lakini kuwa mstahimilivu watakuja wenye ushauri wenye manufaa kwako
 
Tractor yako aina gani.km unataka mjini lichongee trailer ili ubebee container empty kutoa ktk ma Icd kupeleka bandalini japo rushwa itakutoka sana maana yalipigwa marufuku lakini ya wahindi yanafanya.ila ningekushauri rudi shamba
 
Back
Top Bottom